Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

5th JULY 2025


 

WAFANYAKAZI WA AMANI!





“MBEGU ZA UZIMA”
Jumapili, Julai, 6, 2025. 
Dominika ya 14 ya mwaka wa Kanisa

Isa 66: 10-14; 
Zab 66: 1-7, 16, 20;
Gal 6: 14-18; 
Lk 10: 1-12, 17-20.

WAFANYAKAZI WA AMANI!

“Mavuno ni mengi lakini wafanyakazi ni wachache.” Hakika usemi huu wa Yesu ulionekana wazi wazi katika jumuiya ndogo ya wakristo wa Kwanza. Wakati huo, Kanisa lilikuwa kama mbegu ndogo ya haradali iliofunikwa kwenye kipande kikubwa cha ardhi. Leo hii duniani kuna Wakristo zaidi ya billioni moja. Kwakweli wafanyakazi wa mwanzo hawakufanya kazi bure. Mbegu ya haradali imekuwa na kuwa mti mkubwa kwaajili ya makao ya watu maelfu. Chachu ndogo ya Amira imafanya unga wote ukaumuka. Kwakuiweka vizuri zaidi ni kwamba, nne kati ya tano hawajaupokea ujumbe wa Kristo bado

Kati ya mabilioni haya ni wangapi wanaweza kuwa wafanyakazi hodari katika Shamba la Bwana? Kwani mavuno bado ni mengi na kwa ujumla “wafanyakazi” tunadhani ni mapadre au mabruda au masister, ndio “walioitwa”. Lakini, nina mashaka kwamba Yesu alikuwa aikiwafikiria Mapare au watawa wakati akiongea maneno haya. Katika hali ya kweli, kipindi cha mwanzoni mwa Agano la Jipya hakukuwa na mapadre au masister kama tunavyoelewa siku hizi. Katika akili ya Yesu na pia kwa wahubiri wa kwanza- kila mmoja aliyejulikana kama mfuasi wa Yesu alijulikana kuwa mfanyakazi katika shamba la Bwana. Mfano, Mt. Paulo, alikuwa mtume, na muhubiri maarufu lakini hakuwa Askofu wala Padre. Sisi tunadhani kufanya kazi katika shamba la Bwana ni lazima uwe Padre au mtawa. 

Kuwa Mkristo sio mwisho. Bali ni muda muafaka, wakuamini, njia iliyo sahihi zaidi ya kuwa viumbe vipya ambao Yesu na Paulo waliongelea. Kuwa watu wapya inamaana kuzama ndani ya Mungu aliye ukweli wa yote na mweza wa yote, Mungu anayetuita kila siku zaidi ya sehemu tuliopo na ambaye, kwa wakati huo anaingia ndani kabisa ya nafsi zetu na yote tunayofanya. Mtu huyu mpya huishi maisha ya utu na ukweli, maisha ya huruma ya kweli na kujali. Mtu huyu huishi katika uhuru wa kweli na Amani. Neno moja ambalo linatokea katika masomo yote matatu leo ni “Amani”. Katika somo la kwanza Nabii Isaya anasema Mungu “atatuelekezea Amani kama mto”. Paulo anaongelea kuhusu Amani na rehema itakayokuja kwa wote walio viumbe vipya ndani ya Kristo. Na katika Injili, Yesu anawaambia wafuasi wake walete Amani kila watakapo ingia. Amani hii sio tegemezi kwa mambo ya nje. Inaweza ikawapo hata kukiwa na machafungo. Ni Amani aliopata Yesu baada ya sala yake bustanini. Ni Amani ambayo Paulo aliipata, kwa “kushiriki msalaba wa Kristo” na kubeba alama za majeraha na mateso ya Yesu katika mwili mwake.

Kwahiyo kazi yetu kama Wakristo ni kuleta Amani. Na zaidi ya yote, tunahitaji Amani na usalama ndani ya roho zetu kabla ya vyote. Ni Amani ambayo mfuasi wa Karibu wa Yesu anaweza kuileta. Tunaitwa leo na Yesu kuwa wafanyakazi pamoja na Yesu katika shamba lake ambalo ni jamii zetu tunamoishi. Pengine ni jamii inayo onekana kuwa na mafanikio ya nje na watu wanasitawi lakini kwa bahati mbaya ni jamii iliyokosa Amani na iliyo maskini kiroho na yenye utapia mlo wa kiroho. Tunaitwa leo tuwe wafanyakazi ili jamii zetu zibadilike na thamani ya Injili ambayo inajulikana kidogo sana hata kwetu iweze kuonekana. Tuwaombee wale wote walioitwa kwa namna ya pekee kulitumikia kundi la Mungu. Baba Mtakatifu wetu Fransisko, Maaskofu wote, Mapadre, Mashemasi, Watawa, Walei wote, ili Mungu awajaliye neema yakutimiza majukumu yao yakumtangaza Kristo kwa watu wote. Pia kwa namna ya Pekee, tuwaombee wale watakao pewa daraja la upadre wiki hii, Jimbo la Moshi na leo hii katika jimbo la Zanzibar Mungu awabariki siku zote na awajaliye hekima itakayo kaa nao na kufanya kazi ndani yao. Mungu awe nao daima. 

Sala: Bwana! Tusaidie tuwe wajumbe wa Amani yako duniani. Amina


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JULAI 6, 2025



MASOMO YA MISA, JULAI 6, 2025
DOMINIKA YA 14 YA MWAKA C

SOMO 1
Isa. 66:10 – 14

Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea Amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu. Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa Bwana utajulikana, uwaelekeao watumishi wake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 66:1 – 7, 16, 20 (K) 1

(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote.

Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Imbeni utukufu wa jina lake.
Tukuzeni sifa zake, 
Mwambieni Mungu, matendo yako yanatisha kama nini! (K)

Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,
Naam, italiimbia jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu,
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)

Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tulikomfurahia,
Atawala kwa uweza wake milele. (K)

Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Name nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Na ahimidiwe Mungu aliyeyakataa maombi yangu,
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)


SOMO 2
Gal. 6:14 – 18

Mimi, hasha, nisione fahari juu ya kito chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu. Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya. Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, Amani na iwe kwao rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu. Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu. Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 1:12, 14

Aleluya, aleluya,
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu.
Aleluya.


INJILI
Lk. 10:1 – 12, 17 – 20

Baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenye kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apelike watenda kazi katika mavuno yake. Enendeni, angalieni, nawatuma kama wanakondoo kati ya mbwa-mwitu. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani. Na nyumba yoyote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa Amani, Amani yenu itamkalia; la, hayumo, Amani yenu itarudi kwenu. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihamehame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii. Na mji wowote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu; wapozeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia. Na mji wowote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni, Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yenu tunayakung’uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia. Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo.

Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahaini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2025  www.fur-kat.blogspot.com.

YESU BWANA HARUSI WETU MPENDWA!



"ASALI ITOKAYO MWAMBANI"
Tafakari ya Kila siku
Jumamosi, Julai 5, 2025 
Juma la 13 la Mwaka

Kumbukumbu ya Bikira Maria ya Jumamosi

Mwa 27: 1-5, 15-29; 
Zab 135: 1-6; 
Mt 9: 14-17


YESU BWANA HARUSI WETU MPENDWA!

Dira ni kifaa kinachotumika na watu kama wanajeshi, nahodha nk. Masomo ya leo ni kama dira, yana tufunulia Umungu wa kweli ndani ya Yesu. Kama dira inavyo muongoza nahodha ili kufika mwisho wa safari yake. Pia Yesu ni dira yetu anatuongoza ili tufike kwenye furaha ya milele. Lakini furaha hii haipatikani hivi hivi, ni lazima kupitia mawimbi mbali mbali kama nahodha anapopitia njia mbali mbali na sehemu asiyo ifahamu ili kufikia lengo lake. Yesu ni nahodha pekee aliyekuwa na hakika ya ushindi wake, mateso, kifo na ufufuko. Hata njia yetu itakuwa hivyo hivyo. Pili maisha yetu ni kama kioo kinacho tuonesha jinsi tulivyo. Lakini tunapomchukua Yesu, kama divai mpya na mawazo mapya na mtazamo mpya wa ukweli, yeye anakuwa kioo chetu cha kumulika maisha yetu nakutambua ukweli halisi ya kuwa tunapaswa kuwa tofauti zaidi na jinsi tulivyo sasa. Maisha ya zamani tuliyo jijengea yenye sheria ngumu na tena nyingine zenye ubinafsi na chovu au mambo mengine yanayopingana na upendo wa Yesu yanapaswa yaondolewe na kuwa kiumbe kipya na kuweka mambo mapya yaliosimikwa katika upendo wa Yesu.

Kwa hiyo kuna ulazima wa kubadili maisha yetu. Kwakumweka Yesu kama kioo mbele yetu ili amulike maisha yetu. Hapo tutaona nafsi yetu ilivyo tofauti na nafsi ya Yesu ambaye sisi wote tumeitwa kuishi maisha yake. Maisha yangu yanapaswa yawe kama maisha ya Yesu, kama nashindwa kuishi kama Yesu alivyo basi napaswa kubadili mienendo yangu. Tutafute ukweli kuhusu nafsi zetu zaidi na tuondoe ile hali yakutaka kujua tuu ukweli kuhusu maisha ya wengine na kuficha yetu. Tunapoteza muda mno kutaka kujua nafsi za wengine, tuanze na nafsi zetu na moja kwa moja mafanikio yataonekana na wengine. Tuombee neema ya Mungu ituongoze ili tuweze kubadili maisha yetu kwanza katika kweli ya Yesu kabla hatuja thubutu kuwarekebisha wengine.

Kwa upande mwingine, tunaitwa kuwa huru. Tumeitwa kuwa huru na kufurahai maisha katika hali kamili na kufurahi furaha kamili anazo toa Mungu ili tuzifurahie kama Mungu anavyo penda. Uhuru ulio wa kweli kabisa ni ile hali ya kuwa na Bwana harusi kati yetu. Ni furaha ya harusi ya mwana-kondoo. Tumeitwa kusherekea umoja wetu na yeye milele. Kwa hiyo wageni hawawezi kuomboleza wakati wapo na Bwana harusi kati yao. Lakini siku zinakuja ambapo Bwana harusi ataondolewa kati yao, ndipo wakatapo funga.

Kuna muda katika maisha yetu ambapo Bwana harusi anachukuliwa. Muda huu unaweza kuwa muda ule tunao hisi kumkosa Kristo katika maisha yetu. Hili linaweza kuja kwasababu ya matokeo ya dhambi zetu, lakini pia inaweza kuja kwasababu ya sisi kuwa karibu na Kristo. Kufunga inaweza kutusaidia sana kuepuka na mambo mengi tulio jifunga nayo katika maisha yetu. Imejaa hali ya kutusaidia kuongoza matamanio yetu na kutakasa tamaa zetu. Kufunga ni sehemu ya kuzamisha imani kutusaidia kukutana na Bwana Harusi. Kufunga inaweza kuchukua hali mbali mbali, lakini moyoni ni kitendo cha kujikatalia na kusogea karibu zaidi na Mungu. Inatusaidia kuepukana na tamaa zetu za kidunia na kutuvuta karibu zaidi na Kristo.

Tafakari ni mara ngapi unatamani kuzama katika maisha ya Kristo. Je, unatamani kukutana na furaha ya Yesu? Je, unatamani kumuiga yeye? Kama unapenda kuhisi furaha ya Bwana harusi, Yesu, kabidhi kila kitu kwake katika sala. Na hapo endelea kumtolea hali zote za kufunga, na kujikatalia. Endelea kutolea sadaka kwa Mungu na utaona matunda yake.

Sala: Bwana, natamani kuwa nawe katika maisha yangu zaidi ya chochote. Nisaidie kuona vile vitu vinavyo endana na upendo wako na unitakase ili moyo wangu uweze kuishi katika uhuru na furaha unayopenda mimi niishi. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, JULAI 5, 2025



MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, JULAI 5, 2025
JUMA LA 13 LA MWAKA


SOMO 1 
Mwa. 27 :1-5, 15-29

Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Nave akamwitikia, Mimi hapa. Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu. Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo; ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa.

Na Rebeka akasikia, Isaka aliposema na Esau mwanawe. Basi Esau akaenda nyikani awinde mawindo, ayalete. Kisha Rebeka akatwaa mavazi mazuri ya Esau mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo. Na ngozi za wana-mbuzi akamvika mikononi, na katika ulaini wa shingo yake. Naye akampa Yakobo mwanawe mikononi mwake hicho chakula kitamu na mkate alioufanya.

Akaja kwa baba yake, akasema, Babangu. Akasema, Mimi hapa, U nani wewe, mwanangu? Yakobo akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondo- ka, tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako inibariki. Isaka akamwuliza mwanawe, Imekuwaje umepata upesi namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu Bwana, Mungu wako, amenifanikisha. 

Isaka akamwambia Yakobo, Karibu, tafadhali, ili nikupapase, mwanangu, nione kwamba wewe ndiwe mwanangu Esau, ama siyo. Basi Yakobo akamkaribia Isaka, babaye, naye akampapasa, akasema, Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau. Wala hakumtambua, kwa maana mikono yake ilikuwa kama mikono ya Esau, ndugu yake, yenye malaika; basi akambariki. Akamwuliza, Wewe ndiwe kweli mwanangu Esau? Akasema, Ndimi. Akasema, Niletee karibu nami nipate kula mawindo  ya mwanangu, ili roho yangu ikubariki. Akamsogeza karibu, naye akala; kisha akamletea mvinyo, akanywa. Isaka, baba yak, akamwambia, Njoo karibu sasa, ukanibusu, mwanangu.

Akamkaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema, Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba alilolibariki Bwana. Mungu na akupe ya umande wa mbingu, Na ya manono ya nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo, Mataifa na wakutumikie Na makabila wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie, atakayekulaani alaaniwe, Na atakayekubariki abarikiwe.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.




WIMBO WA KATIKATI
Zab. 135 :1-6 (K) 3

(K) Msifuni Bwana kwa kuwa ni mwema.

Aleluya.
Lisifuni jina la Bwana,
Enyi watumishi wa Bwana, sifuni.
Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana,
Nyuani mwa nyumba ya Mungu wetu. (K)

Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema.
Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza.
Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo,
Na Israeli, wawe watu wake hasa. (K)

Maana najua ya kuwa Bwana ni mkuu.
Na Bwana wetu yu juu ya miungu yote.
Bwana amefanya kila lililompendeza,
Katika mbingu na katika nchi,
Katika bahari na katika vilindi vyote. (K)



SHANGILIO
Mt 4:4

Aleluya, aleluya,
Mtu hataishi kwa mkate tu, 
ila kwa kila neno litokalo katika 
kinywa cha Mungu. 
Aleluya.



INJILI
Mt 9:14-17

Wanafunzi wake Yohane walimwendea Yesu wakusema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, bali wanafunzi wako hawafungi? Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda Bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga. Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; maana kile kilichotiwa huonndoa kipande cha lile vazi, na pale palipotatuka huzidi. Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama wakitia, vile viriba hupasuka, divai ikamwagika, na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya, vikahifadhika vyote.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

4th JULY 2025


 

MDHAMBI ANAKARIBISHWA KWA HURUMA



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Julai 4, 2025 
Juma la 13 la Mwaka

Mwa 23:1-4,19, 24:1-8,62-67; 
Zab 105: 1-5; 
Mt 9: 9-13


MDHAMBI ANAKARIBISHWA KWA HURUMA

Embu jaribu kufikiri mtu anakuwa daktari asiyependa kuona au kushughulika na wagonjwa, yeye anapenda tu watu wenye afya njema. Nadhani atakosa kabisa wakutibu kwasababu watu wenye afya njema hawahitaji kutibiwa. Huu ndio msemo anaotumia Yesu katika Injili baada ya kulaumiwa kuwa rafiki wa wenye dhambi. Ingekuwa ni ajabu kabisa kwa yeye kuja ulimwenguni kama asingekuja kumpatanisha mwanadamu mkosefu na Mungu Baba yake. Tunajua nikwa jinsi ghani alivyofanikiwa katika hili, ambapo Mathayo aliyekuwa mdhambi sio tuu anabadilika bali anakuwa pia mtume wa kazi yake. Ni kitu ghani kilichopo ndani ya Kristo kinachowavutia wenye dhambi kwenda kwake? Ni kwasababu ya upendo aliokuwa nao na huruma. Pale ambapo Mafarisayo walikimbilia ili kwenda kuhukumu, Yesu aliangalia uzuri uliopo ndani ya mtu na watu walimwitikia kwa jinsi yake yakuwaita kwa upendo. Yesu hakuja kwa ajili ya wale wanaojiona wenye haki, bali alikuja kuwaita wakosefu kutoka katika utumwa wa dhambi na kuwaleta katika uhuru wa watoto wa Mungu, naye alifanya hivyo kwakuwa kati yao.

Sisi nasi tunaalikwa kuwa na huruma kwa ndugu zetu na watu wote wanaliotukosea. Pia kama wajumbe wa neno la Mungu tusijione kwamba sisi tunastahili zaidi kuliko wengine, vyeo vyetu tujue ni jukumu tulilopewa la kuwa watumishi, kuwatumikia wote bila kuwatenga wengine. Baba Mtakatifu Fransisko alisema “Mchungaji anapaswa kunukia harufu za kondoo wake” wale waliopewa jukumu la kuwachunga kondoo wa Mungu, tunaitwa kuwa watumishi waaminifu, wenye kupata muda wa kuongea na kondoo wetu na kuwatumikia, usiwe juu sana kiasi cha kondoo kushindwa kukufuata na kutaka ushauri kwako. Kuwa mchungaji sio kuwa “Boss” badala yake ni kuwa mtumishi wa watumishi wa Mungu. Katika kitabu cha Malaki 2:5..kuwa kuhani/Padre/mjumbe wa Mungu nikutambua “kwa midomo yako utawapa watu akili na matashi mema na watu watataka ushauri na maelekezo kutoka kwako kwakuwa wewe ni mjumbe wa Mungu….”.

Kwa wale waliochaguliwa viongozi wa jumuiya au uongozi wowote ni lazima kutambua kuwa kwakuwa hivyo sio kuwa Mkristo zaidi ya wengine bali ni utumishi wa watumishi wa Mungu. Tuombe neema yakutumia uongozi tuliopewa na Mungu ili kuwaongoza wote bila kuwapenda matajiri tuu na kuwaacha maskini au kuwapenda wanaosali na kuwachukia wasio Sali. Badala yake tutumie njia njema ya kuwaonesha upendo na huruma kama Yesu, wanaweza kurudi na kuwa wema tena. Sisi zote kwa maisha yetu tumlete Kristo aonekane kwa watu.

Sala: Bwana, ninarudi kwako katika mahitaji yangu kwako ninakiri dhambi zangu. Ninakuomba unisamehe kwa kukukosea wewe na ninatambua kuwa ni wewe tu jibu pekee kuhusu dhambi zangu. Naomba Bwana uwe na huruma kwangu na unisamehe dhambi zangu zote. Amina

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, IJUMAA, JULAI 4, 2025



MASOMO YA MISA, IJUMAA, JULAI 4, 2025
JUMA LA 13 LA MWAKA


SOMO 1 
Mwa. 23:1-4, 19; 24:1-8, 62-67

Umri wake Sara ulikuwa miaka mia na ishirini na saba, ndio umri wake Sara. Sara akafa katika Kiriath-arba, ndio Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Ibrahimu akaja kumlilia Sara na kumwombolezea. Akaondoka Ibrahimu kutoka mbele ya maiti wake, akasema na bani Hethi, akinena, Mimi ni mgeni, ninatembea kwenu; nipeni mahali pa kuzikia kwenu, pawe pangu, nimzike maiti wangu atoke mbele yangu.

Basi baada ya hayo Ibrahimu akamzika Sara mkewe katika pango ya shamba la Makpela kuelekea Mamre, ndiyo Hebroni, katika nchi ya Kanaani.

Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote. Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke. Yule mtumishi akamwambia, Labda yule mwanamke hatakubali kufuatana nami mpaka nchi hii, Ibrahimu akamwambia, Ujihadhari, usimrudishe mwanangu huko. Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya babaangu, na kusema nami katika nchi niliyozaliwa, aliniapia akisema, Nitawapa uzao wako nchi hii; yeye atampeleka malaika wake mbele yako, anwe utamtwalia mwanangu mke tokea huko; na yule mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi, utafunguliwa kiapo changu hiki; lakini usimrudishe mwanangu huko.

Basi isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana laikaa katika nchi ya kusini. Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja. Rebeka akainua macho, anaye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia. Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika. Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda. Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamaake.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.




WIMBO WA KATIKATI
Zab. 106:1-5 (K) 1

(K) Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema.

Aleluya.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema,
kwa maana fadhili zake ni za milele.
Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana,
kuzihubiri sifa zake zote. (K)

Heri washikao hukumu,
Na kutenda haki sikuzote.
Ee Bwana, unikumbuke mimi,
Kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako. (K)

Unijilie kwa wokovu wako,
Ili niuone wema wa wateule wako.
Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako,
Na kujisifu pamoja na watu wako. (K)



SHANGILIO
Zab. 130:5
Aleluya, aleluya,
Roho yangu inamngoja Bwana, 
na Neno lake nimelitumainia.
Aleluya.



INJILI
Mt. 9:9 – 13

Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata. 

Ikawa alipoketi nyumbani ale chakula, tazama, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuja wakaketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake. Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi? Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi. Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

3rd JULY 2025


 

KUTOA USHUHUDA KWA YESU MFUFUKA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Julai 3, 2025
Juma la 13 la Mwaka
Sikukuu ya Mt. Toma, Mtume

Efe 2:19-22
Zab 117:1-2;
Yn 20:24-29.


KUTOA USHUHUDA KWA YESU MFUFUKA!

Leo tuna sheherekea sikukuu ya Mt. Thomasi, Mtume. Thomas ni maarufu sana kwa maswali yake aliyeyaleta, na tunaweza kutulia kwasababu ya maneno ya kwanza aliyosema Yesu, wakti Tomasi akiwa na mashaka: “Amani iwe nanyi”. Yesu hakumwaibisha au kupatwa na hasira bali alimpa Amani. Yesu ambaye anatufahamu sisi katika ubinadamu wetu na ambaye anatufahamu undani wetu kabisa, anatupatia sisi amani wakati tukiwa katika hofu na mashaka yetu. Wakati Thomasi anatoa ishara kwa ajili ya ombi lake la kuingia katika hali hiyo ya Imani au kuamini, haombi kitu kigeni zaidi ya ile Imani ambayo kila mfuasi alikuwa ameshapokea. Ni wazi kwamba yeye alitaka kupata naye muda wakushuhudia kama wengine walivyo fanya-kabla haja amini jambo hilo kubwa linalo shangaza.

Lakini tukio haliishi hapa, kwa Yohane au kwa Bwana mfufuka mwenyewe anaendelea na kusema “je, una amini kwasababu umeniona? Wana heri wale wasio ona na kuamini”. Kwetu sisi maneno haya ni ya muhimu sana. Kwasababu hatukuona, sasa inakuwaje tuna amini? Tomasi hakuweza kuamini mpaka alipo ona. Petro hakuweza kaumini mpaka alivyo ona. Maria Magdalena hakuweza kuamini mpaka alivyo ona. Sasa tuta aminije wakati sisi hatujaona? Inawezekana kwasababu sisi tumesha barikiwa, “wamebarikiwa wale wasio ona lakini wana amini.”. Ni lazima tutambue na kukubali kwamba Imani yetu sio kutokana na juhudi zetu wenyewe au labda dini tunayo fuata bali ni “zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu”. Mungu Baba ametupa kitu ambacho kina saidia Imani yetu kwa Bwana mfufuka iwezekane-hata pale ambapo hatuja muona Yesu mfufuka kwa macho yetu ya kibinadamu.

Sala: Bwana, imarisha Imani yangu kama Tomasi alivyolia “Bwana wangu na Mungu wangu”. Yesu nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.