Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
MBEGU NI NENO LA MUNGU
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JANUARI 28, 2026

FAMILIA YA MUNGU!
MASOMO YA MISA, JANUARI 27, 2026
WAJUMBE WA AMANI
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JANUARI 26, 2026
MWANGA KWA WALE WALIO GIZANI!
MASOMO YA MISA, JANUARI 25, 2026
VIPINGAMIZI KATIKA KUMFUATA YESU!
ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Januari
24, 2026
JUMA LA 2 LA MWAKA WA KANISA
KUMBUKUMBU YA MT. FRANSISKO WA SALES
2Sam.
1:1-4, 11-12, 17, 19, 23-27
Zab.
80:1-2, 4-6 (K) 3
Mk
3: 20-21
VIPINGAMIZI
KATIKA KUMFUATA YESU!
Yesu
ni Hekima ya Mungu na ni Mungu. Kila kitu alichofanya na kusema kilifunua
upendo kamili wa Utatu Mtakatifu. Baadhi ya watu walimsikiliza kwa makini na
kwa Imani na utukufu wa mshangao kwa maneno yake na matendo yake. Waliweza
kuona Umungu wake ukingaa na kutambua kweli alikuwa Mwana wa Mungu, mkombozi wa
Ulimwengu. Lakini walikuwepo wengine, hata wengine waliokuwa ndugu zake,
waliodhani “hayupo vizuri kiakili”.
Kama
haya yalisemwa kwa Yesu pamoja na ukamilifu wake, yatasemwa pia kwetu
tunaofuata njia zake. Kumfuata Yesu na kutimiza mapenzi yake sio kila mara
itawapendeza ndugu zetu. Yapo mambo mengi tunayoitwa na Injili kufanya na
kusema, ambayo yatapingwa tu na ndugu au jirani zetu. Wakati haya yanatokea,
tusishangae au kuogopa au kutu umiza. Tusipatwe na hasira wala kukata tamaa.
Bali, tunapaswa kujiona wenyewe tukifuata katika njia za Kristo. Tunapaswa
kufikiria pia kuhusu kusingiziwa kwake kwa uongo na kuhukumiwa kwa uongo na
tusikubali tunayosikia kwa wenzetu yatuweke mbali na kufuata mapenzi ya Mungu.
Sala:
Bwana, ninatambua kuwa ulishindwa kueleweka na ukahukumiwa vibaya na watu
wengine, wengine watu wa wakaribu kabisa. Nisaidie daima niweze kukubali pale
ninaposhindwa kueleweka katika maisha hasa pale ninapo kufuata wewe katika
maisha. Nisaidie nikutafute wewe na kufanya mapenzi yako licha ya vipingamizi
kutoka kwa wengine. Yesu, nakuamini wewe. Amina.
-------------------------
Copyright
© 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JANUARI 24, 2026
MASOMO YA MISA, JANUARI 24, 2026
JUMAMOSI,
JUMA LA 2 LA MWAKA
KUMBUKUMBU YA MT. FRANSISKO WA SALES
SOMO
1
2Sam.
1:1-4, 11-12, 17, 19, 23-27
Ikawa
baada ya kufa kwake Sauli, hapo daudi aliporudi katika kuwaua Waamaleki, naye
Daudi amekaa siku mbili katika Siklagi; hata siku ya tatu ikawa, tazama! Akaja
mtu kutoka kambi ya Sauli, nguo zake zimeraruliwa, tena ana mavumbi kichwani
mwake; basi, ikawa alipomfikia Daudi, akaanguka chini, akamsujudia. Daudi
akamwambia, Umetoka wapi? Akamwambia, Nimeokoka katika kambi ya Israeli. Daudi
akamwambia, Yalikwendaje? Tafadhali uniambie. Akajibu, Watu wamekimbia vitani,
tena watu wengi wameanguka wamekufa; hata Sauli naye na Yonathani, mwanawe,
wamekufa.
Ndipo
Daudi akashika nguo zake akazirarua; na kadhalika watu wote waliokuwa pamoja
naye; wakaomboleza, wakalia, wakafunga hata jioni, kwa ajili ya Sauli, na kwa
ajili ya Yonathani mwanawe, na kwa ajili ya watu wa Bwana, na kwa ajili ya
nyumba ya Israeli; kwa sababu wameanguka kwa upanga.
Basi
Daudi akamwomboleza Sauli, na Yonathani, mwanawe, maombolezo haya,
Walio
fahari yako, Ee Israeli juu ya mahali pako palipoinuka wameuawa; jinsi mashujaa
walivyoanguka. Sauli na Jonathani walipendwa na kupendeza maishani wala mautini
hawakutengwa; walikuwa wepesi kuliko tai.
Walikuwa
hodari kuliko simba. Enyi binti za Israeli, mlilieni Huyo Sauli, ambaye
aliwavika mavazi mekundu kwa anasa, Akazipamba nguo zenu dhahabu. Jinsi
mashujaa walivyoanguka katikati ya vita! Ee Yonathani, wewe umeuawa juu ya
mahali pako palipoinuka! Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu,
ulikuwa ukinipendeza sana; upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, unaopita upendo
wa wanawake. Jinsi mashujaa walivyoanguka wakiwa na silaha za vita
zilivyoangamia!
Neno
la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO
WA KATIKATI
Zab.
80:1-2, 4-6 (K) 3
(K)
Ee Mungu, uangazishe uso wako nasi tutaokoka.
Wewe
uchungaye Israeli, usikie,
Wewe
umwongozaye Yusufu kama kundi.
Wewe
uketiye juu ya Makerubi, utoe nuru.
Mbele
ya Efraimu, na Benyamini, na Manase,
Uziamshe
nguvu zako,
Uje,
utuokoe. (K)
Ee
Bwana, Mungu wa majeshi,
Hata
lini? Utayaghadhibikia maombi ya watu wako?
Umewalisha
mkate wa machozi,
Umewanywesha
machozi kwa kipimo kikuu.
Unatufanya
sababu ya ugomvi kwa jirani zetu,
Na
adui zetu wanacheka wao kwa wao. (K)
SHANGILIO
Mdo.
16:14
Aleluya,
aleluya.
Ufungue
Moyo wetu, ee Bwana, ili tuyatunze maneno ya Mwanao.
Aleluya.
INJILI
Mk.
3:20-21
Yesu
aliingia nyumbani na mkutano wakakusanyika tena, hao wao wenyewe wasiweze hata
kula mkate. Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana
walisema, Amerukwa na akili.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright
© 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.



