Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUSHIKA SHERIA!



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya kila Jumapili
Jumapili, Februari 15, 2026
Dominika ya 6 ya Mwaka A wa Kanisa

YbS 15:16-21;
Zab 118:1-2, 4-5, 17-18, 33-34;
1Kor 2:6-10;
Mt 5:17-37


KUSHIKA SHERIA!


Mungu anatuita sio katika maisha ya maadili tu, lakini katika hali ya kuishi ya juu zaidi. Tunatembea kuelekea ukamilifu kwa kujitahidi daima kuchagua kufanya mazuri. Katika hali ya asili sisi sio wakamilifu, lakini Mungu anatuita tutafakari jinsi tunavyo ishi na kutambua ni kipi kimeenda vibaya na kipi kimeenda vizuri. Kwa kutafakari maisha yetu kwa kupitia njia ya Imani maisha yetu yanakuwa katika hekima. Yesu anatufundisha dini ambayo itatufanya ikuwa ndani yetu na kuwa sehemu ya maisha yetu.

Somo la kwanza linatualika tufanye kila jitihada ya kufanya uchaguzi sahihi katika maisha. Yoshua bin Sira anatangaza kwamba amri za Mungu zina nguvu ya kuokoa. Musa aliwaambia watu alivyokuwa karibu na mto Yordani kwamba anawapa nafasi yakuamua: maisha na mafanikio, kifo na maangamizi. Uchaguzi ulikuwa wao kuamua. Yoshua bin Sira sasa anawaambia watu, akisisitiza ujumbe ule wa Musa kwamba Mungu ameweka mbele yao moto na maji, maisha na kifo, mema na mabaya. Wanatusukuma nasi tufanye uchaguzi sahihi kwa kusema kwamba macho ya Mungu huwaelekea wale wenye kutenda mema. Ni ujumbe mzito kwetu kwamba hatuwezi kufuta mawazo yetu na matendo yetu kutoka kwa Mungu.

Injili ya Mathayo kwa asili iliandikwa kwa ajili ya Wayahudi Wakristu, inaweza kuonekana kama maneno ya kufariji kwao. Mathayo daima amekuwa akirejea Agano la Kale kuwaonesha kuwa maisha ya Yesu hajaja kuvunja sheria za zamani za Wayahudi bali ni mwendelezo wa yote ambayo yalitabiriwa na manabii hapo zamani. Maisha na mafundisho ya Yesu hayapaswi kuonekana kama ni dini mpya, maisha ya Yesu ni maisha ya asili ya habari ya Ukombozi. Anawahakikishia wasomaji wake kwamba Yesu hakuja kutengua Sheria bali amekuja kuikamilisha. Kwa hiyo, sheria bado ina nafasi yake na hivyo haitatupwa mbali hadi pale itakapo timiza jukumu lake. Kwasababu kwa Yesu, maana halisi ya sheria inaweza kufupishwa kwa neno moja “heshima”. Heshima kwa Mungu, kwa jina lake, kwa siku yake, heshima kwa wazazi, heshima kwa uhai, utu, heshima kwa ukweli na heshima kwa jina la mtu na hatimaye heshima kwa nafsi. Kwa maneno mengine sheria yote inahitimishwa kwa ‘heshima kwa Mungu’ na ‘heshima kwa nafsi” na jirani. Kwasababu heshima hii haijalimbikizwa katika visheria vidogo na miiko bali imejibeba katika amri ya mapendo: Upendo kwa Mungu na upendo kwa jirani. Yesu hakutambulisha sheria mpya bali alitambulisha njia mpya yakufikiria na kuelewa sheria. Hakutengua sheria wala kubadili bali alienda mbele zaidi ya kile kinacho hitaji. Kwasababu kwa Yesu, hali ya nje tu ya kushika sheria haitoshi. Kuwa mfuasi wa Yesu ni vizuri kutambua sheria iliojengwa katika mapendo. Kushika sheria bila mapendo ni sawa na kuwa na mwili bila roho. Ndio maana anawaambia wafuasi wake kwamba fadhila zao zisipo zidi zile za Mafarisayo na Waandishi, hawataingia katika Ufalme wa Mungu.

Ili kuwafanya wafuasi wake waelewe mafundisho yake, Yesu aliwapa mifano sita mizito na katika injili ya leo tuna minne, tuna kuhusu: hasira, uasherati, talaka na kiapo. Anasema wazi kwamba haitoshi tu kushika ambacho sheria inatuambia bila kutenda fadhila zinazo ambatana nazo. Kwa Yesu, hakuwezi kuwa na utengano kati ya uhusiano wetu na Mungu na watu. Mkristo anapaswa kumpata Mungu kwa watu wote na katika uumbaji.

Sala: Bwana, nifanye niwe safi moyoni. Nifanye niweze kuwa mtu mwaminifu na mwenye kujali utu. Ninaomba ukweli ulio uweka ndani ya moyo wangu uweze kuwa msingi wa matendo yangu na maneno yangu. Ninaomba niongee nikiwa na dhamiri safi kila wakati nikiongea ulichonipa niongee. Yesu, nakumini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 15, 2026



MASOMO YA MISA, FEBRUARI 15, 2026
DOMINIKA YA 6 YA MWAKA A


WIMBO WA MWANZO:
Zab. 31:2 – 4
Uwe kwangu mwamba wa nguvu, nyumba yenye maboma ya kuniokoa. Ndiwe genge langu na ngome yangu; kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge.



SOMO 1
YbS. 15:15 – 20

Ukipenda utazishika amri zake, na kutenda amini ni shauri lako. Ameweka mbele yako moto na maji; utanyosha mkono wako uchaguavyo. Mbele ya mwanadamu upo uzima na muti, naye atapewa apendavyo. Mradi hekima ya Bwana yatosha, Mkuu mwenye uweza hutazama vyote. Macho yake ni juu yao wamchao, naye atapeleleza kila kazi ya watu. Hakumwamuru mtu yeyote awe asi, wala kumruhusu atende dhambi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 118:1 – 2, 4 – 5, 17 – 18, 33 – 34 (K) 1

(K) Heri waendao katika sheria ya Bwana.

Heri walio kamili njia zao,
Waendao katika sheria ya Bwana.
Heri wazitiio shuhuda zake,
Wamtafutao kwa moyo wote. (K)

Wewe umetuamuru mausia yako,
Ili sisi tuyatii sana.
Ningependa njia zangu ziwe thabiti,
Nizitii amri zako. (K)

Umtendee mtumishi wako ukarimu,
Nipate kuishi, nami italitii neno lako.
Unifumbue macho yangu niyatazame
Maajabu yatokayo katika sheria yako. (K)

Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako,
Nami nitaishika hata mwisho.
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako,
Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote. (K)



SOMO 2
1Kor. 2:6 – 10

Iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika; bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu; lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu).

Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.



SHANGILIO
Yn. 14:6

Aleluya, aleluya.
Mimi ndimi Njia, na Ukweli, na Uzima, asema Bwana; Mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Aleluya.



INJILI
Mt. 5:17:37

Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukata moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

Mwaana nawaaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue; na mtu akiua itampasa hukumu. Bali mimi nawaambieni, kila amwonaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, ukapatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako. Patina na mshitaki wako upesi wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi na kadhi akakupeleka  kwa askari, akatupwa gerezani. Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.
Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee, wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini. Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usizuru, ila mtimizie Bwana nyapo zako; lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji Mfalme mkuu. Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

JE UNA NJAA YA MUNGU?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Februari 14, 2026, 
Juma la 5 la Mwaka wa Kanisa

Kumbukumbu ya Mt. Skolastika Bikira 

1Fal 12:26-32;13:33-34
Zab 106:6-7.19-22
Mk 8: 1-10.


JE UNA NJAA YA MUNGU?


Sehemu ya Injili inaweza kuonekana katika hali mbali mbali inayo funua huruma ya Yesu. Kulikuwa na mkusanyiko mkubwa ulio wahusianisha Wayahudi pia Wayunani, waume na wake pamoja na watoto. Na wote walikuwa na kitu kimoja tu muhimu. Walikuwa na njaa. Walikuwa na njaa ya mafundisho ya Yesu-ni kitu kipi kingine kinacho weza kuwaweka pamoja namna ile kwa siku tatu? Na kwasababu ya njaa yao ya kiroho, walihisi pia njaa ya kimwili. Je, ulishawahi kuwa na njaa ya Mungu? Ulishawahi kuhisi kutaka kuwa na Mungu zaidi ya kutaka kukaa mahali na kupata mambo mengine ya maisha? 

Umati walikuwa wamevutwa sana na Yesu kiasi kwamba walikaa siku tatu wakiwa naye, wakimsikiliza wakiwa katika jangwa pamoja na kwamba hawakuwa na chakula. Walimchagua Yesu zaidi ya chakula na faraja ya nyumbani kwao. Inaonesha ni kwa jinsi ghani walivyokuwa wamevutwa naye. Hakuna kitu kingine kilichokuwa na thamani, walitaka tu wawe na Yesu. Ujumbe huu pia unaonesha jinsi Yesu alivyo onesha kujali watu. Moyo wake ulijazwa na huruma juu yao. Alifurahi pia kwa uwepo wao lakini pia alijali pia kuhusu usalama wao wa mwili hata kuliko wao wenyewe. Yesu, baada ya kutambua tatizo la watu kuwa bila chakula kwa muda mrefu anawaalika pia Mitume wake watambue tatizo hilo. Pengine, Yesu alitaka mitume waweze kuwa na upendo na kujali watu katika mioyo yao. Pengine, ilikuwa ni wakati ambapo alikuwa akiwajaribu na kuwafundisha wawe wakiwaza kuhusu mahitaji ya watu. Yesu alitaka mioyo yao isukumwe na “huruma kwa ule umati” kama yeye alivyokuwa.  

Tuangalie pia leo: je, Yesu ni kiini cha maisha yako? Je, mioyo yetu inasukumwa na tamaa ya kutaka kuwa naye zaidi ya chochote kile? Je, tunatambua jinsi Yesu anavyo tujali? Je tupo tayari kuruhusu upendo na huruma anayo tupa Yesu, kuipeleka kwa wengine pia? Ni kwa jinsi hii tu twaweza kuitwa wafuasi wake.

Sala: Bwana, nisaidie niweze kuvutwa kwako kwa tamaa kubwa kabisa. Nisaidie niweze kukuona wewe kama kiini na chanzo cha yote ninayo tafuta. Ninaomba nikuchague wewe zaidi ya yote, nikikuamini wewe na kufahamu kwamba wewe ndiye utakaye ridhisha hamu ya moyo wangu. Nikiwa navutwa kwako nisaidie moyo wangu ujazwe na huruma nyingi kwa wote. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 14, 2026



MASOMO YA MISA, FEBRUARI 14, 2026
JUMAMOSI YA WIKI YA 5 YA MWAKA

KUMBUKUMBU YA WAT. CYRILI NA METHODIUS


SOMO 1
1Fal. 12:26-32; 13:33-34


Yeroboamu alisema moyoni mwake: Basi ufalme utairudia nyumba ya Daudi. Kama watu hawa wakipanda kwenda kutoa dhabihu katika nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, ndipo mioyo ya watu hawa itamrudia bwana wao, yaani Rehoboamu, mfalme wa Yuda; nao wataniua mimi, na kumrudia Rehoboamu, mfalme wa Yuda.

Kwa hiyo mfalme akafanya shauri, akafanyiza ng’ombe wawili wa dhahabu, akawaambia watu, Ni vigumu kwenu kupanda kwenda Yerusalemu; tazama, hii ndiyo miungu yenu, enyi Israeli, iliyowapandisha kutoka nchi ya Misri. Akamweka mmoja katika Betheli, na wa pili akamweka katika Dani. Jambo hili likawa dhambi, maana watu walikwenda kuabudu mbele ya kila mmoja, hata huko Dani. Tena akafanya nyumba za mahali pa juu, akafanya na watu wowote, watu wasio wa wana wa Lawi, kuwa makuhani.

Yeroboamu akaamuru kushika sikukuu katika mwezi wa nane, siku ya kumi na tano ya mwezi, mfano wa sikukuu iliyokuwa katika Yuda, akapanda juu ili kuiendea madhabahu. Akafanya vivyo katiak Betheli akiwatolea dhabihu wale ng’ombe aliowafanya; akawaweka katika Betheli wale makuhani wa mahali pa juu alipokuwa amepafanya.

Baada ya hayo Yeroboamu hakuiacha njia yake mbovu, lakini akafanya tena makuhani wa mahali pa juu, wa watu wowote. Kila aliyetaka akamfanya wakfu, ili wawepo makuhani wa mahali pa juu. Jambo hilo likawa dhambi kwa nyumba ya Yeroboamu, hata kuiharibu, na kuifuta usoni pa nchi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 106:6-7, 19-22 (K) 4


(K) Ee Bwana, unikumbuke mimi, kwa kibali uliyonayo kwa watu wako.


Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu,
Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.
Baba zetu katika Misri
Hawakufikiri matendo yako ya ajabu. (K)


Walifanya ndama huko Horebu,
Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.
Wakaubadili utukufu wao
Kuwa mfano wa ng’ombe mla majani. (K)


Wakamsahau Mungu mwokozi wao,
Aliyetenda makuu katika Misri:
Matendo makuu katika nchi ya Hamu,
Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu. (K)



SHANGILIO
Mt. 4:4


Aleluya, aleluya,
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
Aleluya.



INJILI
Mk. 8:1 – 10


Katika siku zile, kwa vile ulivyokuwa mkuu tena ule mkutano, nao wamekosa kitu cha kula, Yesu aliwaita wanafunzi wake, akawaambia, Nawahurumia mkutano kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami, wala hawana kitu cha kula; nami nikiwaaga waende zao nyumbani kwao hali wanafunga, watazimia njiani; na baadhi yao wametoka mbali. Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani? Akawauliza, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba.

Akawaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wake waaandikie; wakawaaandikia mkutano. Walikuwa na visamaki vichache; akavibariki, akasema wawaandikie na hivyo pia. Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba. Na watu waliokula wapata elfu nne. Akawaaga. Mara akapanda chomboni pamoja na wanafunzi wake, akaenda pande za Dalmanutha.


Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

EPHATHA, FUNGUKA!



“ASALI ITOKAYO MWAMABANI”
Februari 13, 2026, Ijumaa

JUMA LA 5 LA MWAKA 

1Fal 11:29-32;12:19
Zab 81:9-14
Mk 7: 31-37.


EPHATHA, FUNGUKA!

“Funguka!” haya ni maneno mazito katika kitendo cha kuamuru. Yapo wazi na ni ya mwisho. “Funguka” sio swali wala sio mwaliko, ni amri. Neno hili lina dhihirisha kwamba Yesu ameamua sasa kutenda. Linaeleza kwamba hana wasi wasi katika kuamua kwake na kutenda. Ameamua sasa kutimiza na anongea mapenzi yake. Na kwa kitendo hiki, kwa upande wake, ndicho kinacho onesha tofauti. Neno hili anavyo liongea linaonesha kwamba Mungu hana wasi wasi anavyo ongea. Kama yeye anaiongoza dunia (kusikia kwa kawaida), ni wazi na dhahiri kwamba anaongoza pia ulimwengu wa kiroho. Anauwezo wakufanya yote yawe mazuri. 

Huyu kiziwi hakuweza kuomba msaada, kwasababu hakusikia neno la kuongea. Hakuna aliye elewa alichosema. Lakini watu wenye huruma walimuonea huruma wakamleta kwa Yesu.Yesu anamchukua pembeni kutoka kwenye umati, na anamgusa kwa kidole chake machoni, masikioni na kwenye ulimi, na anasema “efata” (funguka) na masikio yake yanafunguka, ulimi na macho pia. Yesu alitaka kumuonesha huyu kiziwi jinsi alivyomjali na furaha ya huyu aliyeponywa inapaswa imfanye aweze kutenda mema na kuepuka kufanya mabaya kwa masikio yake na ulimi wake. Kwa namna ya pekee, huyu mtu anapaswa kufungua masikio yake kusikiliza neno la Mungu, na kutumia ulimi wake kutangaza huruma ya Bwana.
Tutafakari juu ya neno hilo la Yesu. Tunaomba mamlaka haya matakatifu na ya Kimungu ya Yesu yaongoze maisha yetu. Tunamuomba yeye atuamuru sisi. Tuweze ‘funguka’ leo. Ili tuweze kutumia masikio yetu kusikiliza neno lake na kutumia ulimi wetu kutangaza neno na kuimba sifa zake, kuwa na adabu ya macho pia, kutazama mambo mema na kuacha kutazama yanayo haribu moyo. 

Sala: Bwana, ninakuamini wewe na nina amini unaweza kufanya mambo yote. Ninatambua unapenda kuwa na mamlaka kamili ya maisha yangu. Nisaidie niweze kurudisha maisha yangu kwako na kukuamini wewe unayetosha kuongoza na kuelekeza kila kitendo cha maisha yangu. Yesu, nakuamini wewe kabisa. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 13, 2026


MASOMO YA MISA, FEBRUARI 13, 2026
IJUMAA YA WIKI YA 5 YA MWAKA


SOMO 1
1Fal. 11:29-32; 12:19

Ikawa zamani zile Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya, Mshiloni, alikutana naye njiani; naye Ahiya amevaa vazi jipya, na hao wawili walikuwa peke yao mashambani. Ahiya akalishika lile vazi jipya alilokuwa amelivaa, akalirarua vipande kumi na viwili. Akamwmbia Yeroboamu, Twaa wewe vipande kumi, maana Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nitaurarua ufalme, na kuuondoa katika mkono wa Sulemani, nami nitakupa wewe kabila kumi; lakini yeye atakuwa na kabila moja kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalemu, mji ule niliouchagua katika miji yote ya kabila za Israeli. Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi hata leo.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 81:9-14 (K) 10, 8

(K) Mimi ndimi Bwana Mungu wako: Isikieni sauti yangu.

Usiwe na mungu mgeni ndani yako
Wala usimsujudie mungu mwingine.
Mimi ndimi Bwana Mungu wako
Niliyekupandisha toka nchi ya Misri. (K)

Watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,
Wala Israeli hawakunitaka. 
Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,
Waenende katika mashauri yao. (K)

Laiti watu wangu wangenisikiliza,
Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Ningewadhili adui zao kwa upesi,
Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu. (K)


SHANGILIO
Mdo. 16:14

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana ufungue moyo wetu, ili tuyatunze maneno ya Mwanao.
Aleluya.


INJILI
Mk. 7:31 – 37

Yesu alitoka katika mipaka ya Tiro, akapita katikati ya Sidoni, akaenda mpaka bahari ya Galilaya, kati ya mipaka ya Dekapoli. Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi, wakamsihi amwekee mikono. Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi, akataama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri. Akawaonya wasimwambie mtu; lakini kadiri ya alivyozidi kuwaagiza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari; wakashangaa mno kupita kiasi, wakinena, Ametenda mambo yote vema; viziwi awafanya wasikie, na bubu waseme.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUDHIHIRISHA IMANI!




 “ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Februari 12, 2026,
Juma la 5 la Mwaka wa Kanisa
 
1 Fal 11:4-13;
Zab 106:3-4, 35-37, 40;
Mk 7: 24-30.
 

KUDHIHIRISHA IMANI!

 
Ndugu wapendwa, karibuni kwa adhimisho la Misa Takatifu asubuhi ya leo. Leo katika wimbo wetu wa katikati tunakutana na Zaburi isemayo: heri kila mtu amchaye Bwana, hakika huyu amebarikiwa. Huyu atakuwa na uzao uliobarikiwa, na hakika atabarikiwa zaidi na Bwana. Kumcha Mungu ndio chanzo cha Mwanadamu kubarikiwa.

Tunaona kwamba zaburi hii inatumika leo kusisitizia kile kinachoelezwa katika somo la kwanza ambapo tunakutana na mwanadamu anaumbwa katika hali ya unyenyekevu, hana hata nguo ya kuvaa-lakini wanadamu hawa wangejibariki kwa kumcha Bwana, kumcha Bwana ndiko kutakakowawezesha kukabiliana na kila aina ya changamoto. Kumcha Bwana ndiyo iliyopaswa kuwa rasilimali yao kuu. Tunatambua katika Biblia kwamba pale walipokataa kumcha Bwana, hakika walianguka vibaya. Sisi tusiache kumcha Bwana, tutambue kwamba tumeumbwa ili tumche Bwana, huu ndio wajibu wetu wa kwanza. Hivyo lazima kumcha Bwana kila siku.

Tuibariki siku yetu kila siku. Tukikataa kumcha Bwana, ndipo tutakapoanguka. Wengi tupo katika maisha ya duni kwa sababu ya kukataa kumcha Mwenyezi Mungu.

Katika somo la injili, Yesu anamjibu kwa ukali mama ya kutoka Tiro na Sidoni. Jibu hili halijajaa ukatili kama tukilichunguza vizuri-Yesu alitaka kuitambua imani yake, hii ni kwa sababu mama huyu alikua amezoea imani ya mazingaumbwe, maajabu yaliyofanywa na baadhi ya wanamazingaumbwe katika nchi yake ya Kiyunani. Hivyo kuna hatari kwamba angaliishia kumuona Yesu kama miongoni mwa wanamazingaumbwe, na ndio sababu za Yesu kumjibu kwa ukali namna hii ili kumpatia ujumbe kwamba miujiza yake ipokelewe kiimani na si waichukulie kama mazingaumbwe.

Mama huyu alikuwa na imani, na jibu lake laonesha unyenyekevu, na pia alielewa kwamba miujiza ya Yesu ni kwa ajili ya watu wenye imani na si kwa ajili ya wale wanaomuona Yesu kuwa kama wanamazingaumbwe.

Sisi tuwe watu wa imani ndugu zangu. tutambue kwamba huwezi kutendewa muujiza na Yesu kama huna imani, sisi tuwe watu wa imani. Tusije mbele ya Yesu tukiwa katika hali ya kutokujiandaa, lazima tujiandae kila siku. Tumuache Yesu atende mwenyewe. Tumsifu Yesu Kristo.
  
-------------------------
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 12, 2026


 
MASOMO YA MISA, FEBRUARI 12, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 5 LA MWAKA
 

SOMO 1
1Fal 11:4-13

Mfalme Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni. Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni. Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu. Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili, akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana. Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako. Walakini katika siku zako sitafanya haya, kwa ajili ya Daudi baba yako; nitaurarua utoke katika mkono wa mwana wako. Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 106:3-4, 35-37, 40

(K) Ee Bwana utukumbuke kwa kibali uliyonayo kwa watu wako.

Heri washikao hukumu, Na kutenda haki sikuzote.
Ee Bwana, unikumbuke mimi,
Kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako.
Unijilie kwa wokovu wako,

Bali walijichanganya na mataifa,
Wakajifunza matendo yao.
Wakazitumikia sanamu zao,
Nazo zikawa mtego kwao.

Naam, walitoa wana wao na binti zao 
Kuwa dhabihu kwa mashetani.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya watu wake,
Akauchukia urithi wake.
 

SHANGILIO
Zab. 119:135
 
Aleluya, aleluya,
Umwangazie mtumishi wako uso wako, na kunifundisha amri zako.
Aleluya.
 

INJILI
Mk. 7:24 – 30
 
Yesu aliondoka Nazareti akaenda zake hata mipaka ya Tiro na Sidoni. Akaingia katika nyumba, akataka isijulikane na mtu; lakini hakuweza kusitirika. Ili mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo mchafu, alisikia habari zake, akaja akamwangukia miguuni pake. Na yule mwanamke ni Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake. Akamwambia, Waache watoto washibe kwanza; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto, na kuwatupia mbwa. Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto. Akamwambia, Kwa sababu ya neno hilo, enenda zako; pepo amemtoka binti yako. Akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule pepo amekwisha kumtoka.
 
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
 
-------------------------
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

NDANI NA NJE!



ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Februari 11, 2026

JUMA LA 5 LA MWAKA 

1 Fal 10:1-10,
Zab 37:5-6,30-31,39-40
Mk 7: 14-23


NDANI NA NJE!


Kile kinacho mtoka mtu kutoka ndani ndicho kinacho mfanya mtu huyo Mtakatifu! Mara nyingi, tunashugulika sana na vitu vilivyopo nje kuliko vile vya ndani. Tunaogopa sana na kuwa na hofu nyingi wenzetu wanasema nini juu yetu, jinsi ninavyo onekana, na muonekano wangu mbele za watu na ulimwengu. Injili ya leo inaelezea swala la Mafarisayo kuhusu kula chakula kinacho mtia mtu najisi. Lakini Yesu kwa upande mwingine anaongelea kuelekea mioyo yetu. Ni kitu ghani kilichopo mioyoni mwetu? Hiki ndicho kinacho tufanya jinsi tulivyo. 

Yesu anataka kutuelekeza kuhusu kushika sheria ya Mungu katika hali ya utakatifu. Anaelezea kuhusu namna ya Mafarisayo kuhusu hofu yao ya jinsi wanavyo onekana mbele ya watu. Muonekano wao wa njee wa jinsi ya kushika sheria inaonekana jinsi ghani walivyo na wasi wasi juu ya jinsi watu wanavyo waona na jinsi wanavyo onekana machoni pao. Wanataka kuonekana watakatifu machoni pao. Lakini huo ni muonekano tuu wa nje sio ukweli halisi. Kwasababu hii Yesu anawasisitizia juu ya mambo ya ndani ya moyo. Hata kama watu hawataona lakini Mungu anaona yote. Kile kilichopo ndani ya mioyo yetu kinaweza kuleta uharibifu mkubwa au kikatujenga sana na kuleta mambo mazuri. Kuna kitu kimoja tu ambacho ni muhimu. Mungu ananifikiria je? Au Mungu ananiona je? 

Tutafakari leo, juu ya kile ambacho kipo ndani ya mioyo yetu. Kwanini tunafanya tunacho fanya na kwanini tuna amua kama tulivyo amua? Je, ni uchaguzi unaotoka katika moyo ulio mwaminifu? Au je, ni uchaguzi uliojikita juu ya jinsi nitakavyo onekana? Tujichunguze kama misukumo yetu inatoka katika moyo ambao umejiunga ndani na mwaminifu kama ule wa Kristo. 

Sala: Bwana, fanya misukumo yangu iwe mitakatifu. Nisaidie niweze kutambua kuwa utakatifu unapatikana katika kukutumikia wewe na sio katika kutafuta sifa binafsi na kujitumikia. Ninakupenda Bwana wangu. Yesu, ninakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 11, 2026



MASOMO YA MISA, FEBRUARI 11, 2026
JUMATANO YA WIKI YA 5 YA MWAKA

KUMBUKUMBU YA BIKIRA MARIA WA LOURDES

SOMO 1
1Fal. 10:1-10

Malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la Bwana, alikuja ili amjaribu kwa maswali ya fumbo. Akaingia Yerusalemu na wafuasi wengi sana, na ngamia wachukuao manukato, na dhahabu nyingi sana, na vito vya thamani; alipomfikilia Sulemani, akazungumza naye mambo yote aliyokuwa nayo moyoni. Naye Sulemani akamfumbulia maswali yake yote; wala hakukuwa na neno alilofichiwa mfalme asimwambie.

Naye malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani, na nyumba aliyokuwa ameijenga na chakula cha mezani pake, na watumishi wake walivyokaa, na kusimamia kwao wangoje wake, na mavazi yao, na wanyweshaji wake, na daraja yake ya kupandia mpaka nyumba ya Bwana, roho yake ilizimia. Akamwambia mfalme, Ndizo kweli habari zile nilizozisikia katika nchi yangu za mambo yako na za hekima yako. Lakini mimi sikuzisadiki habari hizo, hata nilipokuja na kuona kwa macho yangu; tena, tazama, sikuambiwa nusu; wewe umezidi kwa hakima na kufanikiwa kuliko habari nilizozisikia. Heri watu wako, na heri watumishi hawa wako, wasimamao mbele yako sikuzote, wakisikia hekima yako. Na ahimidiwe Bwana, Mungu wako, aliyependezwa naye, ili akuweke juu ya kiti cha enzi cha Israeli; kwa kuwa Bwana amewapenda Israeli milele, kwa hiyo amkufanya kuwa mfalme, ufanye hukumu na haki.

Basi akampa mfalme talanta za dhahabu mia na ishirini, na manukato mengi, mengi sana, na vito vya thamani; wala haukuja tena wingi wa manukato, kama hayo malkia wa Sheba aliyompa mfalme Sulemani.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 37:5-6, 30-31, 39-40 (K) 30

(K) Kinywa cha mwenye haki hunena hekima.

Umkabidhi Bwana njia yako,
Pia umtumaini naye atafanya.
Akaitokeza haki yako kama nuru,
Na hukumu yako kama adhuhuri. (K)

Kinywa cha mwenye haki hunena hekima,
Na ulimi wake husema hukumu.
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake,
Hatua zake hazitelezi. (K)

Wokovu wa wenye haki una Bwana,
Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.
Naye Bwana huwasaidia na kuwaopoa,
Huwaopoa wasio haki na kuwaokoa,
Kwa kuwa wamemtumaini Yeye. (K)


SHANGILIO
Yn. 17:17

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, neno lako ndiyo kweli, uwatakase kwa hiyo kweli.
Aleluya.


INJILI
Mk. 7:14 – 23

Yesu aliwaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu. Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu. Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.

Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano. Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi; kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote. Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.