Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUJAA NEEMAA: NI KUISHI KATIKA KILE MUNGU ALICHOKUPA!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Aprili 16, 2026
Juma la 2 la Pasaka

Mdo 5:27-33
Zab 33: 2, 9, 17-20
Yn 3:31-36


KUJAA NEEMAA: NI KUISHI KATIKA KILE MUNGU ALICHOKUPA!


Wakati lipo tokea janga linalotokana na asili, au vita vya kisiasa, na chakula ni vigumu kupata, watu hushikilia na kupangilia kile walicho nacho. Na wasipofanya hivyo wanaona wanaweza kukosa chakula na kufa kwa njaa. Hivi kama Roho Mtakatifu ange tuambiae “nitawasaidia kwa kiwango fulani tu. Na kama ukimaliza neema zako, basi utajitambua mwenyewe” Mmm!

Kwa neema kwetu, Mungu hutenda tofauti kabisa na sisi. Anatupatia na kutumiminia Roho Mtakatifu katika hali yote na kutupatia neema zote tunazo hitaji. Shida ni kwamba hatuzitumii zote, na badala yake tuna acha kuzitumia. Hii si kwamba hatumwamini Mungu ni mkarimu. Bali ni kwasababu tunaogopa kumruhusu Mungu amimine nguvu zake katika maisha yetu.

Tujaribu kufikiria hivi maisha yangu yatafananaje nitakapo mruhusu Mungu afanye chochote anachopenda katika maisha yangu. Hivi, maisha yetu ya kila siku yangekuwaje, mahusiano yetu, maneno yetu na wakati wetu ujao hautakuwa tofauti? Tunatambua kuwa ni haki kumkumbatia Mungu katika kila kitu. Lakini inapofikia sasa ni wakati wa kukitenda, tunakuwa na wasi wasi mwingi. Inaweza kuwa ni wasi wasi wakitu kisicho julikana. Au kunaweza kuwa hatutaki kubadilika. Vyovyote inavyoweza kuwa Mungu anatupa neema zake zisizo pimika kwa kutumiminia Roho wake. Ni juu yako kuchagua kuamua kumsikiliza na kumchagua au unajipimia na kuchagua mambo mengine. Kumchagua Mungu ni jambo kubwa kuliko kitu chohcote unacho weza kufanya katika maisha yako.

Sala: Bwana, ninataka wewe ufanye chochote unachopenda katika maisha yangu. Ninataka niingie kabisa ndani ya neema zako. Nisaidie niweze kusema “ndio” kwako bila kujali chochote kwa utukufu wa kusema “ndio” uliyo niitia. Yesu nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 16, 2026

 


MASOMO YA MISA, APRILI 16, 2026

IJUMAA, JUMA LA 2 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo 5:27-33

Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti. Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio. Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua.

Neno la Bwana… Tumshukuru Bwana.



WIMBO WA KATIKATI
Zab 34:1, 8, 15-19

(K)Maskini huyu aliita, Bwana akasikia.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumaini. (K)

Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,
Na masikio yake hukielekea kilio chao.
Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya,
Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Walilia, naye Bwana akasikia,
Akawaponya na taabu zao zote(K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa.
Mateso ya mwenye haki ni mengi,
Lakini Bwana humponya nayo yote(K)



SHANGILIO
Yn. 20:29

Aleluya, aleluya,
Umesadiki, Toma, kwa kuwa umeniona, wa heri wale wasioona, wakasadiki. Aleluya



INJILI
Yn 3:31-36

Yeye ajaye kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote. Yale aliyoyaona na kuyasikia ndiyo anayoyashuhudia, wala hakuna anayeukubali ushuhuda wake. Yeye aliyeukubali ushuhuda wake ametia muhuri ya kwamba Mungu ni kweli. Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo. Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake. Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 15, 2026



MASOMO YA MISA, APRILI 15, 2026
JUMATANO, JUMA LA 2 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo 5:17-26

Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza; lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu. Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete. Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari, wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani. Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo. Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu. Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab 34:1-8

(K) Maskini huyu aliita, Bwana akasikia.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,
Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. (K)

Mtukuzeni Bwana pamoja nami,
Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Nalimtafuta Bwana akanijibu,
Akaniponya na hofu zangu zote. (K)

Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,
Wala nyuso zao hazitaona haya.
Maskini huyu aliita, Bwana akasikia,
Akamwokoa na taabu zake zote. (K)

Malaika wa Bwana hufanya kituo,
Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumaini. (K)



SHANGILIO
Rum. 6:9

Aleluya, aleluya,
Kristo akiisha kufufuka, katika wafu hafi tena. Mauti haimtawali tena.
Aleluya.



INJILI
Yn 3:16-21

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika Mungu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUVUTWA KWENYE MWANGA!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Aprili 15, 2026
Juma la 2 la Pasaka

Mdo 5:17-26
Zab 34:2-9
Yn 3:16-21


KUVUTWA KWENYE MWANGA!


Mungu Baba amemtuma Mwanae aje ulimwenguni kuwa mwanga wetu wote. Yeye ni Mwanga ambao unaondoa giza lote. Lakini Injili inasema kwamba “watu wamependa giza zaidi ya mwanga”. Wamechagua dhambi zao zaidi kuliko uhuru wa kutoka kwenye dhambi. Tv au magazeti huvutia watu zaidi wanapotoa habari za udhaifu wa watu, na watu hukimbilia hizi kwasababu ndicho chenye maana kwao. Kwasababu tunavutwa zaidi kupenda kusikia mambo ya giza kuliko ya mwanga.

Ni wazi kwamba sio kwa kila mtu. Walio wengi hawapendezwi na giza la ulimwengu pia na mambo ya kudhalilisha wengine. Lakini ukweli ni kwamba giza lipo mbele na tunapaswa kuwa makini kwasababu ya hali yetu yakuweza kuanguka. Tunapenda kwenda kwenye matope na kudhani tuna furaha.

Pasaka ni kipindi cha kuchunguza tunavutwa na nini zaidi. Je, tunajiruhusu sisi wenyewe kuvutwa kwenye mwanga? Je, tunavutwa na hali mbali mbali ambazo Mungu yupo karibu yetu hapa duniani? Lakini upo mvuto wa kutopenda mpangilio, nakuvutwa kwenye dhambi, mapambano ya ndani ambayo kila mtu yanamkuta. Pasaka ni kipindi cha kuwa makini na haya, kuya chunguza na kuyaona na kuamua kumchagua Yesu, kuanza kujenga maisha yetu ya fadhila kwa kuiga fadhila za maisha ya Yesu.

Kama wafuasi wa Yesu tunaitwa kuelekeza macho yetu kwake pekee. Tunapaswa kupenya giza kwa Imani na kuacha mambo yetu yavutwe kwa Yesu Kristo. Tujikite kwenye Mwanga katika kipindi hiki cha Pasaka. Tuache mwanga huu uongoze maisha yetu.

Sala: Nisaidie mimi niweze kuishi kwenye mwanga. Nisaidie niweze kuelekeza macho yangu kuelekea kwenye utukufu wa ufufuko wako. Ninaomba furaha hiyo iweze kuondoa uharibifu wa mabaya ndani mwangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUZALIWA UPYA!

 


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Aprili 14, 2026
Juma la 2 la Pasaka

Mdo 4: 32-37 
Zab 92: 1-2, 5 
Yn 3: 7-15


KUZALIWA UPYA!


Sehemu ya Injili ya leo inafunga kwa kuonesha Yesu akijilinganisha mwenyewe na yule nyoka wa shaba katika jangwa la Sinai (Hes 21:9). Wayahudi wale wote walionyanyua macho yao na kumtazama yule nyoka wa shaba waliponywa na madonda na maumivu wa wale nyoka wa moto. Sisi ambao tunatazama kwa Imani kwa Yesu tunapaswa kupata maisha mapya sasa. Kama vile Kristo alivyoteseka na kuingia katika utukufu hata wafuasi wake pia watapatwa na hayo hayo. Hakuna njia nyingine. Maisha ya Mkristo yanabeba mateso, yananabeba pia kufa kinafsi lakini macho yote ambayo yamekazwa kwa Yesu yanaondoa mashaka yote.

Leo pia katika somo la kwanza tunaona pia jumuiya ya kwanza wakiamua kuchagua kuishi pamoja maisha ya ufukara uliojaa upendo wa ajabu. Walikubali hata kuvunja ile hali ya kuwa na mali binafsi na kuamua kuwa na vitu vyote katika umoja. Hali hii liliwezekana kwasababu waliungana kwa moyo mmoja na roho mmoja katika Kristo ambaye wote walimwamini na kumuishi katika maisha yao. Wakristo wasasa sio wote waliotayari kutoa mali zao kwasababu ya Kristo, kanisa halimlazimishi mtu kufanya hivyo ila ni lazima mtu aguswe mwenyewe kutoka moyoni. Lakini kilicho cha muhimu kabisa ni kuhakikisha parokia zetu na nyumba zetu za kitawa pia zinabaki katika moyo mmoja na roho mmoja katika Kristo. Kujitoa kwa hali zote na kukamilishana na kuleta furaha katika jumuiya yetu ya kuabudu pamoja. Inapendeza kabisa kuona kama Parokia inakuwa na hii hali ya moyo mmoja na roho moja katika Kristo.

Wengi wetu tunamfahamu Mungu kwa njia ya pilli. Tunamfahamu Mungu kwa yale ambayo tumeambiwa na wengine au yale ambayo tumesoma kutoka katika vitabu, nk. Moyo mmoja na Roho moja katika Kristo inakuja kwa kuona upendo wa Yesu aliokufa na kufufuka kwa jili yetu. Tunaona upendo huu kwa kukubali kuzaliwa upya katika maisha mapya. Ni kwa njia ya kujikita katika huo upendo wa Mungu unaobadilisha na kuwa wapya. Tunamuomba Mungu tuzaliwe upya kwa maisha mapya na kubaki katika upendo wa Kristo.

Sala: Njoo, Roho Mtakatifu na utufanye upya. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 14, 2026




MASOMO YA MISA, APRILI 14, 2026
JUMA LA PILI LA PASAKA, JUMANNE

SOMO 1
Mdo 4:32-37

Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote. Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa, wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji. Na Yusufu, aliyeitwa na mitume Barnaba, (maana yake, Mwana wa faraja), Mlawi, asili yake ni mtu wa Kipro, alikuwa na shamba akaliuza, akaileta fedha, akaiweka miguuni pa mitume.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 93:1-2, 5

(K)Bwana ametamalaki, amejivika adhama.

Bwana ametamalaki, amejivika adhama, 
Bwana amejivika, na kujikaza nguvu. (K)

Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike; 
Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; 
Wewe ndiwe uliye tangu milele. (K)

Shuhuda zako ni amini sana; 
Utakatifu ndio uifaao nyumba yako, 
Ee Bwana, milele na milele. (K)


SHANGILIO
Yn. 10:14

Aleluya, aleluya,
Bwana asema: mimi ndimi mchungaji mwema; Nao walio wangu nawajua, nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.


INJILI
Yn 3:7-15

Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho. Nikodemo akajibu, akamwambia, Yawezaje kuwa mambo haya? Yesu akajibu, akamwambia, Je! Wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu? Amin, amin, nakuambia kwamba, Lile tulijualo twalinena, na lile tuliloliona twalishuhudia; wala ushuhuda wetu hamwukubali. Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni? Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu. Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa; ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUZALIWA MARA YA PILI KWA MAJI NA KWA ROHO




“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Aprili 13, 2026 
JUMA LA PILI LA PASAKA

Mdo. 4:23-31
Zab. 2:1-9 (K) 13
Yn. 3:1-8

KUZALIWA MARA YA PILI KWA MAJI NA KWA ROHO

Ndugu zangu karibuni kwa adhimisho la Misa Takatifu asubuhi hii ya leo. Sasa tumemaliza octava ya pasaka na habari tulizokuwa tunazisikia katika octava hii hasa katika injili zilihusu ufufuko, asubuhi ile jinsi Yesu alivyofufuka na kuiletea dunia furaha. Hivyo kila siku kwenye ile octava katika injili tulisikia habari ya Yesu kufufuka, asubuhi ile siku ya kwanza ya juma. Sasa, hiki kipindi kingine cha pasaka, tunaanza kusikia zaidi maana ya ufufuko na umuhimu wake na namna tuwezavyoshiriki katika ufufuko.

Hivyo, injili zitakazokuwa zinatumika zitatoka sehemu mbalimbali, sio lazima ziwe juu ya ile siku ambapo yesu alifufuka. Mfano, katika injili ya leo, tunakutana na mazungumzo kati ya Yesu na Nikodemus na Yesu anamwambia Nikodemo kwamba ili mtu kuurithi ufalme wa mbinguni, yabidi kuzaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho-yaani yabidi kubatizwa, kumpokea Kristo na Roho mtakatifu atakayekufanya kuwa kiumbe kipya na kukufikisha mbinguni. Kwa namna nyingine, Yesu anamweleza Nikodemo kwamba yeyote anayetaka kwenda mbinguni, ni lazima akubali kuifia dhambi na kuiacha katika kaburi kama Yesu alivyofanya ili aweze kufufuka pamoja na Yesu na kuwa kiumbe kipya. Huo ndio ufufuko Yesu anaotueleza leo.

Katika somo la kwanza, tunaona kwamba wanafunzi wa Yesu walikuwa wanapigana ili watu waupate ufufuko huu, ili watu waache dhambi na kukubali kubatizwa na kumpokea Kristo. Huu ndio ufufuko ambao hata Yesu anamweleza Nikodemo. Mitume tunaowasikia katika somo la kwanza walipambana kweli kweli kuhakikisha kwamba wanahubiri, wanaambia watu waache dhambi na kumpokea Kristo na kubatizwa na kuwa viumbe vipya. Walitetea ufufuko huu hadi wakakubali kupelekwa gerezani ambako walichapwa na leo wanafunguliwa na wanapokutana na wakristo wenzao, wanamuomba Mungu aendelee kuwapa nguvu ya kufundisha ufufuko huu. Wanamuomba pia Mungu awape nguvu ya kutenda miujiza ili watu wapate kuamini na kumpokea zaidi Kristo na kweli walijitahidi na kufanikiwa sana katika hili.

Katika hili tunalokubwa la kujifunza ndugu zangu. Sisi lazima tukubali kuwa wahubiri wa ufufuko wa Bwana, yaani tuwaambie watu waache dhambi na kumpokea Kristo. Kwa kweli duniani tunavumiliana sana na kuruhusu dhambi zitendeke tena mbele ya macho yetu. mfano: unakuta mimi natambua kwamba mfanyabiashara wa maziwa huongeza maji katika maziwa yake ili apate faida awauziapo watu. Lakini mimi nakaa kimya na kuruhusu watoto wanaonunuliwa yale maziwa wanywe maji tu na kupatwa utapia mlo, ninapaswa kumwambia huyu mfanyabishara rafiki yangu kwamba acha tabia hizi, tusijidai kulindana lindana.

Au unakuta kwamba nafahamu kabisa mtu fulani duka lake yeye ananunua bidhaa za magendo zilizofeki na kuja kuwauzia watu. Mimi nakaa kimya, mwisho wa siku watu wanauziwa simu feki, vifaa vya umeme feki na betri feki. Au mimi katika duka langu najua kabisa bidhaa ninayomuuzia huyu mtu ni feki lakini nakaa tu kimya. Jamani hapa duniani tuoneane huruma, tulindane, tusikubali wengine wadhulumiwe au kupatwa na shida. Namna hii ndiyo tuwezayo kusema kwamba hakika tunaishi ufufuko tulioletewa na Kristo. Tumsifu Yesu Kristo.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com


MASOMO YA MISA, APRILI 13 2026





MASOMO YA MISA, APRILI 13, 2026
JUMA LA PILI LA PASAKA, JUMATATU


SOMO 1
Mdo. 4:23-31

Walipofunguliwa, Petro na Yohane wakaenda kwa watu wao, wakawapasha habari ya mambo yote waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee. Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako.

Mbona mataifa wamefanya ghasia, na makabila wametafakari ubatili? Wafalme wa dunia wamejipanga, na wakuu wamefanya shauri pamoja juu ya Bwana na juu ya Kristo wake.

Maana ni kweli, Herode na Pontio Plato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambyo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 2:1-9 (K) 13

(K) Heri wale wanaomkimbilia Mungu. au Aleluya.

Mbona mataifa wanafanya ghasia,
Na makabila wanatafakari ubatili?
Wafalme wa dunia wanajipanga,
Na wakuu wanafanya shauri pamoja,
Juu ya Bwana, Na juu ya masihi wake,
Na tuvipasue vifungo vyao,
Na kuzitupia mbali nasi Kamba zao. (K)

Yeye aketiye mbinguni anacheka,
Bwana anawafanyia dhihaka.
Ndipo atakaposema nao kwa hasira yake,
Na kuwafadhaisha kwa ghadhabu yake.
Nami nimemweka mfalme wangu,
Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu. (K)

Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia,
Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.
Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako,
Na miisho ya dunia kuwa milki yako.
Utawaponda kwa fimbo ya chuma,
Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi. (K)



SHANGILIO
Lk 24:25-26

Aleluya, aleluya,
Ilimpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake.
Aleluya.



INJILI
Yn. 3:1-8

Palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi. Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.

Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

HURUMA YA MUNGU: MSAMAHA WA DHAMBI



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakri ya Pasaka
Aprili 12, 2026 
------------------------------------------------
JUMAPILI, DOMINIKA YA 2 YA PASAKA, JUMAPILI YA HURUMA YA MUNGU. 
------------------------------------------------

HURUMA YA MUNGU: MSAMAHA WA DHAMBI

Leo ni siku ya nane naya mwisho katika oktava ya Pasaka. Na siku ya leo tunaadhimisha Jumapili ya huruma ya Mungu. Ni siku ambayo geti la huruma ya Mungu hufunguliwa kwetu na Mungu kutukirimu huruma yake hata zaidi ya jinsi ambavyo tunaweza kudhani au kutumaini. Leo tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu isiyo na mipaka. Injili ya leo inaonesha mamlaka ya Yesu yakuwapa mitume Roho Mtakatifu ambaye ndiye atakaye wasamehe watu dhambi zao. Yesu Mfufuka anakuwa hai tena kati ya wafuasi wake. Anafungua miyo yao na kuitia shauku na kuwafungulia maandiko, na kuumega mkate. Anafungua macho yao na kujidhihirisha kwao. 

Sehemu ya kwanza katika Injili Yesu anawahidia Roho Mtakatifu wafuasi wake. Kwa njia hiyo anawapa mamlaka yakuangusha uovu wote na nguvu za muovu. Na sehemu ya pili inaonesha sehemu maarufu ya Tomasi yakutokuamini. Ingawaje inaonekana kuwa katika methali hivi. Tomasi anaonekana kutokutenda chochote kibaya, alitaka tu aone kile kitu ambacho wengine wameona. Injili ya Marko inasema kwamba Yesu aliwatokea wale kumi na mmoja na kuwaonya juu ya ugumu wa mioyo yao, kwasababu hawakuamini kwamba amefufuka” (Mk 16:14). Katika Injili ya Luka Yesu mfufuka anaongea na mioyo ya mitume ambayo ina wasi wasi “kwanini mna wasi wasi mioyoni mwenu?” (Lk 24:38). Katika sehemu ya mwisho ya Injili ya Mathayo inasema pia wakati Yesu alivyo watokea mitume katika mlima wa Galilaya, wenigne walikuwa na wasi wasi (Mt 28:17). Kwahiyo wote pia walikuwa na wasiwasi, sio tu maskini Tomasi. 

Yohane Mwinjili anawakilisha habari hii sio kwamba anataka Tomasi aonekane mbaya au kumuweka mtume katika hali mbaya. Alitaka kusisitiza juu ya swali la jumuiya yake ya Kikristo ambalo daima walisisitiza na kuuliza. Iliwawia vigumu sana kuamini, wakajikuta katika msongo wa mawazo yenye mashaka mengi, walitaka kuona na ikiwezekana washike na kuhakikisha ni kweli Bwana amefufuka kweli. Walishangaza: je hata sisi hatuwezi kuwa kama wao? Haya ni maswali ambayo sisi wenyewe tunauliza kila wakati. Je, inawezekana na sisi tuweze kushuhudia Bwana Mfufuka? Je, kuna chochote cha kuonesha kwamba yuu mzima? Sasa inakuwaje hata atutokei ? Haya ni maswali ambayo sisi tunauliza siku hizi. Yohane anataka kumchukua Tomasi kama sehemu ya kila mfuasi anayepata shida katika kumwamini Yesu. Yohane anataka kuwafundisha waumini wa jumuiya ya kwanza na sisi kwamba maisha ya Yesu mfufuka yanaenda zaidi ya fahamu zetu, maisha ambayo huwezi kuyashika, kuyanusa, wala kuyaona. Yanaweza kupatikana tu kwa Imani. Mtu hawezi kuwa na Imani kwenye kitu ambacho kinaonekana. Kama mmoja anataka kuona, kupata jibu, kugusa lazima aikatae Imani. Lakini kwa Yesu, wana heri ambao hawajaona lakini wanaamini. Wana heri kwasababu Imani yao ni ya kweli na haina mashaka. Ambaye anaona anauhakika na ushahidi, ana nyenzo zisizopingika. Sasa inakuwaje kwa ambaye hajakutana na Yesu mfufuka? Kama Tomasi atahitaji kuona na ushahidi ili aweze kuamini, lakini ni wazi kwamba hatapa kamwe ushahidi. 

“Hakuna hata mmoja aliyetengwa na huruma ya Mungu na kanisa linawakaribisha wote bila kumkataa yeyote. Milango yake daima ipo wazi, ili wale wote wanaoguswa na neema ya Mungu waweze kuja kusamehewa. Hata Dhambi ikiwa kubwa vipi, ndivyo kanisa linavyo ongeza upendo wakukupenda na kukuribisha yule anayetubu…” . Maneno haya aliyasema Baba Mtakatifu Fransisko wakati akitangaza mwaka wa huruma ya Mungu (2016)

Alirudia kwakusema “Mungu daima hachoki kutusamehe sisi, bali sisi wanadamu tunachoka kumuomba msamaha na kutafuta huruma yake. Yesu ambaye ametuambia tuwasamehe ndugu zetu saba mara sabini, ametupatia sisi mfano.  Mfano ambao daima unatupatia tena sisi furaha yetu, anatufanya sisi tunyanyue tena vichwa vyetu na kuanza maisha mengine. Kwahiyo tusikimbie kutoka katika ufufuko wa Yesu, wala tusikate tamaa, hata lije jambo la namna gani. Tunaomba chochote kisitutie nguvu isipokuwa ufufuko wa Yesu mwenyewe, ambao unatupatia nguvu daima” (FURAHA YA INJILI, 3)

”Jumapili ya huruma ya Mungu imekuwa ikiadhimishwa tangu siku nyingi kama ibaada binafsi. Lakini mwaka 2000, Baba Mtakatifu, Mt. Paulo wa II, ambaye kwakweli katika hali ya kawaida alionesha mfano mzuri wa huruma ya Mungu, aliiweka Jumapili hii ya huruma ya Mungu wakati alipo mtangaza sister Faustina kuwa Mtakatifu. Ambaye alipata Baraka ya kushuhudia huruma ya Mungu na kuandika katika kitabu chake cha kumbukumbu ambacho alikiita huruma ya Mungu. Alikuwa akiandika kila siku ya nane baada ya Pasaka, undani wa huruma umefunguliwa. Ninamwaga huruma kama bahari kwa roho zote zile ambazo zinahitaji huruma yangu. Roho ambayo itaenda katika kitubio na kupokea Yesu wa Ekarisi (Komunyo) itapokea msamaha kamili na maondoleo ya adhabu. Siku hiyo milango yote ya huruma ya Mungu hufunguliwa kama bahari. Msikubali roho yoyote ile kuacha kuja kwangu, hata kama dhambi zake ni nyekundu kiasi ghani. Huruma yangu ni kubwa kiasi kwamba hata roho ya mwanadamu hata malaika hainauwezo wakuishinda milele yote.”

Leo katika jumapili ya huruma ya Mungu, tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu iliyo kuu. Injili yenyewe inaonesha Yesu akitoa mamlaka kwa mitume wake kwa kuwapatia Roho Mtakatifu kuondolea watu dhambi. Tusiache kukimbilia huruma hii ya Mungu. Lakini sisi pia tunapaswa kuwa mawakala wa huruma ya Mungu. Mungu anatuonesha huruma nyingi, lakini sisi nasi anatuhitaji tuoneshe huruma hiyo kwa wengine. Tukisikia sauti ya Yesu mfufuka ambayo ipo kwa ndugu zetu kama Tomasi basi tumgeukie Mungu na kuwa naye daima. Tushirikishane mapaji yetu kama jumuiya ya kwanza ilivyofanya katika somo la kwanza. Kama vile Yesu alivyokuja katikati ya mitume, sisi nasi tukishirikishana mapaji yetu, Yesu naye atakuja kati yetu nasi tutamtambua kwakushirikishana zawadi /mkate anao tujalia kila siku.

Sala: Bwana wa huruma, nisaidie leo niweze kuelewa nini maana ya huruma yako. Nisaidie niweze kuingia katika huruma yako ambayo unataka kunipatia mimi. Nikiwa napokea huruma yako mwenyewe, nisaidie na mimi pia niweze kuwa mjumbe wa huruma hiyo ili wote waweze kuona na kukutukuza wewe. Yesu, ninakutumaini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com