Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

CHUMVI NA MWANGA

 

ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Jumanne, Juni 9, 2026,
Juma la 10 la Mwaka


1 Fal 17: 7-16;
Zab 4: 1-4,6-7;
Mt 5: 13-16

CHUMVI NA MWANGA
 
Yesu anawaambia Wafuasi wake: ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Ninyi ni mwanga wa ulimwengu. Maneno haya ni utangulizi wa maneno ambayo Yesu atayasema katika hutuba ya mlimani. Wafuasi wa Yesu wanatakiwa maneno ya Yesu yapenye ndani yao, ya watawale na wayaishi.

Katika Agano la Kale, WaisraelI walipewa Amri kumi na Agano likafanywa kati yao likiwataka waishi kitakatifu na kwa haki kama wanavyotakiwa na Agano. Je, walitambua wao ni chumvi ya ulimwengu?. Walisisitiza sana kuhusu sheria, mpaka wakaua ile roho. Yesu anaonesha hili kwa wafuasi wake kwakuwaambia, wema wao usipozama ndani nakuushinda ule wa Walimu wa sheria na Mafarisayo, hawawezi kuwa chumvi ya ulimwengu. Yesu aliwataka Wafuasi wake wawe chumvi ya ulimwengu, si kwakusimama na kuonekana kama watakatifu machoni pa watu bali kwa maadili mema na utu ambao umevishwa taji ya upendo kwa Mungu na kwa jirani. Kwa wema, maadili na utu huu uliovishwa taji, na kungarishwa na Imani, matumaini na mapendo, wakristo wanaalikwa kuwa mwanga wa Ulimwengu. Hawahitaji kujitangaza kwamba wao ni Wakristu. Wataonesha kwamba wao ni Wakristo “kwanjia hii wote watajua ya kuwa ninyi ni wafuasi wangu, kama mna pendana ninyi kwa ninyi” (Yn 13: 35).

Kama tunavyoweza kufikiri mlo bila chumvi, au kupotelea msituni wakati wa usiku, tutatambua ni kitu ghani Yesu anatuambia. Kiasi kidogo cha chumvi au kiasi kidogo cha mwanga kina badili kila kitu. Mt. Fransisko wa Assis anatuambia giza lote la ulimwengu mzima haliwezi kuzima hata mwanga wa mshumaa mmoja. Ulimwengu tunaoishi upo gizani katika hali mbali mbali. Mungu anatuita mimi na wewe tuweze kuwa chumvi na mwanga na kuwaonesha watu njia. Mungu anataka kungara kupitia wewe na mimi, na anakutaka wewe uangaze. Jukumu letu ni kuwa wawazi.

Sala: Bwana, ninataka kutumiwa na wewe. Ninataka kuwa chumvi na mwanga. Ninataka kufanya mabadiliko ulimwenguni. Ninajitoa kwako kwa huduma yako. Yesu, ninakuamini wewe. Amina.

------------------------
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 9, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 9, 2026
JUMANNE, JUMA LA 10 LA MWAKA


SOMO 1 
l Fal. 17:7-16

Baada ya siku kupita, kite kijito kikakauka, kwa sababu mvua haikunya katika nchi. Neno la Bwana likamjia Eliya, kusema, Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe. Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa.

Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi
mwako. Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili nilngie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.

Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ilc chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi.

Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya.



WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 4 :1-4, 6-7 (K) 6

(K) Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; 
Umenifanyizia nafasi wakati wa shida;
Unifadhili na kuisikia sala yangu.
Enyi wanadamu,
hata lini utukufu wangu utafedheheka? (K)

Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa;
Bwana atasikia nimwitapo.
Mwe na hofu wala msitende dhambi,
Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. (K)

Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mcma?
Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.
Umenitia furaha moyoni mwangu,
Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai. (K)


SHANGILIO 
Zab. 27:11

Aleluya, alcluya, Ee Bwana, unifundishe njia yako, na kuniongoza katika njia iliyonyoka. Aleluya.


INJILI
Mt. 5:13-16

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

HERI WALIO…..!




“ASALI ITOKAYO MWAMBENI”
Tafakari ya kila Siku
Jumatatu, Juni 8, 2026
Juma la 10 la Mwaka


1 Fal 17 :1-6;
Zab 121: 1-8;
Mat 5: 1-12


HERI WALIO…..!

Yesu leo anaanza mazungumzo yake kwa maneno ya pekee ya heri. Zipo heri nane, kila moja ikianza kwa “heri walio..”. Yesu anatumia neno hili la heri ambalo kwa Kigirini ni Makarios ambalo ndani yake halibebi tuu furaha bali linabeba neno bahati nzuri ya kupata baraka maalumu. Kwahiyo tunaweza kusema, “heri walio…” au “Wanabahati kweli walio….”

Ufalme wake ni ufalme uliojaa huruma na msamaha. Na kama tutakavyokuwa tayari kuwasamehe wenzetu tutajikuta pia wenzetu wanatusamehe tunapo wakosea. Katika sala ya Bwana, ambayo ni sala ya Ufalme, huwa tunaomba hili, “tusamehe dhambi zetu kama na sisi tunavyo wasamehe waliotukosea”. Kwa kawaida ni vigumu sana kwa wale walio katika ufalme huu kutokusamehe, wao kawaida ni wepesi kusamehe na kukaribisha amani. Hii haimaanishi kwamba tuwatendee kila ubaya. Haki pia lazima iwepo. Kupinga na kukataa uovu haina maana ya kuacha kusamehe na kuponya vidonda vilivyo sababishwa na wengine.

Na huruma inayoeleweka katika nyanja ya kujali wengine ndio inayojenga Ufalme huu ndani ya mtu. Mtu huyu sio kwamba anaona huruma kwa wanaoteseka tuu bali anajua pia jinsi yakujiingiza katika matatizo ya wengine na kuhuzunika nao katika hali yao. Hii ndio sifa aliokuwa nayo Yesu katika hali zote. Aliingia katika maisha ya watu na kukaa nao na kuleta furaha na matumaini mapya.

Sala: nisaidie niweze kuwa mpole na mwenye huruma, maskini wa roho, mwenye kuleta Amani na mtu mwenye kukubali mateso. Nisaidie mimi niweze kupokea kwa shauku na kwa furaha ufalme wako. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2026
JUMATATU, JUMA LA 10 LA MWAKA


SOMO 1 
1 Fal. 17 :1-6

Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.

Neno la Bwana likamjia, kusema, Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani. Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko. Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani. Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 121:1-8 (K) 2

(K) Msaada wangu u katika Bwana, aliyezifanya mbingu na nchi.

Nitayainua macho yangu niitazamc milima;
Msaada wangu utatoka wapi?
Msaada wangu u katika Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi. (K)

Asiuache mguu wako usogezwe;
Asisinzie akulindaye;
Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,
Yeye aliye mlinzi wa Israeli. (K)

Bwana ndiye mlinzi wako;
Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.
Jua halitakupiga mchana,
Wala mwezi wakati wa usiku. (K)

Bwana atakulinda na mabaya yote,
Atakulinda nafsi yako.
Bwana atakulinda utokapo na uingiapo,
Tangu sasa na hata milele. (K)


SHANGILIO 
Zab. 119:34

Aleluya, aleluya, Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote. Aleluya.


INJILI
Mt 5:1-12

Yesu alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia; akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema, 

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.
Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.
Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.
Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.
Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

EKARISTI-UJUMBE MKUBWA WA UPENDO WA NYAKATI ZOTE.




“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya kila Jumapili
Jumapili, Juni 6, 2026
Juma la 11 la Mwaka wa Kanisa

Sherehe ya Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristu (Corpus Christi)

Kumb 8: 2-3, 14-16;
Zab 147;
1 Kor 10: 16-17;
Yn 6: 51-58.


EKARISTI-UJUMBE MKUBWA WA UPENDO WA NYAKATI ZOTE.

Sister Muagustiniani, sister Juliana wa Liège (Belgium) alipata maono ya kanisa likiwa chini ya mwezi unaongaa wenye kidoti kimoja cheusi. Doti hii ikionesha kutokuwepo kwa sherehe ya Ekaristi. Hii ilifanya baadaye kuwepo na sherehe ya Mwil na Damu ya Kristo ambayo iliwekwa kwenye kalenda ya Litirujia ya Kanisa mwaka 1264 chini ya Papa Urban wa IV. Je kulikuwa na haja ya kuwa na sherehe hii ya Ekaristi? Sherehe kama hii kawaida inatupa nafasi ya pekee ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uwepo wa Kristo kuwa nasi daima, ambaye yupo kweli katika Ekaristi Takatifu. Kwa upande mwingine, ni wakati wetu wakutafakari fumbo hili kubwa la upendo. Ekaristi Takatifu ni Sakramenti ambayo ni kilele cha Sakramenti zote, ndani yake Sakramenti nyingine zote huadhimishwa, kwasababu ni “Fumbo la mafumbo yote” na “Taji la Sakrament zote” sakramenti zote zinavishwa taji na Ekaristi Takatifu. Katika Ekaristi Takatifu hatupokei tuu neema bali tunampokea Bwana wa Neema.

Ekaristi Takatifu ni kilele cha sala sote na kuabudu kwetu. Hakuna njia nyingine ya kuwasiliana na Mungu, yenye undani na ukuu zaidi ya Ekaristi Takatifu. Hapa watu wawili (mtoaji na mpokeaji) wanakuwa katika umoja wa kweli, (ndani yake, naye ndani mwako). Tunapaswa kusali mara nyingi katika hali zote na sehemu yeyote kwasababu sala hizi zinatufanya tuunganike na Bwana na kujenga umoja naye. Lakini kwakweli, hakuna sala yeyote inayotoa muunganiko mkuu zaidi ya Ekaristi Takatifu. Hakuna yeyote wala chochote kinachopaswa kutufanya tushindwe kuwa wamoja na Kristo, na kwa njia ya umoja huu tupate nguvu tunayohitaji katika maisha yetu.

Jumapili hii tumekuja pamoja kuadhimisha Ekaristi Takatifu kwa roho ya furaha na mapendo. Kwa bahati mbaya kuna baadhi ya Wakatoliki wengi ambao hawaioni Ekaristi Takatifu katika hali tena. Idadi ya Wakatoliki wanao shiriki adhimisho la Ekaristi jumapili, baadhi ya sehemu inashuka kila mara. Misa sio sehemu ya maonesho, hawapati kile wanachotaka, watu wanapenda kitu kipya kila wakati na tena pengine chenye mtizamo wanaotaka wao. Ni ajabu utakuta Misa zinazo hudhuriwa mara nyingi ni, Jumatano ya Majivu, Jumapili ya Matawi, Jumapili ya pasaka na Noeli kwasababu kuna vitu ninaongezwa ndani yake kwa mfano, matawi, majivu, mishumaa nk. Wengi wanategemea Padre aweke utani kwenye mahubiri ili afanye watu wachangamke, wengine wanataka kwaya waimbe vizuri sana kwa sauti zenye kupendeza na pengine wacheze sana kwa midundo ya kisasa zaidi, vifaa bora zaidi vya muziki, wengine wanataka wasomaji wenye sauti nzuri zakupendeza masikioni mwao, viti vizuri vya kukaa, taa zenye mwanga mzuri wa kupendeza na vifaa vizuri vya sauti. Kwa kweli, haya yote ni mitazamo na matarajio. Mbaya zaidi, pengine wapo pia baadhi ya makuhani wamenaswa kwenye mtego huu. Badala ya kuwapa watu anachosema Mungu, anawapa watu wanachopenda kusikia na kuona. Kwa matokeo haya, neno la Mungu halihubiriwi kiaminifu na katika unabii na maana halisi ya Uwepo wa Mungu inapotezwa. Kumekuwako na ile hali ya mlalo (mwanadamu kwa mwanadamu) na kuacha ile hali ya wima (Mungu kwenda kwa Mwanadamu) ya liturujia.

Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikti XVI alikuwa akisisitiza kila wakati kwamba “Liturjia ni Tendo la Mungu”. Hatupaswi kusahau kwamba kiini cha liturujia na maadhimisho ya Sakramenti ni Mungu na sio mwanadamu. Aliendelea pia kusema; “Katekesi nzuri juu ya Ekarisiti ni Ekaristi yenyewe ikiadhimishwa vizuri”. Kufahamu na kuamini kwamba Yesu yupo kweli katika adhimisho la Ekaristi, tunapaswa wote tufanye jitihada kufanya adhimisho hili lenye maana na furaha. Bila kusahau kwamba Ekaristi haiwi Ekaristi kwasababu ya Imani ya padre au Muumini. Baada ya sala ya Ekaristi (Konsekratsio) Yesu anakuwa kweli chini ya Maumbo ya mkate na divai. Uwe na Imani au usiwe na Imani, Yesu anabaki kuwa Yesu katika maumbo hayo daima. Tunadaiwa kuwa na Imani ili tuweze kushirikiana na neema ya Mungu lakini hata tusipokuwa nayo haimaanishi utamzuia Yesu kuwa katika maumbo hayo. Tushirikiane naye kwa Imani ili tupate neema.

Ni Mtakatifu Maximiliani Kolbe ambaye aliwahi kusema kwa hakika kwamba, “Utimilifu wa Misa sio wakati wa mageuzo bali ule umoja mtu anaoupokea wakati wa komunyo”. Tunaamini kwamba Ekaristi ni sadaka ile ile aliyo itoa Yesu pale msalabani na sio kumbukumbu ya kihistoria ya tukio lililopita, na kwamba mkate na divai unakuwa kweli mwili na damu ya Kristo, na pia tunaamini kwamba Ekaristi ni sakramenti ya Upendo wa Mungu kwetu. Sakramenti inayo adhimishwa katika Imani hiyo inatusaidia tuweze kuuona umoja wa ndani wa mtu na Mungu. “Wakati tunatazama Msalaba, unatambua ni kwajinsi ghani Yesu alitupenda, na ukitazama Ekaristi Takatifu unatambua ni kwa jinsi ghani Yesu ananipenda sasa” (Mt. Teresa wa Kolkota). Je, wakati tunautazama mkate wa uzima, tunatambua tunamtazama Mungu? Leo tunaalikwa tutafakari na kutambua sio tuu vipaji vya ajabu tulivyopewa bali tuangalie wema na unyenyekevu wa yule aliyejitoa mwenyewe.

Katika sherehe hii ya Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, tufufue tena Imani yetu juu ya uwepo wa kweli wa Yesu katika Ekaristi Takatifu. Imani hii itujalie na kutusukuma kila wakati tuende kanisani kila jumapili tukiwa na furaha na hamu ya kukutana na Yesu ili maadhimisho ya Ekaristi yaweze kuwa yenye uhai na kweli nakuleta maana mbele ya Mungu. Kama kila wakati tutakuwa na haya mioyoni mwetu, itatusaidia kujitayarisha vyema- kimwili, kiakili na kiroho, ili tuweze kuadhimisha tukiwa wenye uchangamfu na kushiriki kikamilifu kwenye misa, nakumpokea Yesu katika komunyo Takatifu tukiwa tunastahili. Na hapo maadhimisho ya Ekaristi yataacha kuonekana kama tendo linalotuchosha nakuchukua muda wetu. Badala yake linakuwa kwetu kiini, chanzo na kilele cha maisha yetu kama Wakristo.

Sala: ninakuabudu wewe Mungu uliye jificha kweli katika Ekaristi, katika maumbo ya mkate na divai. Moyo wangu wote unajikabidhi kwako, kwa kukutafakari wewe unajikabidhi kwako. Asante Bwana kwakungarisha maisha yangu kila siku kwa chakula cha malaika. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 6, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 6, 2026

SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU


MWANZO:
Zab. 80:17
Nimewalisha kwa unono wa ngano na kuwashibisha asali itokayo mwambani.


SOMO 1
Kum. 8:2-3;14-16

Musa aliwaambia makutano: Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 147:12-15,19-20 (K) 12

(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Ndiye afanyaye amani mipakani mwako,
Akushibishaye kwa unono wa ngano.
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua.
aleluya. (K)


SOMO 2
1Kor. 10:16-17

Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


SHANG1LIO
Yn. 6:51

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; asema Bwana; mtu akila chakula hiki, ataishi milele.
Aleluya.


INJILI
Yn. 6:51-58

Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUTEMBEA KATIKATI YA MITEGO!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Juni 6, 2026
Juma la 9 la Mwaka


Tob 12:1, 5-15, 20;
Tob 13:2, 6-8;
Mk 12: 38-44.


MKARIMU KAMA MJANE MASKINI!


Somo la Injili linatoa picha Yesu akiwa na wafuasi wake, akiwa amekaa akiangalia watu wakiwa wanatoa sadaka hekaluni. Wale watu waliopenda kuonekana kuwa watu wa karimu walitoa nyingi sana. Lakini tazama anatokea mjane maskini, ambaye katika hali ya ukimya na unyofu anaweka senti mbili. Yesu mara moja anavutwa na kitendo hichi na anawaambia wafuasi wake. Aliweka senti mbili tu kiasi ambacho kilikuwa ni kidogo sana. Lakini tazama Yesu anamtangaza kwamba ametoa nyingi zaidi kuliko wengine. Yesu anaelezea tofauti juu ya utajiri wa kimwili na utajiri wa kiroho. Utajiri wa kiroho na ukarimu wa kiroho ni muhimu zaidi kuliko utajiri wa kimwili. Mjane huyu alikuwa maskini kimwili lakini alikuwa tajiri kiroho. Wale waliokuwa na kiasi kikubwa cha fedha walionekana kuwa matajiri wa kimwili lakini maskini wa kiroho kuliko mjane huyu.

Katika ulimwengu wa kutafuta mali tunaoishi katika, ni vigumu kuamini. Ni vigumu kugeuza dhamiri na kugeukia utajiri wa kiroho wenye Baraka nyingi. Tunapaswa kuwa kama huyu mjane maskini na kutoa yote tulionayo. Alitaka kuleta tofauti. Alitoa yote aliokuwa nayo.

Kila mtu anapaswa kuangalia ni kwa jinsi ghani hili linaingia katika maisha yake. Tunapaswa kuwa na hali ya ndani ya kuwa na ukarimu na hali ya kuachia. Kuanzia hapa, Bwana atakuonesha ni kwa jinsi ghani ya kutumia mali zetu kwa ajili ya faida ya uzuri wetu na kwa ajili ya wengine pia. Toa ulionayo na jinsi ulivyo kwake, naye ataelekeza moyo wako kadiri ya utukufu wake mkamilifu.

Sala: Bwana, ninaomba unipe moyo wa ukarimu na uondoe moyo wa ubinafsi kama yule mjane. Nisaidie mimi nitafute njia za kujitoa kabisa kwako, bila kushikilia mambo mengine nyuma yangu, na zaidi kutafuta utukufu wa kiroho katika ufalme wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUNI 6, 2026



MASOMO YA MISA JUNI 6, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 9 LA MWAKA


SOMO 1
2 Tim. 4:1-8

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake; lihubirini neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho. Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masi- kio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.

Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nime- ilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 71:8-9, 14-17, 22

Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa.

Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote. 
Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa;


Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako. 
Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo. 

Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu.
Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli. 


SHANGILIO
Mt 5:3

Aleluya, aleluya
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 
Aleluya


INJILI
Mk. 12:38-44

Yesu aliwaambia katika mafundisho yake: Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele katika karamu; ambao hula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu; hawa watapata hukumu iliyo kubwa.

Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa. Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.
-------------------------
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

FURAHIA NDANI YA BWANA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Juni 5, 2026
Juma la 9 la Mwaka

Mt Bonifasi, Askofu na Mfiadini 

2 Tim 3: 10-17
Zab 119: 157, 160, 161, 165, 166, 168
Mk 12: 35-37.


FURAHIA NDANI YA BWANA!


Sisi Wakristo tunafahamu kwamba Yesu ni Masiha, Mwana wa Daudi. “Mwana wa Daudi” jina linalo mwakilisha Yesu huku likitengeneza uti wa mgongo wa Injili. Katika Maamkio ya Bikira Maria alipokea ujumbe huu “Na Bwana Mungu atampa kiti cha Daudi Baba yake, na atatawala nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na Mwisho” (Lk 1:32-33). Yule Maskini aliyekuwa mwombaji alimwomba Yesu amponye, akisema “Yesu Mwana wa Daudi, unihurumie mimi” (Mk 10:48). Wakati Yesu alivyokuwa akiingia Yerusalemu walimshangilia wakisema “Mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, hosanna juu mbinguni” (Mk 11:10).

Lakini sio tu Mwana wa Daudi, yeye pia ni Bwana. Analionesha hili yeye mwenyewe kwa kunukuu zaburi ya Daudi 110. Mt. Petro, aliye shahidi wa ufufuko wa Bwana, aliona wazi kwamba Yesu amethibitiswa “Bwana wa Daudi”, kwasababu “ndugu zangu nina waambia kwa ujasiri kwamba Babu yetu Daudi alikufa na akazikwa na kaburi lake lipo hapa hadi leo…lakini Yesu ambaye ni Mungu alifufuka, ambao sisi ni mashahidi wake.” (Mdo 2:29-32).

Leo Yesu anajaribu kuwaelewesha Wayahudi kuhusu Masiha au Kristo. Masiha atakuwa Daudi mpya, akitawala juu ya Ufalme wake, lakini atatawala milele katika ufalme wa milele, kama Malaika Garieli alivyo tangaza kwa Maria (Lk 1:32-33; Is 9:7). Atakuwa Mwana wa Mungu kwa asili, na hivyo atakuwa Mungu mwenyewe, mwenye Umungu sawa na Baba.

“Umati mkubwa walisikia hili kwa shauku na furaha (Mark 12:37). Mafundisho ya Yesu yalileta furaha sana katika mioyo yao. “Je, mimi nina yarufahia maneno ya Yesu?” ni mara nyingi tunayaona maneno ya Yesu kama mzigo, au kuwa kikwazo kwa mambo ambayo tunataka kufanya katika maisha. Furaha katika Bwana ni kitu ambacho kinatufanya kukuwa zaidi kila siku. Tujiruhusu kufurahi katika Bwana na kufurahia uwepo wa maneno yake. Tukiwa “tumeiva vizuri” tutamtafuta yeye zaidi.

Sala: Bwana Yesu, Mwana wa Daudi, ninatamani kufurahia katika wewe. Nisaidie niweze kuacha mambo yote ya ulimwengu yanayo niweka mbali nawe. Nisaidie niweze kukutafuta wewe na neno lako daima. Jaza roho yangu na furaha yako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUNI 5, 2026

 



MASOMO YA MISA JUNI 5, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 9 LA MWAKA

KUMBUKUMBU YA MTAKATIFU BONIFASI, ASKOFU NE MFIADINI

SOMO 1 
2 Tim. 3 :10-17

Wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili; naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.

Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, Iafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 119 : 157, 160-161, 165-166, 168 (K) 165

(K) Wana amani nyingi waipendao sheria yako.

Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, 
lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
Jumla ya neno lako ni kweli,
na kila hukumu ya haki yako ni ya milele. (K)

Wakuu wameniudhi bure,
ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
Wana amani nyingi waipendao sheria yako, 
wala hawana la kuwakwaza. (K)

Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako, 
na maagizo yako nimeyatenda.
Nimeyashika mauasi yako na shuhuda zako, 
maana njia zangu zote zi mbele zako. (K)


SHANGILIO 
Zab. 111 :7, 8

Aleluya, aleluya, Maagizo yako yote, ee Bwana, ni amini, yamethibitika milele na milele. Aleluya.


INJILI 
Mk. 12:35-37

Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu, alijibu, akasema, Husemaje waandishi ya kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi? Daudi mwenyewe alisema, kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, hata niwawekapo adui zako kuwa chini ya miguu yako. Daudi mwenyewe asema ni Bwana; basi amekuwaje mwanawe? Na mkutano mkubwa walikuwa wakimsikiliza kwa furaha.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.