Tafakari ya kila siku
Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
NYUMBA MPYA, FAMILIA MPYA
Tafakari ya kila siku
MASOMO YA MISA, JUNI 28, 2026
MWANZO:
Zab. 47:2
Enyi watu wote, pigeni makofi, mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe.
SOMO 1
2 Fal 4:8-11,14-16
Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula. Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo. Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1
(K) Fadhili za Bwana nitaziimba milele.
Fadhili za Bwana nitaziimba milele;
Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;
Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)
Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe,
Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako.
Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,
Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)
Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe,
Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.
Maana ngao yetu ina Bwana,
Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)
SOMO 2
Rum. 6:3-4,8-11
Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika
wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Mt. 11:25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10:37-42
Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.
Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki. Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.
KILIO CHA SALA!!

MASOMO YA MISA, JUNI 27, 2026
MASOMO YA MISA, JUNI 27, 2026
KUWA KAMA KRISTO KATIKA KUPENDA NA HURUMA
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Juni 26, 2026,
Juma la 12 la Mwaka
2 Fal 25: 1-12;
Zab 137: 1-6;
Mt 8: 1-4
KUWA KAMA KRISTO KATIKA KUPENDA NA HURUMA
Katika somo la Injili Yesu anatenda kisicho fikirika. Anamgusa “mkoma” ambae hapaswi kuguswa. Wakoma walikuwa watu wasio thaminika kabisa na kutengwa katika jamii ya Wayahudi. Hawakuwa wametengwa tu bali walikuwa wanachukuliwa kama “wameshakufa tayari”! hata na ndugu zao. Sheria za Kiyahudi zilikataza mtu yeyote kusogelea mkoma au kumgusa, kwani atatiwa najisi. Akitambua hili, mkoma kwa kushangaza anamkaribia Yesu kwa ujasiri na unyenyekevu, akitazamia uponyaji kutoka kwa Yesu. Yesu hakumpa tu huyu mkoma kile alichokuwa akihitaji bali anaonesha upendo na huruma na ukarimu wa Kimungu kwa kumgusa. Anaonesha upendo na huruma ya Kimungu katika hali ya kugusa zaidi badala ya maneno matupu. Alimgusa mkoma na anamfanya awe safi tena-sio kimwili tu bali pia kiroho. Matokeo yake ni kwamba alirudishiwa tena afya yake na kuwa mzima kabisa.
Yesu alimpenda huyu mkoma alipenda kumpa zawadi yake ya thamani ya uponyaji. Alifanya haya kwa huruma, na alihitaji ashukuru. Hakupenda kufanya hili hadharani. Sisi nasi tunapaswa kuiga hilo. Tunapaswa kutambua kuwa Mungu anatupenda sana kiasi kwamba anataka kutunyanyua juu kutoka katika mizigo yetu na kutuponya kutoka katika madhaifu yetu kwasababu tu, anatupenda.
Tutafakari leo, juu ya kinacho sababisha sisi tuwe na ukarimu kwa watu. Tuombe ili nasi tuweze kufanya katika hali ambayo haitafuti heshima ili tuweze kuiga tabia za Kimungu.
Sala: Bwana, ninaomba nikuwe katika mapendo kwa wengine na nioneshe mapendo hayo katika hali ya ukamilifu wako. Ninaomba nisivutwe na tamaa ya kusifiwa. Yesu nakuamini wewe. Amina.
MASOMO YA MISA JUNI 26, 2026
MASOMO YA MISA JUNI 26,
2026
IJUMAA YA 12 YA
MWAKA
SOMO1
2 Fal 25: 1-12
Ikawa katika mwaka wa
kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo,
Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja yeye na jeshi lake lote, kupigana na
Yerusalemu, akapanga hema zake kuukabili; bao wakajenga ngome juu yake pande
zote. Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na moja wa mfatae Sedekia.
Siku ya kenda ya mwezi wa nne njaa ilikuwa nzito ndani ya mji, hata hapakuwa na
chakula kwa watu wa nchi. Ndipo mahali pakabomolewa katika ukuta wa maji, watu
wote wa vita wakakimbia usiku kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta
mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wakiuzuia mji
pande zote;) mfalme akaenda kwa njia ya Araba. Lakini jeshi la Wakaldayo
wakamfuatia mfalme, wakampata katika nchi tambarare ya Yeriko; na jeshi lake
lote walikuwa wametawanyika na kumwacha. Ndipo wakamkamata mfalme, wakamchukua
kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. wakatoa
hukumu juu yake. Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, wakampofusha
macho Sedekia, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.
Hata mwezi wa tano,
siku ya saba ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza,
mfalme wa Babeli. Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, mtumishi wa mfalme wa
Babeli, akaingi Yerusalemu. Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme;
na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto. Na
jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi,
wakazibomoa kuta za Yerusalemu pande zote. Na mabaki ya watu waliosalia katika
mji, nao wale walioasi, na kumkimbilia mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu wote
wengine, watu hao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka.
Lakini huyo amiri wa askari walinizi akawaacha watu walio maskini ili wawe
watunza mizabibu na wakulima.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 137 : 1-6 (K). 6
(K) Ulimi wangu
ugandamane nisipokukumbuka.
Kando ya mito ya
Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia
tulipoikumbuka Sayuni.
Katika miti iliyo
katikati yake
Tulivitundika vinubi
vyetu. (K)
Maana huko
waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea
walitaka furaha;
Tuimbieni baadhi ya
nyimbo za Sayuni. (K)
Tuuimbeje wimbo wa
Bwana
Katika nchi ya ugeni?
Ee Ycrusalemu,
nikikusahau wewe,
Mkono wangu wa kuume
na usahau. (K)
Ulimi wangu na
ugandamane
Na kaakaa la kinywa
changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza
Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu
iliyo kuu. (K)
SHANGILIO
Yn. 10:27
Aleluya, aleluya, Kondoo
wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata. Aleluya.
INJILI
Mt. 8:1-4
Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema, Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika. Yesu akamwambia, Angalia usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwao.
-------------------------
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
NAWEZAJE KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU?
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com





