Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

HURUMA YA MUNGU: MSAMAHA WA DHAMBI



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakri ya Pasaka
Aprili 12, 2026 
------------------------------------------------
JUMAPILI, DOMINIKA YA 2 YA PASAKA, JUMAPILI YA HURUMA YA MUNGU. 
------------------------------------------------

HURUMA YA MUNGU: MSAMAHA WA DHAMBI

Leo ni siku ya nane naya mwisho katika oktava ya Pasaka. Na siku ya leo tunaadhimisha Jumapili ya huruma ya Mungu. Ni siku ambayo geti la huruma ya Mungu hufunguliwa kwetu na Mungu kutukirimu huruma yake hata zaidi ya jinsi ambavyo tunaweza kudhani au kutumaini. Leo tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu isiyo na mipaka. Injili ya leo inaonesha mamlaka ya Yesu yakuwapa mitume Roho Mtakatifu ambaye ndiye atakaye wasamehe watu dhambi zao. Yesu Mfufuka anakuwa hai tena kati ya wafuasi wake. Anafungua miyo yao na kuitia shauku na kuwafungulia maandiko, na kuumega mkate. Anafungua macho yao na kujidhihirisha kwao. 

Sehemu ya kwanza katika Injili Yesu anawahidia Roho Mtakatifu wafuasi wake. Kwa njia hiyo anawapa mamlaka yakuangusha uovu wote na nguvu za muovu. Na sehemu ya pili inaonesha sehemu maarufu ya Tomasi yakutokuamini. Ingawaje inaonekana kuwa katika methali hivi. Tomasi anaonekana kutokutenda chochote kibaya, alitaka tu aone kile kitu ambacho wengine wameona. Injili ya Marko inasema kwamba Yesu aliwatokea wale kumi na mmoja na kuwaonya juu ya ugumu wa mioyo yao, kwasababu hawakuamini kwamba amefufuka” (Mk 16:14). Katika Injili ya Luka Yesu mfufuka anaongea na mioyo ya mitume ambayo ina wasi wasi “kwanini mna wasi wasi mioyoni mwenu?” (Lk 24:38). Katika sehemu ya mwisho ya Injili ya Mathayo inasema pia wakati Yesu alivyo watokea mitume katika mlima wa Galilaya, wenigne walikuwa na wasi wasi (Mt 28:17). Kwahiyo wote pia walikuwa na wasiwasi, sio tu maskini Tomasi. 

Yohane Mwinjili anawakilisha habari hii sio kwamba anataka Tomasi aonekane mbaya au kumuweka mtume katika hali mbaya. Alitaka kusisitiza juu ya swali la jumuiya yake ya Kikristo ambalo daima walisisitiza na kuuliza. Iliwawia vigumu sana kuamini, wakajikuta katika msongo wa mawazo yenye mashaka mengi, walitaka kuona na ikiwezekana washike na kuhakikisha ni kweli Bwana amefufuka kweli. Walishangaza: je hata sisi hatuwezi kuwa kama wao? Haya ni maswali ambayo sisi wenyewe tunauliza kila wakati. Je, inawezekana na sisi tuweze kushuhudia Bwana Mfufuka? Je, kuna chochote cha kuonesha kwamba yuu mzima? Sasa inakuwaje hata atutokei ? Haya ni maswali ambayo sisi tunauliza siku hizi. Yohane anataka kumchukua Tomasi kama sehemu ya kila mfuasi anayepata shida katika kumwamini Yesu. Yohane anataka kuwafundisha waumini wa jumuiya ya kwanza na sisi kwamba maisha ya Yesu mfufuka yanaenda zaidi ya fahamu zetu, maisha ambayo huwezi kuyashika, kuyanusa, wala kuyaona. Yanaweza kupatikana tu kwa Imani. Mtu hawezi kuwa na Imani kwenye kitu ambacho kinaonekana. Kama mmoja anataka kuona, kupata jibu, kugusa lazima aikatae Imani. Lakini kwa Yesu, wana heri ambao hawajaona lakini wanaamini. Wana heri kwasababu Imani yao ni ya kweli na haina mashaka. Ambaye anaona anauhakika na ushahidi, ana nyenzo zisizopingika. Sasa inakuwaje kwa ambaye hajakutana na Yesu mfufuka? Kama Tomasi atahitaji kuona na ushahidi ili aweze kuamini, lakini ni wazi kwamba hatapa kamwe ushahidi. 

“Hakuna hata mmoja aliyetengwa na huruma ya Mungu na kanisa linawakaribisha wote bila kumkataa yeyote. Milango yake daima ipo wazi, ili wale wote wanaoguswa na neema ya Mungu waweze kuja kusamehewa. Hata Dhambi ikiwa kubwa vipi, ndivyo kanisa linavyo ongeza upendo wakukupenda na kukuribisha yule anayetubu…” . Maneno haya aliyasema Baba Mtakatifu Fransisko wakati akitangaza mwaka wa huruma ya Mungu (2016)

Alirudia kwakusema “Mungu daima hachoki kutusamehe sisi, bali sisi wanadamu tunachoka kumuomba msamaha na kutafuta huruma yake. Yesu ambaye ametuambia tuwasamehe ndugu zetu saba mara sabini, ametupatia sisi mfano.  Mfano ambao daima unatupatia tena sisi furaha yetu, anatufanya sisi tunyanyue tena vichwa vyetu na kuanza maisha mengine. Kwahiyo tusikimbie kutoka katika ufufuko wa Yesu, wala tusikate tamaa, hata lije jambo la namna gani. Tunaomba chochote kisitutie nguvu isipokuwa ufufuko wa Yesu mwenyewe, ambao unatupatia nguvu daima” (FURAHA YA INJILI, 3)

”Jumapili ya huruma ya Mungu imekuwa ikiadhimishwa tangu siku nyingi kama ibaada binafsi. Lakini mwaka 2000, Baba Mtakatifu, Mt. Paulo wa II, ambaye kwakweli katika hali ya kawaida alionesha mfano mzuri wa huruma ya Mungu, aliiweka Jumapili hii ya huruma ya Mungu wakati alipo mtangaza sister Faustina kuwa Mtakatifu. Ambaye alipata Baraka ya kushuhudia huruma ya Mungu na kuandika katika kitabu chake cha kumbukumbu ambacho alikiita huruma ya Mungu. Alikuwa akiandika kila siku ya nane baada ya Pasaka, undani wa huruma umefunguliwa. Ninamwaga huruma kama bahari kwa roho zote zile ambazo zinahitaji huruma yangu. Roho ambayo itaenda katika kitubio na kupokea Yesu wa Ekarisi (Komunyo) itapokea msamaha kamili na maondoleo ya adhabu. Siku hiyo milango yote ya huruma ya Mungu hufunguliwa kama bahari. Msikubali roho yoyote ile kuacha kuja kwangu, hata kama dhambi zake ni nyekundu kiasi ghani. Huruma yangu ni kubwa kiasi kwamba hata roho ya mwanadamu hata malaika hainauwezo wakuishinda milele yote.”

Leo katika jumapili ya huruma ya Mungu, tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu iliyo kuu. Injili yenyewe inaonesha Yesu akitoa mamlaka kwa mitume wake kwa kuwapatia Roho Mtakatifu kuondolea watu dhambi. Tusiache kukimbilia huruma hii ya Mungu. Lakini sisi pia tunapaswa kuwa mawakala wa huruma ya Mungu. Mungu anatuonesha huruma nyingi, lakini sisi nasi anatuhitaji tuoneshe huruma hiyo kwa wengine. Tukisikia sauti ya Yesu mfufuka ambayo ipo kwa ndugu zetu kama Tomasi basi tumgeukie Mungu na kuwa naye daima. Tushirikishane mapaji yetu kama jumuiya ya kwanza ilivyofanya katika somo la kwanza. Kama vile Yesu alivyokuja katikati ya mitume, sisi nasi tukishirikishana mapaji yetu, Yesu naye atakuja kati yetu nasi tutamtambua kwakushirikishana zawadi /mkate anao tujalia kila siku.

Sala: Bwana wa huruma, nisaidie leo niweze kuelewa nini maana ya huruma yako. Nisaidie niweze kuingia katika huruma yako ambayo unataka kunipatia mimi. Nikiwa napokea huruma yako mwenyewe, nisaidie na mimi pia niweze kuwa mjumbe wa huruma hiyo ili wote waweze kuona na kukutukuza wewe. Yesu, ninakutumaini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 12, 2026



MASOMO YA MISA, APRILI 12, 2026
DOMINIKA YA 2 YA PASAKA

SOMO 1
Mdo 2:42-47

Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali. Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika, wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja. Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, walimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe, wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 11:2-4, 13-15, 22-24

(K) Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele.


Israeli na aseme sasa,
Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Mlango wa Haruni na waseme sasa,
Ya kwamba fadhili zake ni za milele. (K) 

Ulinisukuma sana ili nianguke;
Lakini Bwana akanisaidia.
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu,
Naye amekuwa wokovu wangu.
Sauti ya furaha na wokovu
Imo hemani mwao wenye haki. (K) 

Jiwe walilolikataa waashi
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Neno hili limetoka kwa Bwana,
Nalo ni ajabu machoni petu.
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana,
Tutaishangilia na kuifurahia. (K)


SOMO LA 2
1 Pet. 3 – 9

Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu. Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya Imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho. Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; ili kwamba kujaribiwa kwa Imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufufunuliwa kwake Yesu Kristo. Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamwoni sasa, mnamwamini; na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu, katika kuupokea mwisho wa Imani yenu, yaani, wokovu wa roho zenu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 20:29

Aleluya, aleluya,
Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadfiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. Aleluya.



INJILI
Yn. 20:19 – 31

Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana. Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wowote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa. Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati akasema, Amani iwe kwenu. Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kole chako, uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu; wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye. Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. Basi kuna ishara nyingine nyingi alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake, zisizoandikwa katika kitabu hiki. Lakini hizi zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini na uzima kwa jina lake.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 2026 "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

IMANI INATUONGOZA KWENYE UKWELI WA UFUFUKO!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Aprili 11, 2026 
Oktava ya Pasaka

Mdo 4:13-21
Zab 118:14-21
Mk 16:9-15


IMANI INATUONGOZA KWENYE UKWELI WA UFUFUKO! 

Kukosa Imani kunamfanya mtu akose ukweli mwingi katika maisha. Imani juu ya uzuri wa ndugu zetu inatufanya tujenge ulimwengu kuwa sehemu nzuri ya kuishi. Imani juu yetu wenyewe inatufanya kuachia mawimbi mbali mbali yanayokuja kwetu tusio yafahamu. Imani juu ya utume wetu inatufanya tuishi vizuri wito wetu. Imani katika mapendo kwa Mungu inatufanya sisi tusiwe watu wazama za dhambi na kuwa “washindi wa wakati huu”. Imani kwa Yesu mfufuka inatusaidia tuweze kutangaza habari za ufufuko. Zaidi ya nyakati zote, ulimwengu wa sasa unahitaji watu wenye Imani.

Kwanini mitume walishindwa kuamini kwamba Yesu amefufuka kutoka wafu? Walikuwa wameshaona miujiza mingi sana kwa Yesu kabla ya kufa. Walimsikia akifundisha kwa mamlaka makubwa na neema. Na sasa, baada ya kufufuka kutoka wafu mioyo yao imekuwa migumu na hawakuamini mara moja. Yesu alibidi kuwatokea mara nyingi na kuonesha ushuhuda huo mbele ya macho yao. Walitaka kuamini lakini hawakuweza kuruhusu wao wenyewe kuamini ufufuko kwa Imani ya kweli mpaka Yesu atoe ushuhuda. Baada ya muda walitambua hata ushuhuda waliohitaji ulikuwa ndani yao.

Mara nyingi tuna alikwa na Yesu kuwa na Imani na kumwamini yeye na kukubali mambo mengi kwa Imani. Zawadi ya Imani ni sawa na moto mdogo ndani mwetu ambao mara nyingi kwa kutojali tunaruhusu uzimwe na mambo mbali mbali bila kukuwa. Nia ya Ukristo wetu ni kuruhusu moto huo ukuwe na kufikia kilele ambacho Mungu anapenda. Inawezekana kuwasha moto huo na kuwa mkubwa na hatimaye kuchoma chochote kinacho taka kuingia ndani. Njia ya moto huu unajali sana namna tulivyoshikilia ule moto mdogo ambao tayari umeshaingia ndani mwetu. Tunapaswa kuukuza na kuulinda ili ukuwe. Hili linawezekana kwa kuacha ulegevu katika kusali. 

Sala ni ufunguo wa kumruhusu Mungu akue ndani mwetu. Yupo ndani, akiongea nasi na kutuita tuamini. Kila mara tunapo kaza macho katika moto huo, tuna uwezesha ukuwe na kuchukua nafasi. Na kama Wafuasi wangeweza kuacha tu zawadi hiyo ya Imani ikuwe wangeweza mara moja kumtambua Yesu na kumwamini mara moja, bila hata yeye kujidhihirisha kwenye macho yao. Je, unafanya nini katika maisha yako ili kuruhusu moto mdogo wa Imani uliopo ndani mwako kukuwa? Jikite daima kwenye sala, na tazama Imani yako kwa Yesu itakuwa na kungara. 

Sala: Bwana nakupenda wewe na nakuamini wewe. Ninakuomba unisaidie kukuza moto wa imani uliopandwa ndani mwangu uweze kukuwa. Nitakase moyo wangu kwa moto huu na niweke huru kutoka katika moyo wangu mgumu. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 11, 2026




MASOMO YA MISA, APRILI 11, 2026
JUMAMOSI KATIKA OKTAVA YA PASKA


SOMO 1
Mdo. 4:13 – 21

Siku ile, makuhani na akida wa hekalu walipoona ujasiri wa Petro na Yohane, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu. Na wakimwona yule aliyeponywa akisimama pamoja nao hawakuwa na neno la kujibu. Wakawaamuru kutoka katika baraza, wakafanya shauri wao kwa wao, wakisema, Tuwafanyieni watu hyawa? Maana ni dhahiri kwa watu wote wakaao Yerusalemu ya kwamba ishara mashuhuri imefanywa nao, wala hatuwezi kuikana. Lakini neno hili lisije likaenea katika watu, na tuwatishe wasiseme tena na mtu awaye yote kwa jina hili. Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu. Petro na Yohane wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 118:1, 14 – 21 (K) 21

(K) Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

Aleluya,
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema,
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu,
Naye amekuwa wokovu wangu.
Sauti ya furaha na wokovu,
Imo hemani mwao wenye haki. (K)

Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa;
Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
Sitakufa bali nitaishi,
Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
Bwana ameniadhibu sana,
Lakini hakuniacha nife. (K)

Nifungulieni malango ya haki,
Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Lango hili ni la Bwana,
Wenye haki ndio watakaoliingia.
Nitakushukuru kwa maana umenijibu,
Nawe umekuwa wokovu wangu. (K)



SHANGILIO
Zab. 118:24

Aleluya, aleluya,
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutaishangilia na kuifurahia.
Aleluya.



INJILI
Mk. 16:9 – 15

Yesu alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba. Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia. Walakini hao waliposikia kama yu hai, naye amemwona, hawakusadiki.

Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba. Na hao wakaenda zao wakawapa habari wale wengine; wala hao hawakuwasadiki.

Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutokuamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu. Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

UFUFUKO: WITO MPYA



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Aprili 10, 2026
Oktava ya Pasaka

Mdo 4:1-12
Zab 118:1-2,4,22-27
Yn 21:1-14


UFUFUKO: WITO MPYA

Leo, tunasikia tena habari nyingine ya ufufuko ya Bwana kuwatokea wafuasi wake. Baada ya kuona hamna namna nyingine na kuamua kurudi katika kazi yao ya uvuvi, wakiwa wamekata tamaa na kuchoka, wanarudi ufukweni mwa bahari bila kupata kitu. Mara moja wanamsikia Yesu, (hawakumtambua) akiwaambia waende kuvua tena upande mwingine. Walimtii na tazama nyavu zilijaa samaki wengi. Muujiza huu ulitosha kwa Yohane kutambua kuwa ni “Bwana”.

Hiki kitendo cha kushika samaki wengi kilikuwa kama zawadi ya Yesu kwao kuwasaidia katika kazi yao. Ilikuwa ni ishara kubwa. Ishara kubwa ni kwamba Yesu alikuwa akiwapa mitume wito mpya. Walikuwa sasa sio kuwa tena wavuvi wa samaki, bali wavuvi wa roho za watu. Na kwamba kama watajaribu kufanya haya kwa nguvu zao wenyewe, wataishia kutokupata kitu. Lakini kama watafanya kwa amri ya Bwana, watapata matunda mengi. Hata kwa jinsi wasivyo dhani. 

Muujiza huu wa Yesu unaanza kufunua kwa mitume na kwetu pia juu ya wito wa kuhubiri habari njema ulimwenguni. Ufunuo huu ulikuja baada ya ufufuko, ambapo Yesu anawapa mitume maelezo wa kuchukua ujumbe wa ukombozi. Tunapaswa kuona katika muujiza huu juu ya wito wetu wa kuhubiri habari njema. Na tunapaswa kuona katika muujiza huu kutangaza habari njema kwa amri ya Yesu, katika hali yake na ndani ya mapenzi yake.

Mara nyingi wakristo wanakuja na mawazo mazuri ya jinsi ya kuhubiri Injili. Lakini ufunguo ni kujinyenyekesha sisi wenyewe mbele za Mungu na kutambua kwamba sisi hatuwezi kuhubiri habari njema bila kuongozwa na Yesu katika muelekeo sahihi. Tunapaswa kuisikiliza sauti yake na kuitika wakati anaelekeza. Kuhubiri habari njema ni jibu zuri la kuitika wito wa Yesu zaidi ya kitu chochote ambacho twaweza kufanya. Tunapo endelea na kipindi cha pasaka ni vizuri kila mtu akatafakari juu ya jukumu lake la kuhubiri habari njema. Tumuache Bwana aongee na sisi nasi tufuate muelekeo wake. Mungu anapenda kututumia sisi, tumpe nafasi.

Sala: Bwana, nipo tayari unitumie kuhubiri habari njema. Nisaidie kwa ujasiri niweze kuitika wito, na nisaidie nifuate kwa uaminifu muelekeo unao niongoza. Yes, nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 10, 2026


MASOMO YA MISA, APRILI 10, 2026
OKTAVA YA PASAKA, IJUMAA


SOMO 1
Mdo 4:1-12

Petro na Yohane walipokuwa wakisema na watu wale, makuhani na akida wa hekalu na Masadukayo wakawatokea, wakifadhaika sana kwa sababu wanawafundisha watu na kuhubiri katika Yesu ufufuo wa wafu. Wakawakamata, wakawaweka gerezani hata asubuhi; kwa kuwa imekwisha kuwa jioni. Lakini wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya watu waume ikawa kama elfu tano. Hata asubuhi wakubwa na wazee na waandishi wakakusanyika Yerusalemu, na Anasi Kuhani Mkuu, na Kayafa pia, na Yohane na Iskanda, na wote wale waliokuwa jamaa zake Kuhani Mkuu. Walipowaweka katikati wakawauliza, Kwa nguvu gani na kwa jina la nani ninyi mmefanya haya? Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab 118:1-2, 4, 22-27

(K) Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema,
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Israeli na aseme sasa,
Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
Wamchao Bwana na waseme sasa,
Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

Jiwe walilolikataa waashi
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Neno hili limetoka kwa Bwana,
Nalo ni ajabu machoni petu.
Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana,
Tutashangilia na kuifurahia.

Ee Bwana, utuokoe, twakusihi;
Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana;
Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru.



INJILI
Yn 21:1-14

Baada ya hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi wake, penye bahari ya Tiberia, naye alijidhihirisha hivi. Simoni Petro, na Tomaso aitwaye Pacha, na Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, na wana wa Zebedayo, na wengine wawili wa wanafunzi wake, walikuwapo pamoja. Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu. Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu. Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La. Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki. Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini. Na hao wanafunzi wengine wakaja katika mashua; maana hawakuwa mbali na nchi kavu; ila yapata dhiraa mia mbili; huku wakilikokota lile jarife lenye samaki. Basi waliposhuka pwani, wakaona huko moto wa makaa, na juu yake pametiwa samaki, na mkate. Yesu akawaambia, Leteni hapa baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi. Basi Simoni Petro akapanda chomboni, akalivuta jarife pwani, limejaa samaki wakubwa, mia hamsini na watatu; na ijapokuwa ni wengi namna hiyo, jarife halikupasuka. Yesu akawaambia, Njoni mfungue kinywa. Wala hakuna mtu katika wale wanafunzi aliyethubutu kumwuliza, U nani wewe? Wakijua ya kuwa ni Bwana. Yesu akaenda akautwaa mkate, akawapa, na samaki vivyo hivyo. Hiyo ndiyo mara ya tatu ya Yesu kuonekana na wanafunzi wake baada ya kufufuka katika wafu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 9, 2026



MASOMO YA MISA, APRILI 9, 2026
OKTAVA YA PASAKA, ALHAMISI

SOMO 1
Mdo 3:11-26

Siku zile, kiwete yule aliyeponywa alipokuwa akiwashika Petro na Yohane, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana. Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kana kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi, au kwa utauwa wetu sisi? Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe. Bali ninyi mlimkana yule Mtakatifu, yule Mwenye haki, mkataka mpewe mwuaji; mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake. Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote. Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda. Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo. Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani; ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu. Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, kama mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi. Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake. Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena, walihubiri habari za siku hizi. Ninyi mmekuwa watoto wa manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na baba zenu, akimwambia Ibrahimu, Katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa. Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 8:1, 4-8 

(K)Ee, Mungu, Bwana wetu; jinsi lilivyo tukufu jna lako duniani mwote.

Wewe, Mungu, Bwana wetu 
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! 
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; 
Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, 
Na binadamu hata umwangalie? (K)

Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; 
Umemvika taji ya utukufu na heshima;
Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; 
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (K) 

Kondoo, na ng'ombe wote pia; 
Naam, na wanyama wa kondeni; 
Ndege wa angani, na samaki wa baharini; 
Na kila kipitacho njia za baharini. (K)


INJILI
Lk 24:35-48

Wanafunzi waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate. 

Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu. 

Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho. Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo. Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake. Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa? Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa. Akakitwaa, akala mbele yao. 

Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

UFUFUKO: YESU YUPO HAI KATIKA EKARISTI TAKATIFU.



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Aprili 8, 2026
Oktava ya Pasaka

Mdo 3:1-10
Zab 105:1-4,6-9
Lk 24:13-35


UFUFUKO: YESU YUPO HAI KATIKA EKARISTI TAKATIFU.


Kutokea kwa Yesu kwa wafuasi wake wawili inaonekana kuleta hisia. Walikuwa wameshakuwa na matumaini kwamba yeye ni Masiha lakini aliuawa. Na tazama kuna wengine wanasema kaburi lake liko wazi. Kadiri ujumbe unapo endelea, Yesu “anawaelezea yote yaliosemwa kuhusu yeye katika maandiko”. Kwa njia hiyo wale wafuasi wakatambua huyu mtu wanaye ongea naye ana uelewa wa juu na hekima ya hali ya juu, hivyo wanamualika akae nao. Yesu alikaa na kuketi nyumbani kwao. Wakiwa pale, maandiko yanasema “alichukua mkate, akaubariki, akaumega na kuwapa. Kwa njia hiyo macho yao yalifumbuliwa, wakamtambua na ghafla akaondoka machoni mwao”. Kwanini Yesu, alificha wafuasi wake wasimtambue alikuwa nani, na kuwaruhusu wamtambue tu, na ghafla akaondoka machoni mwao?

Yesu alipenda wale wafuasi na sisi wote pia, kwamba huyu ambaye amefufuka kutoka wafu yupo hai kweli na kwamba tutamtambua katika kuumega mkate. Tutamtambua katika Ekaristi Takatifu. Kutokea kwa Yesu kwa wafuasi wake, ni wazi, kwamba Yesu anakuwa wazi katika Ekaristi Takatifu. Yesu yupo hai katika Ekaristi! Lakini inatuambia kuwa amejificha ndani ya Ekaristi Takatifu. Muunganiko huu wa kujificha na uwepo wake kweli unatupa muongozo mzuri wa Imani yetu.

Wafuasi walikuwa mbele ya Yesu lakini hawakuweza kumtambua. Pengine na sisi ni wazi pia. Hili ni kweli hasa wakati tukiwa kanisani wakati wa misa lakini pia kwa upande mwingine tunamtambua. Tunapaswa kujikita katika kumuona yeye, kumtumbua na kumwabudu. Tunapaswa kutambua uwepo wa Yesu mfufuka kati yetu. Yupo nasi sasa, anatupenda sisi, anaongea na sisi, na anatuita tumpende. Tumtafute na kusikiliza sauti yake. Unaweza kushangazwa ni kwa jinsi ghani anaweza kuwa.

Sala: Bwana, ninakushukuru kwa kunipenda mimi kila wakati. Ninaomba unipe macho ya Imani niweze kukuona daima katika Ekaristi Takatifu, na naomba unisaidie niweze kutambua uwepo wako katika kila tukio la maisha yangu. Ninakupenda, Bwana mpendwa.  Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.