Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

EKARISTI-UJUMBE MKUBWA WA UPENDO WA NYAKATI ZOTE.




“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya kila Jumapili
Jumapili, Juni 6, 2026
Juma la 11 la Mwaka wa Kanisa

Sherehe ya Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristu (Corpus Christi)

Kumb 8: 2-3, 14-16;
Zab 147;
1 Kor 10: 16-17;
Yn 6: 51-58.


EKARISTI-UJUMBE MKUBWA WA UPENDO WA NYAKATI ZOTE.

Sister Muagustiniani, sister Juliana wa Liège (Belgium) alipata maono ya kanisa likiwa chini ya mwezi unaongaa wenye kidoti kimoja cheusi. Doti hii ikionesha kutokuwepo kwa sherehe ya Ekaristi. Hii ilifanya baadaye kuwepo na sherehe ya Mwil na Damu ya Kristo ambayo iliwekwa kwenye kalenda ya Litirujia ya Kanisa mwaka 1264 chini ya Papa Urban wa IV. Je kulikuwa na haja ya kuwa na sherehe hii ya Ekaristi? Sherehe kama hii kawaida inatupa nafasi ya pekee ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uwepo wa Kristo kuwa nasi daima, ambaye yupo kweli katika Ekaristi Takatifu. Kwa upande mwingine, ni wakati wetu wakutafakari fumbo hili kubwa la upendo. Ekaristi Takatifu ni Sakramenti ambayo ni kilele cha Sakramenti zote, ndani yake Sakramenti nyingine zote huadhimishwa, kwasababu ni “Fumbo la mafumbo yote” na “Taji la Sakrament zote” sakramenti zote zinavishwa taji na Ekaristi Takatifu. Katika Ekaristi Takatifu hatupokei tuu neema bali tunampokea Bwana wa Neema.

Ekaristi Takatifu ni kilele cha sala sote na kuabudu kwetu. Hakuna njia nyingine ya kuwasiliana na Mungu, yenye undani na ukuu zaidi ya Ekaristi Takatifu. Hapa watu wawili (mtoaji na mpokeaji) wanakuwa katika umoja wa kweli, (ndani yake, naye ndani mwako). Tunapaswa kusali mara nyingi katika hali zote na sehemu yeyote kwasababu sala hizi zinatufanya tuunganike na Bwana na kujenga umoja naye. Lakini kwakweli, hakuna sala yeyote inayotoa muunganiko mkuu zaidi ya Ekaristi Takatifu. Hakuna yeyote wala chochote kinachopaswa kutufanya tushindwe kuwa wamoja na Kristo, na kwa njia ya umoja huu tupate nguvu tunayohitaji katika maisha yetu.

Jumapili hii tumekuja pamoja kuadhimisha Ekaristi Takatifu kwa roho ya furaha na mapendo. Kwa bahati mbaya kuna baadhi ya Wakatoliki wengi ambao hawaioni Ekaristi Takatifu katika hali tena. Idadi ya Wakatoliki wanao shiriki adhimisho la Ekaristi jumapili, baadhi ya sehemu inashuka kila mara. Misa sio sehemu ya maonesho, hawapati kile wanachotaka, watu wanapenda kitu kipya kila wakati na tena pengine chenye mtizamo wanaotaka wao. Ni ajabu utakuta Misa zinazo hudhuriwa mara nyingi ni, Jumatano ya Majivu, Jumapili ya Matawi, Jumapili ya pasaka na Noeli kwasababu kuna vitu ninaongezwa ndani yake kwa mfano, matawi, majivu, mishumaa nk. Wengi wanategemea Padre aweke utani kwenye mahubiri ili afanye watu wachangamke, wengine wanataka kwaya waimbe vizuri sana kwa sauti zenye kupendeza na pengine wacheze sana kwa midundo ya kisasa zaidi, vifaa bora zaidi vya muziki, wengine wanataka wasomaji wenye sauti nzuri zakupendeza masikioni mwao, viti vizuri vya kukaa, taa zenye mwanga mzuri wa kupendeza na vifaa vizuri vya sauti. Kwa kweli, haya yote ni mitazamo na matarajio. Mbaya zaidi, pengine wapo pia baadhi ya makuhani wamenaswa kwenye mtego huu. Badala ya kuwapa watu anachosema Mungu, anawapa watu wanachopenda kusikia na kuona. Kwa matokeo haya, neno la Mungu halihubiriwi kiaminifu na katika unabii na maana halisi ya Uwepo wa Mungu inapotezwa. Kumekuwako na ile hali ya mlalo (mwanadamu kwa mwanadamu) na kuacha ile hali ya wima (Mungu kwenda kwa Mwanadamu) ya liturujia.

Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikti XVI alikuwa akisisitiza kila wakati kwamba “Liturjia ni Tendo la Mungu”. Hatupaswi kusahau kwamba kiini cha liturujia na maadhimisho ya Sakramenti ni Mungu na sio mwanadamu. Aliendelea pia kusema; “Katekesi nzuri juu ya Ekarisiti ni Ekaristi yenyewe ikiadhimishwa vizuri”. Kufahamu na kuamini kwamba Yesu yupo kweli katika adhimisho la Ekaristi, tunapaswa wote tufanye jitihada kufanya adhimisho hili lenye maana na furaha. Bila kusahau kwamba Ekaristi haiwi Ekaristi kwasababu ya Imani ya padre au Muumini. Baada ya sala ya Ekaristi (Konsekratsio) Yesu anakuwa kweli chini ya Maumbo ya mkate na divai. Uwe na Imani au usiwe na Imani, Yesu anabaki kuwa Yesu katika maumbo hayo daima. Tunadaiwa kuwa na Imani ili tuweze kushirikiana na neema ya Mungu lakini hata tusipokuwa nayo haimaanishi utamzuia Yesu kuwa katika maumbo hayo. Tushirikiane naye kwa Imani ili tupate neema.

Ni Mtakatifu Maximiliani Kolbe ambaye aliwahi kusema kwa hakika kwamba, “Utimilifu wa Misa sio wakati wa mageuzo bali ule umoja mtu anaoupokea wakati wa komunyo”. Tunaamini kwamba Ekaristi ni sadaka ile ile aliyo itoa Yesu pale msalabani na sio kumbukumbu ya kihistoria ya tukio lililopita, na kwamba mkate na divai unakuwa kweli mwili na damu ya Kristo, na pia tunaamini kwamba Ekaristi ni sakramenti ya Upendo wa Mungu kwetu. Sakramenti inayo adhimishwa katika Imani hiyo inatusaidia tuweze kuuona umoja wa ndani wa mtu na Mungu. “Wakati tunatazama Msalaba, unatambua ni kwajinsi ghani Yesu alitupenda, na ukitazama Ekaristi Takatifu unatambua ni kwa jinsi ghani Yesu ananipenda sasa” (Mt. Teresa wa Kolkota). Je, wakati tunautazama mkate wa uzima, tunatambua tunamtazama Mungu? Leo tunaalikwa tutafakari na kutambua sio tuu vipaji vya ajabu tulivyopewa bali tuangalie wema na unyenyekevu wa yule aliyejitoa mwenyewe.

Katika sherehe hii ya Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, tufufue tena Imani yetu juu ya uwepo wa kweli wa Yesu katika Ekaristi Takatifu. Imani hii itujalie na kutusukuma kila wakati tuende kanisani kila jumapili tukiwa na furaha na hamu ya kukutana na Yesu ili maadhimisho ya Ekaristi yaweze kuwa yenye uhai na kweli nakuleta maana mbele ya Mungu. Kama kila wakati tutakuwa na haya mioyoni mwetu, itatusaidia kujitayarisha vyema- kimwili, kiakili na kiroho, ili tuweze kuadhimisha tukiwa wenye uchangamfu na kushiriki kikamilifu kwenye misa, nakumpokea Yesu katika komunyo Takatifu tukiwa tunastahili. Na hapo maadhimisho ya Ekaristi yataacha kuonekana kama tendo linalotuchosha nakuchukua muda wetu. Badala yake linakuwa kwetu kiini, chanzo na kilele cha maisha yetu kama Wakristo.

Sala: ninakuabudu wewe Mungu uliye jificha kweli katika Ekaristi, katika maumbo ya mkate na divai. Moyo wangu wote unajikabidhi kwako, kwa kukutafakari wewe unajikabidhi kwako. Asante Bwana kwakungarisha maisha yangu kila siku kwa chakula cha malaika. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 6, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 6, 2026

SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU


MWANZO:
Zab. 80:17
Nimewalisha kwa unono wa ngano na kuwashibisha asali itokayo mwambani.


SOMO 1
Kum. 8:2-3;14-16

Musa aliwaambia makutano: Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 147:12-15,19-20 (K) 12

(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Ndiye afanyaye amani mipakani mwako,
Akushibishaye kwa unono wa ngano.
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua.
aleluya. (K)


SOMO 2
1Kor. 10:16-17

Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


SHANG1LIO
Yn. 6:51

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; asema Bwana; mtu akila chakula hiki, ataishi milele.
Aleluya.


INJILI
Yn. 6:51-58

Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUTEMBEA KATIKATI YA MITEGO!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Juni 6, 2026
Juma la 9 la Mwaka


Tob 12:1, 5-15, 20;
Tob 13:2, 6-8;
Mk 12: 38-44.


MKARIMU KAMA MJANE MASKINI!


Somo la Injili linatoa picha Yesu akiwa na wafuasi wake, akiwa amekaa akiangalia watu wakiwa wanatoa sadaka hekaluni. Wale watu waliopenda kuonekana kuwa watu wa karimu walitoa nyingi sana. Lakini tazama anatokea mjane maskini, ambaye katika hali ya ukimya na unyofu anaweka senti mbili. Yesu mara moja anavutwa na kitendo hichi na anawaambia wafuasi wake. Aliweka senti mbili tu kiasi ambacho kilikuwa ni kidogo sana. Lakini tazama Yesu anamtangaza kwamba ametoa nyingi zaidi kuliko wengine. Yesu anaelezea tofauti juu ya utajiri wa kimwili na utajiri wa kiroho. Utajiri wa kiroho na ukarimu wa kiroho ni muhimu zaidi kuliko utajiri wa kimwili. Mjane huyu alikuwa maskini kimwili lakini alikuwa tajiri kiroho. Wale waliokuwa na kiasi kikubwa cha fedha walionekana kuwa matajiri wa kimwili lakini maskini wa kiroho kuliko mjane huyu.

Katika ulimwengu wa kutafuta mali tunaoishi katika, ni vigumu kuamini. Ni vigumu kugeuza dhamiri na kugeukia utajiri wa kiroho wenye Baraka nyingi. Tunapaswa kuwa kama huyu mjane maskini na kutoa yote tulionayo. Alitaka kuleta tofauti. Alitoa yote aliokuwa nayo.

Kila mtu anapaswa kuangalia ni kwa jinsi ghani hili linaingia katika maisha yake. Tunapaswa kuwa na hali ya ndani ya kuwa na ukarimu na hali ya kuachia. Kuanzia hapa, Bwana atakuonesha ni kwa jinsi ghani ya kutumia mali zetu kwa ajili ya faida ya uzuri wetu na kwa ajili ya wengine pia. Toa ulionayo na jinsi ulivyo kwake, naye ataelekeza moyo wako kadiri ya utukufu wake mkamilifu.

Sala: Bwana, ninaomba unipe moyo wa ukarimu na uondoe moyo wa ubinafsi kama yule mjane. Nisaidie mimi nitafute njia za kujitoa kabisa kwako, bila kushikilia mambo mengine nyuma yangu, na zaidi kutafuta utukufu wa kiroho katika ufalme wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUNI 6, 2026



MASOMO YA MISA JUNI 6, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 9 LA MWAKA


SOMO 1
2 Tim. 4:1-8

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake; lihubirini neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho. Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masi- kio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.

Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nime- ilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 71:8-9, 14-17, 22

Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa.

Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote. 
Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa;


Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako. 
Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo. 

Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu.
Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli. 


SHANGILIO
Mt 5:3

Aleluya, aleluya
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 
Aleluya


INJILI
Mk. 12:38-44

Yesu aliwaambia katika mafundisho yake: Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele katika karamu; ambao hula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu; hawa watapata hukumu iliyo kubwa.

Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa. Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.
-------------------------
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

FURAHIA NDANI YA BWANA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Juni 5, 2026
Juma la 9 la Mwaka

Mt Bonifasi, Askofu na Mfiadini 

2 Tim 3: 10-17
Zab 119: 157, 160, 161, 165, 166, 168
Mk 12: 35-37.


FURAHIA NDANI YA BWANA!


Sisi Wakristo tunafahamu kwamba Yesu ni Masiha, Mwana wa Daudi. “Mwana wa Daudi” jina linalo mwakilisha Yesu huku likitengeneza uti wa mgongo wa Injili. Katika Maamkio ya Bikira Maria alipokea ujumbe huu “Na Bwana Mungu atampa kiti cha Daudi Baba yake, na atatawala nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na Mwisho” (Lk 1:32-33). Yule Maskini aliyekuwa mwombaji alimwomba Yesu amponye, akisema “Yesu Mwana wa Daudi, unihurumie mimi” (Mk 10:48). Wakati Yesu alivyokuwa akiingia Yerusalemu walimshangilia wakisema “Mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, hosanna juu mbinguni” (Mk 11:10).

Lakini sio tu Mwana wa Daudi, yeye pia ni Bwana. Analionesha hili yeye mwenyewe kwa kunukuu zaburi ya Daudi 110. Mt. Petro, aliye shahidi wa ufufuko wa Bwana, aliona wazi kwamba Yesu amethibitiswa “Bwana wa Daudi”, kwasababu “ndugu zangu nina waambia kwa ujasiri kwamba Babu yetu Daudi alikufa na akazikwa na kaburi lake lipo hapa hadi leo…lakini Yesu ambaye ni Mungu alifufuka, ambao sisi ni mashahidi wake.” (Mdo 2:29-32).

Leo Yesu anajaribu kuwaelewesha Wayahudi kuhusu Masiha au Kristo. Masiha atakuwa Daudi mpya, akitawala juu ya Ufalme wake, lakini atatawala milele katika ufalme wa milele, kama Malaika Garieli alivyo tangaza kwa Maria (Lk 1:32-33; Is 9:7). Atakuwa Mwana wa Mungu kwa asili, na hivyo atakuwa Mungu mwenyewe, mwenye Umungu sawa na Baba.

“Umati mkubwa walisikia hili kwa shauku na furaha (Mark 12:37). Mafundisho ya Yesu yalileta furaha sana katika mioyo yao. “Je, mimi nina yarufahia maneno ya Yesu?” ni mara nyingi tunayaona maneno ya Yesu kama mzigo, au kuwa kikwazo kwa mambo ambayo tunataka kufanya katika maisha. Furaha katika Bwana ni kitu ambacho kinatufanya kukuwa zaidi kila siku. Tujiruhusu kufurahi katika Bwana na kufurahia uwepo wa maneno yake. Tukiwa “tumeiva vizuri” tutamtafuta yeye zaidi.

Sala: Bwana Yesu, Mwana wa Daudi, ninatamani kufurahia katika wewe. Nisaidie niweze kuacha mambo yote ya ulimwengu yanayo niweka mbali nawe. Nisaidie niweze kukutafuta wewe na neno lako daima. Jaza roho yangu na furaha yako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUNI 5, 2026

 



MASOMO YA MISA JUNI 5, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 9 LA MWAKA

KUMBUKUMBU YA MTAKATIFU BONIFASI, ASKOFU NE MFIADINI

SOMO 1 
2 Tim. 3 :10-17

Wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili; naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.

Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, Iafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 119 : 157, 160-161, 165-166, 168 (K) 165

(K) Wana amani nyingi waipendao sheria yako.

Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, 
lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
Jumla ya neno lako ni kweli,
na kila hukumu ya haki yako ni ya milele. (K)

Wakuu wameniudhi bure,
ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
Wana amani nyingi waipendao sheria yako, 
wala hawana la kuwakwaza. (K)

Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako, 
na maagizo yako nimeyatenda.
Nimeyashika mauasi yako na shuhuda zako, 
maana njia zangu zote zi mbele zako. (K)


SHANGILIO 
Zab. 111 :7, 8

Aleluya, aleluya, Maagizo yako yote, ee Bwana, ni amini, yamethibitika milele na milele. Aleluya.


INJILI 
Mk. 12:35-37

Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu, alijibu, akasema, Husemaje waandishi ya kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi? Daudi mwenyewe alisema, kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, hata niwawekapo adui zako kuwa chini ya miguu yako. Daudi mwenyewe asema ni Bwana; basi amekuwaje mwanawe? Na mkutano mkubwa walikuwa wakimsikiliza kwa furaha.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com. 

UPENDO WA AGAPE

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Alhamisi, Juni, 4, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 9 la Mwaka wa Kanisa

2 Tim 2: 8-15; 
Zab 25: 4-5, 8-10, 14; 
Mk 12: 28-34


UPENDO WA AGAPE!

Kwakusoma Injili tunaweza kufanya muktasari wa nafsi ya Yesu kwa neno moja tu, nalo ni UPENDO. Yesu anatuambia kwamba sheria zote zinaweza kufupishwa katika sheria mbili tuu. Ya kwanza kabisa ambayo ni muhimu sana ni upendo kwa Mungu usio na kikwazo chochote, ya pili ni matokea ya hiyo ya kwanza, kwasababu wakati mwanadamu anapendwa, Mungu anapendwa, kwasababu mwanadamu ameumwa kwa sura na mfano wa Mungu

Upendo ulimsukuma Yesu aweze kuwanyanyua wanyonge, kuwasaida waliotengwa, kuponya walioumizwa, kuwafanya huru wafungwa na akatoa maisha yake msalabani ili kutukomboa sisi kutoka utumwa wa dhambi. Upendo wa Mungu hauna masharti. Yesu kwa maneno na matendo yake anatuhimiza kutimiza na kutenda “UPENDO huu” kwaajili ya ukombozi wetu na ukombozi wa ulimwengu mzima. Na hiki ndicho kitambulisho chetu kama Wakristo wanaomfuata Yesu kwa uaminifu. Kwa namna hiyo tutakuwa wakristu wa kweli “kama Kristo”. Pengine tujiulize swali lingine ambalo hatujazoea sana kujiuliza, tunajua Mungu anatupenda wote bila ubaguzi. Je, ninampenda mwenzangu/jirani yangu kama Mungu anavyompenda?

Sala: Bwana; nisaidie niweze kuwa Mkristo wa kweli kwa kuishi na kutimiza Upendo usio na masharti wala kikomo. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA JUNI 4, 2026


MASOMO YA MISA JUNI 4, 2026

ALHAMISI, JUMA LA 9 LA MWAKA

SOMO 1
2Tim. 2:8-15

Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu. Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi. Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. Ni neno la kuaminiwa.

Kwa maana, kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia; kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi; kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.

Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao. Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

(K) Ee Bwana, unijulishe njia zako.

Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako,
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha. (K)

Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu,
Nakungoja Wewe mchana kutwa.
Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Wenye upole atawaongoza katika hukumu,
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)

Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli,
Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.
Siri ya Bwana iko kwao wamchao,
Naye atawajulisha agano lake. (K)

SHANGILIO
Yn. 8:12

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema, Bwana, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Aleluya.

INJILI
Mk. 12: 28-34

Mmoja wa waandishi alifika kwa Yesu akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza? Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja. nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.

Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye; na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhabihu zote pia. Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MIMI NI UFUFUO NA UZIMA!

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Juni, 3, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 9 la Mwaka wa Kanisa


2 Tim 1: 1-3, 6-12; 
Zab 122: 1-2; 
Mk 12: 18-27.


MIMI NI UFUFUO NA UZIMA!


Somo la kwanza la leo linatuonesha jinsi ghani Mtume Paulo alivyo elewa kwamba Injili inaweza kuhubiriwa kwa mataifa yote tu, kwa nguvu ya Yesu mfufuka. Kwa kujikita kwenye faida yetu, au vipaji vyetu au nguvu zetu wenyewe maisha yatakuwa kama balbu ya umeme isiokuwa na umeme. Hitaji la sasa nikumtumikia Bwana wetu kwa moyo safi tukijikita katika ahadi zake za uzima wa milele alizo tuachia Yesu mwenyewe. 

Katika somo la Injili Yesu anatuambia ni wale tuu wanao elewa maandiko matakatifu na nguvu ya Mungu wataamini katika ufufuo wa wafu. Hili lilikuwa jibu kwa swali lililoulizwa na Masadukayo. Yesu anawajibu kwamba mambo ya ndoa ni mambo ya dunia hii. Baada ya kufa tunakuwa kama malaika wa mbinguni. Yesu kwa njia ya ufufuko wake ameyashinda mauti na kutupatia uzima wa milele. Yeye ni Bwana wa uzima. Maisha yetu yapaswa yamwelekee yeye zaidi, tukitazamia lililo kubwa zaidi kuliko maisha yetu ya dunia, tukijua uzima wa milele ndio lengo letu baada ya maisha haya. Tusifungwe na malimwengu tushindwe kumuona Mungu baada ya maisha haya. Kwa mfano wa mfiadini Mt.Yustino tujifunze kutoa maisha yetu kwa Kristo mfufuka ili tuweze kupata lile taji lisilofifia (uzima wa milele).

Sala. Bwana Yesu, hatuweze kuwa Wakristo wenye kuzaa matunda mema kama tutajitenga nawe. Tunaomba utusaidie tuweze kupata kitambulisho chetu, kuishi kwetu na maisha yetu kutoka kwako. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA JUNI 3, 2026



MASOMO YA MISA JUNI 3, 2026
JUMATANO, JUMA LA 9 LA MWAKA

KUMBUKUMBU YA WATAKATIFU KAROLI LWANGA NA WENZAKE, WAFIDIANI

SOMO 1
2Tim. 1:1-3, 6-12

Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa ajili ya ahadi ya uzima ulio katika Kristo Yesu; kwa Timotheo, mwanangu mpendwa. Neema na iwe kwako, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

Namshukuru Mungu, nimwabuduye kwa dhamiri safi tangu zamani za wazee wangu, kama vile nikukumbukavyo wewe daima, katika kuomba kwangu usiku na mchana.

Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu; ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele, na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu; aliyebatili mauti, na kuufunua uzima na kutokuharibika, kwa ile Injili; ambayo kwa ajili ya hiyo naliwekwa niwe mhubiri na mtume na mwalimu.

Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, wala sitahari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba aweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hata siku ile.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 123:1-2 (K) 1

(K) Nimekuinulia macho yangu, ee Bwana.

Nimekuinulia macho yangu,
Wewe uketiye mbinguni.
Kama vile macho ya watumishi
Kwa mkono wa bwana zao. (K)

Kama macho ya mjakazi
Kwa mkono wa bibi yake;
Hivyo macho yetu humwelekea Bwana, Mungu wetu.
Hata atakapoturehemu. (K)

SHANGILIO
Lk. 8:15

Aleluya, aleluya.
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno la Mungu, na kulishika.
Aleluya.

INJILI
Mk. 12:18-27

Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, walimwendea Yesu, wakamwuliza na kusema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao. Basi kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao. Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika; hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye. Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.

Yesu akajibu, akawaambia, Je! hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu? Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni. Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahi- mu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.