Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MUNGU ASIYE JULIKANA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Mei 13, 2026 
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 17: 15, 22-18:1;
Zab 148: 1-2,11-14;
Yn 16:12-15.

MUNGU ASIYE JULIKANA!

Katika somo la kwanza, Mt. Paulo anawavuta watu wa Atheni katika utambuzi kuhusu altare zao walizojenga kwa “Mungu asiye julikana”. Anawaeleza kwamba amekuja kuwafunulia ukweli juu ya huyu Mungu asiye julikana wanaye mwabudu waweze kumtambua yeye ni nani. Wakati mwingine tunamtazamia Mungu ambaye tunataka kumuona au kumshika. Wakati mwingine tunajikuta tunakimbilia mara nyingi sehemu ambazo tunaona Mungu amechorwa katika picha ya kibinadamu. Lakini tunapaswa kutambua kwamba Mungu wetu ni Mungu aliyefichika (Is 45: 15). Amefichika katika ufahamu wetu. Katika wimbo wa kuabudu tunaimba ‘Yafichika machoni Imani yaona’, fahamu haiwezi kutambua fumbo hili bali Imani inatusaidia.

Katika Injili Yesu anatufunulia kuhusu Utatu Mtakatifu. “Roho atakayekuja atachukua kila kilicho changu” (Yn 16:14). “kila alicho nacho Baba ni changu” (Yn 16: 15). Hapa umoja wa Utatu Mtakatifu na asili ya nafsi tatu unafunuliwa.

Hii inamaana kwamba tunapaswa kuwa wazi katika maisha yetu juu ya nguvu na uwepo wa Roho Mtakatifu, yeye aliyebeba ukweli wote. Roho Mtakatifu anapaswa kuwa hai ndani mwetu, akifunua ukweli. Na tukiwa wazi kiakili na mioyo yetu kwa Roho Mtakatifu, tutakuwa watu wakutamani ukweli. Tutakuwa na hamu ya kuelewa vitu ambavyo vitafungua mioyo yetu. Tutakuwa na uwezo wakutazama mambo katika hali ya upya. 

Wewe ni wazi kiasi ghani katika uweli? Ni mara ngapi katika hali ya kweli unakumbatia yote ambayo Mungu ameyafunua kwako? Jifungue zaidi kwa Roho Mtakatifu na tafuta yote ambayo anayafunua kwako. 

Sala: Roho Mtakatifu, ninaomba uje utawale maisha yangu. Nifundishe na kuniongoza katika ukweli wote. Roho Mtakatifu, Bwana Mtakatifu, Baba mwenyewe huruma, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 13, 2026


MASOMO YA MISA, MEI 13, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMATANO

SOMO 1 
Mdo. 17 :15, 22-18:1

Siku zile, wale waliomsindikiza Paulo wakampeleka mpaka Athene; nao wakiisha kupokea maagizo kuwapelekea Sila na Timotheo, ya kwamba wasikawie kumfuata, wakaenda zao. Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini. Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, kwa Mungu asiyejulikana.

Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua. Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono; wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote. Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu. Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wetu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu. Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu. Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo. Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha. Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, Mwareopago, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao. Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 148:1-2, 11-14

(K) Utukufu wako unajaza mbingu na ulimwengu. 
Au: Aleluya.

Aleluya. 
Msifuni Bwana kutoka mbinguni;
Msifuni katika mahali palipo juu.
Msifuni. enyi malaika zake wote;
Msifuni, majeshi yake yote. (K)

Wafalme wa dunia, na watu wote,
Wakuu, na makadhi wote wa dunia.
Vijana waume, na wanawali,
Wazee, na watoto. (K)

Na walisifu jina la Bwana,
Maana jina lake peke yake limetukuka;
Adhama yake i juu ya nchi na mbingu. (K)

Naye amewainulia watu wake pembe,
Sifa za watauwa wake wote;
Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. (K)


SHANGILIO 
Ufu. 1 : 5

Aleluya, aleluya, 
Ee Kristo, yu shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. 
Aleluya.

INJILI 
Yn. 16:12-15

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Bado ningali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa. Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza mimi; kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari. Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasha habari.

Neno la Bwana... Sifa kwako ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MAISHA NDANI YA ROHO MTAKATIFU

 


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Mei 12, 2026
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 16: 22-34;
Zab 138: 1-3,7-8 (K.7);
Yn 16:5-11.


MAISHA NDANI YA ROHO MTAKATIFU


Katika somo la kwanza, tunakutana na Paulo akiwa amejazwa na Roho Mtaktifu akisifu na kumshukuru Mungu kwa kumpa yeye pamoja na ndugu zake kushiriki katika mateso ya Kristo. Hii ni neema kamili ya Roho Mtakatifu ilikuwa ikifanya kazi ndani mwao. Akiwafundisha wafanye mema na kwa wakati muafaka. Hata milango ya gereza ilipo funguka yeye na wenzake hawakukimbia. Ushuhuda huu na wa wenzake ulimfanya yule mlinzi wa gereza kubadili maisha yake yeye na familia yake. Wanaongozwa na Roho Mtakatifu kuokoa maisha ya yule mlinzi wa Gereza, aliyekuwa sababu ya mateso yao pia.

Katika somo la Injili, mioyo ya wafuasi ilijazwa na huzuni, lakini pia walikuwa wakijitahidi kuamini kile ambacho Yesu alikuwa akiwaambia.Yesu aliwaambia kwamba atapaa kwenda kwa Baba yake na kwamba ilikuwa ni vizuri yeye aondoke. Kwasababu akiondoka atamtuma Msaidizi kwao.

Katika hali yya kibinadamu, ilikuwa vigumu kwa wafuasi kumwacha Yesu aondoke tu kwasababu ya wao kumzoea na kuongea naye kila wakati. Ni hakika kwamba walimkosa sana kuendelea kumuona kwa macho yao kama walivyo zoea kumuona, kumshika na kumsikia akiongea. Lakini Yesu aliweka wazi kwamba hata kama anaondoka bado atakuwa nao daima. Na kwamba atamtuma Msaidizi Roho Mtakatifu ambaye atakuwa pamoja nao na kuwaongoza katika ukweli wote, akiwapa nguvu, na kuwafundisha ukweli wote. Watakuwa wawakilishi wake sasa ulimwenguni kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Hatukuwa na bahati ya kumuona Yesu kama wanafunzi wake walivyokuwa. Lakini tuna bahati ya kuwa nasi kila siku. Na tuna bahati ya kupokea utimilifu wa Roho Mtakatifu. Tumepokea kipaimara, lakini tunaweza kushindwa kumruhusu Roho Mtakatifu akae ndani yetu na kutufanya wapya. Tunapo karibia sikukuu ya Pentekoste, kubali na jinyenyekeshe na kukiri kwamba unamhitaji Roho Mtakatifu aweze kuwa ndani ya maisha yako. Amini kwamba Yesu anataka umpokee yeye katika Utimilifu. Na wala usiwe na wasi wasi kuruhusu muunganiko huu utokee kwako. Tunapaswa kuisikiliza sauti ya Roho Mtakatifu ambaye yupo ndani mwetu na ambaye anajaribu daima kutuelekeza kwenye ukweli.

Sala: Roho Mtakatifu, naomba uje ndani mwangu. Ninaomba unisaidie kuwasha moto wako katika maisha yangu. Ninakuomba nikupokee wewe ambaye uliahidiwa na Yesu katika utimilifu wote. Roho Mtakatifu, Yesu mwana wa Mungu, Mungu Baba mwenye huruma, najiaminisha chini yako. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 12, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 12, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMANNE

SOMO 1
Mdo. 16:22-34

Siku ile, pale Filipi, wenyeji waliwakamata Paulo na Sila, wakawaendea, makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora. Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana. Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale. Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.

Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati huo huo. Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 138; 1-3, 7-8 (K) 7

(K) Utanyosha mkono, Ee Bwana, utaniokoa. aur Aleluya.

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,
Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, (K)

Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Siku ile niliyokuita uliniitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu,
Na mkono wako wa kuume utaniokoa.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)


SHANGILIO 
Kol 3:1

Aleluya, aleluya, 
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, amcketi mkono wa kuume wa dunia. 
Aleluya.


INJILI 
Yn 16:5-11

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi? Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu. Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi; kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

ROHO MTAKATIFU: MSAIDIZI




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Mei 11, 2026.
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 16: 11-15;
Zab 149: 1-6, 9;
Yn 15:26 - 16:4.

ROHO MTAKATIFU: MSAIDIZI

Kanisa lenye msingi wake kwa Yesu linaongozwa na Roho Mtakatifu tangu Pentekoste. Mtakatifu Paulo na wengine walihubiri Injili ya Yesu. Sehemu yeyote lilipo hubiriwa neno la Mungu, Roho Mtakatifu ndiye aliyesababisha wongofu wa mioyo ya watu. Lidia alimsikia Paulo na wengine wakihubiri Injili ya Yesu. Alifungua moyo wake kwa Bwana. Ina maana kwamba kwanza kabisa alifungua masikio yake akamsikiliza Yesu, naye Roho Mtakifu akamtia nguvu. Moyo wake na utayari wake wakukaribisha ujumbe wa Kristo moyoni mwake haukuwa tuu kwaajili yake binafsi bali ulibadilisha nyumba yake yote. 

Wafuasi walimsikiliza Yesu akiwaambia kwamba watafukuzwa katika masunagogi na hata kuuwawa, maneno haya hawakuyaelewa. Huenda iliwasumbua kidogo, lakini mara moja kwenda kwa mambo mengine ili wasiyawaze zaidi na kuwasumbua. Na bila shaka mitume walipo adhibiwa na Mafarisayo na waandishi, waliyakumbuka maneno haya ya Yesu. Walitambua walipaswa wawaongoze kwenda kwa Mungu, wana sababisha adha katika maisha yao. Watakuwa walijaribiwa katika hali ya kutaka wapoteze Imani yao. Lakini Yesu alitabiri jaribu hili kuu litakuja, lakini akawaonya na kuwaambia kuwa yatakuja. 

Lakini kinacho vutia ni kile ambacho Yesu hakusema. Hakuwaambia kwamba watapigana na kurudisha, kuanza fujo, au mapinduzi yeyote nk. lakini tunamuona Yesu akiwaaambia Roho Mtakatifu ndiye atakaye shughulika na hayo. Atawaongoza na kuwawezesha kumshuhudia Yesu. Kuwa mkristo maana yake umekubali mateso.
Roho Mtakatifu anaitwa “Msaidizi”, huwafariji waamini, hasa wakati wauhitaji na mateso. Pia, wakati mwingine kile tunacho dhani ni ukweli kinaweza kisiwe ni ukweli kabisa, kinaweza kuchanganywa na uongo. Yeye pia ni “Roho wa Ukweli”, anayetuonyesha ukweli- kwamba ni Yesu aliyesema ‘mimi ni ukweli, njia na uzima’ (Yn 14:6). Leo tujiulize kama maisha yetu yanaongozwa na Roho Mtakatifu?

Sala: Bwana, ninapo elemewa na mzigo wa ulimwengu au mateso nipe Amani ya mwiili na Roho. Ninaomba unipe nguvu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili niweze kuwa shahidi wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 11, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 11, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMATATU

SOMO 1
Mdo. 16:11-15

Tuling’oa nanga kutoka Troa, tukafika Samothrake kwa tanga moja, na siku ya pili tukafika Neapoli; na kutoka hapo tukafika Filipi, mji wa Makedonia, mji ulio mkuu katika jimbo lile, mahali walipohamia Warumi; tukawa katika mji huu, tukikaa siku kadha wa kadha. Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.

Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambave moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo. Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 149 :16, 9 (K) 4

(K) Bwana awaridhia watu wake. au Aleluya.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,
Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba wenye upole kwa wokovu. (K)

Watauwa na waushangilic utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wote. (K)


SHANGILIO 
Rum. 6 : 9

Aleluya, aleluya, 
Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena wala mauti haimtawali tena. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 15:26-16:4

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia. Nanyi pia mnashuhudia, kwa kuwa tangu mwanzo mmekuwapo pamoja nami.

Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

ROHO MTAKATIFU, MSAIDIZI!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 10, 2026
Dominika ya 6 ya Pasaka

Mdo 8: 5-8, 14-17;
Zab 65: 1-7, 16, 20;
1 Pet 3: 15-18;
Yn 14: 15-21.


ROHO MTAKATIFU, MSAIDIZI!

Kwa, jumapili ya sita ya Pasaka tunaanza kufungua macho yetu na kuanza kutazamia ujio wa Roho Mtakatifu. Yesu anaongea kuhusu kumuomba Baba alete msaidizi mwingine awe nasi daima. Huyu msaidizi ni Roho Mtakatifu.

Katika somo la kwanza tunasikia kuhusu Filipo. Anafika Samaria na anaanza kuhubiri Injili na kubatiza wote waliopokea Imani. Roho Mtakatifu aliwaimarisha wamisionari hawa wa kwanza kwa kuwapa nguvu katika maneno yao kwa kudhihirisha uwepo wake kwa ishara. Watu wa mji ule walibadilika na wakajazwa na furaha. Sehemu ya pili ya somo inamuonesha Petro na Yohane wakiwatembelea wabatizwa huko Samaria. Mitume hawa wawili waliwawekea mikono ili Roho Mtakatifu aweze kuwa juu yao. Walishangazwa Wasamaria waliobatizwa na Filipo walikuwa hawajapokea Roho Mtakatifu. Uwepo wa Mungu ulikosa ishara ya njee ambayo ilikuwepo wakati wa Kanisa la mwanzo. Luka anaunganisha matukio haya mawili, kutuonesha kwamba kila sehemu Injili ilipo hubiriwa kuna jumuiya mpya inayokuwa. Lakini, hawakuhitaji kukuwa, kuendelea na kuishi katika hali ya pekee kabisa na inayo jitegemea. Ni vizuri walianzisha umoja wa kuunganisha na kanisa nzima. Ni Roho pekee atakaye jidhihirisha ndani yao wote.

Katika somo la Injili tunaona ujumbe wa wosia wa Yesu. Mitume wanahuzuni kwababu ya kuondoka kwa Yesu, na wana ahidiwa msaidizi mwingine Yesu anaeleza wazi kwamba Roho Mtakatifu watampokea tu wale waIe walioungana naye, katika mipango yake na katika kazi zake za upendo. Huyu Roho anaitwa kwa majina mawili. Mfariji na Roho wa kweli.

Msaidizi ni neno linalo onesha kwamba ni yule aliyeitwa ili aweze kuambatana. Hapo kale kulikuwa hamna kuanzishwa kwa sheria, kila mtu alipaswa kujitetea na kujilinda mwenyewe. Ilitokea mara chache kwamba, mtu hana kosa, lakini mtu haweze kudhihirisha kwamba hana hatia. Kwake kilicho salia ni tumaini moja tu: kwamba mtu mmoja wa heshima atatokea katika mkutano aongee bila kusita na kutoa ushahidi wa kumtetea. Ishara hii ni sawa na kufunguliwa gerezani. Na wala hakuna yeyote atakaye kushutumu tena. Huyu anaitwa “Msaidizi” maana yake yule anayeitwa ili aweze kuwa karibu na mwingine ambaye amepata matatizo. Yesu aliwahidia wafuasi wake msaidizi, kwasababu tayari wamesha mpata wa kwanza ambaye ni Yesu mwenyewe. Roho Mtakatifu ni Msaidizi kwasababu anawasaidia Wafuasi katika vita dhidi ya malimwengu hasa maovu. Yohane anawakumbusha wafuasi juu ya ukweli huu ili wanapo kutana na ugumu katika maisha, wasikatishwe tamaa, kupoteza tumaini, bila kupoteza Amani ya moyo na furaha. Wafuasi waliamini juu ya usaidizi wa Roho Mtakatifu. Wana amini nguvu ya Msaidizi huyu na kwamba hatashindwa.

Roho wa ukweli anafanya kazi katika huduma ya kweli. Ujumbe wa Yesu umeelekezwa kwa watu wote. Unapaswa kuhubiriwa mpaka miisho ya ulimwengu. Roho Mtakatifu anadhihirisha kwamba hatashindwa, na wala hayata fafanuliwa vibaya na kuharibiwa, mafundihso ya Kristo. Yeye haondoi tu makosa yanayo fanywa na kukosewa katika kurithisha ujumbe wa Yesu. Anawatambulisha wafuasi katika ukweli wote. Yeye yupo katika kuwaelekeza wafuasi katika kutambua ukweli wote. Hatasema kitu kingine kipya kinacho pinga ujumbe wa Yesu. Atasaidia katika kuendeleza ujumbe wa Yesu mpaka miisho yote. Kazi ya Wakristo nikubaki imara katika kazi hii ya Roho Mtakatifu ambaye daima anafunua mambo mapya. Yeye kwa asili ndiye anaye ufanya upya uso wa Nchi (104:30). Ni dhambi juu ya Roho Mtakatifu kupinga kufanywa upya, kukataa kufanya mabadiliko katika maisha ya jumuiya, ambayo yanawaleta watu karibu na Yesu na wandugu, ambayo huongeza furaha na amani ambayo yanawafanya watu wasali vizuri na kufanya moyo uwe huru na kuondoa hofu zote.

Kama tupo wazi kwa ujio wa Roho Mtakatifu, tutapokea Msaidizi mzuri kabisa katika maisha yetu yote. Roho Mtakatifu ndiye msaidizi tunaye mhitaji. Kuzama ndani ya Roho Mtakatifu inatufanya tujazwe na neema zote katika maisha. Sali sala ya Roho Mtakatifu na kutarajia kusherekea dominika ya Pentekoste jumapili mbili zijazo.

Sala: Ee, Mungu, wewe ambaye kwa Roho Mtakatifu, unaongoza Roho za Waamini wako, jalia kwa Roho huyo huyo, tuweze kuwa wakweli na wenye hekima na kufurahia faraja yake, kwa Njia ya Kristo Bwana wetu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 10, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 10, 2026
DOMINIKA YA 6 YA PASAKA


MWANZO:
Isa. 48:20
Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni, Bwana amelikomboa taifa lake, aleluya.


SOMO 1
Mdo. 8:5-8, 14-17

Filipo alitelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo. Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifa- nya. Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na wratu wengi waliopooza, na viwete, wakaponywa. Ikawa furaha kubwa katika mji ule.

Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohane; ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu; Kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu. Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 66 :1-7, 16, 20, (K) 1

(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote, au: Aleluya.

Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Imbeni utukufu wa jina lake,
Tukuzeni sifa zake.
Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! (K)

Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,
Naam, italiimbia jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu;
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)

Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tulikomfurahia.
Atawala kwa uweza wake milele. (K)

Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu,
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)



SOMO 2
1 Pet. 3 :15-18

Mwe tayari sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo. Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikrwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.

Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Yn. 14:23

Aleluya, aleluya,
Yesu alisema: Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake. Aleluya.



INJILI
Yn. 14 :15-21

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Mkinipenda, mtazishika amri zangu. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.

Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai. Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu. Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUKUTANA NA MATESO



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Mei 9, 2026
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 16: 1-10;
Zab 100: 1-3,5 (K. 1);
Yn 15: 18-21.


KUKUTANA NA MATESO

Mkristo kwa Sakramenti ya Ubatizo ni mmisionari. Anaitwa kushirikisha Habari Njema kwa kila mtu . katika ubatizo, Mkristo hufufuka kutoka katika hofu ya kifo, na kwenda kwenye utukufu wa uzima wa milele. Sisi sio watu tuliofungwa na dunia bali watu tuliofungwa na Mbinguni. Na hii safari ya kwenda mbinguni sio rahisi, kwasababu thamani na hali ya maisha ya Kikristo ni tofauti na hali ya kawaida ya kufikiri. 

Ni rahisi kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa karibu na Yesu ni kadiri hiyo hiyo tutakavyo pendwa na kueleweka na Ulimwengu. Tunadhani kwamba kila mtu atapendezwa na kuvutwa na utakatifu wetu na kuwa watu wazuri kwetu. Lakini sivyo. Tukiangalia maisha ya Yesu, tunatambua kuwa haikuwa hivyo. Alikuwa wazi ni mkamilifu kwa kila kitu. Lakini, walimtenda vibaya na kumsulubisha. Alishikwa na kupigwa na kutukanwa na kuhukumumiwa kifo. 

Kama tungekuwa pale, tungeweza kushangazwa sana, na kuchanganyikiwa. Tunaweza kufikiri kwamba Yesu alikosea na hivyo kupoteza matumani kwake. Lakini mpango wake ulikuwa mkamilifu kwa kila njia na mpango wake ulikuwa katikati na kumfanya yeye kuvumilia dhuluma za uongo na kuteswa. Na kwa uhuru kukubali kushutumiwa, aliikomboa dunia. 

Ukristo ni dini inayo onewa kuliko zote duniani. Asimilia kumi ya wakristo ulimwenguni wananyanyaswa na kuonewa kwasababu tu ya imani yao. Kunyanyaswa na kuonewa kunaleta hofu na uchungu. Lakini sio kitu ambacho tunapaswa kukikimbia. Hatupaswi kupoteza matumaini yanavyotokea haya. Kwanini? Kwasababu manyanyaso ni ishara wazi tunafuata njia sahihi ya Yesu. Tumeungana na Yesu zaidi katika njia ya kuonewa na kudhulimiwa kuliko hata tunavyofikiri. Ufunguo ni kutambua kwamba Mungu atatumia madhulumu yote kuwa furaha yetu kama tutamruhusu. Na tutamrushu ayatumie kwa kuleta mema kama tutajikabidhi kwake kwa uhuru kabisa. Majibu yetu yanapaswa kuwa “furahi na kushangilia” kwani tumekuwa sahihi katika kufuata njia ya Bwana wetu, Mwana wa Mungu. 

Leo tutazame katika hali yeyote ya kuonewa na kudhulumiwa au kukosewa haki tunayo ipata kwasababu ya Imani yetu na kushika Injili. Tuwaombee pia Wakristo wanaodhulumiwa huko Syria, Misri, China, Pakistani, India nk. 

Sala: Bwana, nina kabidhi kwako yale yote yanayo niangusha chini. Ninatoa sadaka yote ninayo pokea kwa kuwa mtumishi na mfuasi wako. Ninaomba nisikuige wewe tu katika mateso yako, bali kutii mapenzi yako daima. Yesu, nakuamini wewe. Amina. 

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 9, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 9, 2026
JUMA LA 5 LA PASAKA, JUMAMOSI


SOMO 1 
Mdo 16:1-10

Siku zile, Paulo alifika Derbe na Listra na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio. Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani. Basi walipokuwa wakipita kati ya miji ile, wakawapa zile amri zilizoamriwa na mitume na wazee walioko Yerusalemu, ili wazishike. Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.

Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia, wakajaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemka Troa. Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie. Basi alipo- kwisha kuyaona vale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia. kwa kuwa tuliena hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATI KATI 
Zab. 100 :1-3, 5 (K) I

(K) Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote. au: Aleluya.

Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yole.
Mtumikieni Bwana kwa furaha.
Njoni mbelc zake kwa kuimba; (K)

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake:
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)


SHANGILIO 
Yn. 20-29

Aleluya, aleluya, 
Wewe Toma, umesadiki kwa kuwa umeniona, 
wa heri wale wasioona wakasadiki. 
Aleluya,


INJILI 
Yn 15 : 18-21

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia. Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu. Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.