Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

YESU, MWANGA KWA ULIMWENGU!




“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Aprili 29, 2026. 
Juma la 4 la Pasaka


Mdo 12:24-13:5;
Zab 67:2-3,5-6,8 (K. 4);
Yn 12:44-50.


YESU, MWANGA KWA ULIMWENGU!


Kumfahamu Yesu ni kumfahamu Baba pia. Ukweli ni kwamba uwepo wa Baba umefunikwa kama Umungu wa Kristo ulivyo funikwa. Ingawaje hatuna uzoefu wa kumuona Yesu akitembea kama wale wafuasi wa kwanza walivyo muona, tunakutana na ukweli huo huo katika Ekaristi Takatifu. Wakati tunapo ingia kanisani na kupiga goti kuelekea Tabernakulo, ni vizuri kuwa na uelewa na kufahamu kuwa tupo mbele ya uwepo wa Mungu Mwana. Na kwa njia hiyo tupo pia mbele ya uwepo wa Mungu Baba! Uwepo wao ni wazi na hakika. Ni kwasabau tu wamefichwa kutoka katika milango yetu mitano ya fahamu. 

Katika Injili, Yesu anakuja kama nuru ili tusiwe tena kwenye giza. Anakuja kwa lengo hili: tumuamini yeye na kuwa na ukweli na uzima. Zaburi ya 27 mstari wa 1, unasema “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu”. Kama ilivyo mwanga wa kawaida hufunua kile kilicho fichwa kwanye giza, vivyo hivyo Neno la Mungu huleta nuru ili tuweze kutambuaa ukweli ulio fichika ndani ya Ufalme wa Mungu. Kama nuru, huleta furaha na uzima kwa wengine. Inafanya mbegu ya imani ikue ndani yetu, ili tuweze kushiriki furaha ya Mungu na uzima na wengine. Sisi mara nyingi tunachagua kubaki kaburini kama Mafarisayo bila kufufuka. Lakini Yesu ni mlango wa uzima wa milele. Kwani Yesu ni uzima na ufufuo na wote wale wanao mwamini watakuwa na uzima wa milele. 

Sala: Bwana, nisaidie niweze kukuelewa wewe na kukupenda wewe na katika uhusiano huo niweze kumfahamu na kumpenda Baba na Roho Mtakatifu. Bwana, ninaomba wewe uwe mwanga ambapo kwa njia yako niweze kukuona wewe na ulimwengu. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 29, 2026




MASOMO YA MISA, APRILI 29, 2026
JUMATANO, JUMA LA 4 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 12:24-13:5

Siku zile, Neno la Bwana likazidi na kuenea. Na Barnaba na Sauli, walipokwisha kutimiza huduma yao, wakarejea kutoka Yerusalemu, wakamchukua pamoja nao Yohane aitwaye Marko.

Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.

Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro. Na walipokuwa katika Salami waklihubiri neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 67:1-2, 4, 5, 7 (K) 3

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu,
Watu wote na wakushukuru. au Aleluya.

Mungu na atufadhili na kutubariki,
Na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
Wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

Mataifa na washangilie,
Naam, waimbe kwa furaha,
Maana kwa haki utawahukumu watu,
Na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

Watu na wakushukuru, Ee Mungu,
Watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
Miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)


SHANGILIO
Yn. 10:14

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi mchungaji mwema,
Nao walio wangu nawajua, nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.


INJILI
Yn. 12:44-50

Siku ile Yesu alipaza sauti, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka. Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenipeleka. Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani. Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu. Yeyey anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumu siku ya mwisho. Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema. Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

IMANI NI LUGHA YA KUMFAHAMU MUNGU!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Aprili 28, 2026,
Juma la 4 la Pasaka.

Mdo 11:19-26;
Zab 87:1-7 (R. 117:1);
Yn 10:22-30



IMANI NI LUGHA YA KUMFAHAMU MUNGU!


Katika somo la kwanza Barnaba anaona Roho Mtakatifu akifanya kazi ndani ya watu wa Antokia na hivyo anawatia moyo na kuwapa nguvu “Wakristo”. Katika somo la Injili, Wayahudi wanakataa kumkaribishi Yesu. Wanamuuliza “kama wewe ni Kristo tueleze wazi”. Na Yesu anajibu kwamba, “nime waambia lakini hamkusadiki”. Je wewe unasadiki Yesu ni nani kwetu? Je tupo wazi kwa kazi ya Roho Mtakatifu?

Pengine umemtaka Mungu ashuke kutoka mbinguni aje akupe majibu wazi ya kwanini baadhi ya mambo yapo kama yalivyo au kama yanavyo tokea? Au kukupa majibu wazi ya maswali yako. Lakini hafanyi hivyo. Anafanya hivyo katika hali ya njia yake kamili kwa lugha yake kamili. Ni kwa lugha ya Imani na hii inahitaji kujikabidhi kwa Mungu kabisa na mapenzi yetu yote ili tuweze kusikia na kuelewa. Hii ndio njia ya kweli ya kuongoka na kuwa katika njia ambayo Mungu anataka sisi tuwe. Tukitegemea akili na utashi wetu wenyewe, tutashindwa kuona uwepo wa Mungu, na kama tutataka akili yetu itoe majibu yote, ni wazi kwamba tutafikia mahali pakuona hamna haja ya Mungu kwasababu tunajitosheleza kwa akili zetu. Imani yaweza kutupa majibu ambayo akili zetu haziwezi kutambua.

Sala: Bwana, mara nyingi nimeshindwa kukusikiliza wewe na kukuelewa kwa njia ya zawadi ya Imani. Mara nyingi nimependa kupata majibu marahisi kwa maswali magumu. Nisaidie niweze kukuwa katika uvumilifu ili niweze kukufahamu na kukuruhusu kuwa Mchungaji wangu. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 28, 2026





MASOMO YA MISA, APRILI 28, 2026
JUMANNE, JUMA 4 LA PASAKA
KUMBUKUMBU YA BIKIRA MARIA WA FATIMA
 

SOMO 1
Mdo 11:19-26

Siku zile, wale waliotawanyika kwa sababu ya ile dhiki iliyotukia kwa habari ya Stefano, wakasafiri hata Foinike na Kipro na Antiokia, wasilihubiri lile neno ila kwa Wayahudi peke yao. Lakini baadhi ya hao walikuwa watu wa Kipro na Kirene, nao walipofika Antiokia wakasema na Wayahudi wa Kiyunani, wakihubiri habari njema za Bwana Yesu. Mkono wa Bwana ukawa pamoja nao; watu wengi wakaamini, wakamwelekea Bwana.

Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia. Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo. Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na Imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.

Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli; hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakausanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 87:1-7 (K) 117:1

(K) Enyi mataifa yote, msifuni Bwana.
Au Aleluya.

Msingi wake upo
Juu ya milima mitakatifu.
Bwana ayapenda malango ya Sayuni
Kuliko maskani zote za Yakobo.
Umetanjwa kwa mambo matukufu,
Ee Mji wa Mungu. (K)

Nitataja Rahabu na Babeli
Miongoni mwao wanaonijua.
Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi;
Huyu alizaliwa humo.
Naam, mintarafu Sayuni itasemwa,
Huyu na huyu alizaliwa humo. (K)

Na Yeye Aliye juu
Ataufanya imara.
Bwana atahesabu, awaandikapo mataifa,
Huyu alizaliwa humo.
Waimbao na wachezao na waseme,
Visima vyangu vyote vimo mwako. (K)



SHANGILIO
Lk. 24:25-26

Huko Yerusalemu ilikuwa Sikukuu ya Kutabaruku; ni wakati wa baridi. Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani. Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia. Lakini ninyi hamsadiki, kwa sababu hammo miongoni mwa kondoo wangu. Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata. Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu. Mimi na Baba tu umoja.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUMFUATA MCHUNGAJI MWEMA!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Aprili 27, 2026
Juma la 4 la Pasaka

Mdo 11:1-18;
Zab 42:2-3,43:3-4 (K. 42:3);
Yn 10:11-18.


KUMFUATA MCHUNGAJI MWEMA!

Sehemu ya Injili ya mchungaji mwema inatupa mambo manne kuhusu Yesu. Kwanza kabisa Yesu kwa kuwa Neno wa Mungu mwenyewe, sio tu mchungaji bali yeye mwenyewe ni chakula-malisho ya kweli ambaye hutoa uzima kwa wingi. Anatupa uzima kwa kujitoa mwenyewe, kwani yeye ni uzima (Yn 1: 4). Pili, huyu Mchungaji mwema anatoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake (Yn 10: 11). Msalaba upo katikati ya maelezo ya Mchungaji mwema. Na unaoneshwa sio kama kitendo cha vita kinacho mshtukiza Yesu bila kujua na kumshambulia kutoka nje, bali ni kama zawadi huru kutoka kwake. “Nayatoa maisha yangu, ili niya twae tena. Hakuna awezaye kuyatwaa kutoka kwangu, bali ninayatoa kwa hiari yangu mwenyewe”.

Tatu, kondoo ni wake katika hali ya kufahamiana na mchungaji, na hali hii ya kufahamiana ni hali ya kukubali kutoka ndani. Ina maanisha hali ya kuwa wake katika hali ya ndani ambayo ni zaidi ya ile hali ya kuwa na vitu vya kawaida. Na mwisho Kabisa, Mungu ndiye mchungaji ambaye anawaunganisha tena Waisraeli waliogawanyika na kutawanyika na kuwafanya watu wamoja kwani sio mataifa mawili tena (Ez 37: 15-17, 21). Hili ndilo la Muhimu kwa wayahudi walipo mpinga Petro kwa kutembelea nyumba ya Kornelio kama inavyo oneshwa katika somo la kwanza. 

Sisi nasi tunaalikwa kwenye utume sisi kama wachungaji wa Kristo tunapaswa kuziokoa roho kwa ajili ya Mungu kwa kulijenga na kulifanya kanisa la Mungu kuwa moja. Je, tupo tayari kuchukua jukumu hili na kukumbana na changamoto? 

Yesu, Mchungaji Mwema, anatuita sisi "kondoo," kwamba sisi ni dhaifu na wanyonge. Bila yeye, hatuwezi kufanya kitu (Yn 15: 5). Mchungaji Mwema atosha, Yeye atawaongoza kwenye malisho ya majani mabichi (Zab 23: 2). Jambo pekee linalohitajika kutoka kwetu sisi kondoo, ni kusikia sauti yake daima na kuifuata. Sisi sote kama kondoo lazima tuikimbie sauti ya yule muovu (Shetani). Sauti ya Yesu inahitaji kujitoa kweli, kujikana nafsi na kuacha yote, kubeba misalaba yetu, tofauti na sauti nyingine za ulimwengu huu zinazo onekana kuwa tamu na rahisi kuzifuata lakini mwisho wake kuangamia milele. Kusikiliza sauti ya Yesu ni katika Sala na Tafakari juu ya Biblia, kuwasikiliza ndugu zetu katika hali mbali mbali na mengine yanayo tujenga kiroho. Kusikiliza huja kwa Neno la Kristo (Rum 10:17). Tumuombe Mungu atusaidie kuisikia sauti ya Yesu ndani ya sauti nyingi za ulimwengu huu. 

Sala: Bwana, nisaidie niweze kutambua na kufuata sauti yako ya upole siku zote za maisha yangu. Ninaomba sauti hiyo iweze kushinda sauti zote zinazo shindana na utulivu wangu kwako. Ninakuchagua wewe, Bwana mpendwa kama mchungaji wa kuniongoza. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA,APRILI 27, 2026




MASOMO YA MISA, 
APRILI 27, 2026
JUMA LA 4 LA PASAKA, JUMATATU

SOMO 1
Mdo 11:1-18

Siku zile, mitume na ndugu waliokuwako katika Uyahudi wakapata habari ya kwamba watu wa Mataifa nao wamelipokea neno la Mungu. Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye, wakisema, uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao.

Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema, Nalikuwa katika mji wa Yafa, nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono; chombo kinashuka, kama nguo kubwa inatelemshwa kutoka mbinguni kwa pembe zake nne, kikanifikia. Nikakitazama sana, nikifikiri, nikaona wanyama wan chi wenye miguu mine, na wanyama wa mwituni, nao watambaao, na ndege wa angani. Nikasikia na sauti ikiniambia, Ondoka, Petro, ukachinje ule. Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu. Sauti ikanijibu mara ya pili kutoka mbinguni, Alivyovitakasa Mungu, usivinene wewe najisi. Jambo hili likatendeka mara tatu, kisha vitu vyote vikavutwa tena juu mbinguni.

Na tazama, mara hiyo watu watatu wakasimama mbele ya nyumba tuliyokuwamo waliotumwa kwangu kutoka Kaisaria. Roho akaniambia nifuatane nao, nisione tashwishwi. Ndugu hawa sita nao wakaenda nami, tukaingia katika nyumba ya mtu yule; akatueleza jinsi alivyomwona malaika aliyesimama nyumbani mwake na kumwambia, Tuma watu kwenda Yafa ukamwite Simoni aitwaye Petro, atakayekuambia maneno ambayo yatakuokoa, wewe na nyumba yako yote.

Ikawa nilipoanza kunena, Roho Mtakatifu akawashukuia kama alivyotushukia sisi mwanzo. Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, Yohane alibatiza kwa maji kweli, bali ninyi mtabatiza kwa Roho Mtakatifu. Basi ikiwa Mwenyezi Mungu amewapa wao karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani niweze kumpinga Mungu?

Waliposikia maneno haya wakanyamaza, wakamtukuza Mungu, wakisema, Basi, Mungu amewajalia hata mataifa nao toba lilitalo uzima.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 42:1-2, 43:2-3 (K) 42:2

(K) Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu aliye hai.
Au Aleluya.

Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji,
Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, ee Mungu. (K)

Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu aliye hai,
Lini nitakapoikuja nionekane mbele za Mungu? (K)

Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, 
Zinifikishe kwenye mlima wako
mtakatifu na hata maskani yako. (K)

Hivyo nitakwenda madhabahuni mwa Mungu,
Kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu;
Nitakusifu kwa kinubi, ee Mungu, Mungu wangu. (K)


SHANGILIO
Ufu. 1:5

Aleluya, aleluya,
Ee Kristo, yu shahidi aliye mwaminifu mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia.
Aleluya.


INJILI
Yn. 10:1-10

Yesu aliwaambia Wayahudi: Amin, amin, nawaambieni, Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang’anyi. Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo wake wote, huwatangulia; na awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.

Mithali hiyo Yesu aliwaambia; lakini wao hawakuelewa na mambo hayo aliyowaambia.

Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia. Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 26, 2026



MASOMO YA MISA, APRILI 26, 2026
DOMINIKA YA 4 YA PASAKA
JUMAPILI YA MCHUNGAJI MWEMA


MWANZO:
Zab. 33:5–6
Nchi imejaa fadhili za Bwana. Kwa neno la Bwana mbingu zilifanyika, aleluya.


SOMO 1
Mdo 2:14, 36– 41

Siku ya Pentekoste Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia,

Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyesulibisha kuwa Bwana na Kristo.

Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Krito, mpate kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 23:1 – 6 (K) 1

(K) Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika. (K)

Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)



SOMO 2
1Pet. 2:20– 25

Kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu. Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogopfya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki. Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti; ili, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa. Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi war oho zenu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Yn. 10:14

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.



INJILI
Yn. 10:1 – 10

Yesu aliwaambia Wayahudi, Amin, amin, nawaambieni, Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang’anyi. Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo. Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje. Naye awatoapo kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.

Mithali hiyo Yesu aliwaambia; lakini wao hawakuelewa na mambo hayo aliyowaambia.

Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia. Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo..


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Aprili 25, 2026
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 9: 31-42;
Zab 116: 12-17;
Yn 6: 60-69.


UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!


Yohane anataka kutuonesha kwamba Yesu ndiye anayetulisha chakula cha uzima wa Kimungu, kwakutupa sisi maisha yake mwenyewe na mwili wake. Kula mkate na samaki aliowapa Yesu ilikuwa rahisi lakini kusikiliza maneno yake ilikuwa vigumu, baada ya haya Injili inasema wazi kwamba wafuasi wengi walimwacha na wengine waliacha kuambatana naye. Lakini wakati Yesu alipowauliza wale kumi na wawili, kama na wao wanataka kuondoka pia, Petro alijibu, “Bwana tuende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele” Ndio, Petro anatambua japo kuwa si kwahakika sana kipindi hicho, kwamba “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu”

Swali hili la Yesu kwa Mitume wake ni muhimu sana. Kwa kuwauliza wao moja kwa moja, Yesu anawapa uhuru kamili wa kuchagua. Hawashinikizi kukubali au kuamini alichokuwa amefundisha mara. Hili lilikuwa muhimu kwa sababu kwa kiasi ambacho Yesu anatoa cha kuachia yote ni mwaliko wa kuwa na uhuru kamili, kwa upande wa mitume, kwa mafundisho yake ya utukufu juu ya Ekaristi. Wapo huru kabisa kukubali au kukataa. Ni uhuru huu utawafanya wazame katika Imani yao juu ya Yesu.

Tutafakari leo, juu ya kujikabidhi kwetu kwa Yesu. Tupo huru kabisa kumfuata yeye au kumkataa. Yesu hapendi tumchague na kumfuata nusu nusu. Maneno ya Yesu yana nguvu, yana changamoto na yanahitaji sadaka. Anataka tumwamini yeye na kumfuata kwa moyo wote na kujikabidhi kweli. Ni Yesu mwenyewe mwenye maneno ya uzima wa milele na tunapaswa tukubali maneno yake na kuamini kwa nguvu zetu zote.

Ni neno la Mungu kweli linalo tutakasa na kutuburudisha. Linatupa uzima; kwahiyo kinachotupa uzima ni Neno la Mungu, kwani maneno anayosema Yesu ni roho tena ni uzima. Jumuiya ya Wakristo kama tunavyosikia katika Somo la kwanza leo, walijenga msingi wao juu ya uzima huu walioupokea kutoka kwa Yesu na faraja ya Roho Mtakatifu. Sisi tuna uhai na uzima, ila uzima wetu na maisha yetu tuyaweke ndani ya Bwana wa uzima Yesu Kristo mwenyewe. Ni maneno haya yenye uzima ya Yesu yalioweza kumrudishia uzima Dorcasi kama tunavyosikia katika somo la kwanza.

Sala: Bwana Yesu, ni wewe pekee ninaye kuchagua kukuamini na kukufuata. Nisaidie nikumbatie yote uliyo fundisha na nisaidie kukuchagua kwa uhuru katika maisha yangu ya kila siku. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2026




MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 9:31-42

Kanisa lilipata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongoezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.

Hata Petro alipokuwa akizunguka-zunguka pande zote akawatelemkia na watakatifu waliokaa Lida. Akamwona mtu mmoja huko, jina lake Ainea, mtu huyo amelala kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza. Petro akamwambia. Ainea, Yesu Kriso akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka. Na watu waliokaa Lida na Sharani wakamwona, wakamgeukia Bwana.

Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani. Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.

Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao. Petro akawatoa nje wote, akapiga maogi, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi. Akampa mkono, akamwinua, hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai. Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 116:12-17 (K) 12

(K) Nimrudishie Bwana nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?

Nimrudishie Bwana nini
Kwa ukarimu wake wote alionitendea?
Nitakipokea kikombe cha wokovu;
Na kulitangaza jina la Bwana. (K)

Nitaziondoa nadhiri zangu kwa Bwana,
Naam, mbele ya watu wake wote.
Ina thamani machoni pa Bwana
Mauti ya wacha Mungu wake. (K)

Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako,
Mtumishi wako, mwana na mjakazi wako,
Umenifungua vifungo vyangu.
Nitakutolea dhabihu ya kushukuru;
Na kulitangaza jina la Bwana. (K)



SHANGILIO
Kol. 3:1

Aleluya, aleluya,
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.
Aleluya.



INJILI
Yn. 6:60:69

Siku ile, watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia maneno ya Yesu juu ya mkate wa uzima, walisema: Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia? Naye Yesu akafahamu nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanalinung’unukia neno hilo, akawaambia, Je! Neno hili linawakwaza? Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza? Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.

Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasiomini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti. Akasema, kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu. Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma wasiandamane naye tena.

Basi Yesu akawambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.