Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

NINI MAANA YA UKWELI?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Julai 2, 2026,
Tafakari ya kila siku 
Juma la 13 la Mwaka wa Kanisa


Amo 7: 10-17; 
Zab 18: 8-11; 
Mt 9: 1-8


NINI MAANA YA UKWELI?

Ingawaje mwanadamu anatafuta ukweli daima, lakini yeye mwenyewe ni sababu yakuto kuutambua. ‘Ukweli ni kitu ghani?’ swali maarufu lililoulizwa na Pilato ambalo hadi leo husikika masikioni mwetu. Lakini pilato hakuwa na subira (Yn 18: 38) yakutosha kusubiri jibu kutoka kwa Bwana wetu Yesu ambaye ni njia, ukweli na uzima. Sisi tunapenda sana kujua ukweli kuhusu wengine, sio tu kupenda bali tunapoteza muda mwingi kujaribu kutaka kujua ukweli kuhusu wengine. Lakini pia tunajaribu kwa njia zote kukwepa ukweli kuhusu sisi wenyewe! Ukimya ! tunachukia ukimya-kwasababu ukimya nisilaha kubwa ya kugundua ukweli. Ukweli unaweza kukutana nao moja kwa moja-kwanjia ya ukimya na tafakari au pia unaweza kufunuliwa na Mungu mwenyewe-ambaye ni Ukweli wote-kwa njia ya manabii, maandiko matakatifu au watu wake aliowachagua. 

Katika somo la kwanza, tunapata tukio kama hilo ambapo nabii Amosi anashuhudia ukweli-mchanganyo uliopo katika kuabudu, katika maisha ya pamoja na maisha binafsi. Lakini anakataliwa na Amasia kuhani wa Betheli. Katika injili tunaona mtu aliyepooza analetwa kwa Yesu. Tofauti na madakatari wa sasa, daktari mkuu anamponya kabla ya kuuliza sababu. Kristo kamwe hakumponya mtu kabla hajampa ukombozi kwanza na msamaha. Leo tunaalikwa tuingie ndani ya nafsi zetu wenyewe tugundue ukweli kuhusu sisi wenyewe. Tufungue moyo wetu tupokee ujume wa Yesu na mpango wake juu yetu. 

Sala: Bwana, naomba unisaidie niweze kukuona wewe ndani yangu nami ndani yako. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 2, 2026




MASOMO YA MISA, JULAI 2, 2026
ALHAMISI , JUMA LA 13 LA MWAKA


SOMO 1
Amo. 7:10 – 17

Amazia kuhani wa Betheli, alipeleka habari kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosi amefanya fitina juu yako kati ya nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote. Kwa maana Amosi asema hivi, Yeroboamu atakufa kwa upanga, na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali, hali ya kufungwa, atoke katika nchi yake. Tena Amazia akamwambia Amosi, Ewe mwona, nenda zako, ikimbilie nchi ya Yuda, ukale mkate huko, ukatabiri huko; lakini usitabiri tena huku Betheli; kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme, nayo ni nyumba ya kifalme. Ndipo Amosi akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu; naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwabarie watu wangu Israeli.
Basi, sasa lisikie neno la Bwana; Wewe unasema, Usitabiri, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka; kwa hiyo, 
Bwana asema hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa kutoka nchi yake. 

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 19: 7 – 10 (K) 9

(K) Hukumu za Bwana ni kweli, zina haki kabisa.

Ushuhuda wa Bwana ni amini,
humtia mjinga hekima.
Maagizo ya Bwana ni ya adili,
Huufurahisha moyo. (K)

Amri ya Bwana ni safi,
huyatia macho nuru.
Kicho cha Bwana ni kitakatifu,
kinadumu milele. (K)

Hukumu za Bwana ni kweli,
zina haki kabisa. (K)

Ni za kutamanika kuliko dhahabu,
Kuliko wingi wa dhahabu safi.
Nazo ni tamu kuliko asali,
Kuliko sega la asali. (K)


SHANGILIO
Zab. 119:105

Aleluya, aleluya.
Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.
Aleluya.


INJILI
Mat 9: 1-8

Yesu alipanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao. Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu; umesamehewa dhambi zako. Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. Naye Yesu hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (akamwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwake. Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

UTUOPOE MAOVUNI!

 



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Julai, 01, 2026, 
Juma la 13 la Mwaka wa Kanisa

Amo. 5 : 14-15,21-24; 
Zab 50 : 7-13, 16-17; 
Mt 8: 28-34


UTUOPOE MAOVUNI!

Watu waliokuwa na pepo wakitokea makaburini walikutana na Yesu wakati Yesu akikaribia kijiji hicho. Walikuwa wakali mno kiasi kwamba hakuna mtu aliye jaribu kupita katika njia ile. Walilia kwa sauti “una nini nasi, Mwana wa Mungu?” sehemu hii inaonesha kwamba pepo ni hatarishi na kwamba Yesu ana mamlaka makubwa. Yesu anaingia mjini kwa kuwaponya hawa watu wawili waliokuwa na pepo na hivyo kuonesha nguvu yake juu ya kuondoa uovu.

Ni wazi kwamba hawa pepo waliowashika hawa watu wawili walikuwa wakali na hivyo kufanya watu wakae kwa hofu na wasi wasi. Watu kuwa na wasiwasi kiasi kwamba hakuna mtu aliye thubutu kupita maeneo hayo. Tunaweza tusikutane na uovu kama huo mara kwa mara, lakini ni hakika kwamba tulisha kutana na uovu wakati mwingine. Muovu yupo daima na anazunguka kutafuta sehemu ya kujenga ufalme wake hapa duniani. Yesu ana mamlaka makubwa kuliko muovu. Jambo lakushangaza, aliwatoa pepo hawa na wakawaingia kundi kubwa la nguruwe na hivyo kuteremkia baharini na kufa. Watu wa mji ule wanaogopa kiasi cha kumwambia Yesu aondoke katika mji wao. Kwa kiasi, sababu inaonekana Yesu kuwaponya hawa watu wawili ilileta mtafaruku mkubwa sana katika mji. Uovu uliojikita hauondoki kimya kimya. Kuna mahangaiko!

Watu hawa wawili walitoka makaburini , kama sisi tunavyotoka katika makaburi ya dhambi-tuliko naswa, anasa, kuhukumu kwetu wengine, dhuluma, na mitazamo yetu mibaya kwa wengine inayoleta maumivu kwa wengine. Kwasababu ya hili watu wanaweza kutuogopa sana! Lakini Yesu yupo tayari kuja kukutana na sisi sehesmu tulipo. Uovu wetu humtambua Yesu na tunafanywa kuwa huru kama tukienda karibu na Yesu.

Lakini mara nyingi, Yesu anapokuja kuondoa uovu ndani mwetu, tunaweza tusitambue uponyaji. Ni mara ngapi Roho Mtakatifu anataka kutufanya upya nasi tunakataa? Tuna furaha kuishi katika hali ya dhambi na hatutaki kuacha. Hatutaki mtu atusumbue tunapo endelea kufurahia raha za ulimwengu. Tutafakari juu ya maisha yetu na kujaribu kuwa tayari katika maongozi ya Mungu na wala tusimuombe aondoke kama wale watu kwenye Injili, ili tupate kuishi katika maisha ya neema tele.

Sala: Bwana, nisaidie niweze kubaki imara ninapo kumbana na muovu na utawala wake wa giza. Nisaidie niweze kushinda utawala wake kwa ujasiri, upendo na ukweli ili kuleta ufalme wako sehemu yake. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JULAI 01, 2026

 



MASOMO YA MISA, JULAI 01, 2026
JUMATANO, JUMA LA  13 LA MWAKA WA KANISA


SOMO 1
Amo. 5 : 14-15,21-24

Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo Bwana, Mungu wa majeshi, aiakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo. Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba Bwana, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.

Mimi nazichukia sikukuu zenu, asema Bwana nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini. Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona. Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu. Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 50 : 7-13, 16-17 (K) 23

(K) Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena,
Mimi nitakushuhudia, Israeli;
Mimi ndimi niliye Mungu, Mungu wako. (K)

Sitakukemca kwa ajili ya dhabihu zako,
Na kafara zako ziko mbelc zangu daimu.
Wala beberu katika mazizi yako. (K)

Maana kila hayawani ni wangu.
Na makundi juu ya milima eltu.
Nawajua ndege wote wa milima,
Na wanyama wote wa mashamba ni wangu. (K)


Kama ningekuwa na njaa singekuambia
Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.
Je! Nile nyama ya mafahali!
Au ninywe damu ya mbuzi! (K)

Maana wewe umechukia maonyo,
na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. (K)


SHANGILIO
2 Kor. 5 :19

Aleluya, aleluya, Mungu alikuwa ndani ya Kristu, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, ametia ndani yetu neno la upatanisho. Aleluya.


INJILI
Mt. 8 :28-34

Yesu alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja Kututesa kabla ya muhula wetu?

Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha. Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe. Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini. Lakini wachungaji walikimbia, wakaenda zao mjini, wakazieneza habari zote, na habari za wale wenye pepo pia. Na tazama, mji wote ukatoka kwenda kumlaki Yesu; nao walipomwona, walimsihi aondoke mipakani mwao.



Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

ALIPO YESU PANA UTULIVU!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Juni 30, 2026, 
Juma la 13 la Mwaka wa Kanisa


Amo 3: 1-8, 4:11-12; 
Zab 5: 5-8; 
Mt 8: 23-27


ALIPO YESU PANA UTULIVU!


Yesu alikemea upepo wa bahari na hali ikawa shwari. Kama sentensi hii inamaanisha kutuliza bahari tuu, mmoja anaweza kujiuliza swali, kwanini Yesu hafanyi sasa? Kwanini anaruhusu wapendwa wake wakumbwe na mawimbi makubwa ya maisha? Je, hayupo tayari kutuokoa kama alivyo waokoa mitume? Kuna mambo makubwa zaidi kutoka sentensi hii, ni zaida yakutuliza tu bahari. Sehemu yeyote alipo Yesu pana utulivu, upole na Amani. Haijalishi ni kwakiasi ghani maisha yanaweza kuwa mabaya na kukumbwa na mawimbi makubwa, uwepo wa Yesu tuu, unabadilisha hata kile tunachodhani hakiwezekana na hali ya utulivu hurudi tena. Tukiwa na Yesu katika boti yetu ya maisha hakuna mawimbi yatakayo tuangusha na kutupeleka mbali. Tatizo letu sisi tumekuwa watu wa Imani kidogo/hafifu. Imani yetu ni hafifu sana kiasi ambacho mambo yetu yasipoenda kama yalivyopangwa tunaanza kuwa na wasi wasi kuhusu uwepo wa Mungu ndani yetu. Ni kwa wale tuu waliojishika na Mungu na kuhisi uwepo wake ndani yao wanaosimama imara na kubaki vizuri bila kuyumbishwa. Watu hawa wanahisi Amani na utulivu katika hali zote, hata katika hali mbaya kabisa inayotisha katika maisha. 

Mtakatifu Ireneo tunaye mwadhimisha leo, alipenda Amani na alitoa maisha yake yote kutetea Amani na kuhakikisha kanisa linabaki katika Amani kila wakati. Sisi tunapenda Amani? Sisi sio watu wa chanzo cha fujo na magomvi? Tunafurahi tunapoona watu wanaishi kwa Amani? Au tunatafuta mbinu za kuchafua Amani yao? je, unafanya jitihadi za kuleta Amani kati ya watu au maisha yako yamekuwa ya furaha kwasababu adui yako hana Amani au amepatwa na matatizo? Tunahimizwa ndugu zangu tuwe wajumbe wa kuleta furaha na Amani kati ya watu, tuache wivu usio na sababu, tujikubali wenyewe na tuwakubali ndugu zetu, tuwasamehe wakikosa, tuwe na moyo wakuomba msamaha tunapokosea, haya yote tukiyashika yatatufanya tuishi vizuri kwa Amani na furaha kati yetu. Tukiiishi kwa utulivu na Amani Yesu atakuwa kati yetu. Kwa maombezi ya Mt. Ireneo tuombe neema hiyo yakutunza Amani katika nafsi zetu, familia, ndugu wote na kanisa la Mungu.

Sala: Bwana, niongezee Imani na zamisha Imani yangu juu ya uwepo wako, ili niweze kuwa na utulivu mkubwa na Amani. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 30 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 30 2026
JUMANNE, JUMA LA 13 LA MWAKA WA KANISA


SOMO 1
Am. 3:1-8;11-12

Lisikieni neno hili alilolisema Bwana juu yenu, enyi wana wa Israeli, juu ya jamaa yote niliowapandisha kutoka nchi ya Misri, nikisema, Ni ninyi tu niliowajua katika jamaa zote zilizo duniani; kwa sababu hiyo nitawapatiliza ninyi maovu yenu yote.

Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana? Je! Simba atanguruma mwituni, asipokuwa na mawindo? Mwanasimba atalia pangoni mwake, ikiwa hakupata kitu? Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu chochote? Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta Bwana? Hakika Bwana Mungu hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake. Simba amekwisha kuunguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana Mungu amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri? Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora, nanyi mkawa kama kinga kilichonyakuliwa motoni; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. Basi nitakutenda hivi, Ee Israeli; na kwa sababu nitakutenda hivi, ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 5:4 – 7 (K)8

(K) Bwana uniongoze kwa haki yako.

Huwi Mungu apendezwaye na ubaya;
Mtu mwovu hatakaa kwako;
Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako. (K)

Unawachukia wote watendao ubatili.
Utawaharibu wasemao uongo;
Bwana humzira mwuaji na mwenye hila. (K)

Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, 
Nitaingia nyumbani mwako;
Na kusujudu kwa kicho,
Nikilielekea hekalu lako takatifu. (K)


SHANGILIO
Yn. 15:15

Aleluya, aleluya,
Bwana anasema, Siwaiti tena watumwa, lakini ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Aleluya.


INJILI
Mt. 8:23-27

Yesu alipanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata. Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia. Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu. Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.©, These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MATESO YETU YA KILA SIKU YANATUSAIDIA KUKUWA KATIKA UHUSIANO NA YESU!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku 
Jumatatui, Juni, 29, 2026, 
Juma la 13 la mwaka wa Kanisa.


Sherehe ya Watakatifu Petro na PauloMitume

Mdo 12:1-11; 
Zab 33:2-9; 
2Tim 4:6-8, 17-18; 
Mt 16:13-19


MATESO YETU YA KILA SIKU YANATUSAIDIA KUKUWA KATIKA UHUSIANO NA YESU!


Watakatifu Petro na Paulo wanachukuliwa kama nguzo mbili kubwa za kanisa Katoliki lililowekwa na Kristo mwenyewe. Wote walikufa mashahidi huko Roma, wote wawili walionesha upendo wao kwa Kristo kwa kutoa maisha yao. Mt. Petro alichaguliwa na Yesu kama kiongozi wa Mitume na pia kuwa vika wake hapa duniani. Yesu alimpa ufunguo za mbinguni na mamlaka ya kuchunga kundi lake. Mt. Paulo alichaguliwa na Yesu mwenyewe wakati akielekea Dasmeski na kuwa mtume wa mataifa. Kwa jinsi Kanisa la Yesu lilivyo leo ni kwasababu ya Imani na utume waliofanya watakatifu Petro na Paulo. Ni kweli kwamba leo tuna sheherekea mitume Petro na Paulo katika Kanisa, tujaribu kujiuliza maisha yao yalikuwaje kabla? 

Tuna angalia maisha ya Petro. Alikuwa mvuvi. Petro hakuwa mtu wa Imani kubwa. Leo katika Injili tunamuona Yesu akiwauliza wafuasi wake, watu wanadhani yeye ni nani? Na pia anawauliza mitume wake, na nyie mnasema mimi ni nani? Petro kwa niaba yao anajibu, “wewe ni Kristo Mwana wa Mungu aliye hai”. Ni baada ya maelezo haya Yesu anawaeleza mitume wake kuhusu mateso yake na ufufuko. Je, Petro alisema nini kuhusu hili? “…haya hayatakupata! Kamwe”. Yesu anamkemea “rudi nyuma yangu shetani!”. Hapa ndipo tunapoona kiini cha Imani ya Petro. Haikuwa sahihi. Katika sehemu nyingine wakati Yesu anatembea juu ya maji, Petro alimwambia Yesu, “Bwana, kama ni wewe uniruhusu nije kwako nikitembea juu ya maji”. Yesu alimwambia amfuate akitembea juu ya maji. Mara baada ya kutembea alianza kuzama na anamlilia Yesu amuokoe. “Ewe mwenye Imani haba, mbona uliona shaka?”. Baada ya ufufuko wa Yesu, Petro huyu huyu alikuwa mtu mwingine tofauti. Akijazwa na Roho Mtakatifu alienda huko na huko akitangaza habari njema. Imani yake sasa imekuwa yenye nguvu na imara. Tunaona pia muda wote jinsi Bwana alivyokuwa naye katika magumu yote aliyopata. Katika somo la kwanza la leo tunamuona malaika akimuokoa Petro kutoka gerezani. 

Je, Paulo alikuwaje kabla? Alikuwa ni Myahudi aliyeshika sheria. Alikuwa amechukua kiapo cha kuwaangamiza waamini wote waliomwamini Yesu. Ili kutimiza haja yake alikuwa njiani akielekea Dameski akiwa njiani alitokewa na Yesu. Kukutana na Yesu huku kulimfanya Paulo awe kiumbe kipya na mtu mpya. Mtu ambaye alikuwa anataka kuwaangamiza waamini wote sasa na yeye anakuwa muamini. Anakuwa mwenye Imani kubwa kiasi cha kusema kwamba “sio mimi tena naishi bali Kristo anaishi ndani yangu” (Gal 2:20). Bwana pia alikuwa na Paulo katika magumu na mateso yake. Leo katika somo la pili linashuhudia hilo. Kwahiyo mateso haya yote walioteseka watakatifu hawa, mateso yote na manyanyaso yote waliokutana nayo hawakumwacha Bwana hata kidogo, bali walikuwa na kuongezeka sana ndani ya Bwana wao. Zaidi sana, Imani yao juu ya Mwana wa Mungu iliimarika sana. Kwa mfano wa watakatifu hawa, sisi pia tukuwe katika uhusiano wetu na Yesu Mwana wa Mungu. 

Wote wawili Mt. Paulo na Mt Petro walikirimiwa kwa uaminifu wao mkubwa katika utume. Katika sherehe hii ya watakatifu Petro na Paulo, tunaomba Kristo atupe sisi wote, ujasiri, ukarimu, na hekima tunayo hitaji ili tuweze kuwa vyombo vya kufanya ulimwengu uwe huru. Kwa kuchukua mfano wa Watakatifu hawa tuweze kukuwa katika uhusiano na Yesu, Mwana wa Mungu. 

Sala: Bwana, ninakushukuru kwa zawadi ya Kanisa lako na Injili yenye kuleta uhuru linayo ihubiri. Nisaidie mimi niweze kuwa mjumbe wa ukweli huo kwa wale wote wanao uhitaji. Ninaomba tuweze kubaki tumeungana na waridhi wa mitume wako. Tuongezee uaminifu katika Injili yako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 29, 2026





MASOMO YA MISA, JUNI 29, 2026
JUMATATU, JUMA LA 13 LA MWAKA

SHEREHE YA WATAKATIFU PETRO NA PAULO (MITUME)

SOMO 1
Mdo. 12:1 – 11

Herode mfalme alinyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohane, kwa upanga. Na akiona ya kuwa imewapendenza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa amelala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwangukia mikononi. Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha.

Hata Petrao alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 34:1 – 8 (K) 7

(K) Malaika wa Bwana awaokoa wamchao.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake kinywani mwangu daima.
Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,
Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. (K)

Mtukuzeni Bwana pamoja nami,
Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Nalimtafuta Bwana akanijibu,
Akaniponya na hofu zangu zote. (K)

Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,
Wala nyuso zao hazitaona haya.
Maskini huyu aliita, Bwana akasikia,
Akamwokoa na taabu zake zote. (K)

Malaika wa Bwana hufanya kituo,
Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema,
Heri mtu yule anayemtumaini. (K)


SOMO 2
2 Tim. 4: 6 – 8, 17 – 18

Mimi sasa namiminiwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa  katika kinywa cha simba. Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.


SHANGILIO 
Mt. 16:18

Aleluya, aleluya, 
Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, wala milango ya kuzimu haitalishinda. 
Aleluya.


INJILI 
Mt. 16 :13-19

Yesu alienda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena u Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

NYUMBA MPYA, FAMILIA MPYA



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Juni 28, 2026.
Dominika ya 13 ya Mwaka

2 Fal 4: 8-11, 13-16;
Zab 88: 2-3, 16-19;
Rom 6: 3-4, 8-11;
Mt 10: 37-42.


NYUMBA MPYA, FAMILIA MPYA

Neno nyumba katika lugha ya Kiebrania haina maana tu ya jengo bali pia familia. Mtu hawezi kufanya lolote tofauti na maana hii: “kwa wengine ni vitu ambavyo huwezi kuishi bila hivyo: maji, chakula, nguo na nyumba kwa ajili ya makazi” (YbS 29:21). Lakini yule ambaya anataka kuanzisha familia mpya, anapaswa kuacha nyumba yake: “Mwanaume atamuacha Baba yake na mama yake na ataungana na mkewe na wote wawili takuwa mwili mmoja” (Mwa 2:24). Ni kitendo cha kuacha nyumba moja na kuingia katika nyumba nyingine au familia mpya. Yesu pia ana uacha mji wake mwenyewe Nazarethi, “Mwana wa mtu hana mahali pa kulaza kichwa chake” (Mt 8:20). Aliacha familia yake: ‘Mama yangu ni nani’? ‘Kaka zangu ni akina nani?’ na kwenda katika familia mpya ‘tazama! Wapo hapa mama yangu na kaka zangu (rejea. Mt 12:48-50). Kwa wale wote wanaopenda kumfuata Yesu, anawaambia wachukue jukumu hilo hilo: ujasiri wakujitenga, kuchukua hatua kubwa kuelekea katika ukweli halisi, kutambulishwa katika nyumba mpya, familia mpya, familia ya wana wa Mungu.

Katika somo la kwanza tunamuona nabii Elisha akibariki wana ndoa wawili, waliokuwa wana umri mkubwa bila kuwa na watoto, na hivyo anawahidia mtoto. Kwa kujua kwamba Elisha ametokea katika nchi ya mbali na hakuwa na nyumba wala familia alimkaribisha na kumshirikisha. Huyu mwanamke ambaye alikuwa tajiri, alikuwa na uwezo wa kumpatia Elisha fedha kidogo na kumwacha aondoke, lakini hakumpa tu msaada bali alimkaribisha pia nyumbani kwao, na kumkaribisha na kujisikia kama mmoja wao katika familia. Ishara anazofanya huyu mwanamke zina mfurahisha Mungu, na hivyo Mungu anampa furaha kubwa ambayo alikuwa akiitamani: alimpa mtoto wa kiume. Elisha ana wakilisha mitume, ambao hata leo, wana acha nyumba zao, nchi yao, familia zao na kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu na Injili.

Katika somo la pili, tunaona kwamba Ubatizo ulikuwa ni utamaduni uliokuwepo kipindi cha Yesu. Wale wote walioufuata walibatizwa. Ilikuwa ni ishara iliyo fanya mabadiliko makubwa katika maisha: kifo kwa mambo ya zamani na kuzaliwa upya. Hata ubatizo wa Kikristo una maana hiyo hiyo. Maji ya ubatizo yalichukuliwa kama maji tumboni mwa mama ambamo mtoto mdogo huishi katika mazingira hayo na baadaye huzaliwa kama mtoto wa Mungu. Paulo anasema “kwa njia ya ubatizo, tunazikwa pamoja na Kristo ili tufufuke naye katika maisha mapya” . kama ubatizo ni ishara ya kuzaliwa upya, ina dhihirisha mwanzo wa maisha yote ya maaldili mapya, mkristo hawezi kuendelea kutenda vitu vya zamani, anapaswa kuchukulia yeye mwenye kama mfu katika dhambi, na mzima na anayeishi kwa Mungu ndani ya Kristo”.

Katika Injili, Mathayo anaendeleza na utume wa wanafunzi wa Yesu. Kwanza kabisa, wito wa Yesu kuhusu ufuasi umeonesha katika hali yote. Kuacha na kukataa yote inahitajika katika maisha ya ufuasi. Kila agizo linafuatiwa na ugumu na hali ya kweli ya kuacha yote. Zaidi ya yote, Yesu anataka wafuasi wake kuondoka katika hali za ndani za hisia zao, kama vile kuwapenda wazazi au watoto.

Yesu hafanyi hivi kutaka kukataa sheria ya Musa (Torati), inayo amuru kuwa heshimu Baba na Mama. Ni hakika kwamba, ameirudia amri kwa msisitizo (Mt 15:4). Matayo ameandika Injili yake kipindi cha madhulumu. Wafuasi walikuwa wameshapatwa na magumu ya kubaki waaminifu kwa Kristo, walipaswa kuvunja vifungo ambavyo walikuwa wamejifungia na watu muhimu tu kwao. Marabi walikuwa wamesha amua kuwatenga wafuasi watakao amua kumfuata Yesu, na kuwatenga na sinagogi, na kuwaona kama wazushi, na wala familia zao wasiwatii. Yesu aliwaamuru wafuasi wake wawe na ujasiri wa kusimama imara hata kama hawana wa kuwaunga mkono, kuwalinda, na hata bila mali kwa ajili ya Injili. Na pia aliendelea na ombi lingine, tena lenye maana kubwa zaidi: kuwa tayari kuyatoa maisha yao.

Ishara ya msalaba ni ishara ambayo haikwepeki kwa mfuasi yeyote anayependa kumfuata Kristo na kuishi matakwa ya Injili: kama Bwana wao, watakutana na msalaba, nao ni machungu ya ulimwengu. Hata kama maisha hayataondolewa kwa njia ya kuuwawa, wanapaswa kutoa kuyatoa maisha yao kwa ukarimu na kama sadaka kwa ajili ya watu.

Katika upande wa pili wa Injili, ni zawadi kwa wale wote watakao wakaribisha wale wanao ihubiri Injili, “Kila anaye wakaribisha ninyi, ana nikaribisha mimi” (mstari. 40). Hii ni kama ule ukaribisho aliopokea Elisha katika somo la kwanza. Kila anaye mkaribisha nabii kwasababu ni nabii, atapokea zawadi ya kinabii. Hata upendo kidogo ukao tolewa kama vile kumpatia mfuasi kikombe kidogo cha maji ya baridi, ingawaje ni kidogo, hakika hakita sahaulika.

Kwa hiyo kila mfuasi anaitwa kuwasaidia wale wote waliojitoa kwa ajili ya kutangaza neno la Mungu. Kila Mkristo ana alikwa kuwakaribisha katika familia zao, watu kama hao, walio acha, nyumba, wake, waume, watoto kwa ajili ya kuwa na muda wote na Kristo na watu wake.

Tafakari leo ni kwa jinsi gani wewe ni sehemu ya familia ya Mungu. Tafakari kama unatamani kuwakaribisha nyumbani kwako hao wafuasi kama vile mapadre, watawa, na waamini, ambao kwa moyo usio gawanyika wameyatoa maisha yao kwa ajili ya kazi ya Bwana, kwa ajili ya kuwa tayari kwa ajili ya maisha yako ya kiroho. Viongozi wa dunia tafakari kama unampa Yesu nafasi ya kwanza katika maisha yako. Tujiunge pamoja ili kujenga familia ya Kristo.

Sala: Bwana, ninakupa maisha yangu yote kwako akili, moyo, utashi na nguvu. Nisaidie nikupende wewe zaidi ya yote na katika yote, na katika mapendo hayo nisaidie mimi niweze kuwapenda wale wote uliowaweka katika maisha yangu. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 28, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 28, 2026
DOMINIKA LA 13 LA MWAKA


MWANZO:
Zab. 47:2
Enyi watu wote, pigeni makofi, mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe.


SOMO 1 
2 Fal 4:8-11,14-16

Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula. Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo. Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1

(K) Fadhili za Bwana nitaziimba milele.
Fadhili za Bwana nitaziimba milele;
Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;
Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe,
Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako.
Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,
Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe,
Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.
Maana ngao yetu ina Bwana,
Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)


SOMO 
Rum. 6:3-4,8-11

Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika

wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO 
Mt. 11:25

Aleluya, aleluya, 
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. 
Aleluya.


INJILI 
Mt. 10:37-42

Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.

Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki. Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.