Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

--KUPONYWA KWA UPOFU--

 


“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumapili, Machi 15, 2026.
Dominika ya 4 ya Kwaresima

1Sam 16: 1, 6-7,10-13;
Zab 23: 1-6;
Ef 5: 8-14;
Yn 9: 1-41.


KUPONYWA KWA UPOFU


Kulikuwa na kijana mmoja alyezaliza kipofu katika kijiji kimoja. Kila siku jioni alikuwa akichukua taa ili kuvuka msitu mmoja wenye giza kuelekea nyumbani kwake. Mtu mmoja mpita njia alikutana na huyu kipofu akamuuliza swali “je, wewe si kipofu; sasa inakuwaje umebeba taa?’ Yule kipofu akajibu akasema hii taa ni kwa ajili yenu ili msije mkagongana na mimi.

Katika maisha, macho yenye afya hayawezi kuona yote. Tunaweza kuona vitu vingine tunapokuwa na wengine. Elimu ya kisayansi ambayo inaweza kutusaidia kuchunguza na kujaribu yale yote yanayo shikika, na kutufanya tuwe na hali ya kutaka kujua zaidi, kufurahia na kuamini yote yanayo onekana kwa macho, kugundulika kwa kutumia milango ya fahamu, na kuangalia na vyombo vya maabara na kusema ni kweli. Kuna upofu mwingine pia ambao umejikita katika mizani ya ulimwengu,: pesa, mafanikio, kazi, mapenzi, afya na ugonjwa, ujana na uzee n.k. lakini uwezo wa kuamini kuona vizuri unafunga ndani na macho ya kiroho yanayo tusaidia kuzama katika mafumbo ya Mungu, maana ya maisha na kifo, na kilele cha historia ya mwanandamu.

“Mwanga wa kweli unao mwangaza kila mtu umekuja ulimwenguni” (Yn 1:9). Yesu alikuja kufukuza giza letu, kuangaza usiku wetu, kukaa katika “watoto wa mwanga na watoto wa mchana” (1 Thes 5:5). Tunaitwa kuangalia katika upofu wetu wa roho. Tunaitwa kuushinda kwa kufungua macho yetu ya kiroho.

Katika somo la kwanza tunamwona Mfalme Sauli anashindwa kumtii Mungu. Anakiuka amri za Mungu, Sauli alimhifadhi Mfalme wa Ameleki na kujipatia vingi kwasababu ya vita. Ndipo Mungu akamkataa Sauli akamtuma Samueli kwenda katika mji wa Bethlehemu kumchagua Mfalme atakaye muonesha. Samueli anaenda katika nyumba ya Yese na baada ya kumuona mtoto wa kwanza wa Yese ambaye alikuwa na nguvu, mzuri, na mrefu. Samueli alidhani huyu ndiye aliyechaguliwa na Bwana, na hapo anasikia sauti kwamba “Mungu haangalii kama Mwanadamu anavyo angalia; mwanadamu hutazama sura ya nje bali Mungu huangalia unyofu wa moyo”. Samueli anaoneshwa Daudi na anamchagua, akiwa ni mtoto wa mwisho wa Yese ambaye alikuwa akichunga kondoo. Wanadamu wana mambo mengi katika akili, ambayo hayawa saidii kufikia hitimisho.

“Upofu” ni kushindwa kuona mkono wa Mungu ukifanya kazi kati yetu. Tunakazana kutafuta miujiza ya Neema za Mungu zinazo onekana kwetu na kwa wengine. Kwahiyo kitu cha kwanza kabisa ambacho tunapaswa kufanya ndicho ambacho tunapata katika Injili ni kutambua upofu wetu. Ni lazima tukazane na kukubali kwamba tumeshindwa kumuona Mungu akiwa kazini akitenda kazi. Kukazana huku kutatusaidia kutambua na kutamani uponyaji wa kiroho. Kitu kizuri ni kwamba Yesu alimponya huyu mtu na kwamba atatuponya sisi pia. Kurudisha hali ya kuona ni rahisi sana kwa Yesu. Kwahiyo sala ya kwanza kabisa ambayo tunapaswa kuisali kutokana na ujumbe huu wa Injili “Bwana naomba niweze kuona” unyenyekevu wa kukiri upofu wetu utatusaidia Mungu aje kutenda kazi kwetu. Na kama hatutakiri kwa unyenyekevu upofu wetu, hatutakuwa katika nafasi ya kuomba uponyaji.

Alifanyaza tope kwa mate yake na kumpaka huyu kijana katika macho, kitendo hiki kina onesha kuwa ni ajabu. Lakini inaonesha kwamba Yesu anaweza kutumia kitu ambacho hatudhani kwa ajili ya kazi yake ya Kimungu. Ni mara nyingi tuna angalia kazi za Mungu katika hali ya juu kabisa. Lakini ni mara nyingi yupo nasi katika yale ya kawaida. Pengine tunaweza kushawishika kufikiri kwamba Mungu anafanya matendo yake kwa njia ya upendo au sadaka. Pengine tunaweza kushawishika kudhani kwamba Mungu hawezi kutumia mambo yetu ya kawaida kutenda miujiza yake. Lakini hili si kweli. Ni hakika kabisa maisha ya kawaida na vitu vya kawaida kabisa katika maisha ndipo Mungu alipo. Kwa hakika, kazi inapokuwa ya kwaida ndipo tukazane zaidi kuona Mungu akitenda kazi. Na tutakapo “muona” yeye akiwa katika mambo ya kawaida ya maisha, tunakuwa tumeponywa na upofu wetu wa roho.
               
Sala: Bwana, ninaomba nione. Nisaidie mimi niponywe na upofu wangu. Nisaidie mimi niweze kukuona katika kila kazi ya maisha yangu. Ninaomba unisaidie niweze kukuona katika matukio madogo ya kila siku katika maisha. Na ninapo kuona wewe ukiwa ndani, jaza Moyo wangu kwa shukrani kwa kuona huku. Yesu, nakuamini Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MACHI 15, 2026


MASOMO YA MISA, MACHI 15, 2026
DOMINIKA YA 4 YA KWARESIMA


MWANZO
Isa. 66:10 – 11

Furahi, Jerusalemu, mshangilieni ninyi nyote mmpendao; furahini, ninyi nyote mliao kwa ajili yake, mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake.



SOMO 1
1Sam. 16:1, 6-7, 10-13

Bwana akamwambia Samweli, Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

Ikawa walipokuja, Samweli alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa Bwana yupo hapa mbele zake. Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.

Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli, Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku. Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbu lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye.

Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
ZAB. 23 (K) 1

(K) Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika. (K)

Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)



SOMO 2
Efe. 5:8 – 14

Zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru; Kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru; maana kila kilichodhihirika ni nuru. Hivyo husema, Amka wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Yn. 8:12

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye atakuwa na nuru ya uzima.



INJILI
Yn. 9:1 – 41

Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu, kipofu tangu kuzaliwa. Wanafunzi wake wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu? Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi, wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake. Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana; usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi. Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.

Alipokwisha kusema hayo alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona.

Basi jirani zake, na wale waliomwona zamani kuwa ni mwombaji, wakasema, Je! Huyu siye yule aliyekuwa akiketi na kuomba  wengine wakasema, Ndiye. Wengine wakasema, La; lakini amefanana naye. Yeye mwenyewe alisema, Mimi ndiye.

Basi wakamwambia, Macho yako yalifumbuliwaje? Yeye akajibu, Mtu yule aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka macho akaniambia, Nenda Siloamu ukanawe; basi nikaenda na kunawa, naikapata kuona. Wakamwambia Yuko wapi huyo? Akasema, Mimi sijui.

Basi wakampeleka kwa Mafarisayo yule aliyekuwa kipofu zamani. Nayo ilikuwa sabato, hapo Yesu alipofanya zile tope na kumfumbua macho. Basi Mafarisayo nao wakawmuliza tena jinasi gani alivyopata kuona. Akawaambia, Alinitia tope juu ya macho, nami nikanawa, na sasa naona. Basi baadhi ya Mafarisayo wakasema, Mtu huyo hakutoka kwa Mungu, kwa sababu haishiki sabato. Wengine wakasema, Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo? Kukawa matengano kati yao. Basi wakamwambia yule kipofu mara ya pili, Wewe wasemaje katika habari zake kwa vile alivyokufumbua macho? Akasema, Ni nabii.

Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona. Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa? Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu; lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe. Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu waliwaogopa Wayahudi; kwa maana Wayaahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba mtu akimkiri kuwa ni Kristo, atatengwa na sinagogi. Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.

Basi mara ya pili wakamwita yule mtu aliyekuwa kipofu, wakamwambia, Mpe Mungu utukufu. Sisi tunajua ya kuwa mtu huyo ni mwenye dhambi. Basi yule mtu akajibu, Kwamba yeye ni mwenye dhambi sijui. Najua neno moja, kuwa mimi nilikuwa kipofu na sasa naona. Basi wakamwambia, Alitutendea nini? Alikufumbua macho jinsi gani? Akawajibu, Nimekwisha kuwaambia, wala hamkusikia; mbona mnataka kusikia tena? Ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake? Basi wakamshutumu, wakasema, Wewe u mwanafunzi wake yule; sisi tu wanafunzi wa Musa. Sisi tunajua ya kuwa Mungu alisema na Musa; bali yule hatujui atokako. Yule mtu akajibu, akawaambia, Hili ni ajabu! Kwamba ninyi hamjui atokako, naye alinifumbua macho! Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake; humsikia huyo. Tokea hapo haijasikiwa ya kuwa mtu ameyafumbua macho ya kipofu, ambaye alizaliwa hali hiyo. Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lolote.

Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje. Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.

Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu. Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu? Yesu akamwambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo

Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

SALA NI KUJIONA MWENYEWE KWA NJIA YA JICHO LA MUNGU



“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumamosi, Machi 14, 2026 
Juma la 3 la Kwaresima

Hos 14:2-10;
Zab 81:6-11,14,17;
Mk 12:28-34

SALA NI KUJIONA MWENYEWE KWA NJIA YA JICHO LA MUNGU

Mungu anaenda kwa watu aliowachangua, mpendwa Efraim na Yuda, ambao wapo mbali na Mungu, waliokamatwa katika matatizo yao. Mungu alitaka watambue kwamba ingawaje ndiye yeye aliyewapa adhabu lakini pia ni yeye atakaye ponya magonjwa yao. Kama tutajitahidi kwenda kwa Bwana atakuja kwetu upesi kama vile mvua inavyo inyeshea ardhi. Lakini Mungu anaifahamu Efraim na Yuda na sisi pia. Fadhila yetu ni kama tone la umande ambalo hupotea. Uaminifu wetu ni mdogo na hafifu.

Mfano wa Yesu wa Mafariyo na watoza ushuru unaelekezwa kwao wote ambao hujiamini wenyewe kama watakatifu na kuona wengine wadhambi. Watu wawili walioenda hekaluni kusali. Mmoja anasimama mbele ya Mungu bila kujinyenyekesha na kusali kwa nguvu, huku akiwalaumu mwengine na kujiinua na kujitakia haki. Mwingine ni Mtoza ushuru anaye kakaa nyuma na kujiona mdhambi na kumwambia Mungu “unihurumie mimi kwani ni mdhambi”.

Je, tunasalije? Huwa tunamwambia Mungu ni kwa jinsi ghani tulivyowazuri na kutaka Mungu atusifie? Au je huwa tunaona uhusiano wetu wa kweli na Mungu? Kama ukweli wa Mungu ukitujaza sisi lazima tutajazwa na ukweli kuhusu dhambi zetu na ukosefu wetu wa mapendo. Sisi ni wadhambi na tunahitaji huruma ya Yesu hata katika kusali tunahitaji Roho atuongoze ili tuweze kumwomba Mungu vizuri.

Leo hii tunakazana kwa akili zetu wenyewe. Na tunajiona wenyewe kwamba kitu fulani ni hakika. Mungu anatuaona sisi kama tulivyo. Anaona mambo yote mazuri na yale ambayo tunapaswa kukazana kuyapigania. Anaona yale mambo ambayo yapo ndani kabisa mwa mioyo yetu, ambayo ni upofu katika maisha yetu. Mungu anatupenda kama tulivyo. Hivyo tujiangalie sisi wenyewe kwa jicho la mkombozi wetu. Tukijiona wenyewe kama Mungu anavyofanya tutakuwa tayari kupokea huruma yake na neema.

Sala: Bwana, upendo wako unaniambia kwamba niungame na kurudi kwako. Kujitakia kwangu haki kunanifunga mimi nishindwe kuona makosa yangu. Ninaomba neema yako inisaidie mimi niweze kuona neema yako kama wewe unavyo niona mimi. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 14, 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 14, 2026
JUMAMOSI , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1
Hos. 5:15-6:6

Bwana asema: Katika taabu yao watanitafuta kwa bidii:
Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tuataishi mbele zake. Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyeshayo nchi.

Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema. Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinya vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa change na hukumu yangu itatokea kama mwanga. Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 51:1-2, 16-19 (K) Hos. 6:6

(K) Ninavyotaka ni fadhili, si sadaka.

Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu. (K)

Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,
Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
Dhabihu za MUngu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau. (K)

Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,
Uzijenge kuta za Yerusalemu.
Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,
Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. (K)



SHANGILIO
Eze. 18:3

Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa yote, asema Bwana, jifanyieni moy mpya na roho mpya.



INJILI
Lk. 18:9-14

Yesu aliwaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mpato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

CHAGUA KUMPENDA MUNGU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kwaresima
Ijumaa, Machi 13, 2026, 
Juma la 3 la Kwaresima

Hos 14:2-10;
Zab 81:6-11,14,17;
Mk 12:28-34

CHAGUA KUMPENDA MUNGU!

Mwandishi alimuuliza Yesu, “ni amri ipi iliyokuu?” na Yesu akajibu ni “Upendo”. Upendo tunao ufahamu na kuhisi katika maisha ni “hali ya kujisikia/kuhisi kutoka ndani mwetu”; hisia, au hali ya kujisikia tunayo ilinganisha na vitu tulivyopokea au kutamani. Katika hali fulani vitu na watu huongoza upendo wetu.

Lakini, anachosema Yesu kuhusu “upendo” ni kitu kingine tofauti. Huu ni upendo ambao tunaweza kuumudu, tunao amua kuutoa. Mungu haitaji upendo wetu ili yeye aweze kuishi. Lakini ameamua kutupatia maisha. Hii si kwasababu anatuhitaji sisi, bali kwasababu anapenda kuutoa. Hii ndio maana ya upendo wa Mungu usio na masharti. Anachotaka Mungu kutoka kwetu ni kuchagua kumpenda yeye kama yeye alivyo chagua kutupenda sisi. Na tunapo fanya hivyo tunapokea upendo wake zaidi, kwani tunabaki katika upendo wake. Kwahiyo, leo tuchague kumpenda Mungu kwa akili zetu zote, na hapo hatutakuwa mbali na ufalme wake.

Hatua ya kwanza katika kumpenda Mungu ni kutaka kumfahamu. Hii ina maana tunapaswa kutafuta jinsi ya kumfahamu, na kutaka kumuelewa na kumwamini Mungu na yote yaliyo funuliwa kwetu kuhusu yeye. Ina maana tumeamua kujikita katika kuingia kufahamu mafumbo ya maisha ya Mungu, hasa kwa njia ya Maandiko Matakatifu na kwa njia ya ufunuo wa mafundisho ya Kanisa katika historia ya Kanisa. Pili, tunaingia katika undani kwa kufuata njia zake. Jambo hili la uhuru kamili linapaswa kufuata akili yetu kuhusu yeye na kuwa kitendo cha Imani kwake. Tatu, tunapo ingia katika kutaka kuyaelewa mafumbo ya maisha ya Kimungu na kuchagua kumwamini na yote aliyo tufunulia, tutaona maisha yetu yatabadilika. Njia maalumu itakayo badilika ni kwamba tuta tamani kuwa na Mungu na kufanya mapenzi yake katika maisha yetu, tuta tamani kumtafuta zaidi, tutapata furaha kwa kumfuata na tuta tambua kuwa upendo wa roho yetu kama wanadamu utazama katika upendo wake na katika njia yake. Tafakari ni mara ngapi umetamani kumfahamu Yesu na kutaka kufahamu yote aliyo tufunulia.

Sala: Bwana, ninaomba niwe mwaminifu katika kujikita kwangu ili niweze kukufahamu zaidi na kufahamu ukweli wa utukufu wa maisha yako. Ninakushukuru kwa yote ulionifunulia mimi na ninajitolea maisha yangu, leo, katika harakati za kufahamu maisha yako na ufunuo wako. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 13, 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 13, 2026
IJUMAA , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1
Hos. 14:2-9

Bwana asema: Ee Israeli, mrudie Bwana, Mungu wako; maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako. Chukueni maneno pamoja nayi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo tutakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe. Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaimbia tena kazi ya mikono yutu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema.

Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha. Nitakuwa kama umande kwa Israeli; naye atachanua maua kama nyinyoro, na kuieneza miziz yake kama Lebanoni. Matawi yake yatatandaa, na uzuri wake utakuwa kama uzuri wa mzeituni, na harufu yake kama Lebanoni.

Na wao wakaao chini ya uvuli wake w2atarejea; watafufuka kama ngano, na kuchanua maua kama mzabibu; harufuyake itakuwa kama harufu ya divai ya Lebanoni. Efraimu atasema, Mimi nina nini tena na sanamu? Mimi nimeitika, nami nitamwangalia. Mimi ni kama mberoshi wenye majani mabichi. Kwangu mimi yamepatikana matunda yako.

Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 81:6-10, 13, 16 (K) 10, 11

(K) Mimi ndimi Bwana Mungu wako, Sikiliza sauti yangu.

Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Nimelitenga bega lake na mzigo,
Mikono yake ikaachana na kikapu.
Katika shida uliniita nikakuokoa. (K)

Nalikuitikia katika sitara ya radi;
Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,
Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza. (K)

Usiwe na mungu mgeni ndani yako;
Wala usimsujudie mungu mwingine.
Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,
Niliyekupandisha toka nchi ya Misri. (K)

Laiti watu wangu wangenisikiliza,
Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano,
Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani. (K)


SHANGILIO
Zab. 95:7, 8

Leo msifanye migumu mioyo yenu; 
Lakini msikie sauti yake Bwana.


INJILI
Mk. 12:28-34

Mmojawapo wa waandishi alifika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza.

Yesu akamjibu, ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja. Nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.

Yule mwandishi akamwambia,Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye; na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhabihu zote pia. Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

JE, TUME NYAMAZISHWA KUHUBIRI INJILI?


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kwaresima
Alhamisi, Machi 12, 2026
Juma la 3 la Kwaresima

Yer 7:23-28;
Zab 95:1-2, 6-9;
Lk 11:14-23


JE, TUME NYAMAZISHWA KUHUBIRI INJILI?

Leo, katika Injili Yesu analaumiwa kwa kutoa pepo kwa kutumia mkuu wa pepo. Wapinzani wa Yesu walishindwa kuona kidole cha Mungu ndani ya Yesu kwa huruma yake kwa wagonjwa. Hali hii inaonesha wazi kutokuamini kwa Mafarisayo na viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ni Masiha. Injili ya leo inaongeleo mtu ambaye alikuwa bubu kwasababu ya pepo. Wakati pepo alivyotolewa na Yesu, huyu mtu aliyekuwa bubu alianza kuongea, watu wakashangaa sana. Ni hakika kwamba huyu pepo alikuwa amemshika huyu mtu kiasi kwamba alikandamizwa kabisa mpaka akashindwa kuongea. Baada ya kuwekwa huru kutoka katika huyu pepo, ana anza kuongea kwa uhuru.

Ingawaje hatuwezi kuhisi uwepo wa pepo katika hali kama hii, lakini katika hali fulani tunakutana na ukandamizaji kama wa huyu pepo wa kutufanya tubaki kimya. Yule muovu anajaribu kutuogopesha kiasi kwamba tunakuwa waoga kutangaza Injili kwa uhuru na kwa uaminifu, na kwa jinsi Mungu anavyopenda ujumbe wake uwafikie watu. “pepo wa ububu” anaweza kututawala, kutuchanganya au kutujaza hofu fulani wakati muda umefika wa kushirikisha Imani yetu na wengine. Ingawaje ni vigumu kuanguka moja kwa moja mikononi mwao, lakini mara nyingi tunajaribiwa kila mara na wao. Yesu ana nguvu kamilifu juu ya pepo wa aina zote, yeye hasiti kuwanyamazisha pepo hao kama ukimruhusu. Yesu anataka kutuweka huru ili tuweze kuongea kwa kuhubiri neno lake la upendo bila kujibakiza ili wengine waweze kumfahamu yeye na upendo wake mkamilifu. Mwache yeye akutumie kama moja ya chombo cha ukweli na upendo.

Sala: Bwana, wakati mwingine naingiwa na hofu na kuwa kimya na kushindwa kutangaza neno lako vizuri kwa wale wahitaji. Wakati mwingine nahisi kama nimefungwa kinywa kuongea, au kuchanganyikiwa niseme nini. Bwana naomba unifungue kinywa changu niweze kuongea, Bwana wangu, ili niweze kuwa chombo chako kitakatifu cha neno lako na kwa ujasiri na uaminifu niweze kutangaza neno lako kwa wote walio wahitaji. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Tendo la Kwaresima: Andika mistari yenye ujumbe kutoka katika Biblia - inagonga katika mioyo ya watu na kuacha uvuvio. Tunaomba neno la Mungu liwainue kutoka katika  matatizo yao. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 12, 2026


MASOMO YA MISA, MACHI 12, 2026
ALHAMISI, JUMA  LA 3 LA KWARESIMA


SOMO 1
Yer. 7:23-28

Naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru, mpate kufanikiwa. Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kw amashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele. Tokea siku ile baba zenu walipotoka katika nchi ya Misri hata leo, nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu ninyi, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma. Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao. Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya Bwana, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali vinywa vyao.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 95:1-2, 6-9 (K) 7

(K) Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu.

Njoni, tumwimbie Bwana,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)

Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.
Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
Kama vile huko Meriba,
Kama siku ya Masa jangwani.
Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)


SHANGILIO
Zab. 51:10, 12

Ee Mungu, uniumbie moyo safi, 
Unirudishie furaha ya wokovu wako.


INJILI
Lk. 11:14-23

Yesu alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu. Wengine wao wakasema, Atoa pepo kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo. Wengine walimjaribu, wakitaka ishara itokayo mbinguni. Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka. Basi, ikiwa Shetani naye amefitinika juu ya nafsi yake, ufalme wake utasimamaje? Kwa kuwa ninyi mnasema kwamba mimi natoa pepo kwa Beelzebuli, wana wenu je! Huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo, hao ndio watakaowahukumu. Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama; lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang’anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake.

Mtu ambaye si pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

YESU: UTIMILIFU WA SHERIA



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kwaresima
Jumatano, Machi 11, 2026 
Juma la 3 la Mwaka wa Kanisa

Kumb 4:1, 5-9
Zab 147: 12-13,15-16,19-20;
Mt 5:17-19

YESU: UTIMILIFU WA SHERIA

Masomo ya leo yanatupa picha kuhusu sheria ya Mungu. Ni za taratibu na kamilifu. Yesu alifanya kurejea “sheria na Manabii” akisema kwamba hakuja kutengua sheria za manabii bali kuzitimiza. Zilikuja kutimizwa baada ya miaka elfu na zaidi. Ilichukuwa muda kwa utimilifu wa mpango wa Mungu kujifunua. Lakini ulijifungua kwa wakati wake na kwa jinsi yake. Ni hakika, wale wote waliokuwa katika Kipindi cha Agano la Kale walikuwa na shauku ya Masiha kuja ili kutimiza vitu vyote. Nabii baada ya nabii alikuja akinyoosha kidole mbele kwa wakati ujao kwamba Masiha atakuja. Hata sheria za Agano la Kale katika hali Fulani zilikuwa ni kwa ajili ya kuwaandaa watu wa Mungu kwa ajili ya ujio wa Masiha. Lakini ilikuwa ni hali ya taratibu ya kutengeneza sheria, kuziweka kwa watu wa Israeli, kuwasaidia ili kuzielewa, na kuanza kuziishi. Hata Masiha alivyokuja, kuna wengine kwasababu ya shauku na furaha walitaka atimize yote kwa wakati mmoja. Walitaka Ufalme wao wa dunia uanzishwe na walitaka Masiha wao mpya achukue Ufalme wake.

Lakini mpango wa Mungu ni tofauti kabisa na hekima ya Binadamu. Njia zake zilikuwa tofauti kabisa na njia zetu. Na njia zake zikaendelea kuwa mbali kabisa na njia zetu! Yesu alitimiza kila sheria katika Agano la Kale na Manabii, na si kama vile watu walivyokuwa wanadhani. Wayahudi wakati wa Yesu walikuwa wamejikita mno katika sheria binafsi na mapokeo katika sheria ya Musa kiasi kwamba walipoteza picha halisi. Iliwawia vigumu kumtambua Yesu kwamba yeye mwenyewe ndiye mtimilifu wa sheria, kwamba alikuwa sheria ya Mungu iliochukuwa umwilisho. Kwa maneno yake na matendo yake alileta sheria katika maisha. Sio tena mlolongo wa Maandishi, sheria sasa zilikuwa kitu cha kuishi katika uhalisia na kila mtu alihisi. Tafakari kwa kujitafiti mwenyewe kama nawe ni mtu wa kuangalia tu karibu kama Wayahudi! Je, unamuona Yesu kama anayeishi na mtilifu wa sheria?

Sala: Bwana, ninakabidhi maisha yangu kwako. Nina amini kwamba una mpango kamili kwangu na kwa watoto wako wapendwa. Nipe subira niweze kukusubiri wewe na nikuache wewe ulete mapenzi yako ya Kimungu yatimie katika maisha yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 11, 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 11, 2026
JUMATANO, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1
Kumb. 4:1, 5-9

Musa aliwaambia makutano: Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mmzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.

Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwmingiayo ili kuimiliki. Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili. Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo? Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.

Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 147:12-13, 15-16, 19-20 (K) 12

(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana.
Ndiye atoaye theluji kama sufu,
Huimwaga barafu yake kama majivu. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua. (K)


SHANGILIO

Mbegu neno la Mungu, 
mpanzi lakini ni Kristu; 
Yeyote ampataye, ataishi milele.


INJILI
Mt. 5:17-19

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.