Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

USIOGOPE




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumapili, Agosti 9 2026
Juma la 19 la Mwaka

1 Fal. 19:9, 11-13
Zab. 85 :8-13, (K)7
Rum 9: 1-5
Mt 14:22-33


USIOGOPE

Upo msemo usemao “bahari shwari haitoi wanamaji stadi.” Bahari yenye mawimbi mazito huwaimarisha wanamaji wake. Matatizo kama mawimbi yanaweza kukuimarisha. Tuwe tayari kuyapokea mawimbi yanayojitokeza ndani ya maisha yetu. Kuwa na mtazamo hasi dhidi ya matatizo ni kama kupambana na ukuta. “Wavuvi wanajua kuwa bahari ni hatari na ina dhoruba za kuogopesha, lakini hawajawahi kuona hatari hizi kama sababu tosha za kubaki kandokando ya bahari au ufukweni,” alisema Vincent van Goth. Wavuvi hujitosa kwenye maji marefu. Wavuvi ni mfano wa kuigwa tunapokumbana na mawimbi ya matatizo katika bahari ya maisha. Kuna mtu aliyemwambia mvuvi hivi: “wewe hauogopi kwenda baharini kuvua samaki? Mjomba wako, kaka yako na babu yako wote walikufa maji, kwa nini hauogopi?” Mvuvi alijibu hivi: “watu wengi hufa wakiwa vitandani lakini watu hawaachi kulala vitandani.” “Kuna mambo ambayo unajifunza vizuri sana wakati kuna utulivu na mengine wakati kuna dhoruba,” alisema Willa Cather

Kwa Yesu si kila mara mawingu yalibaki bluu. Kuna wakati wingu lilikuwa jeusi likiashiria dhoruba na matatizo. Alikataliwa na wasamaria katika kijiji cha Wasamaria (Lk 9:51-56). Pia kwa Ayubu mawingu hayakuwa kila mara ya bluu. Katikati ya mawimbi ya matatizo, Ayubu alizidi kuimarika. Ni kama jani la chai linapata nguvu ya kugeuza rangi ya maji likiwa kwenye maji moto. Ukiwa kwenye mawimbi ya matatizo kumbuka ukweli huu: Kwanza, tuko salama kwenye mawimbi ya matatizo tukiwa na Mungu kuliko tukiwa pasipokuwa na mawimbi ya matatizo bila Mungu. Mungu anaweza kutuliza mawimbi au akayaacha mawimbi akamtuliza binadamu. Pili, maisha bila mawimbi ya matatizo hufanya uwezekano wa mazuri kuwa sifuri. Tatu, tukumbuke kwamba joto likizidi, kutanuka kunazidi-matatizo makubwa yanaweza kukufanya uwe mkubwa. Kuna methali isemayo: “anayesema sijawahi kuliona jambo hili, si mkubwa kiumri.” Nne, ukiomba mvua inyeshe-kuwa tayari kukanyaga matope. Tano, tambua kwamba mawimbi ya matatizo yanakujia ili kukuimarisha na si kukudhoofisha.


“Ewe mwenye imani haba mbona uliona shaka” (Mathayo 14:31) Maisha ni kigeugeu. Mambo yalimgeuka mtume Petro. Petro alikuwa mtu wa kufanya maamuzi kwa ghafla na haraka. Hakufikiri sana kabla ya kutenda. Jambo hili pengine ni busara likilinganishwa na mtu ambaye anafikiri sana mwishowe hatendi lolote. Katika nafsi ya Petro, kuna mchanganyiko wa mambo. Anatamani kuwa na Yesu. Pia anatamani kuonesha kuwa anaweza kutenda analolitenda Yesu: kutembea juu ya maji. Kuna upendo na majivuno kama ilivyo kwa kila mmoja wetu. Petro ana ujasiri na woga. Anaanza vizuri, anaona dhoruba na kuogopa. Anakosa imani.

Sababu kubwa ya kupotea kwa imani ya Petro ni kwa kuwa macho yake, mawazo yake na moyo wake alivielekeza kwenye dhoruba badala ya Kristu. Alipomtazama Yesu Kristu, imani ilipatikana akalia kwa sauti, “ Bwana, niokoe!” (Mt 14; 30). Licha ya Petro kuwa na imani haba, Yesu alimuokoa. “Hapo, Yesu akanyosha mkono wake, akamshika … wakapanda mashuani, na upepo ukakoma” (Mt 14: 31-32). Nasi tunapambana na matatizo. Matatizo ya siku hizi ni kama: umasikini, makazi duni, ukosefu wa kazi, magonjwa yasiyo na tiba, ukosefu wa riziki, uzinifu, uzazi kwa namna isiyo halali, ukatili na vita, ukabila- damu inakuwa nzito kuliko maji ya ubatizo. Tumwombe Yesu atuokoe.

Katika kilele cha dhoruba, Yesu alijitokeza. Katika kilele cha hatari, katika upeo wa wasiwasi, Yesu alijitokeza. Anakuja wakati ambapo hategemewi kabisa. Mitume walifikiri ni mzuka wakauotea mbali. Yesu ni Mkombozi tunayeweza kumkimbilia. Alifanya kile ambacho binadamu hawezi kufanya. Alitembea juu ya maji. Vile ambavyo hatuwezi kufanya tumuachie yeye. Wakati tunapozama kwenye bahari ya matatizo, tulie kwa sauti: “Bwana utuokoe !” Shibisha imani yako na mashaka yako. Imani ikiongezeka, mashaka yanapungua na kinyume chake ni kweli. “Imani si kujaribu kuamini jambo bila ya kuzingatia ushahidi: imani ni kujaribu kufanya jambo bila kuzingatia matokeo,” alisema Sherwood Eddy. “Wanashinda wale wanaoamini wanaweza,” alisema Virgil. Ni katika mtazamo huo Erasmus alisema, “Amini kuwa unacho na unakuwa nacho.” Swali kubwa hapa si kuwa una imani au hauna imani. Jambo la msingi ni imani katika nini na imani katika nani. Ili kufanikiwa na kushinda, unahitaji kuwa na imani katika Mungu na kujiamini hata ikiwa imani ndogo au haba inatosha kukuondolea vikwazo, vihunzi na vizingiti. Tunasoma hivi katika Biblia, mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani. Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii” (Luka 17: 5-6).

Kifungu cha Biblia hicho kinabainisha ukweli huu, imani kidogo yaweza kufanya mambo makubwa. Ni ukweli unaoendana na ujumbe wa methali ya Kiswahili, “Kidogo kidogo kamba ukatika.” Nguvu ya mbegu haitegemei ukubwa au udogo wake inategemea uhai uliofichwa katika mbegu hiyo. Kuna nguvu ambayo imefichwa ndani mwako. Kama ni hivyo unahitaji kujiamini kuwa utaweza kufanikiwa katika maisha. Kwa imani na kujiamini ndege imevumbuliwa. Kwa imani na kujiamini, simu za mkononi zimegunduliwa. Kwa imani na kujiamini utalaamu wa kutengeneza runinga umefunuliwa.

Mitume walipoomba kuongezewa imani, Yesu hakusema nimewaongezea imani. Hakuahidi kuwaongezea imani. Ni kama aliwaambia anza na mlicho nacho, kidogo huvuta kikubwa, kidogo huzaa kikubwa, laini huzaa ngumu. Walikuwa kama mfanyabiashara asemaye nina pesa kidogo sana ngoja iwe nyingi ndipo nianze kufanya biashara. Je, itaongezekaje bila kuzalisha, kuuza na kununua? Walikuwa kama mkulima asemaye ‘nina mbegu lakini hazitoshi nitalima nikiwa na mbegu za kutosha.’ Anza na ulicho nacho. Hawezi kusema sina pesa yote ya kujenga na kumalizia nyumba. Anza kujenga na pesa uliyo nayo. Ili kuwa na zaidi, anza na ulicho nacho. Aliyenacho ataongezewa-ndivyo Bwana Yesu alivyofundisha.

Imani ni ufunguo wa mafanikio. Na sifa ya mtu anayefanikiwa ni kuwa ana imani. Imani kamili ndiyo kumtegemea Mungu na kumtumaini na kumtii. Tukiwa na imani kwa Mungu twaweza kusema, “Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa” (Waebrania 13:6). Hatuna budi kuwa na imani na uwezo Mungu aliotujalia yaani kujiamini. Kuna hadithi juu ya wakristu ambao walimuomba mchungaji wakati wa ibada ya Jumapili iliyokuwa inafuata waombe kupata mvua baada ya mvua kutonyesha kwa kipindi cha muda mrefu. Walishangaa siku hiyo ya maombi ya Jumapili mchungaji aliposema hayuko tayari kuomba kupata mvua maana watu hawaonyeshi imani kwa vile hawakwenda na miavuli ya kujikinga mvua. Imani lazima ionekane katika matendo. Mungu anasaidia na wewe unaweka juhudi na maarifa. Henry Ford alisema, “Kama unaamini unaweza kufanya jambo fulani au hauamini kama unaweza kufanya jambo fulani, uko sawa.” Usipoamini kwamba jambo fulani linaweza kufanyika, halitafanyika. Ukiamini, litafanyika. Imani inafukuza mashaka kama mwanga ufukuzavyo giza. Mashaka yakibisha hodi mlangoni mwako, itume imani-ijibu mashaka. Sala yetu iwe kama ya kijana mmoja kwenye Biblia, “Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu” (Marko 9: 24).

Dunia ni bahari yenye mawimbi-inahitaji wanamaji stadi. Duniani kuna mengi sawasawa na bahari. Kuna papa na nyangumi tena wale wa hatari. Lakini ukweli unabaki: Bahari shwari haitoi wana maji stadi. Bahari iliyotulia haiwezi kuwatoa wanamaji hodari. Kuna methali ya Kiswahili isemayo: Bahari haishi zinge. Zinge ni machafuko ya mara kwa mara (mabadiliko ya ghafla). Bahari daima imo katika mabadiliko wala haitabiriki. Maisha kama vile bahari yamejawa na mema na maovu na yanapotujia sharti tuwe tayari kuyakabili. Tukabili mawimbi kwa utulivu bila hofu. Tukabili mawimbi ya mawazo mabaya, mahusiano mabaya na kushindwa.

Sala: Ee Bwana ninakuomba unipe imani niweze kupambana na dhoruba za maisha nikitambua kwamba hakuna mawimbi yasiyokuwa na Mwisho. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 9, 2026



MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 9, 2026
JUMA LA 19 LA MWAKA 


SOMO 1
1 Fal. 19:9, 11-13

Eliya alifika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia. Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi: na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu. Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi vake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 85 :8-13, (K)7

(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.

Nisikie atakavyosema Mungu Bwana,
Maana atawambia watu wake amani.
Hakika wokovu wake u karibu na wamchao,
Utukufu ukae katika nchi yetu. (K)

Fadhili na kweli zimekutana,
Haki na amani zimebusiana.
Kweli imechipuka katika nchi,
Haki imechungulia kutoka mbinguni. (K)

Naam, Bwana atatoa kilicho chema,
Na nchi yetu itatoa mazao yake.
Haki itakwenda mbelc zake,
Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia. (K)


SOMO 2 
Rum 9: 1-5

Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, ya
kwamba nina huzuni nyingi  na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu. Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili; ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu 


SHANGILIO 
Lk. 19:38

Aleluya, aleluya, 
Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana;
Aleluya.


INJILI 
Ml 14:22-33

Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambe. wakati yeye alipokuwa akiwaaga makutano. Nave alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea. akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli, wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akanena, akawaambia, Jipeni movo; ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma. Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia wakisema, Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

IMANI KUBWA!

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 8 2026
Juma la 18 la Mwaka
 
Hab. 1: 12 - 2: 4;
Zab. 9 : 7-12 (K) 10;
Mt 17: 14-20.
 
 
IMANI KUBWA!

 

Katika Injili ya leo, baada ya wanafunzi wa Yesu kurudi katika utume wao, walishangaa kwanini hawakuweza kumponya kijana aliyekuwa ana pepo mchafu. “kasababu ya Imani yenu ndogo” Yesu aliwaambia. Mngekua na Imani ndogo kama chembe ya haradani” aliwaambia, “hakuna chochote ambacho kingeshindikana kwenu”.Mwaliko huu wa Yesu sio kiingiilio cha kumpa rushwa Mungu atafanyie maajabu, bali ni mwito wa kuweka matumaini yetu yote kwake kwa chochote kitokeacho kwetu, yeye tayari ajua lipi bora kwetu kulingana na mapenzi yake.Imani hii ikiwa ndani ya upendo mkuu, ndio iletayo furaha na amani katika maisha yetu, hata katika kipindi kigumu cha maisha yake.

 

Sala: Ee Bwana, Nakutumainia wewe. Amina.

 

------------------------

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, AGOSTI 8, 2026





MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, AGOSTI 8, 2026
JUMA LA 18 LA MWAKA

SOMO 1
Hab. 1: 12 - 2: 4

Ee Bwana, Mungu wangu, mtakatifu wangu, wewe si wa milele? hatutakufa. Ee Bwana, umemwandikia hukumu, nawe, Ee Jabali, umemweka imara ili aadhibishwe.

Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu. wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya. hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye; na kufanva wanadamu kuwa kama samaki wa baharini, kama vitu vitambaavyo. ambavyo havina mtawala?

Yeye huwatoa wote kwa ndoana yake, huwakamata katika wavu wake, na kuwakusanya katika
juya lake: ndiyo sababu afurahi na kupendezwa. 

Kwa sababu hiyo huutolea wavu wake sadaka, na kulifukizia uvumba juya lake; kwa sababu kwa vitu vile fungu lake limenona, na chakula chake kimekuwa tele.

Je! atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima? Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara. nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomave apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia. ingojee: kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia. Tazama. roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 9 : 7-12 (K) 10

(K) Wewe Bwana, hukuwaacha wakutafutao.

Bwana atakaa milele,
Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu.
Nave atauhukumu ulimwengu kwa haki;
Atawaamua watu kwa adili. (K)

Bwana atakuwa ngome kwake aliyeonewa,
Naam, ngome kwa nyakati ya shida.
Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe,
Maana Wewe, Bwana, hukuwaacha wakutafutao. (K)

Mwimbieni Bwana akaaye Sayuni,
Yatangazeni kati ya watu matendo yake.
Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka,
Hakukisahau kilio cha wanyonge. (K)


SHANGILIO 
Yn. 10: 27

Aleluya, aleluya,
Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata.
Aleluya.



INJILI

Mt. 17: 14-20

 

Mtu mmoja alimjia Yesu, akampigia magoti, akisema, Bwana, umrehemu mwanangu, kwa kuwa ana kifafa, na kuteswa vibaya; maana mara nyingi huanguka motoni, na mara nyingi majini. Nikamleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponva. Yesu akajibu, akasema. Envi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu. Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile.

 

Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema, Mbona sisi hatukuweza ku- mtoa? Yesu akawaambia, Kwa sababu va upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. 


Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUPOTEZA MAISHA YA NAFSI ILI KUPATA YOTE!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Agosti 7, 2026, 
Juma la 18 la Mwaka

Nah 2:1, 3:1-3, 6-7; 
Kumb 32:35, 39, 41; 
Mt 16:24-28


KUPOTEZA MAISHA YA NAFSI ILI KUPATA YOTE!

Yesu anatuambia katika Injili kwamba, ni lazima kujikana nafsi ili kumfuata. Kujikana maana yake ni, kutokujibakiza, kutokujijengea heshima, kukataa, kujiachia, kujiweka huru kutoka mambo ya vionjo binafsi. Ni kusema “Ndio” kwa Kristo na kusema “Hapana” kwa nafsi. Sababu ya kujikana ni kwamba mioyo yetu ni muhimu zaidi kuliko ulimwengu mzima. Mwanadamu akishapoteza roho yake, imepotea haiwezi kununuliwa popote nakurudishwa. Mwanadamu atakaye ipoteza, ameipoteza milele. Msalaba unaonekana katika hali ya kawaida kama mateso na kupoteza, lakini kwa kweli ni faida. Sadaka ya Kristo Msalabani imekuwa fidia kubwa kwetu na kuleta wokovu. Je nipo tayari kujikana mwenyewe, kuchukua msalaba wangu na kumfuata Kristo? 

Sala: Mungu wangu, Mungu wangu, chukua yote kwangu yanayoniweka mbali nawe, Mungu wangu, Mungu wangu, nipe yote yanayo nileta karibu nawe, Mungu wangu, Mungu wangu, chukua ubinafsi ndani yangu na unipe yote katika wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 7, 2026




MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 7, 2026
JUMA LA 18 LA MWAKA

SOMO 1
Nah. 1:15; 2:2; 3:1-3, 6-7

Tazama juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema, atangazaye Amani. Zishike sikukuu zako, Ee Yuda, uziondoe nadhiri zako; kwa maana yule asiyefaa kitu hatapita kati yako tena kamwe; amekwisha kukatiliwa mbali.

Kwa maana Bwana anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.

Ole wake mji wa damu! Umejaa mambo ya uongo na unyang’anyi; mateka hayaondoki. Kelele za mjeledi, kelele za magurudumu yafanyayo kishindo; na farasi wenye kupara-para, na magari ya vita yenye kuruka-ruka; mpanda farasi akipanga, na upanga ukimeta-meta, na mkuki ukimemetuka; na wingi wa waliouawa, na chungu kubwa ya mizoga; mizoga haina mwisho; wanajikwaa juu ya mizoga yao. Nani nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dahrau. Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji?

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


WIMBO WA KATIKATI
Kum. 32: 35 – 36, 39, 41 (K) 39

(K) Naua Mimi, nahuisha Mimi.

Maana siku ya msiba wao imekaribia,
Na mambo yatakayowapata yatafanya haraka.
Kwa kuwa Bwana atawaamua watu wake,
Atawahurumia watumwa wake. (K)

Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye.
Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi;
Naua Mimi, nahuisha Mimi,
Nimejeruhi, tena naponya. (K)

Nikiuonoa upanga wangu wa umeme,
Mkono wangu ukishika hukumu,
Nitawatoza kisasi adui zangu,
Nitawalipa wanaonichukia. (K)


SHANGILIO
Lk. 8:15

Aleluya, aleluya,
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno la Mungu, na kulishika.
Aleluya.


INJILI
Mt. 16:24-28

Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 

Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake. 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUITWA KWENYE UTUKUFU!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Agosti 6, 2026 
Tafakari ya kila siku
Juma la 18 la Mwaka Kanisa

Sikukuu ya Kung’ara Bwana wetu 

Dan 7:9-10, 13-14; 
Zab 96:1-2, 5-6, 9; 
2Pet 1:16-19;
Lk 9: 28-36


KUITWA KWENYE UTUKUFU!


Kuna nyakati mbili katika Kalenda ya Lirtujia tunapopata nafasi ya kutafakari juu ya tukio la Kung’ara Bwana, jumapili ya pili ya kwaresima kudhihirisha Umungu wa Kristo kabla ya mateso na kifo, na siku nyingine ni tarehe kama ya leo, tunaadhimisha kutukuka kwa utukufu wa Kristo. Zaidi ya yote Kung’ara Bwana kunaonesha ukweli wa Utatu Mtakatifu: Baba katika sauti, Mwana katika Yesu, Roho katika wingu jeupe linalo nga’ara. Mungu hapa anatupa nafasi yakuona ukuu wake katika maisha ya Utatu. Mt. Leo Mkuu anasema “Lengo kuu la Kung’ara Bwana ilikuwa ni kuondoa ndani ya mioyo ya wafuasi aibu ya Msalaba”. Kati ya mambo mengi tuangalie mambo mawili leo; la kwanza, Yesu ni Mungu kamili na mwanadamu kamili. Maisha yake na mafundisho yake hayajaletwa na mwanandamu. Maneno yake sio tuu maneno ya kawaida. Ni Mungu mwenyewe anayeongea na sisi kupitia Mwanaye wa pekee, Yesu Kristo. La pili, tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na tunaitwa katika maisha ya furaha ya milele, mwili na roho mbinguni. Siku hizi katika jamii zetu tunaona wengi hawajali utu wa mwanadamu (utoaji mimba, kuua mtu kwa kumchoma sindano za dawa kwakisingizio kwamba anateseka mno bora apumzike-najiuliza unawezaje kuondoa mateso ya mtu kwa kumuua?, tunaona pia sheria za kuwanyonga watu, vita na mengine mengi). Tutambue na tusisahau kwamba mwanadamu ni kiumbe pekee duniani ambacho Mungu amependa mwenyewe kwa kumuita kushiriki, kwa njia ya akili, utashi na upendo katika maisha ya Kimungu. 

Sala: Mungu Baba yetu mpendwa, tunakuomba tuige maisha ya Mwanao mpendwa Yesu Kristo yawe maisha yetu. Na hapo tutakuwa na furaha iliyo ndani yetu kama watoto wa Mungu. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA - TAREHE 6, AGOSTI, 2026



MASOMO YA MISA - TAREHE 6, AGOSTI, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 18 LA MWAKA

SIKUKUU YA KUNG’ARA BWANA WETU


SOMO 1 
Dan 7: 9-10, 13-14

Mimi nilitazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.

Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu nave. Nave akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo haitapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 97: 1-2, 5-6, 9 (K) 1, 9 

(K) Bwana ametamalaki, juu sana kuliko nchi yote.

Bwana ametamalaki, nchi na ishangilie,
Visiwa vingi na vifurahi.
Mawingu na giza vyamzunguka,
Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake. (K)

Milima iliyeyuka kama nta mbele za Bwana,
Mbele za Bwana wa dunia yote.
Mbingu zimetangaza haki yake,
Na watu wote wameuona utukufu wake. (K)

Maana Wewe, Bwana, ndiwe Uliye juu,
Juu sana kuliko nchi yote;
Umetukuka sana juu ya miungu yote. (K)


SOMO 2 
2 Pet. 1:16-19

Hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.

Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing’aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


SHANGILIO 
Mt 17: 5

Aleluya, aleluya,
Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye, msikieni yeye.
Aleluya.


INJILI 
Mk 9: 2-10

Yesu aliwatw’aa Petro, na Yakobo, na Yohanc, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani, peke yao; akageuka sura yake mbele yao; mavazi yake yakimeta-meta, meupe mno, jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe. Wakatokewa na Eliya pamoja na Musa, nao walikuwa wakizungumza na Yesu. Petro akajibu, akamwambia Yesu, Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. Maana, hakujua la kunena, kwa kuwa waliingiwa na hofu nyingi. Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile w'ingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye. Mara hiyo wralipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.

Na walipokuwa wakishuka mlimani aliwakataza wasimweleze mtu waliyoyaona, hata Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka katika wafu. Wakalishika neno lile, wakiulizana wao kwa wao, Huko kufufuka katika wafu maana yake nini?

Neno la Bwana...Sifa kwako, Ee Kristo



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

WOTE NI WATOTO WA MUNGU!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Agosti 5, 2026 
Tafakari ya kila siku
Juma la 18 la Mwaka wa Kanisa


Yer. 31:1-7;
Yer. 31:10-13 (K) 10;
Mt 15: 21-28


WOTE NI WATOTO WA MUNGU!


Mwanamke Mkanaani katika Injili anakuwa kielelezo cha Imani. Ni mmoja wa wana Wakanaani, maadui wakubwa wa Waisraeli katika Biblia ambao kwa upagani wao waliwasababisha Waisraeli wamuache Mungu na kuabudu miungu ya uongo.

Yesu hamlaani mwanamke bali anajaribu kuonesha kwamba hakutumwa kwa ajili yao. Ni wazi kwamba alitaka kumpima, kama mwalimu wakati mwingine aliwajaribu wafuasi wake, ila kwakweli alikuwa tayari kujibu ombi lake lakini alijaribu kuweka kikwazo kwa Imani yake. Bilashaka Yesu alitaka mwanamke atambue utume wa kweli wa Yesu na kwamba Yesu ninani. Pia alimtaka atambue upendeleo wa Waisraeli katika mpango wa Mungu, utambuzi ambao utamfanya akiri umuhimu wake wa kujitegemeza kwa Mungu wa kweli. 

Yule mwanamke kwa kumuita Yesu Mwana wa Daudi, tayari ameshamkiri yeye kama Mfalme wa kweli wa taifa ambalo lilishinda juu ya taifa la mababu zake- mkuu zaidi ya wale waliotenda makubwa katika taifa lake. Na sasa anakataa kwakutokukubali kwamba utume wa Yesu ni kwaajili ya Waisraeli kwanza na kwamba yeye ni wa pili baada ya Waisraeli; lakini, anaamini kwamba Yesu atakuwa na nguvu zaidi kuliko hata ya ile wanayohitaji Waisraeli. Yesu anajibu kwasababu ya Imani hii jasiri. Yesu ana mkate wakutosha kwa wana wa Israeli, lakini maelezo yanayofuata yanatoa hakika kwamba yanabaki mengi kwaaajili ya wengine. Sisi tunao muamini Kristo tumekuwa taifa teule la Israeli Mpya. Mathayo alitaka kuwaambia watu wake kwamba, Waisraeli na wasio Waisraeli wote wanaweza kumfuata Mungu kwa Imani ndani ya Masiha, Kristo. 

Sala: Bwana, naomba watu wote wahisi upendo wako kwao kwa kupitia mimi. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUMATANO, AGOSTI 5, 2026




MASOMO YA MISA, JUMATANO, AGOSTI 5, 2026
JUMA LA 18 LA MWAKA 

KUMBUKUMBU YA HIARI YA KUTUBARUKIWA BASILIKA YA MAMA MARIA, ROMA


SOMO 1 
Yer. 31:1-7

Wakati huo, asema Bwana, nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli, nao watakuwa watu wangu.Bwana asema hivi, Watu wale walioachwa na upanga walipata neema jangwani; yaani, Israeli, hapo nilipokwenda kumstarehesha. Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam, nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu. Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli, mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi.

Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake. Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni. tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.

Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa. tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako mabaki ya Israeli.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Yer. 31:10-13 (K) 10

(K) Bwana atatulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.

Lisikieni neno la Bwana,
enyi mataifa, litangazeni visiwani mbali, 
mkaseme, Aliycmtawanya Israeli atamkusanya, 
na kumlinda, kama mchungaji alindavyo kundi lake 
Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo, 
amemkomboa mkononi mwake
aliyekuwa hodari kuliko yeye.(K) 

Nao watakuja, na kuimba katika mlima Sayuni, 
wataukimbilia wema wa Bwana, nafaka, na divai; 
na mafuta, na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe; 
na roho zao zitakuwa kama bustani iliyotiwa maji; 
wala hawatauzunika tena kabisa. (K)

Ndipo bikira atafurahi katika kucheza, 
na vijana na wazee pamoja;
maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha, 
nami nitawafariji,
na kuwafurahisha waache huzuni zao. (K)


SHANGILIO
Zab 119: 105

Aleluya, aleluya,
Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.
Aleluya.


INJILI 
Mt. 15: 21-28

Yesu aliondoka Genezareti akaenda kando pande za Tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana unisaidie. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukavo mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.