Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

NYUMBA MPYA, FAMILIA MPYA



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Juni 28, 2026.
Dominika ya 13 ya Mwaka

2 Fal 4: 8-11, 13-16;
Zab 88: 2-3, 16-19;
Rom 6: 3-4, 8-11;
Mt 10: 37-42.


NYUMBA MPYA, FAMILIA MPYA

Neno nyumba katika lugha ya Kiebrania haina maana tu ya jengo bali pia familia. Mtu hawezi kufanya lolote tofauti na maana hii: “kwa wengine ni vitu ambavyo huwezi kuishi bila hivyo: maji, chakula, nguo na nyumba kwa ajili ya makazi” (YbS 29:21). Lakini yule ambaya anataka kuanzisha familia mpya, anapaswa kuacha nyumba yake: “Mwanaume atamuacha Baba yake na mama yake na ataungana na mkewe na wote wawili takuwa mwili mmoja” (Mwa 2:24). Ni kitendo cha kuacha nyumba moja na kuingia katika nyumba nyingine au familia mpya. Yesu pia ana uacha mji wake mwenyewe Nazarethi, “Mwana wa mtu hana mahali pa kulaza kichwa chake” (Mt 8:20). Aliacha familia yake: ‘Mama yangu ni nani’? ‘Kaka zangu ni akina nani?’ na kwenda katika familia mpya ‘tazama! Wapo hapa mama yangu na kaka zangu (rejea. Mt 12:48-50). Kwa wale wote wanaopenda kumfuata Yesu, anawaambia wachukue jukumu hilo hilo: ujasiri wakujitenga, kuchukua hatua kubwa kuelekea katika ukweli halisi, kutambulishwa katika nyumba mpya, familia mpya, familia ya wana wa Mungu.

Katika somo la kwanza tunamuona nabii Elisha akibariki wana ndoa wawili, waliokuwa wana umri mkubwa bila kuwa na watoto, na hivyo anawahidia mtoto. Kwa kujua kwamba Elisha ametokea katika nchi ya mbali na hakuwa na nyumba wala familia alimkaribisha na kumshirikisha. Huyu mwanamke ambaye alikuwa tajiri, alikuwa na uwezo wa kumpatia Elisha fedha kidogo na kumwacha aondoke, lakini hakumpa tu msaada bali alimkaribisha pia nyumbani kwao, na kumkaribisha na kujisikia kama mmoja wao katika familia. Ishara anazofanya huyu mwanamke zina mfurahisha Mungu, na hivyo Mungu anampa furaha kubwa ambayo alikuwa akiitamani: alimpa mtoto wa kiume. Elisha ana wakilisha mitume, ambao hata leo, wana acha nyumba zao, nchi yao, familia zao na kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu na Injili.

Katika somo la pili, tunaona kwamba Ubatizo ulikuwa ni utamaduni uliokuwepo kipindi cha Yesu. Wale wote walioufuata walibatizwa. Ilikuwa ni ishara iliyo fanya mabadiliko makubwa katika maisha: kifo kwa mambo ya zamani na kuzaliwa upya. Hata ubatizo wa Kikristo una maana hiyo hiyo. Maji ya ubatizo yalichukuliwa kama maji tumboni mwa mama ambamo mtoto mdogo huishi katika mazingira hayo na baadaye huzaliwa kama mtoto wa Mungu. Paulo anasema “kwa njia ya ubatizo, tunazikwa pamoja na Kristo ili tufufuke naye katika maisha mapya” . kama ubatizo ni ishara ya kuzaliwa upya, ina dhihirisha mwanzo wa maisha yote ya maaldili mapya, mkristo hawezi kuendelea kutenda vitu vya zamani, anapaswa kuchukulia yeye mwenye kama mfu katika dhambi, na mzima na anayeishi kwa Mungu ndani ya Kristo”.

Katika Injili, Mathayo anaendeleza na utume wa wanafunzi wa Yesu. Kwanza kabisa, wito wa Yesu kuhusu ufuasi umeonesha katika hali yote. Kuacha na kukataa yote inahitajika katika maisha ya ufuasi. Kila agizo linafuatiwa na ugumu na hali ya kweli ya kuacha yote. Zaidi ya yote, Yesu anataka wafuasi wake kuondoka katika hali za ndani za hisia zao, kama vile kuwapenda wazazi au watoto.

Yesu hafanyi hivi kutaka kukataa sheria ya Musa (Torati), inayo amuru kuwa heshimu Baba na Mama. Ni hakika kwamba, ameirudia amri kwa msisitizo (Mt 15:4). Matayo ameandika Injili yake kipindi cha madhulumu. Wafuasi walikuwa wameshapatwa na magumu ya kubaki waaminifu kwa Kristo, walipaswa kuvunja vifungo ambavyo walikuwa wamejifungia na watu muhimu tu kwao. Marabi walikuwa wamesha amua kuwatenga wafuasi watakao amua kumfuata Yesu, na kuwatenga na sinagogi, na kuwaona kama wazushi, na wala familia zao wasiwatii. Yesu aliwaamuru wafuasi wake wawe na ujasiri wa kusimama imara hata kama hawana wa kuwaunga mkono, kuwalinda, na hata bila mali kwa ajili ya Injili. Na pia aliendelea na ombi lingine, tena lenye maana kubwa zaidi: kuwa tayari kuyatoa maisha yao.

Ishara ya msalaba ni ishara ambayo haikwepeki kwa mfuasi yeyote anayependa kumfuata Kristo na kuishi matakwa ya Injili: kama Bwana wao, watakutana na msalaba, nao ni machungu ya ulimwengu. Hata kama maisha hayataondolewa kwa njia ya kuuwawa, wanapaswa kutoa kuyatoa maisha yao kwa ukarimu na kama sadaka kwa ajili ya watu.

Katika upande wa pili wa Injili, ni zawadi kwa wale wote watakao wakaribisha wale wanao ihubiri Injili, “Kila anaye wakaribisha ninyi, ana nikaribisha mimi” (mstari. 40). Hii ni kama ule ukaribisho aliopokea Elisha katika somo la kwanza. Kila anaye mkaribisha nabii kwasababu ni nabii, atapokea zawadi ya kinabii. Hata upendo kidogo ukao tolewa kama vile kumpatia mfuasi kikombe kidogo cha maji ya baridi, ingawaje ni kidogo, hakika hakita sahaulika.

Kwa hiyo kila mfuasi anaitwa kuwasaidia wale wote waliojitoa kwa ajili ya kutangaza neno la Mungu. Kila Mkristo ana alikwa kuwakaribisha katika familia zao, watu kama hao, walio acha, nyumba, wake, waume, watoto kwa ajili ya kuwa na muda wote na Kristo na watu wake.

Tafakari leo ni kwa jinsi gani wewe ni sehemu ya familia ya Mungu. Tafakari kama unatamani kuwakaribisha nyumbani kwako hao wafuasi kama vile mapadre, watawa, na waamini, ambao kwa moyo usio gawanyika wameyatoa maisha yao kwa ajili ya kazi ya Bwana, kwa ajili ya kuwa tayari kwa ajili ya maisha yako ya kiroho. Viongozi wa dunia tafakari kama unampa Yesu nafasi ya kwanza katika maisha yako. Tujiunge pamoja ili kujenga familia ya Kristo.

Sala: Bwana, ninakupa maisha yangu yote kwako akili, moyo, utashi na nguvu. Nisaidie nikupende wewe zaidi ya yote na katika yote, na katika mapendo hayo nisaidie mimi niweze kuwapenda wale wote uliowaweka katika maisha yangu. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 28, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 28, 2026
DOMINIKA LA 13 LA MWAKA


MWANZO:
Zab. 47:2
Enyi watu wote, pigeni makofi, mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe.


SOMO 1 
2 Fal 4:8-11,14-16

Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula. Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo. Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1

(K) Fadhili za Bwana nitaziimba milele.
Fadhili za Bwana nitaziimba milele;
Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;
Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe,
Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako.
Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,
Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe,
Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.
Maana ngao yetu ina Bwana,
Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)


SOMO 
Rum. 6:3-4,8-11

Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika

wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO 
Mt. 11:25

Aleluya, aleluya, 
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. 
Aleluya.


INJILI 
Mt. 10:37-42

Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.

Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki. Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KILIO CHA SALA!!





ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Juni, 27, 2026, 
Juma la 12 la Mwaka wa Kanisa


Omb 2: 2, 10-14, 18-19;
Zab 74: 1-7, 20-21; 
Mt 8: 5-17


KILIO CHA SALA!!

Masomo yetu ya leo yanatuonesha aina mbili za kilio cha moyo. Kilio cha kwanza ni Kilio cha Waisrael katika hali ya maombolezo, na cha pili ni kilio cha pili cha jemedari katika Injili. Vyote vinamuelekea Mungu wakiwa katika hali ya huzuni. Vilio hivi vyote ni sala ya kumuomba Bwana aje kuwaponya tena, aje apooze tena roho zao zilizo kata tamaa, na kuwakinga na maadui. 

Kilio cha kwanza kipo katika hali ya mateso na woga. Mfalme wa Babiloni ameiteka Yerusalemu na aliwachukuwa mateka watu maelfu kutoka Yerusalemu. Wote waliobaki waliishi katika hali ya uharibifu na kutengwa. Waliteseka kuhusu chakula na matumizi yao muhimu. 

Kilio cha pili ni kile cha jemedari, alikuwa mpagani. Anakuja kwa Yesu kuomba uponyaja wa mtumishi wake. Imani yake ilikuwa kubwa kuliko ya Myahudi yeyote. Alijua na kutambua kwamba Yesu anauwezo wakuamuru kila kitu kitendeke kama yeye alivyokuwa na uwezo wakuwaamuru watumishi waliokuwa chini yake. Lakini pia alitambua nguvu na uwezo wa Yesu ni wa juu kuliko wake. Alitambua kabisa ilitosha kabisa kwa Yesu kusema neno tu hata bila ya kutembelea nyumbani kwake. Hakuna anyeachwa na mkono wa uponyaji wa Yesu. Yeye yupo karibu na wote, hasa kwa wale wanomhitaji na wanaoteseka, kwasababu katika hali ya mateso yao wanamlilia yeye na kilio chao ni cha uaminifu na kweli na Imani yao kubwa wameiweka kwa Mungu kama tumaini lao. 

Sisi nasi tuige mfano huu wakuwa na Imani kwa Yesu, nyakati zote za maisha yetu, tusisubiri tuu tunapatwe na shinda ndio tumkumbuke Mungu. Nyakati zote ziwe za furaha na uchungu Yesu awe ndiye dereva wa maisha yetu yote. Tujikabidhi kwake, Imani yetu, akili yetu na moyo wetu na vyote tulivyo navyo viongozwe na Yesu.

Sala: Bwana sikiliza kilio cha moyo wangu, uniponye mimi, unifanye upya tena na unipe wokovu wako. Amina  .

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 27, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 27, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 12 LA MWAKA

SOMO 1
Omb. 2:2, 10 – 14, 18 – 19

Bwana ameyameza makao yote ya Yakobo, wala hakuona huruma; ameziangusha ngome za binti Yuda katika ghadhabu yake; amezibomoa hata nchi ameunajisi ufalme na wakuu wake.

Wazee wa binti Sayuni huketi chini, hunyamaza kimya; wametupa mavumbi juu ya vichwa vyao, wamejivika viunoni nguo za magunia; wanawali wa Yerusalemu huinama vichwa vyao kuielekea nchi. 

Macho yangu yamechoka kwa machozi, mtima wangu umetaabika; ini langu linamiminwa juu ya nchi kwa uharibifu wa binti ya watu wangu; kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao, huzimia katika mitaa ya mji.

Wao huwauliza mama zao, zi wapi nafaka na divai? Hapo wazimiapo kama waliojeruhiwa katika mitaa ya mji, hapo walipomiminika nafsi zao vifuani mwa mama zao.

Nikushuhudie nini? Nikufananishe na nini, ee Binti Yerusalemu? Nikusawazishe na nini, nipate kukufariji, Ee bikira binti Sayuni? Kwa maana uvunjifu wako ni mkuu kama bahari, ni nani awezaye kukuponya?

Manabii wako wameona maono kwa ajili yako ya ubatili na upumbavu; wala hawakufunua uovu wako, wapate kurudisha kufungwa kwako; bali wameona mabashiri ya ubatili kwa ajili yako na sababu za kuhamishwa.

Mioyo yao ilimlilia Bwana; Ee ukuta wa binti Sayuni! Macho na yachuruzike kama mto mchana na usiku; usijipatie kupumzika; mboni ya macho yako isikome.

Inuka, ulalamike usiku, mwanzo wa makesha yake; mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; umwinulie mikono yako; kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa, mwanzo wa kila njia kuu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 74:1 – 7, 20 – 21 (K) 19

(K) Usiusahau milele uhai wa watu wako walioonewa.

Ee Mungu, mbona umetutupa milele?
Kwa nini hasira yako inatoka moshi
Juu ya kondoo wa malisho yako?
Ulikumbuke kusanyiko lako,
Ulilolinunua zamani.
Ulilolikomboa liwe kabila la urithi wako,
Mlima Sayuni ulioufanya maskani yako. (K)

Upainulie miguu yako palipoharibika milele;
Adui ameufanya kila ubaya katika patakatifu.
Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako;
Wameweka bendera zao ziwe alama. (K)

Wanaonekana kama watu wainuao mashoka, 
Waikate miti ya msituni.
Na sasa nakishi yake yote pia
Wanaivunjavunja kwa mashoka na nyundo.
Wamepatia moto patakatifu pako;
Wamelinajisi kao la jina lako hata chini. (K)

Ulitafakari agano; 
Maana mahali penye giza katika nchi
Pamejaa makao ya kukatili.
Aliyeonewa asirejee ametiwa haya,
Mnyonge na mhitaji na walisifu jina lako. (K)


SHANGILIO
Yn. 8:12

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Aleluya.


INJILI
Mt. 8:5 – 17

Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, amasihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye. Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona. Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.

Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa yeyote katika Israeli. Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki, na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni; bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile.

Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwewe Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.

Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi, ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUWA KAMA KRISTO KATIKA KUPENDA NA HURUMA



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Juni 26, 2026, 
Juma la 12 la Mwaka 

2 Fal 25: 1-12; 
Zab 137: 1-6; 
Mt 8: 1-4


KUWA KAMA KRISTO KATIKA KUPENDA NA HURUMA


Katika somo la Injili Yesu anatenda kisicho fikirika. Anamgusa “mkoma” ambae hapaswi kuguswa. Wakoma walikuwa watu wasio thaminika kabisa na kutengwa katika jamii ya Wayahudi. Hawakuwa wametengwa tu bali walikuwa wanachukuliwa kama “wameshakufa tayari”! hata na ndugu zao. Sheria za Kiyahudi zilikataza mtu yeyote kusogelea mkoma au kumgusa, kwani atatiwa najisi. Akitambua hili, mkoma kwa kushangaza anamkaribia Yesu kwa ujasiri na unyenyekevu, akitazamia uponyaji kutoka kwa Yesu. Yesu hakumpa tu huyu mkoma kile alichokuwa akihitaji bali anaonesha upendo na huruma na ukarimu wa Kimungu kwa kumgusa. Anaonesha upendo na huruma ya Kimungu katika hali ya kugusa zaidi badala ya maneno matupu. Alimgusa mkoma na anamfanya awe safi tena-sio kimwili tu bali pia kiroho. Matokeo yake ni kwamba alirudishiwa tena afya yake na kuwa mzima kabisa.

Yesu alimpenda huyu mkoma alipenda kumpa zawadi yake ya thamani ya uponyaji. Alifanya haya kwa huruma, na alihitaji ashukuru. Hakupenda kufanya hili hadharani. Sisi nasi tunapaswa kuiga hilo. Tunapaswa kutambua kuwa Mungu anatupenda sana kiasi kwamba anataka kutunyanyua juu kutoka katika mizigo yetu na kutuponya kutoka katika madhaifu yetu kwasababu tu, anatupenda.

Tutafakari leo, juu ya kinacho sababisha sisi tuwe na ukarimu kwa watu. Tuombe ili nasi tuweze kufanya katika hali ambayo haitafuti heshima ili tuweze kuiga tabia za Kimungu.

Sala: Bwana, ninaomba nikuwe katika mapendo kwa wengine na nioneshe mapendo hayo katika hali ya ukamilifu wako. Ninaomba nisivutwe na tamaa ya kusifiwa. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUNI 26, 2026


 

MASOMO YA MISA JUNI 26, 2026
IJUMAA YA 12 YA MWAKA 


SOMO1

2 Fal 25: 1-12

 

Ikawa katika mwaka wa kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja yeye na jeshi lake lote, kupigana na Yerusalemu, akapanga hema zake kuukabili; bao wakajenga ngome juu yake pande zote. Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na moja wa mfatae Sedekia. Siku ya kenda ya mwezi wa nne njaa ilikuwa nzito ndani ya mji, hata hapakuwa na chakula kwa watu wa nchi. Ndipo mahali pakabomolewa katika ukuta wa maji, watu wote wa vita wakakimbia usiku kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wakiuzuia mji pande zote;) mfalme akaenda kwa njia ya Araba. Lakini jeshi la Wakaldayo wakamfuatia mfalme, wakampata katika nchi tambarare ya Yeriko; na jeshi lake lote walikuwa wametawanyika na kumwacha. Ndipo wakamkamata mfalme, wakamchukua kwa mfalme wa Babeli  huko Ribla. wakatoa hukumu juu yake. Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, wakampofusha macho Sedekia, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.

 

Hata mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza, mfalme wa Babeli. Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babeli, akaingi Yerusalemu. Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme; na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto. Na jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi, wakazibomoa kuta za Yerusalemu pande zote. Na mabaki ya watu waliosalia katika mji, nao wale walioasi, na kumkimbilia mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu wote wengine, watu hao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka. Lakini huyo amiri wa askari walinizi akawaacha watu walio maskini ili wawe watunza mizabibu na wakulima.

 

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 137 : 1-6 (K). 6

 

(K) Ulimi wangu ugandamane nisipokukumbuka.

 

Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,

Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.

Katika miti iliyo katikati yake

Tulivitundika vinubi vyetu. (K)

 

Maana huko waliotuchukua mateka

Walitaka tuwaimbie;

Na waliotuonea walitaka furaha;

Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni. (K)

 

Tuuimbeje wimbo wa Bwana

Katika nchi ya ugeni?

Ee Ycrusalemu, nikikusahau wewe,

Mkono wangu wa kuume na usahau. (K)

 

Ulimi wangu na ugandamane

Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.

Nisipoikuza Yerusalemu

Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu. (K)

 

 

SHANGILIO

Yn. 10:27

 

Aleluya, aleluya, Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata. Aleluya.

 

 


INJILI

Mt. 8:1-4


Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema, Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika. Yesu akamwambia, Angalia usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwao.


-------------------------


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

NAWEZAJE KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Juni, 25, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 12 la Mwaka wa Kanisa


2 Fal 24: 8-17; 
Zab 78: 1-5, 8-9; 
Mt 7: 21-29


NAWEZAJE KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU?

Ni nani ataingia katika ufalme wa Mungu au mtu gani awezaye kuingia katika ufalme wa Mungu? Ni swali ambalo tunalisikia mara nyingi kutoka kwa watu. Kijana mmoja tajiri anakuja kwa Yesu na anauliza swali hilo hilo (Mk 10: 17-31). Leo katika Injili Yesu anatoa jibu la swali hili, FANYA MAPENZI YA MUNGU (Mt 7: 21). Mapenzi ya Mungu yanafunuliwa kwetu kwa njia mbali mbali. Anayesoma neno la Mungu nakulitafakari atatambua Mungu anataka nini kwake. Yule ambaye anasikiliza pia dhimiri yake na kusikiliza wengine pia atayatambua mapenzi ya Mungu. Yesu aliwafundisha wafuasi wake na pia anatufundisha sisi jinsi yakufanya mapenzi ya Mungu. Wakati aliposema “Mpende Mungu kwa Moyo wako wote na akili yako yote na mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe” (Lk 10: 27), alikuwa anafunua mapenzi ya Mungu kwa wafuasi wake. Maisha ya mtu yakijazwa mapendo kwa Mungu na jirani huyu anayafanya mapenzi ya Mungu. Kwahiyo kwa njia hii ataingia katika ufalme wa Mungu

Maisha ya mtu mwenye hekima, anayelisikia neno la Mungu na kufanya mapenzi ya Mungu, ni kama nyumba iliyojengwa kwenye mwamba mgumu. Hata kama kuna mateso, maumivu, uchungu na matatizo atakuwa na nguvu ya kusimama imara na yote yatapita. Lakini anayesikia neno la Mungu na halitendi atakuwa kama mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga, Yesu alisema. Atatetereka atakapo patwa na matatizo madogo au changamoto za maisha. Leo tunapaswa kuuchukua mfano huu wa Yesu. Alisema “chakula changu nikutenda mapenzi ya Baba yangu” (Yn 4: 34). Akimaanisha kuyafanya mapenzi ya Mungu yaliyo kila kitu katika maisha yake. Tuombe neema yakutenda mapenzi ya Mungu katika maisha yetu.

Sala: Bwana ni ngome yangu, mwamba wangu, na mwokozi wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, kinga yangu na pembe ya wokovu wangu na nguvu zangu. (Zab 18: 2). Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 25, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 25, 2026
ALHAMISI YA 12 YA MWAKA


SOMO 1
2 Fal. 24:8 – 17

Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani wa Yerusalemu. Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya baba yake.

Wakati ule watumishi wa Nebukadreza mfalme wa Babeli wakakwea kwenda Yerusalemu, na mji ukahusuriwa. Na Nebukadreza, mfalme wa Babeli akaufikilia huo mji, hapo watumishi wake walipokuwa wakiuhusuru. Na Yekonia, mfalme wa Yuda, akatoka akamwendea mfalme wa Babeli, yeye na mama yake, na watumishi wake, na wakuu wa watu wake, na maakida wake; mfalme wa Babeli akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.

Akatoa huko hazina zote za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme, akavikatakata vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani, mfalme wa Israeli, alivifanya katika hekalu la Bwana, kama Bwana alivyosema. Akawachukua mateka watu wa Yerusalemu wote pia, na wakuu wote, na mashujaa wote, watu elfu kumi; na mafundi wote, na wafua chuma wote; hapana mtu aliyebaki, ila waliokuwa wanyonge wa watu wa nchi. Akamchukua Yekonia mpaka Babeli; na mama yake mfalme, na wake zake mfalme, na maakida wake, na wakuu wa nchi, aliwachukua mateka toka Yerusalemu mpaka Babeli. Na mashujaa wote, watu elfu saba, na mafundi na wafua chuma elfu moja, wote pia wenye nguvu, tayari kwa vita, hao wote mfalme wa Babeli aliwachukua mateka mpaka Babeli. 

Mfalme wa Babeli akamtawaza Matania, ndugu ya baba yake, awe mfalme badala yake, akalibadili jina lake, akamwita Sedekia.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 79:1- 5, 8 – 9 (K) 9

(K) Utuokoe, Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako.

Ee Mungu, mataifa wameingia katika urithi wako,
Wamelinajisi hekalu lako takatifu.
Wamefanya Yerusalemu chungu ngungu,
Wameziacha maiti za watumishi wako.
Ziwe chakula cha ndege wa angani.
Na miili wa watauwa wako
Iwe chakula cha wanyama wa nchi. (K)

Wamemwaga damu yao kama maji
Pande zote za Yerusalemu,
Wala hapakuwa na mzishi.
Tumekuwa lawama kwa jirani zetu,
Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.
Ee Bwana, hata lini? Utaona hasira milele?
Wivu wako utawaka kama moto? (K)

Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu,
Rehema zako zije kutulaki hima.
Kwa maana tumedhilika sana. (K)

Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie,
Kwa ajili ya utukufu wa jina lako.
Utuokoe, utughfiri dhambi zetu,
Kwa ajili ya jina lako. (K)


SHANGILIO
Zab. 119:105

Aleluya, aleluya,
Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.
Aleluya.


INJILI
Mt. 7:21 – 29

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako hutoa pepo, na kwa jina lako hutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejinga nyumba yake juu ya mwamba; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

ISHARA YA UTUKUFU YA JUA LA HAKI !



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya Jumapili
Jumatano, Juni 24, 2026. 
Juma la 12 la Mwaka wa Kanisa

Sherehe ya kuzaliwa kwa Mt.Yohane Mbatizaji 

Is 49: 1-6; 
Zab 138: 1-3, 13-15; 
Mdo13: 22-26; 
Lk 1: 57-66, 80


ISHARA YA UTUKUFU YA JUA LA HAKI !

Kwa kawaida Kanisa halisheherekei sikukuu za kuzaliwa za watakatifu. Lakini kuna sikukuu nyingine za pekee ambazo ni kuzaliwa Bwana wetu Yesu Kristo-na sherehe za kuzaliwa Bikira Maria naya kuzawaliwa kwa Yohane Mbatizaji. Hii ni kwasababu Maria, tangu kuumbwa kwake kwanza alikingiwa dhambi ya asili. Yohane Mbatizaji alitakaswa kutoka dhambi ya asili akiwa tumboni mwa mama yake. Leo inajulikana kama “Noeli ndogo” kwasababu Yohane alimtangulia Yesu na alimbatiza Kristo. Maisha ya Yohane Mbatizaji yalijazwa na jambo moja-kumuonesha Yesu kwa watu na kuandaa ujio wa Ufalme wa Mungu. Maandiko matakatifu yanatuambia kwamba Yohane Mbatizaji alijazwa na Roho Mtakatifu hata angali tumboni mwa mama yake (Lk 1: 15, 41) na Kristo mwenyewe ambaye Bikira Maria alipata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Moto wa Roho Mtakatifu ulimjaza Yohane na akawa mtangulizi wa Masiha. Yohane alivunja ukimya wa manabii wa karne zilizopita alipoanza kuongelea kuhusu Neno wa Mungu kwa watu wa Israeli. Akiwa katikati ya watu waliopoteza matumaini yao kuhusu Mungu, sasa anaiamsha tena Imani yao, kuwatahadharisha kuhusu usafi wa mioyo yao, kuamsha tena ndani yao mapenzi mema ya kumtambua na kumkubali Masiha anayekuja. Watu walikimbilia jangwani kwenda kumsikiliza na kubatizwa.

Yohane aliitwa kutoka tumboni mwa mama yake kuwa mjumbe wa ufalme wa Mungu. Kwa njia hiyo hiyo Yesu naye anatualika sisi tuliowafuasi wake na tuliobatizwa kwa jina lake, tuweze kuwa manabii- tuwe watu wanaotangaza kwa maneno na matendo ujumbe wa haki na huruma. Tangu ubatizo wetu (Kuzaliwa katika maisha ya Kimungu) sisi kama Yohane, tuna utume wakufanya kutoka katika mpango wa Baba yetu. Sio tuu kumfuata Yesu, bali kutangaza siku ya ukombozi tunayo tumaini ndani ya kristo kwamba itatimilizwa.

Tutafakari leo, hasa katika zile hali ambazo hatukuwa waaminifu kwa Mungu katika maisha yetu. Mungu atatupokea tena na kubadilisha maisha yetu. Mungu anatusubiri na huruma yake haina kikomo. Turuhusu huruma yake ijaze mioyo yetu ili iweze kupokea daima uzuri wa Mungu. Nasi pia kama Yohane, alivyo itwa kuwa mjumbe wa Ufalme wa Mungu, Yesu anampa kila mbatizwa Roho wake kutangaza kwa maneno na matendo ufalme wa haki na huruma. 

Watu wameishia kujidharau na kukataa maisha yao na sasa wanaishi maisha ya wengine. Ishi kuendana na mpango wa Mungu aliouweka katika maisha yako. Watu wengi wamekataa maisha yao ambayo wanapaswa kuyaishi na wameishia kuishi maisha ya wengine. Wewe ni wa thamani sana kwa jinsi ulivyo na Mungu anakupenda kwa jinsi ulivyo. 

Katika maisha ya Yohane Mbatizaji tunaona unyenyekevu wa hali ya juu. Hakujisifu kwa kitu ambacho hakihusiani na yeye. Hata kwa wale ambao walikuwa wakichanganyikiwa kuhusu Masiha na yeye mwenyewe alisema “mimi sie Masiha” (Yn 1:20). Aliendelea hata nakusema kwamba Masiha ni mkubwa kuliko yeye, hivyo anapaswa yeye abatizwe na Masiha sio yeye ammbatize Masiha. (Mat. 3:14). Tunaitwa daima kutafakari juu ya unyenyekevu daima katika maisha yetu. Kilicho muhimu sana katika hili nikufahamu nafasi zetu na kuzikubali na bila kujaribu kuwa mtu mwingine ambaye sio mimi. 

Ukweli ulikuwa ni kilele cha utume wa Yohane Mbatizaji. Tunatambau kwamba yeye alikuja ili aushuhudie ukweli. Bila shaka ukweli wenyewe ni Yesu (Mat. 14:1-12). Maisha yetu yanapaswa yapambwe na ukweli daima. Ukweli unapaswa kusemwa daima kwasababu unamuinua na kumtukuza Mungu. 

Sala: Bwana, nisaidie niweze kuona dhambi zangu za zamani si katika hali ya kupoteza tumaini bali kama sababu ya kurudi kwako kwa uaminifu mkubwa. Bila kujali nimeanguka mara ngapi, nisaidie niweze kunyanyuka na kuimba tena sifa zako. Yesu nakuamini wewe. Mt. Yohane mbatizaji mhubiri wa ukweli usiye kuwa na woga, utuombee. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 24, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 24, 2026
JUMATANO YA 12 YA MWAKA


SHEREHE YA KUZALIWA YOHANE MBATIZAJI


SOMO 1
Isa. 49:1 – 6

Nisikilizeni, enyi visiwa; tegeni masikio yenu, enyi kabila za watu mlio mbali sana; Bwana ameniita tangu tumboni; toka tumbo la mama yangu amenitaja jina langu.

Naye anifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali; katika kivuli cha mkono wake amenisitiri; naye amenifanya kuwa mshale uliosuguliwa; katika podo lake amenificha.

Akaniambia; Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika wewe nitatukuzwa. Lakini nikasema, Nimejitaabisha bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida; lakini hakika hukumu yangu ina Bwana, na thawabu yangu ina Mungu wangu.

Na sasa Bwana asema hivi, yeye aliyeniumba tangu tumboni niwe mtumishi wake, ili nimletee Yakobo tena, na Israeli wakusanyike mbele zake tena; (maana mimi nimepata heshima mbele ay macho ya Bwana, na mungu wangu amekuwa nguvu zangu); naam, asema hivi, Ni neno dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kuziinua kabila za Yakobo, na kuwarejeza watu wa Israeli waliohifandhiwa; zaidi ya hayo nitakutoa uwe nuru ya mataifa, upate kuwa wokovu wangu hata miisho ya dunia.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 139:1 – 3, 13 – 15 (K) 14

(K) Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa.

Ee Bwana umenichunguza na kunijua.
Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;
Umelifahamu wazo alngu toke mbali.
Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu,
Umeelewa na njia zangu zote. (K)

Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu,
Uliniunga tumboni mwa mama yangu.
Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa
Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.
Matendo yako ni ya ajabu. (K)

Na nafsi yangu yajua sansa,
Mifupa yangu haikusitirika kwako,
Nilipoumbwa kwa siri,
Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi. (K)


SOMO 2
Mdo. 13:22 – 26

Paulo alisema, Mungu alimwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yesu, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote. Katika uzao wake mtu huyo Mungu amewaletea Israeli habari za ubatizo wa toba, kabla ya kuja kwake. Naye Yohane alipokuwa akimaliza mwendo wake alinena, Mwanaidhani mimi kuwa nani? Mimi siye. Lakini , angalieni, anakuja mmoja nyuma yangu ambaye mimi sistahili kumlegezea viatu vya miguu yake.

Ndugu zangu, wana wa ukoo wa Ibrahimu, na hao miongoni mwenu wanaomcha Mungu, kwetu sisi neno la wokovu huu limepelekwa.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Lk. 1:76

Aleluya, aleluya,
Nawe, mtoto, utaitwa nabii wake aliye juu. Utatangulia mbele za uso wa Bwana, umtengenezee njia zake.
Aleluya.


INJILI
Lk. 1:57 – 66, 80

Ikawa, siku za kuzaa kwake Elisabeti zilipotimia, alizaa mtoto mwanamume. Wakasikia jirani zake na jamaa zake ya kwamba Bwana amemwongezea rehema zake, wakafurahi pamoja naye.
Ikawa siku ya nane wakaja kutahiri mtoto; wakataka kumpa jina la babaye, Zakaria. Mama akajibu akasema, La, sivyo; bali ataitwa Yohane, wakamwambia, Hapana mtu katika jamaa zako aitwaye jina hilo. Wakamwashiria babaye wajue atakavyo kumwita. Akataka kibao, akaandika ya kwamba, Jina lake ni Yohane. Wakastaajabu wote. Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake pia, akaanza kunena akimsifu Mungu. Wakaingiwa na hofu wote waliokuwa wakikaa karibu nao; na mambo hayo yote yakatangazwa katika nchi yote ya milima na milima ya Uyahudi. Na wote walioyasikia wakayaweka mioyoni mwao, wakisema, Mtoto huyu atakauwa wa namna gani? Kwa sababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.

Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa jangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.