Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUONGEA LUGHA YA MUNGU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Mei 7, 2026
Juma la 5 Pasaka

Mdo 15: 7-21;
Zab 96: 1-3,10 (K. 3);
Yn 15: 9-11.


KUONGEA LUGHA YA MUNGU!

Wanadamu wanatamani kupendwaa na kujaliwa. Lakini ni vigumu kwa njaa ya upendo kutimizwa, katika hali ya kibinadamu. Leo, Yesu anaongea kuhusu upendo unaozalisha furaha isiyo pimika, ambayo ni Baba na Yeye anayo tu kwa wale walio wake. Hatuwezi kumzidi Mungu kwa mapendo kwasababu anatupenda bila kipimo, kwa upendo unaotoa neema, uzima, Amani na furaha.

Upendo wa Mungu ni kamili na hauwezi kuingiliwa. Upendo wa Baba kwa Mwanae ni kamili katika nyanja zote. Hauna masharti na unakamilisha yote. Ni kamili na hauna ubinafsi. Kwa kupokea upendo wa Baba, Yesu alipokea yote aliyo hitaji. Upendo aliopokea Yesu kutoka kwa Baba yake hauwezi kuondolewa. Hauwezi kuwekwa kwa ubinafsi. Unatiririka kutoka katika moyo wa Yesu na kuja kwetu. Mtiririko huu wa upendo, tuliopewa sisi, hauwezi kufungwa ndani ya mioyo yetu bila kwenda kwa wengine. Hivyo kama tunataka kuwa wapokeaji wa zuri wa upendo wa Baba na Mwana, tunapaswa kuruhusu upendo huo uwatiririkie wengine bila “Kikomo” na bila “Masharti”. 

Leo tunaitwa kupenda kwa niaba ya upendo wenyewe, kwa niaba ya Kristo, ambaye ndiye msingi wa upendo wa kweli. Si kwasababu nyingine bali kwa upendo kamili ambao Yesu alitoa kwa ajili yetu. Maisha yetu kama wafuasi wa Yesu yanapaswa kuwa maisha ya kujitoa kwa upendo kwa wengine. Upendo wa Yesu ambao upo ndani yetu unapaswa kutambuliwa, kukukubali na kuupeleka kwa wengine. Hili ndilo lengo la maisha ya Kikristo: kubaki katika upendo wa Kristo na kujazwa furaha. Mimi na wewe tumebarikiwa kufahamu ukweli kwamba MUNGU ni UPENDO. Hivyo tutangaze ukweli huu bila wasi wasi na bila kujibakiza. Kama tutamruhusu Mungu atupende kwa upendo mkamilifu, tutaanza kuona mara moja kwamba upendo huu ukitiririka ndani mwetu kama vile mto wa neema na huruma.

Sala: Bwana, ninakupenda wewe na ninatambua napendwa na wewe. Nisaidie mimi niweze kuwa wazi kwa upendo wako. Nisaidie niweze kufanya upendo huo uzame ndani ili uweze kutiririka kutoka moyoni mwangu na kwenda kwa wengine pia. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 7, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 7, 2026
ALHAMISI YA 5 YA PASAKA

SOMO 1 
Mdo. 15:7-21

Wakati wa Mtaguso wa Yerusalemu, baada ya hoja nyingi Petro alisimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini. Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi; wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani. Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua. Bali twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu vile vile kama wao.

Basi mkutano wote wakanyamaza, wakawasikiliza Barnaba na Paulo wakiwapasha habari za ishara na maajabu, ambayo Mungu aliyafanya kwa ujumbe wao katika Mataifa. Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu, akisema, Ndugu zangu, nisikilizeni. Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake. Na maneno ya manabii yapatana na hayo, kama ilivyoandikwa.

Baada ya mambo haya nitarejea, nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, nami nitaisimamisha; ili wanada- mu waliosalia wamtafute Bwana, na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao; asema Bwana, ajulishaye hayo tangu milele.

Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwata- abishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa; bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu. Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 96:1-3, 10 (K) 3

(K) Wahubirini mataifa habari za utukufu wake.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Mwimbieni Bwana nchi yote.
Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake. (K) 

Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,
Na watu wote habari za maajabu yake. (K)

Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki;
Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, 
Atawahukumu watu kwa adili. (K)



SHANGILIO 
Lk. 24 : 25-26

Aleluya, aleluya, 
Ilimpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 15:9-11

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUONDOA MAJIVUNO NA UBINAFSI!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Mei 6, 2026
Juma la 5 la Pasaka


Mdo 15:1-6;
Zab 122:1-5 (R. 1);
Yn 15:1-8.


KUONDOA MAJIVUNO NA UBINAFSI!


Kupunguza matawi ni muhimu kwa mti kama unapenda uzae mataunda mazuri au maua mazuri. Kama, kwa mfano, mti wa maua ya waridi unakuwa bila kupunguzwa, unatoa vimaua vidogo vingi, amabavyo ni dhaifu. Lakini kwa mti mzuri ulio pruniwa unatoa maua mazuri yenye afya. Yesu anatumia mfano kama huu kutufundisha somo kama hilo katika kuzaa matunda mazuri kwa ufalme wake. Anataka maisha yetu yawe yenye matunda mema na anataka kututumia sisi kama vyombo vyake vyenye nguvu ulimwenguni. Lakini tusipo ingia katika maisha ya kiroho ya kujipruni mara kwa mara , hatutakuwa vyombo ambavyo Mungu anaweza kuvitumia.

Kujipruni kiroho unachukua ile hali ya kumruhusu Mungu aondoe maovu katika maisha yetu ili fadhila ziweze kungaa. Na hili lina fanikiwa hasa tunapo mruhusu atupe unyenyekevu na kutuondoa katika maringo yetu. Hili linaweza kuumiza, lakini maumivu yanayo tokana na kunyenyekeshwa na Mungu ni ufunguo wa kukuwa kiroho. Kwa kukuwa katika unyenyekevu, tunakuwa zaidi katika kujikita katika chanzo chetu kuliko katika kukuwa katika hali zetu wenyewe, mawazo yetu wenyewe na mipango yetu wenyewe. Mungu katika hali ya juu kabisa ana hekima kuliko sisi na kama tutaendelea kumwelekea kila mara kama chanzo chetu, tutakuwa wenye nguvu zaidi na kujiandaa yeye afanye mambo makubwa zaidi kwa njia yetu.

Kujiruhusu kupruniwa kiroho maana yake ni kuachia yaondoke mapenzi yetu wenyewe na mawazo yetu. Maana yake tunaachia kujitawala wenyewe na kumwachia aliye mkuu wa kukuza akuze na kuchukua nafasi. Ina maana tuna mwamini yeye zaidi kuliko tunavyo jiamini sisi wenyewe. Hili linahitaji kufa kwa nafsi zetu wenyewe na unyenyekevu wa kweli na kukiri kabisa kwamba Mungu ndiye tegemeo letu kwa kila kitu, kama tawi linavyo tegemea mti. Bila mti, tutaseka na kufa. Mwamini yeye na mipango yake na tambua kuwa hii ndio njia pekee ya kuzaa matunda mema, ambayo Mungu anayataka kupitia wewe.

Sala: Bwana, ninakuomba upruni majivuno yangu na kuyatupa mbali na pia uovu wangu. Nitakase mimi kutoka katika dhambi zangu nyingi ili niweze kujikabidhi kwako kwa kila kitu. Na ninapo jifunza kujikabidhi kwako, ninakuomba uanza kuzaa matunda mema katika maisha yangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 6, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 6, 2026
JUMATANO, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1 
Mdo. 15:1-6

Siku zile, walishuka watu waliotoka Uyahudi wakawafundisha wale ndugu ya kwamba, Msipotahiriwa kama desturi ya Musa hamwezi kuokoka. Basi baada ya Paulo na Barnaba kushindana na watu hawa na kuhojiana nao Sana, ndugu wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo.

Basi, wakisafirishwa na kanisa, wakapita kati ya nchi ya Foinike na Samaria, wakitangaza habari za kuongoka kwao Mataifa; wakawafurahisha ndugu sana. Walipofika Yerusalemu wakakaribishwa na kanisa na mitume na wazee, nao wakawaeleza mambo yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.

Lakini baadhi. ya madhehebu ya Mafarisayo walioamini wakasimama wakisema, Ni lazima kuwatahiri na kuwaagiza kuishika Torati ya Musa. Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 122:1-5 (K) 1

(K) Nalifurahi waliponiambia, Na Twende nyumbani kwa Bwana. 

Nalifurahi waliponiambia
Na twende nyumbani kwa Bwana.
Miguu yetu imesimama
Ndani ya malango yako, ee Yerusalemu. (K)

Ee Yerusalemu uliyejengwa 
Kama mji ulioshikamana,
Huko ndiko walikopanda kabila,
Kabila za Bwana. (K)

Ushuhuda kwa Israeli,
Walishukuru jina la Bwana.
Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,
Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. (K)


SHANGILIO 
Yn. 10 :14
Aleluya, aleluya, 
Mimi ndimi mchungaji mwema, nao walio wangu nawajua, nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.


INJILI 
Yn. 15 :1-8

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa. Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisi- pokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa notoni yakateketea.

Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

AMANI YA KRISTO INAYO FARIJI!





“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Mei  5, 2026,
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 14: 19-28;
Zab 145: 10-13, 21 (R. 12);
Yn 14: 27-31.


AMANI YA KRISTO INAYO FARIJI!


Wakati Yesu alivyo anza utume wake, wafuasi wake walimwamini kuwa mtu maalumu, na wakaacha kila kitu hata familia zao, miji yao ya nyumbani. Waliamini kwamba Yesu atapindua utawala wa Kirumi na kuanzisha utawala wa utukufu wa Daudi. Kuamini huku kulifungwa na Yesu kwa kuwaambia juu ya mateso na kifo.

Yesu alitambua kukazana kwao na mateso na wasi wasi wao, na nikatika mioyo hii iliyojaa wasi wasi Yesu anawaambia “msifadhaike mioyoni mwenu…..amani na waachia ninyi”. Ni amri ya mapendo kutoka kwa Bwana wetu. Anataka kuwahakikishia kwamba hofu na mioyo iliojaa wasi wasi sio ya watu wake. Kuwa na hofu na wasi wasi ni mzigo mkubwa sana unaoweza kutuangusha chini. Yesu anatu hakikishia kabisa kwamba tunapaswa kuwa huru kutoka katika hali kama hii. Anataka sisi tuwe huru ili tuweze kufurahia furaha ya maisha.

Hatua ya kwanza ya kuwa huru ni kutambua mzigo ni upi. Kuutambua na kutafuta sababu ya mzigo huo. Kama sababu ya mzigo wako ni kwasababu ya dhambi zako, zijute na fanya bidii kuziungama. Hii ni njia bora kabisa ya kuhisi uhuru wa ndani. Lakini pengine mzigo wako ni kwasababu ya matendo ya mwingine au hali Fulani ya maisha ambayo yapo chini ya uwezo wako, hapo upo katika hali ya pekee ya kuikabidhi kwa Bwana wetu, kumpa hali yote ya kumiliki hali yote. Uhuru unapatika katika hali ya kujikabidhi kabisa, kuamini na kujikabidhi katika mapenzi yake. Yesu anataka tuwe huru ili tuweze kuhisi furaha anayotaka kutupatia katika maisha yetu. Tunaomba Amani ya Kristo itiririke katika mioyo yetu na kwa njia yetu, na kukutana na wote tunao kutana nao.

Sala: Bwana, ninataka kuwa huru. Ninataka kuhisi furaha ulionayo kwa ajili yangu. Wakati mizigo ya maisha inapo nielemea, nisaidie niweze kukugeukia daima ukiwa msaada wangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 5, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 5, 2026
JUMANNE, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 14 :19-28

Wayahudi walifika toka Antiokia na Ikonio, wakawashawishi makutano hata wakampiga kwa mawe Paulo, wakamburuta nje ya mji, wakidhania ya kuwa amekwisha kufa. Lakini wanafunzi walipokuwa wakimzunguka pande zote, akasimama, akaingia ndani ya mji; na siku ya pili yake akatoka, akaenda zake pamoja na Barnaba mpaka Derbe.

Hata walipokwisha kuhubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi. Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawa weka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.

Wakapita kati ya Pisidia wakaingia Pamfilia. Na baada ya kuhubiri lile neno katika Perge wakatelemka mpaka Atalia. Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza. Hata walipofika wakalikutanisha kanisa, waka- waeleza mambo yote aliyoyafanya Mungu pamoja nao, na ya kwamba amewafungulia Mataifa mlango wa imani. Wakaketi huko wakati usiokuwa mcha che, pamoja na wanafunzi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145 :10-13, 21 (K) 12

(K) Watawajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari wa zamani zote.
Au: Aleluya.

1. Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru,
Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
Wataunena utukufu wa ufalme wako,
Na kuuhadithia uweza wako,
Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu,
Na utukufu wa fahari ya ufalme wake. (K)

2. Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote. (K)

3. Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana;
Wote wenye mwili na walihimidi jina lake
takatifu milele na milele. (K)



SHANGILIO
Ufu. 1:5

Aleluya, aleluya,
Ee Kristo, yu shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14 : 27-31

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga. Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi. Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, kusudi litakapotokea mpate kuamini. Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu. Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MUNGU ANAISHI NDANI MWETU!





“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Mei 4, 2026
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 14:5-18;
Zab 115:1-4, 15-16;
Yn 14:21-26.


MUNGU ANAISHI NDANI MWETU!

Watoto huwa wanaelewa kwamba Mungu anaishi ndani ya mioyo yao. Lakini, kama ukiwauliza wamejuaje, utaona wanakutazama kama kuchanganyikiwa katika kujibu. Licha ya hayo, wao wanatambua kwamba Mungu anaishi ndani yao. Pengine wewe utajibu nini katika swali hili kwamba, “umejuaje Mungu anaishi ndani mwako?” Pengine unaweza kujikuta ukipotea katika kuelezea hali hii ya juu ya fumbo la Imani yetu. Tunatambua kwamba Mungu anapenda kushikilia mioyo yetu, kuongea na sisi, kutuimarisha, kutuongoza na kutulinda sisi. Tunatambua kwa zawadi ya Imani yetu, kwamba Mungu yupo na anatamani muunganiko wa ndani na sisi. Tunatambua tu hilo.

Imani inatuongoza kwenye uelewa, na kila mara tunapo isikiliza sauti ya Mungu inayo ongea ndani mwetu, ikituongoza na kutulinda sisi, ni mwanzo wa kuanza kuelewa kuishi kwake ndani mwetu. Kama Mt. Agustino anavyosema, “Imani ni kuamini kile usicho kiona. Na matokeo ya imani ni kuona kile unacho kiamini”. Imani kwa uwepo wa Mungu inatuongoza kwenye jibu la swali hapo juu. Nitafahamuje, Mungu anaishi ndani mwangu? Jibu ni kwamba ni kwasababu namuona ndani yangu, naongea na yeye ndani, na anaongea na mimi ndani. Na pia naona matokeo ya Imani yangu kwake kutokana na kuamini huku. 

Muache yeye aongee na wewe, katika maongezi ya ndani, ruhusu kuishi kwake ndani kukuwe na kuthihirika kwa wengine. Mungu hapendi tu kuthihirika ndani mwako lakini pia anataka kungara kupitia wewe.

Sala: Bwana, njoo uishi moyoni mwangu. Fanya moyo wangu sehemu yako ya kuishi. Nisaidie niweze kukuona wewe hapo na kuongea na wewe na kukupenda wewe ndani ya roho yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 4, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 4, 2026
JUMATATU YA 5 YA PASAKA

SOMO 1
Mdo. 14:5-18

Siku zile, palipotokea shambulio la watu wa Mataifa na Wayahudi pamoja na wakubwa wao juu yao, kuwatenda jeuri na kuwapiga kwa mawe, wao wakapata habari wakakimbilia Listra na Derbe, mji wa Likaonia, na nchi zilizo kando kando; wakakaa huko, wakiihubiri Injili. Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa. Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa, akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda.

Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng’ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano. Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi ni wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe. Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha. Na kwa maneno hayo wakawazuia makutano kwa shida, wasiwatolee dhabihu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 115 :1-4, 15-16 (K) 1

(K) Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi, Bali ulitukuze jina lako.

Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi,
Bali ulitukuze jina lako.
Kwa ajili ya fadhili zako,
Kwa ajili ya uaminifu wako.
Kwa nini mataifa kusema,
Yuko wapi Mungu wao? (K)

Lakini Mungu wctu yuko mbinguni,
Alitakalo lote amelitenda.
Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya wanadamu. (K)

Na mbarikiwe ninyi na Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi.
Mbingu ni mbingu za Bwana,
Bali nchi amewapa wanadamu. (K)


SHANGILIO
Col. 3:1

Aleluya, aleluya, 
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 14:21-26

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake. Yuda (siye Iskariote), akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?

Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka. Hayo ndiyo niliyowaambia wakati nilipokuwa nikikaa kwenu. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 3, 2026
Juma la 5 la Pasaka


Mdo 6: 1-7;
Zab 32: 1-5, 18-19;
1 Pet 2: 4-9;
Yn 14: 1-12.


MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


Je umekombolewa? “ndio” tumekombolewa kwa njia tatu: tumekombolewa kwa njia ya neema ya Ubatizo, tunaendelea kukombolewa kwa njia ya neema za Mungu na huruma tunapo amua kumfuata kwa uhuru kamili, na tunatumaini kokombolewa na kuingia katika utukufu wa Mbinguni.

Imekuwaje tumepokea zawadi ya thamani ya ukombozi? Kwa njia ya maisha, mateso kifo na ufufuko wa Yesu Kristo ambaye ndiye pekee aliye njia ya kwenda kwa Baba. Njia pekee ya Ukombozi ni Yesu. Hivyo Yesu Kristo anapaswa kuwa kiini cha maisha yetu, na tunapaswa kumuona kama njia, ukweli na uzima. Yeye ni njia pekee ya Mbinguni, yeye ni utimilifu wa ukweli wote ambao tunapaswa kuuamini, na yeye ni uzima ambao tunapaswa kuuishi na yeye ndiye chanzo cha maisha mapya ya neema. Bila yeye sisi si kitu, bali kwa njia yake unapata maisha makamilifu.

Katika somo la pili, Petro analifananisha Kanisa na jengo la kiroho ambalo mjenzi ni Mungu na mawe yanayoishi ni watu. Msingi ulianza kwa mawe imara kwa jengo lote, Kristo ambaye juu yake Mungu ameweka pia mawe mengine, wale wanao mwamini yeye. Wakiwa wameunganika na Yesu, wanatengeneza hekalu moja la Mungu.

Injili inamuonesha Yesu kama kielelezo cha maisha ‘njia, ukweli na uzima’. Kiini cha ukristo ni Kristo mweyewe. Kazi yetu kwa Yesu na upendo wetu kwa watu, haijalishi tumeitwa katika maisha ya namna ghani, maisha yetu yanatiririka kutoka katika chanzo hiki. Mama Teresa aliulizwa kwanini alifanya aliokuwa akifanya, na alijibu tu “ni kwa ajili ya Yesu”. Hiki ndicho kiini kinacho shikilia ili kusiwe na mtikizo au usumbufu wowote. Ni muunganiko wa ndani na Yesu. Kusoma maisha yake, kupata muda wa kutambua mazingira yake na matukio ya maisha yake, kuwa familia na Injili na kumfahamu katika moyo wa sala, njia yetu ya kuweka msingi wetu na ujasiri wetu kuwa imara kwa Yesu. Hivyo mchague yeye katika hali zote za maisha kama Bwana wako na mkombozi. Kwa unyenyekevu jitambue kuwa bila yeye wewe si kitu, na jikabidhi kwake ili yeye aweze kukuongoza salama kwa Baba yetu wa mbinguni.

Sala: Bwana na Mkombozi, ninakukubali wewe katika maisha yangu kama Bwana na Mkombozi. Ninakushukuru kwa zawadi ya ubatizo iliyo anzisha maisha ya neema ninaomba nibadilishe maisha yangu niendelee kukufuata kikamilifu, leo na siku zote, ili uweze kuingia zaidi ndani ya maisha yangu. Ninaomba matendo yangu yote yaongozwe nawe ili niweze kuwa sadaka ilyio unganika na wewe milele, Yesu mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026


MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026
JUMAPILI, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3

(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)


SOMO 2
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 14 : 6

Aleluya, aleluya,
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14: 1-12

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia, maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaa ndalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendakt mwaijua njia. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia? Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com