Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UDONGO WENYE RUTUBA ILI KUPOKEA BARAKA ZA MUNGU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa, Julai 31, 2026
Juma la 17 la Mwaka wa Kanisa

Yer 26: 1-9;
Zab 68: 5, 8-10, 14;
Mt. 13: 54-58.


UDONGO WENYE RUTUBA ILI KUPOKEA BARAKA ZA MUNGU


Yesu anaenda katika mji wa nyumbani kwake na kuhubiri habari njema lakini anakutana na upinzani wakutokukaribishwa kutoka kwa watu wake. Sio kwamba walikataa tu mafundisho yake na miujiza yake bali walitoa hukumu ambayo ni ya ajabu tena wakiangalia familia yake. “Je, huyu sio Mwana wa seremala? Mama yake sio Mariam”. Walimtazama kama mtu wa kawaida. Na hivyo wakazuia utukufu wa Mungu unaokuja kati yao. 

Ujumbe huu wa Injili unatufundisha kwamba tunapaswa kuwa tayari kujifunza kwa wengine, hasa wale wanaofahamu hata kama tunawafahamu familia yao au tunamfahamu. Kwani Mungu anaweza kutufundisha sisi kupitia kwa ndugu wa familia zetu. Kingine tunapaswa kuchelewa au kutokuhukumu mtu kwa kutazama historia ya familia yake au mambo yake ya zamani. Hakuna mtu ambaye anabaki kama alivyo daima. Tunapaswa kuwatazama watu kwa mtazamo mpya na mtazamo mpya. Tatu, kila wakati tunaposikia neno la Mungu likitangazwa kwetu, tunapaswa kusikiliza sio kwa kutazama mtu bali kutazama Roho Mtakatifu aneyeongea kupitia yeye. Nne, usikatishwe tamaa na watu kutokupokea neno la Mungu wala usikubali kuangushwa na mtu ambaye hataki kukufuata. Zaidi sana usiache kuwatendea mema wengine. 
Matendo matukufu ya Mungu hayakuweza kutendeka kule Nazareti kwasababu ya kukosa kwao Imani. Watu walikuwa na mioyo migumu wakashindwa kuruhusu mioyo na akili zao zipokee neno la Yesu. Kwa njia hii Yesu hakuweza kufanya miujiza mikuu maeneno ya nyumbani kwake. 

Je, unamruhusu Yesu akufanye uwe mpya siku kwa siku? Je, unamruhusu yeye atende mambo makuu katika maisha yako? Kama utakuwa na mashaka katika swali hili ni ishara kwamba Mungu anataka kufanya makuu katika maisha yako. 

Sala: Bwana, ninakuomba moyo wangu uwe na rutuba kwa ajili ya kazi yako kuu. Ninaomba moyo wangu ufanywe upya nawe, maneno yako na uwepo wako katika maisha yangu. Njia katika maisha yangu na unifanye upya chombo cha neema yako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 31, 2026



MASOMO YA MISA, JULAI 31, 2026
IJUMAA, JUMA LA 17 LA MWAKA


SOMO 1
Yer 26:1–9

Mwanzo wa kumiliki kwake Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili lilitoka kwa Bwana, kusema, Bwana asema hivi, Simama katika uwanja wa nyumba ya Bwana, useme na miji yote ya Yuda, wajao ili kuabudu katika nyumba ya Bwana; sema nao maneno yote ninayokuamuru kuwaambia, usizuie hata neno moja. Labda watasikia, na kughairi na kuacha kila mtu njia yake mbaya; ili niyaghairi mabaya niliyokusudia kuwatenda, kwa sababu ya uovu wa matendo yao. Nawe utawaambia, Bwana sema hivi, kama hamtaki kunisikia, kwenda katika sheria yangu, niliyoiweka mbele yenu, kuyasikiliza maneno ya watumishi wangu, manabii, ninaowatuma kwenu, naam, nikiondoka mapema na kuwatuma; lakini ninyi hamkuwasikiliza; basi, nitafanya nyumba hii kuwa kama Shilo, na mji huu nitaufanya kuwa laana kwa taifa zote za dunia. Na makuhani, na manabii, na watu wote, wakamsikia Yeremia, hapo aliposema maneno haya katika nyumba ya Bwana. Ikawa, Yeremia alipokuwa amekwisha kusema maneno yote Bwana aliyomwamuru kuwaambia watu wote, ndipo hao makuhani, na manabii, na watu wote, wakamkamata, wakisema, Bila shaka utakufa. Kwa nini umetabiri kwa jina la Bwana, ukisema, Nyumba hii itakuwa kama Shilo, na mji huu utakuwa ukiwa, hautakaliwa na mtu? Watu wote wakamkusanyikia Yeremia katika nyumba ya Bwana.


Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 69:4, 7–9, 13

(K) Kwa wingi wa fadhili zako, unijibu, Ee Bwana.

Wanaonichukia bure ni wengi
Kuliko nywele za kichwa changu.
Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari,
Adui zangu kwa sababu isiyo kweli.
Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu
Vitu nisivyovichukua.


Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu,
Fedheha imenifunika uso wangu.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila,
Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.

Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana,
Wakati ukupendezao; Ee Mungu,
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu,
Katika kweli ya wokovu wako.


SHANGILIO
1 Sam 3:9, Yn. 6:68

Aleluya, aleluya,
Nena, Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikia: wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Aleluya


INJILI
Mt 13:54-58

Yesu alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe. Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MFINYANZI MTAKATIFU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Julai 30, 2026 
Juma la 17 la Mwaka


Yer 18: 1-6; 
Zab 145: 2-6; 
Mt 13: 47-53


MFINYANZI MTAKATIFU!

Katika lirtujia ya neno la Mungu leo, mwalimu mwenye hekima anatumia mifano miwili kutoka katika uhalisia wa maisha yetu ya kila siku ili kutufundisha kitu cha hali ya juu. Anatumia, udongo, chungu na mfinyanzi na mfano wa neti inayotumiwa na mvuvi kuvulia samaki. Wakati la kwanza likitueleza kuna maovu duniani, mabaya, mapungufu na dhambi ambayo Mungu atahukumu siku moja, na lingine linatuambia kwamba mpango wa Mungu ni kutusafisha nakututakasa kutoka katika maovu yote na kutufinyanga na kutubadili siku kwa siku ili tufanane naye. Ni Neema ya Kimungu ambayo Mungu anaiweka ndani mwetu ambayo itatutakasa na kutubadili. 

Mungu ambaye ni Mfinyanzi Mtakatifu ametupa njia nyingi za sisi kujivika neema yake, Neno la Mungu, sakramenti ya Ekaristi na Kitubio, maisha ya sala, kufunga na kuomba toba, huruma na kufanya matendo ya huruma, kuvumilia kila wakati na kubeba misalaba yetu kila siku na mengine mengi. Yote haya yatatuongoza kwenye njia ya utakatifu na neema. Sasa tujivike neema ya Mungu isiyo na kikomo ambayo yeye mwenyewe kama Mfinyanzi Mtakatifu yupo tayari kutupatia ili kukua katika neema mpaka hapo tutakapo pata yote katika ukamilifu wote kwenye Ufalme wake.

Sala: Ee Bwana Yesu, nifiche katika madonda ya Moyo wako Mtakatifu. Niondoe katika hamu yangu ya kupenda kupendwa na kuheshimiwa. Nifanye mimi niwe mmoja nawe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JULAI 30, 2026




MASOMO YA MISA, JULAI 30, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 17 LA MWAKA


SOMO 1
Yer. 18:1 – 6

Neno hili ndilo lilomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema, Ondoka, ukashuke mpaka nyumba ya mfinyanzi, na huko nitakusikizisha maneno yangu. Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfainyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu. Na chombo kile, alichokuwa akikifinyanga, kilipoharibika mkononi mwake yule mfinyanzi, alikifanyiza tena kuwa chombo kingine, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya.

Ndipo neno la Bwana likamjia, kusema, Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, kama udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 146:1 – 5 (K) 5

(K) Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake.

Ee nafsi yangu umsifu Bwana,
Nitamsifu Bwana muda ninaoishi,
Nitamwimbia Mungu wangu ningali hai. (K)

Msiwatumainie wakuu,
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake,
Siku hiyo mawazo yake yapotea. (K)

Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,
Na tumaini lake ni kwa Bwana, Mungu wake.
Aliyezifanya mbingu na nchi,
Bahari na vitu vyote vilivyomo. (K)



SHANGILIO
1 Pet. 1:25

Aleluya, aleluya,
Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno jema lililohubiriwa kwenu.
Aleluya.



INJILI
Mt. 13:47 – 53

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya wa kila namna; hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam. Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.

Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

NGUVU YA YESU DHIDI YA MAUTI!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Julai 29,  2026 
Juma la 17 la Mwaka

KUMBUKUMBU YA FAMILIA WA MARTA, MARIA NA LAZARO

Yer 13:1-11; 
Kum 32: 18-21; 
Yn 11: 19-27 or Lk 10: 38-42


NGUVU YA YESU DHIDI YA MAUTI!

“Yesu aliwapenda, Martha, Maria na Lazaro” (Yn 11: 5). Maneno haya ya pekee katika Injili ya Yohane yanatueleza juu ya uhusiano wa pekee aliokuwa nao Yesu kati ya Martha, Maria na Lazaro. Inaonekana Yesu alikuwa mgeni wao mara nyingi katika familia hii huko Bethania, kijiji kidogo, maili mbili kutoka mji wa Yerusalemu. Tunasoma safari tatu za Yesu anazofanya ili kuwatembelea, katika Injili ya Luka 10:38-42, Yn 11: 1-53, Yn 12: 1-9. Sisi nasi tujenge Upendo kama huo na Yesu, mwana wa Mungu, tumjue Mungu. Tunaomba yeye asiwe tu mgeni wetu kila Mara katika maisha bali awe sehemu ya kiini cha familia zetu. 

Wakati Yesu alipowatembelea mara ya pili, Martha alikuwa akiomboleza na kulia juu ya kifo cha Lazaro kaka yake, na nyumba ikiwa imejawa pia na waombolezaji wengine. Lakini aliposikia Yesu amefika mahali pale, anasimama mara na kuwaacha wageni wengine na waombolezaji na anaenda kumuona Yesu. Hapa tunamuona Martha aliyebadilika. Pamoja na kwamba yupo katika hali ya majonzi na uchungu anaenda kumuona Yesu. Sasa anatambua lililo muhimu katika maisha. Katika mazungumzo yake anaanza moja kwa moja bila kuwa na wasi wasi kwamba anaamini juu ya nguvu ya Yesu, katika ufufuo wa wafu. Kwasababu ya hili analeta usemi uliomaarufu sana katika Injili ya Yohani. “MIMI (Yesu) ni ufufuo na uzima; aniaminiye mimi, hata kama anakufa ataishi na anayeishi na kuniamini hatakufa kamwe”. Baada ya hili, Martha analeta tena ungamo la Imani “ndio Bwana, ninaamini wewe ni Masiha , Mwana wa Mungu, ajaye ulimwenguni”. Na sasa Yesu anamfufua Lazaro. 

Kwa njia hii tunamuona Martha anavyoshirikiana na Neema ya Mungu katika maongezi yake na Yesu, sisi nasi tumpe Yesu nafasi aongee na sisi, sala zetu zisiwe ni sisi tu tunaongea na kueleza mambo yetu pekee, bali tumruhusu pia Mungu aongee nasi. Tumpe pia Mungu nafasi ajibu maombi yetu. Tuwe na muda wa kutafakari katika ukimya tumsikilize Mungu anataka kusema nini juu yangu? Tuwe na muda pia wa kumshukuru sio kuomba tuu, sala yetu iwe na nyanja mbali mbali. Tuwe na muda wa kumsifu, kumshukuru, kumuomba, kumsikiliza na pia kutafakari juu ya ukuu wake, na zaidi sana juu ya upendo aliotuonesha kupitia kwa Mwanaye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwanjia yake watu wote wapo hai. 

Sala: Bwana, nina amini kwamba utanifufua siku ya mwisho, nizaliwe katika maisha ya umilele. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JULAI 29, 2026



MASOMO YA MISA, JULAI 29, 2026
JUMATANO, JUMA LA 17 LA MWAKA

KUMBUKUMBU YA FAMILIA WA MARTA, MARIA NA LAZARO


SOMO 1 
Yer. 13:1-11

Bwana aliniambia hivi, Enenda, ukajinunulie mshipi wa kitani, ukajivike viuno, wala usiutie majini. Basi nikanunua mshipi sawasawa na neno la Bwana, nikajivika viunoni. Nalo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema, Twaa mshipi ule ulioununua, ulio viunoni mwako, kisha ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukaufiche huko katika pango la jabali. Basi nikaenda, nikauficha karibu na mto Frati, kama Bwana alivyoniamuru.

Hata ikawa baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, Ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukautwae ule mshipi, niliokuamuru kuuficha huko. Ndipo nikaenda mpaka mto Frati, nikachimba, nikautwaa ule mshipi katika mahali pale nilipouficha; na tazama, mshipi ulikuwa umeharibika, haukufaa tena kwa lo lote. Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema, Bwana asema hivi, Jinsi iyo hiyo nitakiharibu kiburi cha Yuda, na kiburi kikuu cha Yerusalemu. Wata hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wanaokwenda kwa ushupavu wa mioyo yao, na kufuata miungu mingine ile kuitumikia na kuiabudu, watakuwa hali moja na mshipi huu, usiofaa kwa lo lote. Maana kama vile mshipi unavyoshikamana na viuno vya mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami nyumba yote ya Israeli, na nyumba yote ya Yuda, asema Bwana; wapate kuwa watu kwangu mimi, na jina, na sifa, na utukufu; lakini hawakutaka kusikia.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu 


WIMBO WA KATIKATI 
Kum. 32:18-21 (K) 18

(K) Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa.

Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa.
Mungu aliyekuzaa umemsahau.
Bwana akaona, akawachukia,
Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake. (K)

Akasema, Nitawaficha uso wangu,
Nitaona mwisho wao utakuwaje;
Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi,
Watoto wasio imani ndani yao. (K)

Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu, 
Wamenikasirisha kwa ubatili wao;
Nami nitawatia wivu kwa wasio watu. 
Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo. (K)


SHANGILIO 
Kol. : 16,17

Aleluya, aleluya, Neno la Kristu likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkimshukuru Mungu Baba kwa Yeye. Aleluya.


INJILI
Yn. 11:19 – 27

Watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao. Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani. Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. Lakini hata sasa najua ya kuwa yoyote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa. Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka. Maratha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.

Yesu akamwambia, Mimi ndimi ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Au

INJILI
Lk. 10:38 – 42

Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake. Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake. Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie. Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi; lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUKUWA KATIKATI YA MAGUGU



“ASALI ITAKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumanne, Julai 28, 2026, 
Juma la 17 la Mwaka wa Kanisa 


Yer 14: 17-22; 
Zab 78: 8-9, 11, 13; 
Mt 13: 36-43.


KUKUWA KATIKATI YA MAGUGU

Injili ya leo inatualika kutafakari juu ya Ufalme wa Mungu. Yesu alikuja kutangaza na kuanzisha Ufalme wa Mungu. Somo la kwanza lina tukumbulisha ujumbe huu kwa kutangaza nguvu na mamlaka ya Mungu, ambaye ni mkarimu na mwenye huruma. Ingawaje ni mkuu juu ya yote anaongea na Musa uso kwa uso kama rafiki. Anatupa muda kuchagua kuwa katika ufalme wake. 

Katika mfano wa magugu na ngano, yote yanakuwa pamoja, yote yanapokea Baraka kipindi cha uhai wao, lakini mwishoni wakati wa mavuno yanatenganishwa na kila moja litaonesha matunda yake. Wengi wetu tumebarikiwa kuzaliwa katika familia ya Kikristo. Mungu ametupatia Baraka ya ubatizo hata kabla hatujauelewa maana yake. Anaendelea kutupatia Baraka kwa njia ya kanisa. Lakini Baraka za kuwa mkristo haina maana tutaenda tuu mbinguni bila kujishughulisha. Uzuri ni kwamba Mungu ametupa uhuru wa kumchagua yeye au kumkataa, wakati wa mavuno itadhihirika kama ulimchagua Mungu au la! .

Tujaribu kufikiria kama Yesu alikuwa aje kesho na atawachukua wale wote wenye haki? Je, wewe utakuwa na wasiwasi? Pengine hapana. Au pengine kutakuwa na muda wa kutazama nyuma na kuwa na Amani na kuona haki inakuja. Mungu daima yupo katika kuongoza. Anatambua anafanya nini na atakuwa na utukufu juu ya vyote. 

Wakristo wanaitwa waweze kuwa kama chachu katika jamii ili ulimwengu uweze kuwa sehemu nzuri ya kukaa. Kama sisi ni mashahidi wa kweli wa Kristo, Injili itaenea daima kila mahali. Kuingia kwetu katika ufalme itategemea kuchagua wema na kuacha yale yalio machukizo mbele ya Mungu. Wito wetu kama Wakristo tumeitwa kuwa mwanga wa ulimwengu, chumvi ya ulimwengu, ngano kati ya magugu, na ushuhuda wa upendo wa Yesu ulimwenguni. Tunaomba hii iwe sala yetu kwa Yesu kwani, ili mioyo mingi iweze kutambua uwezo upendo wa Mungu na kuwa raia wa Ufalme. 

Sala: Bwana Yesu, ninakuomba unisaidie mimi niweze kukaza macho yangu kwako na katika ushindi wa mwisho. Nisaidie mimi niweze kuwa mvumilivu nikwepe maovu ya ulimwengu huu kwa neema utakazo nipatia. Ninakuomba nisisahau ahadi yako siku ya mwisho uliioongea kwetu. Yesu nakuamini
 wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 28, 2026




MASOMO YA MISA, JULAI 28, 2026
JUMANNE, JUMA LA 17 LA MWAKA


SOMO 1
Yer. 14:17-22

Macho yangu na yatiririke machozi, usiku na mchana, wala yasikome; kwa maana bikira, binti ya watu wangu, amevunjika mavunjiko makuu, kwa jeraha isiyoponyeka. Nikitoka kwenda shambani, tazama, wako huko waliouawa kwa upanga! Na nikiingia mjini, tazama, wamo humo wanaougua kwa sababu ya njaa! Maana nabii na kuhani, wote wawili, huenda huko na huko katika nchi, wala hawana maarifa.

Je! Umemkataa Yuda kabisa? Roho yako imeichukia Sayuni? Mbona umetupiga, tusiwe na dawa ya mema yoyote; tulitazamia wakati wa kupona, na tazama, kufadhaika tu!

Ee Bwana, tunakiri uovu wetu, na ubaya wa baba zetu; maana tumekutenda dhambi. Usituchukie, kwa ajili ya jina lako; usikifedheheshe kiti cha enzi cha utukufu wako; kumbuka, usilivunje agano ulilofanya nasi. Je! Katika vitu vya ubatili vya mataifa, kiko kiwezacho kuleta mvua? Je! Mbingu zaweza kutoa manyunyu! Je! Si wewe, Ee Bwana, Mungu wetu? Kwa sababu hiyo tutakungoja; kwa kuwa wewe umevifanya vitu hivi vyote. 

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 79:8-9,11, 13 (K) 9

(K) Kwa ajili ya utukufu wa jina lako, utusaidie, Ee Bwana.

Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu,
Rehema zako zije kutulaki hima.
Kwa maana tumedhilika sana. (K)

Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie,
Kwa ajili ya utukufu wa jina lako.
Utuokoe, utudhofiri dhambi zetu,
Kwa ajili ya jina lako. (K)

Kuugua kwake aliyefungwa na kuingia mbele zako,
Kwa kadiri ya uwezo wa mkono wako
Uwahifadhi wana wa mauti.
Na sisi tulio watu wako, na kondoo za malisho yako,
Tutakushukuru milele;
Tutazisimulia sifa zako kizazi kwa kizazi. (K)


SHANGILIO
Ebr. 4:12

Aleluya, aleluya,
Neno la Mungu li hai tena li na nguvu, li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Aleluya.


INJILI
Mt. 13:36 – 43

Yesu aliwaaga makutano, akaingia nyumbani; wanafunzi wake wakamwendea, wakasema, Tufafanulie mfano wa magugu ya kondeni. Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu; lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu; yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika. Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia. Mwana wa Adamu atawatuma malaika wake machukizo yote, na hao watendao maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Ndipo wenye haki watakapong’aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

UKUBWA MACHONI MWA MUNGU

 



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, 27 Julai, 2026, 
Juma la 17 la Mwaka


Yer. 13:1-11
Kum. 32:18-21 (K) 18
Mt 13:31-35


UKUBWA MACHONI MWA MUNGU

Yesu akiongea kuhusu Ufalme wa Mungu alisema, “Ufalme wa Mungu upo pamoja nanyi” (Lk 17:21). Tunaitwa leo kuendeleza kazi hii ya Ufalme wa Mungu. Tunaweza kuwa na ugumu tuanzie wapi. Yesu anatuambia kwamba hata mbegu ndogo kabisa ya haradali inakuwa na kuwa mti mkubwa. Ni sawa sawa na kitendo kidogo kabisa chaweza kukuza Ufalme wa Mungu. Kwasababu Ufalme wa Mungu upo kati yetu, tunapaswa kuanza kutenda kadiri yake. Tukiwa tunaacha njia za uovu, mawazo mabaya na kugeukia njia ya haki, inaweza ikawa hatua ndogo. Kitendo hiki kidogo chaweza kukuwa na kuwa mti mkubwa ambapo ndege wa angani hupata pumziko. Kitendo kidogo katika familia yangu chaweza kukuza familia yangu na kuwa sehemu kubwa ya kushuhudia kueneza Ufalme wa Mungu. Kitendo cha ukarimu kwa jamii, chaweza kubadilisha jamii nzima na kufanya Ufalme wa Mungu kuenea kama moto mkubwa.

Mara nyingi tunafikiria kwamba maisha yetu sio muhimu sana kama ya wengine. Tunaweza kuwaangalia watu wengi walio endelea na walio maarufu, “hivi kama ningekuwa na hela kama zao?” au hivi kama ningekuwa maarufu kama hao? Ni mara nyingi tumejikuta tukianguka kwenye maswali “hivi kama ningekuwa….” Mbegu ndogo yaweza kuwa msitu mkubwa. Hili linafanya tujiulize swali, Je, unafikiri wewe ni mbegu ndogo sana? Inatokea katika maisha kwamba tunajisikia tupo chini na tunahitaji zaidi. Lakini haya yote hayana tofauti na ndoto zitokanazo na tamaa za dunia. Ukweli ni kwamba kila mmoja wetu ana uwezo wa kufanya mambo makubwa katika dunia hii. Machoni pa Mungu tuna hazina ndani mwetu kubwa mno kuliko yale tunayotamani sisi wenyewe.

Nini maana ya kufanywa upya na Mungu na kuwa mti mkubwa, kama punji ya haradali ilivyo? Ni kwamba kila mmoja wetu amepewa vingi na mengi ya kutimiza ili kujenga ufalme wa Mungu na mpango wa utukufu wa Mungu alionao katika maisha yetu. Ni mpango huu utakao zaa matunda makubwa na uzima wa milele. Tunaweza tusipate jina la kutambuliwa hapa duniani. Lakini, mbinguni lilo la muhimu ni utakatifu wako na jinsi ulivyo timiza mpango wa Mungu ulivyo katika maisha yako.

Alisema Mama Teresa mara nyingi kwamba “tumeitwa ili tuweze kuwa waminifu, na sio kufanikiwa.” Ni uaminifu huu kwa Mungu wenye thamani.

Sala: Bwana, ninatambua kwamba bila wewe mimi si kitu. Bila wewe maisha yangu hayana thamani. Ninaomba niweze kukumbatia mpango wako mkamilifu na wa utukufu katika maisha yangu na katika mpango huo, niweze kupata ukuu ule ulio niandalia na kuniitia mimi. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JULAI 27, 2026

 



MASOMO YA MISA, JULAI 27, 2026
JUMATATU, JUMA LA 17 LA MWAKA WA KANISA


SOMO 1 
Yer. 13:1-11

Bwana aliniambia hivi, Enenda, ukajinunulie mshipi wa kitani, ukajivike viuno, wala usiutie majini. Basi nikanunua mshipi sawasawa na neno la Bwana, nikajivika viunoni. Nalo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema, Twaa mshipi ule ulioununua, ulio viunoni mwako, kisha ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukaufiche huko katika pango la jabali. Basi nikaenda, nikauficha karibu na mto Frati, kama Bwana alivyoniamuru.

Hata ikawa baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, Ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukautwae ule mshipi, niliokuamuru kuuficha huko. Ndipo nikaenda mpaka mto Frati, nikachimba, nikautwaa ule mshipi katika mahali pale nilipouficha; na tazama, mshipi ulikuwa umeharibika, haukufaa tena kwa lo lote. Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema, Bwana asema hivi, Jinsi iyo hiyo nitakiharibu kiburi cha Yuda, na kiburi kikuu cha Yerusalemu. Wata hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wanaokwenda kwa ushupavu wa mioyo yao, na kufuata miungu mingine ile kuitumikia na kuiabudu, watakuwa hali moja na mshipi huu, usiofaa kwa lo lote. Maana kama vile mshipi unavyoshikamana na viuno vya mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami nyumba yote ya Israeli, na nyumba yote ya Yuda, asema Bwana; wapate kuwa watu kwangu mimi, na jina, na sifa, na utukufu; lakini hawakutaka kusikia.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu 


WIMBO WA KATIKATI 
Kum. 32:18-21 (K) 18

(K) Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa.

Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa.
Mungu aliyekuzaa umemsahau.
Bwana akaona, akawachukia,
Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake. (K)

Akasema, Nitawaficha uso wangu,
Nitaona mwisho wao utakuwaje;
Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi,
Watoto wasio imani ndani yao. (K)

Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu, 
Wamenikasirisha kwa ubatili wao;
Nami nitawatia wivu kwa wasio watu. 
Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo. (K)


SHANGILIO 
Kol. : 16,17

Aleluya, aleluya, Neno la Kristu likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkimshukuru Mungu Baba kwa Yeye. Aleluya.



INJILI
Mt.13 : 31-35

Yesu aliwatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.

Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia. Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno; ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.