Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

AMANI YA KRISTO INAYO FARIJI!





“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Mei  5, 2026,
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 14: 19-28;
Zab 145: 10-13, 21 (R. 12);
Yn 14: 27-31.


AMANI YA KRISTO INAYO FARIJI!


Wakati Yesu alivyo anza utume wake, wafuasi wake walimwamini kuwa mtu maalumu, na wakaacha kila kitu hata familia zao, miji yao ya nyumbani. Waliamini kwamba Yesu atapindua utawala wa Kirumi na kuanzisha utawala wa utukufu wa Daudi. Kuamini huku kulifungwa na Yesu kwa kuwaambia juu ya mateso na kifo.

Yesu alitambua kukazana kwao na mateso na wasi wasi wao, na nikatika mioyo hii iliyojaa wasi wasi Yesu anawaambia “msifadhaike mioyoni mwenu…..amani na waachia ninyi”. Ni amri ya mapendo kutoka kwa Bwana wetu. Anataka kuwahakikishia kwamba hofu na mioyo iliojaa wasi wasi sio ya watu wake. Kuwa na hofu na wasi wasi ni mzigo mkubwa sana unaoweza kutuangusha chini. Yesu anatu hakikishia kabisa kwamba tunapaswa kuwa huru kutoka katika hali kama hii. Anataka sisi tuwe huru ili tuweze kufurahia furaha ya maisha.

Hatua ya kwanza ya kuwa huru ni kutambua mzigo ni upi. Kuutambua na kutafuta sababu ya mzigo huo. Kama sababu ya mzigo wako ni kwasababu ya dhambi zako, zijute na fanya bidii kuziungama. Hii ni njia bora kabisa ya kuhisi uhuru wa ndani. Lakini pengine mzigo wako ni kwasababu ya matendo ya mwingine au hali Fulani ya maisha ambayo yapo chini ya uwezo wako, hapo upo katika hali ya pekee ya kuikabidhi kwa Bwana wetu, kumpa hali yote ya kumiliki hali yote. Uhuru unapatika katika hali ya kujikabidhi kabisa, kuamini na kujikabidhi katika mapenzi yake. Yesu anataka tuwe huru ili tuweze kuhisi furaha anayotaka kutupatia katika maisha yetu. Tunaomba Amani ya Kristo itiririke katika mioyo yetu na kwa njia yetu, na kukutana na wote tunao kutana nao.

Sala: Bwana, ninataka kuwa huru. Ninataka kuhisi furaha ulionayo kwa ajili yangu. Wakati mizigo ya maisha inapo nielemea, nisaidie niweze kukugeukia daima ukiwa msaada wangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 5, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 5, 2026
JUMANNE, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 14 :19-28

Wayahudi walifika toka Antiokia na Ikonio, wakawashawishi makutano hata wakampiga kwa mawe Paulo, wakamburuta nje ya mji, wakidhania ya kuwa amekwisha kufa. Lakini wanafunzi walipokuwa wakimzunguka pande zote, akasimama, akaingia ndani ya mji; na siku ya pili yake akatoka, akaenda zake pamoja na Barnaba mpaka Derbe.

Hata walipokwisha kuhubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi. Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawa weka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.

Wakapita kati ya Pisidia wakaingia Pamfilia. Na baada ya kuhubiri lile neno katika Perge wakatelemka mpaka Atalia. Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza. Hata walipofika wakalikutanisha kanisa, waka- waeleza mambo yote aliyoyafanya Mungu pamoja nao, na ya kwamba amewafungulia Mataifa mlango wa imani. Wakaketi huko wakati usiokuwa mcha che, pamoja na wanafunzi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145 :10-13, 21 (K) 12

(K) Watawajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari wa zamani zote.
Au: Aleluya.

1. Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru,
Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
Wataunena utukufu wa ufalme wako,
Na kuuhadithia uweza wako,
Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu,
Na utukufu wa fahari ya ufalme wake. (K)

2. Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote. (K)

3. Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana;
Wote wenye mwili na walihimidi jina lake
takatifu milele na milele. (K)



SHANGILIO
Ufu. 1:5

Aleluya, aleluya,
Ee Kristo, yu shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14 : 27-31

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga. Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi. Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, kusudi litakapotokea mpate kuamini. Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu. Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MUNGU ANAISHI NDANI MWETU!





“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Mei 4, 2026
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 14:5-18;
Zab 115:1-4, 15-16;
Yn 14:21-26.


MUNGU ANAISHI NDANI MWETU!

Watoto huwa wanaelewa kwamba Mungu anaishi ndani ya mioyo yao. Lakini, kama ukiwauliza wamejuaje, utaona wanakutazama kama kuchanganyikiwa katika kujibu. Licha ya hayo, wao wanatambua kwamba Mungu anaishi ndani yao. Pengine wewe utajibu nini katika swali hili kwamba, “umejuaje Mungu anaishi ndani mwako?” Pengine unaweza kujikuta ukipotea katika kuelezea hali hii ya juu ya fumbo la Imani yetu. Tunatambua kwamba Mungu anapenda kushikilia mioyo yetu, kuongea na sisi, kutuimarisha, kutuongoza na kutulinda sisi. Tunatambua kwa zawadi ya Imani yetu, kwamba Mungu yupo na anatamani muunganiko wa ndani na sisi. Tunatambua tu hilo.

Imani inatuongoza kwenye uelewa, na kila mara tunapo isikiliza sauti ya Mungu inayo ongea ndani mwetu, ikituongoza na kutulinda sisi, ni mwanzo wa kuanza kuelewa kuishi kwake ndani mwetu. Kama Mt. Agustino anavyosema, “Imani ni kuamini kile usicho kiona. Na matokeo ya imani ni kuona kile unacho kiamini”. Imani kwa uwepo wa Mungu inatuongoza kwenye jibu la swali hapo juu. Nitafahamuje, Mungu anaishi ndani mwangu? Jibu ni kwamba ni kwasababu namuona ndani yangu, naongea na yeye ndani, na anaongea na mimi ndani. Na pia naona matokeo ya Imani yangu kwake kutokana na kuamini huku. 

Muache yeye aongee na wewe, katika maongezi ya ndani, ruhusu kuishi kwake ndani kukuwe na kuthihirika kwa wengine. Mungu hapendi tu kuthihirika ndani mwako lakini pia anataka kungara kupitia wewe.

Sala: Bwana, njoo uishi moyoni mwangu. Fanya moyo wangu sehemu yako ya kuishi. Nisaidie niweze kukuona wewe hapo na kuongea na wewe na kukupenda wewe ndani ya roho yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 4, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 4, 2026
JUMATATU YA 5 YA PASAKA

SOMO 1
Mdo. 14:5-18

Siku zile, palipotokea shambulio la watu wa Mataifa na Wayahudi pamoja na wakubwa wao juu yao, kuwatenda jeuri na kuwapiga kwa mawe, wao wakapata habari wakakimbilia Listra na Derbe, mji wa Likaonia, na nchi zilizo kando kando; wakakaa huko, wakiihubiri Injili. Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa. Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa, akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda.

Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng’ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano. Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi ni wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe. Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha. Na kwa maneno hayo wakawazuia makutano kwa shida, wasiwatolee dhabihu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 115 :1-4, 15-16 (K) 1

(K) Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi, Bali ulitukuze jina lako.

Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi,
Bali ulitukuze jina lako.
Kwa ajili ya fadhili zako,
Kwa ajili ya uaminifu wako.
Kwa nini mataifa kusema,
Yuko wapi Mungu wao? (K)

Lakini Mungu wctu yuko mbinguni,
Alitakalo lote amelitenda.
Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya wanadamu. (K)

Na mbarikiwe ninyi na Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi.
Mbingu ni mbingu za Bwana,
Bali nchi amewapa wanadamu. (K)


SHANGILIO
Col. 3:1

Aleluya, aleluya, 
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 14:21-26

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake. Yuda (siye Iskariote), akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?

Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka. Hayo ndiyo niliyowaambia wakati nilipokuwa nikikaa kwenu. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 3, 2026
Juma la 5 la Pasaka


Mdo 6: 1-7;
Zab 32: 1-5, 18-19;
1 Pet 2: 4-9;
Yn 14: 1-12.


MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


Je umekombolewa? “ndio” tumekombolewa kwa njia tatu: tumekombolewa kwa njia ya neema ya Ubatizo, tunaendelea kukombolewa kwa njia ya neema za Mungu na huruma tunapo amua kumfuata kwa uhuru kamili, na tunatumaini kokombolewa na kuingia katika utukufu wa Mbinguni.

Imekuwaje tumepokea zawadi ya thamani ya ukombozi? Kwa njia ya maisha, mateso kifo na ufufuko wa Yesu Kristo ambaye ndiye pekee aliye njia ya kwenda kwa Baba. Njia pekee ya Ukombozi ni Yesu. Hivyo Yesu Kristo anapaswa kuwa kiini cha maisha yetu, na tunapaswa kumuona kama njia, ukweli na uzima. Yeye ni njia pekee ya Mbinguni, yeye ni utimilifu wa ukweli wote ambao tunapaswa kuuamini, na yeye ni uzima ambao tunapaswa kuuishi na yeye ndiye chanzo cha maisha mapya ya neema. Bila yeye sisi si kitu, bali kwa njia yake unapata maisha makamilifu.

Katika somo la pili, Petro analifananisha Kanisa na jengo la kiroho ambalo mjenzi ni Mungu na mawe yanayoishi ni watu. Msingi ulianza kwa mawe imara kwa jengo lote, Kristo ambaye juu yake Mungu ameweka pia mawe mengine, wale wanao mwamini yeye. Wakiwa wameunganika na Yesu, wanatengeneza hekalu moja la Mungu.

Injili inamuonesha Yesu kama kielelezo cha maisha ‘njia, ukweli na uzima’. Kiini cha ukristo ni Kristo mweyewe. Kazi yetu kwa Yesu na upendo wetu kwa watu, haijalishi tumeitwa katika maisha ya namna ghani, maisha yetu yanatiririka kutoka katika chanzo hiki. Mama Teresa aliulizwa kwanini alifanya aliokuwa akifanya, na alijibu tu “ni kwa ajili ya Yesu”. Hiki ndicho kiini kinacho shikilia ili kusiwe na mtikizo au usumbufu wowote. Ni muunganiko wa ndani na Yesu. Kusoma maisha yake, kupata muda wa kutambua mazingira yake na matukio ya maisha yake, kuwa familia na Injili na kumfahamu katika moyo wa sala, njia yetu ya kuweka msingi wetu na ujasiri wetu kuwa imara kwa Yesu. Hivyo mchague yeye katika hali zote za maisha kama Bwana wako na mkombozi. Kwa unyenyekevu jitambue kuwa bila yeye wewe si kitu, na jikabidhi kwake ili yeye aweze kukuongoza salama kwa Baba yetu wa mbinguni.

Sala: Bwana na Mkombozi, ninakukubali wewe katika maisha yangu kama Bwana na Mkombozi. Ninakushukuru kwa zawadi ya ubatizo iliyo anzisha maisha ya neema ninaomba nibadilishe maisha yangu niendelee kukufuata kikamilifu, leo na siku zote, ili uweze kuingia zaidi ndani ya maisha yangu. Ninaomba matendo yangu yote yaongozwe nawe ili niweze kuwa sadaka ilyio unganika na wewe milele, Yesu mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026


MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026
JUMAPILI, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3

(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)


SOMO 2
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 14 : 6

Aleluya, aleluya,
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14: 1-12

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia, maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaa ndalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendakt mwaijua njia. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia? Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MUNGU KUDHIHIRIKA NDANI YA MAISHA YETU!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Mei 2, 2026
Juma la 4 la Pasaka


Mdo 13:44-52;
Zab 98:1-4 (R. 3);
Yn 14:7-14.


MUNGU KUDHIHIRIKA NDANI YA MAISHA YETU!


Mara nyingi, hatujui ni kwa jinsi ghani Mungu anajifunua mwenyewe katika maisha yetu kama Filipo, anayetaka kumuona Baba. Alikuwa mbele ya Yesu, na bado anamtafuta Mungu. Sisi pia katika maisha yetu. Mungu yupo nasi daima lakini kwasababu ya mawazo yetu na mitizamo yetu tunamtafuta. Sisi nasi tunamtafuta Mungu na baadae tuna mtambua Yesu mbele yetu.

Paulo na Baranabas walitambua utambulisho wa kweli wa Yesu na wanamhubiri kwa ujasiri mkubwa, kwa mataifa licha ya mateso na vipingamizi. Kama sisi tunajiita wakristo, Kristo anapaswa kudhihirika katika maisha yetu. Kama kumuona Yesu ni kumuona Mungu Baba ni wazi kwa matumaini na katika sala, kutuona sisi ni kumuona Yesu pia.

Injili ya Yohane inatumia lugha hii mara nyingi kuonesha umoja mkamilifu wa Yesu na Baba yake. Ni jambo zuri namna ghani sisi nasi kusema sisi hatuseme wenyewe bali ni Kristo anasema ndani yetu? Hili ndilo linalopaswa kuwa lengo letu la kila mara. Kama tutaongea maneno kwa wengine, tukiwa tumejikita katika hekima yetu wenyewe na uelewa wetu wenyewe, ni lazima tuji nyenyekeshe na kutambua kwamba maneno yetu hayawezi kuwa na nguvu. Lakini kwa upande mwingine, lakini kama tunaweza kusema maneno yaliyo jaa Kristo, maneno ambayo yanasemwa kutoka ndani ya moyo wake, tutaanza kuona maneno hayo yanakuwa na manufaa katika maisha ya watu. Maneno yana maana sana, na tunapaswa kuwa makini katika kuongea na kuwa na ujasiri na kile tunachosema, jinsi ya kusema na tunasemaje. Kumruhusu Baba aongee ndani mwetu na kupitia sisi maneno yetu yanakuwa na ujasiri na nguvu. Yanakuwa maneno ambayo Mungu alitaka kuongea kwa wengine ambayo yanamfanya Mungu afanye mabadiliko katika maisha yao.

Sala: Bwana, nipe maneno yako ya kuongea. Nisaidie mimi nikurudie wewe ndani ya moyo wangu kwa ujasiri ili uweze kuwa chanzo cha ukweli na uzuri. Ninaomba ukweli huo utoke ndani mwangu kila siku. Ninaomba wote wakuone wewe kwa njia ya maisha yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 2, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 2, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 4 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3

(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)



SHANGILIO
Rum. 6:9

Aleluya, aleluya.
Kristo akiisha kufufuka katika wafu, hafi tena wala mauti haimtawali tena.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14:7-14

Yesu aliwambia wanafunzi wake: Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.

Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.

Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Minisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MT. YOSEFU MFANO WA WAFANYA KAZI





“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Mei 1, 2026.
Juma la 4 la Pasaka

Kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi


Mwa 1:26-2:3; 
Zab 90:2-4, 12-14, 16 (K. 17);
Mt 13:54-58.


MT. YOSEFU MFANO WA WAFANYA KAZI


Injili  ya leo inaongelea kuhusu lile kundi la watu wanaomtafuta Yesu, siku baada ya kuongeza ile mikate. Kumtafuta huku haikuwa kwasababu ya upendo kwake, bali kufaidika kutoka kwake. Yesu, anawaambia wazi kwamba wanamtafuta kwasababu walikula mikate, Yesu anawaeleza wawe na lengo lingine la kumtafuta. Sababu iwe ni kwasababu anataka kuwapa chakula cha kiroho.

“Je, unamtafuta Yesu kwasababu njema?” pengine mara nyingi tunamtafuta Yesu kwasababu ya faida fulani, pengine ili kupata gari, nyumba, mchumba, uponyaji wa ugonjwa. Yesu anatuonya tuangalie tusimtafute kwasababu ya vitu vinavyo haribika tu, bali tutafute uzima wa milele.

Kanisa leo lina adhimisha kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi. Mungu alimwamini na kumpa jukumu la kumtunza Mama wa Mungu na Mwana wa Mungu, na kuwa mlinzi wa nyumba ya Mungu. Hakuna mtu mwingine yeyote aliyekuwa na nafasi hii pekee. Kupenda kwake kazi ilionesha unyenyekevu wake, aliishi kwa kadiri ya matakwa ya Mungu. Alikuwa mtu mwenye haki. Kilicho mfanya akubalike machoni pa Mungu ilikuwa kwasababu ya Imani yake na utii wake. Kujitoa kwake kulionesha unyenyekevu na kumtegemea Mungu. Na hata baada ya kupata upendeleo kutoka kwa Mungu, hakuacha kufanya kazi.

Katika hali hii tunaweza kusema kwamba yeye ni somo wa wale wote wanaofanya kazi, kazi ambayo ni kuonesha unyenyekevu na tegemeo letu kwa Mungu. Leo tunawakumbuka watu wote duniani wanao fanya kazi kwa manufaa ya uzuri wa wanadamu wote. Tuwaombee kazi zao zisiharibu mpango wa Mungu kwa mwanadamu bali zilinde utu na uhai wa kila mwanadamu kama Mt. Yosefu alivyo linda uhai wa Yesu dhini ya Herode.

Sala: Asante, Mt. Yosefu kwa kumfundisha Yesu kufanya kazi yako. Tunakushukuru kwa kuzipa kazi za mikono thamani na utakatifu. Tunaomba tuweze kuzipa heshima kazi na kuwa tayari kwa ajili ya wengine kama wewe. Mt. Yosefu, mlinzi wa nyumba ya Mungu. Utuombee.



Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com