Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

ROHO MTAKATIFU, MSAIDIZI!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 10, 2026
Dominika ya 6 ya Pasaka

Mdo 8: 5-8, 14-17;
Zab 65: 1-7, 16, 20;
1 Pet 3: 15-18;
Yn 14: 15-21.


ROHO MTAKATIFU, MSAIDIZI!

Kwa, jumapili ya sita ya Pasaka tunaanza kufungua macho yetu na kuanza kutazamia ujio wa Roho Mtakatifu. Yesu anaongea kuhusu kumuomba Baba alete msaidizi mwingine awe nasi daima. Huyu msaidizi ni Roho Mtakatifu.

Katika somo la kwanza tunasikia kuhusu Filipo. Anafika Samaria na anaanza kuhubiri Injili na kubatiza wote waliopokea Imani. Roho Mtakatifu aliwaimarisha wamisionari hawa wa kwanza kwa kuwapa nguvu katika maneno yao kwa kudhihirisha uwepo wake kwa ishara. Watu wa mji ule walibadilika na wakajazwa na furaha. Sehemu ya pili ya somo inamuonesha Petro na Yohane wakiwatembelea wabatizwa huko Samaria. Mitume hawa wawili waliwawekea mikono ili Roho Mtakatifu aweze kuwa juu yao. Walishangazwa Wasamaria waliobatizwa na Filipo walikuwa hawajapokea Roho Mtakatifu. Uwepo wa Mungu ulikosa ishara ya njee ambayo ilikuwepo wakati wa Kanisa la mwanzo. Luka anaunganisha matukio haya mawili, kutuonesha kwamba kila sehemu Injili ilipo hubiriwa kuna jumuiya mpya inayokuwa. Lakini, hawakuhitaji kukuwa, kuendelea na kuishi katika hali ya pekee kabisa na inayo jitegemea. Ni vizuri walianzisha umoja wa kuunganisha na kanisa nzima. Ni Roho pekee atakaye jidhihirisha ndani yao wote.

Katika somo la Injili tunaona ujumbe wa wosia wa Yesu. Mitume wanahuzuni kwababu ya kuondoka kwa Yesu, na wana ahidiwa msaidizi mwingine Yesu anaeleza wazi kwamba Roho Mtakatifu watampokea tu wale waIe walioungana naye, katika mipango yake na katika kazi zake za upendo. Huyu Roho anaitwa kwa majina mawili. Mfariji na Roho wa kweli.

Msaidizi ni neno linalo onesha kwamba ni yule aliyeitwa ili aweze kuambatana. Hapo kale kulikuwa hamna kuanzishwa kwa sheria, kila mtu alipaswa kujitetea na kujilinda mwenyewe. Ilitokea mara chache kwamba, mtu hana kosa, lakini mtu haweze kudhihirisha kwamba hana hatia. Kwake kilicho salia ni tumaini moja tu: kwamba mtu mmoja wa heshima atatokea katika mkutano aongee bila kusita na kutoa ushahidi wa kumtetea. Ishara hii ni sawa na kufunguliwa gerezani. Na wala hakuna yeyote atakaye kushutumu tena. Huyu anaitwa “Msaidizi” maana yake yule anayeitwa ili aweze kuwa karibu na mwingine ambaye amepata matatizo. Yesu aliwahidia wafuasi wake msaidizi, kwasababu tayari wamesha mpata wa kwanza ambaye ni Yesu mwenyewe. Roho Mtakatifu ni Msaidizi kwasababu anawasaidia Wafuasi katika vita dhidi ya malimwengu hasa maovu. Yohane anawakumbusha wafuasi juu ya ukweli huu ili wanapo kutana na ugumu katika maisha, wasikatishwe tamaa, kupoteza tumaini, bila kupoteza Amani ya moyo na furaha. Wafuasi waliamini juu ya usaidizi wa Roho Mtakatifu. Wana amini nguvu ya Msaidizi huyu na kwamba hatashindwa.

Roho wa ukweli anafanya kazi katika huduma ya kweli. Ujumbe wa Yesu umeelekezwa kwa watu wote. Unapaswa kuhubiriwa mpaka miisho ya ulimwengu. Roho Mtakatifu anadhihirisha kwamba hatashindwa, na wala hayata fafanuliwa vibaya na kuharibiwa, mafundihso ya Kristo. Yeye haondoi tu makosa yanayo fanywa na kukosewa katika kurithisha ujumbe wa Yesu. Anawatambulisha wafuasi katika ukweli wote. Yeye yupo katika kuwaelekeza wafuasi katika kutambua ukweli wote. Hatasema kitu kingine kipya kinacho pinga ujumbe wa Yesu. Atasaidia katika kuendeleza ujumbe wa Yesu mpaka miisho yote. Kazi ya Wakristo nikubaki imara katika kazi hii ya Roho Mtakatifu ambaye daima anafunua mambo mapya. Yeye kwa asili ndiye anaye ufanya upya uso wa Nchi (104:30). Ni dhambi juu ya Roho Mtakatifu kupinga kufanywa upya, kukataa kufanya mabadiliko katika maisha ya jumuiya, ambayo yanawaleta watu karibu na Yesu na wandugu, ambayo huongeza furaha na amani ambayo yanawafanya watu wasali vizuri na kufanya moyo uwe huru na kuondoa hofu zote.

Kama tupo wazi kwa ujio wa Roho Mtakatifu, tutapokea Msaidizi mzuri kabisa katika maisha yetu yote. Roho Mtakatifu ndiye msaidizi tunaye mhitaji. Kuzama ndani ya Roho Mtakatifu inatufanya tujazwe na neema zote katika maisha. Sali sala ya Roho Mtakatifu na kutarajia kusherekea dominika ya Pentekoste jumapili mbili zijazo.

Sala: Ee, Mungu, wewe ambaye kwa Roho Mtakatifu, unaongoza Roho za Waamini wako, jalia kwa Roho huyo huyo, tuweze kuwa wakweli na wenye hekima na kufurahia faraja yake, kwa Njia ya Kristo Bwana wetu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 10, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 10, 2026
DOMINIKA YA 6 YA PASAKA


MWANZO:
Isa. 48:20
Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni, Bwana amelikomboa taifa lake, aleluya.


SOMO 1
Mdo. 8:5-8, 14-17

Filipo alitelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo. Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifa- nya. Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na wratu wengi waliopooza, na viwete, wakaponywa. Ikawa furaha kubwa katika mji ule.

Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohane; ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu; Kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu. Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 66 :1-7, 16, 20, (K) 1

(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote, au: Aleluya.

Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Imbeni utukufu wa jina lake,
Tukuzeni sifa zake.
Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! (K)

Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,
Naam, italiimbia jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu;
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)

Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tulikomfurahia.
Atawala kwa uweza wake milele. (K)

Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu,
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)



SOMO 2
1 Pet. 3 :15-18

Mwe tayari sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo. Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikrwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.

Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Yn. 14:23

Aleluya, aleluya,
Yesu alisema: Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake. Aleluya.



INJILI
Yn. 14 :15-21

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Mkinipenda, mtazishika amri zangu. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.

Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai. Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu. Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUKUTANA NA MATESO



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Mei 9, 2026
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 16: 1-10;
Zab 100: 1-3,5 (K. 1);
Yn 15: 18-21.


KUKUTANA NA MATESO

Mkristo kwa Sakramenti ya Ubatizo ni mmisionari. Anaitwa kushirikisha Habari Njema kwa kila mtu . katika ubatizo, Mkristo hufufuka kutoka katika hofu ya kifo, na kwenda kwenye utukufu wa uzima wa milele. Sisi sio watu tuliofungwa na dunia bali watu tuliofungwa na Mbinguni. Na hii safari ya kwenda mbinguni sio rahisi, kwasababu thamani na hali ya maisha ya Kikristo ni tofauti na hali ya kawaida ya kufikiri. 

Ni rahisi kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa karibu na Yesu ni kadiri hiyo hiyo tutakavyo pendwa na kueleweka na Ulimwengu. Tunadhani kwamba kila mtu atapendezwa na kuvutwa na utakatifu wetu na kuwa watu wazuri kwetu. Lakini sivyo. Tukiangalia maisha ya Yesu, tunatambua kuwa haikuwa hivyo. Alikuwa wazi ni mkamilifu kwa kila kitu. Lakini, walimtenda vibaya na kumsulubisha. Alishikwa na kupigwa na kutukanwa na kuhukumumiwa kifo. 

Kama tungekuwa pale, tungeweza kushangazwa sana, na kuchanganyikiwa. Tunaweza kufikiri kwamba Yesu alikosea na hivyo kupoteza matumani kwake. Lakini mpango wake ulikuwa mkamilifu kwa kila njia na mpango wake ulikuwa katikati na kumfanya yeye kuvumilia dhuluma za uongo na kuteswa. Na kwa uhuru kukubali kushutumiwa, aliikomboa dunia. 

Ukristo ni dini inayo onewa kuliko zote duniani. Asimilia kumi ya wakristo ulimwenguni wananyanyaswa na kuonewa kwasababu tu ya imani yao. Kunyanyaswa na kuonewa kunaleta hofu na uchungu. Lakini sio kitu ambacho tunapaswa kukikimbia. Hatupaswi kupoteza matumaini yanavyotokea haya. Kwanini? Kwasababu manyanyaso ni ishara wazi tunafuata njia sahihi ya Yesu. Tumeungana na Yesu zaidi katika njia ya kuonewa na kudhulimiwa kuliko hata tunavyofikiri. Ufunguo ni kutambua kwamba Mungu atatumia madhulumu yote kuwa furaha yetu kama tutamruhusu. Na tutamrushu ayatumie kwa kuleta mema kama tutajikabidhi kwake kwa uhuru kabisa. Majibu yetu yanapaswa kuwa “furahi na kushangilia” kwani tumekuwa sahihi katika kufuata njia ya Bwana wetu, Mwana wa Mungu. 

Leo tutazame katika hali yeyote ya kuonewa na kudhulumiwa au kukosewa haki tunayo ipata kwasababu ya Imani yetu na kushika Injili. Tuwaombee pia Wakristo wanaodhulumiwa huko Syria, Misri, China, Pakistani, India nk. 

Sala: Bwana, nina kabidhi kwako yale yote yanayo niangusha chini. Ninatoa sadaka yote ninayo pokea kwa kuwa mtumishi na mfuasi wako. Ninaomba nisikuige wewe tu katika mateso yako, bali kutii mapenzi yako daima. Yesu, nakuamini wewe. Amina. 

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 9, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 9, 2026
JUMA LA 5 LA PASAKA, JUMAMOSI


SOMO 1 
Mdo 16:1-10

Siku zile, Paulo alifika Derbe na Listra na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio. Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani. Basi walipokuwa wakipita kati ya miji ile, wakawapa zile amri zilizoamriwa na mitume na wazee walioko Yerusalemu, ili wazishike. Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.

Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia, wakajaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemka Troa. Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie. Basi alipo- kwisha kuyaona vale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia. kwa kuwa tuliena hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATI KATI 
Zab. 100 :1-3, 5 (K) I

(K) Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote. au: Aleluya.

Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yole.
Mtumikieni Bwana kwa furaha.
Njoni mbelc zake kwa kuimba; (K)

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake:
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)


SHANGILIO 
Yn. 20-29

Aleluya, aleluya, 
Wewe Toma, umesadiki kwa kuwa umeniona, 
wa heri wale wasioona wakasadiki. 
Aleluya,


INJILI 
Yn 15 : 18-21

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia. Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu. Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

TUMECHAGULIWA KUWA WA MUNGU!





“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Mei 8, 2026
Juma la 5 la Pasaka

Mdo 15: 22-31;
Zab 57: 8-12 (K. 10);
Yn 15: 12-17.


TUMECHAGULIWA KUWA WA MUNGU!


Watoto wanapenda kucheza michezo. Wakati mchezo unaundwa kwa pande mbili, watoto wanaunga mstari wakisubiri kuchaguliwa. Kila mtoto anategemea kuchguliwa wa kwanza. Inaonesha hamu ya ndani ya kutaka kuchaguliwa kwa ajili ya mchezo. Hili linaonesha hamu iliyopo ndani ya kila mmoja wetu ya kuchaguliwa. Uzuri ni kwamba, Mungu anamchagua kila mmoja wetu. Anatutaka sisi kuwa watoto wa familia yake na anatutaka tuwe watu wake. Hili ni la muhimu kulielewa na likieleweka linadhihirika. Mungu alituchgua sisi hata kabla hatuja zaliwa. Anatufahamu kabla, tangu milele yote na anaweka jicho lake juu yetu, akilenga kutuleta sisi katika kundi lake. Tunapaswa kutambua hili, kulikubali na kuliamini. Sisi ni wake.

Mungu hatuchagui sisi tu kuwa wake, anatuchagua pia kwa utume. Anataka kututumia sisi tuzae matunda kwa Ufalme wake. Anataka kututumia sisi kwa malengo matakatifu na wito wa Kimungu. Haijalishi ni mara ngapi tunaweza kujiona “hatustahili” tunaweza kujisikia kufanya utofauti, tunapaswa kukumbuka kuwa Mungu hatuoni katika hali hiyo. Bali, anaona utajiri mkubwa ndani ya kila mmoja wetu na kuchagua kutumia utajiri huo kujenga ufalme wake. 

Mungu anakuambia “nimekuchagua wewe” na “Nenda ukazae matunda”. Kukubali wito wako kutoka kwa Mungu utabadilisha maisha yako na pia yatabadilisha maisha ya wale ulioitwa kuwatumikia.

Sala: Bwana, ninatambua umenichagua mimi. Ninakubali wito wako katika maisha yangu. Ninakubali ukweli kwamba umenichagua mimi katika hali ya utume wa pekee na hali ya utukufu wa pekee. Nisaidie daima niendelee kusema “ndio” kwa wito wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 8, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 8, 2026
IJUMAA, JUMA LA  5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 15 : 22-31

Siku zile, baada ya Mtaguso wa Yerusalemu, ikawapendeza mitume na wazee na kanisa lote kuwachagua watu miongoni mwao na kuwapeleka Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba; nao ni hawa, Yuda aliyeitwa Barnaba, na Sila, waliokuwa watu wakuu katika ndugu.

Wakaandika hivi na kupeleka kwa mikono yao, Mitume na ndugu wazee, kwa ndugu zetu walioko Antiokia na Shamu na Kilikia, walio wa Mataifa; Salamu. Kwa kuwa tumesikia ya kwamba watu waliotoka kwetu wamewasumbua kwa maneno yao, wakipotosha roho zenu, ambao sisi hatukuwaagiza; sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwapeleka kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Basi tumewatuma Yuda na Sila, watakaowaambia wenyewe maneno yayo hayo kwa vinywa vyao. Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo valiyo lazima, yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo mtafanya vema. Wasalamu.

Hata hao wakiisha kupewa ruhusa wakatelemkia Antiokia; na baada ya kuwakusanyia jamii yote wakawapa ile barua. Nao walipokwisha kuisoma, wakafurahi kwa ajili ya faraja ile.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA K.ATIK.ATI
Zab. 57 : 7-11 (K) 9

(K) Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu.
au: Aleluya.

Ee Mungu, moyo wangu u thabiti,
Moyo wangu u thabiti.
Nitaimba, nitaimba zaburi,
Amka, utukufu wangu.
Amka, kinanda na kinubi,
Nitaamka alfajiri. (K)

Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,
Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,
Na uaminifu wako hata mawinguni.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako. (K)



SHANGILIO
Yn. 10:27

Aleluya, aleluya,
Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata. 
Aleluya.




INJILI
Yn. 15 :12-17

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.

Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni. Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KUONGEA LUGHA YA MUNGU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Mei 7, 2026
Juma la 5 Pasaka

Mdo 15: 7-21;
Zab 96: 1-3,10 (K. 3);
Yn 15: 9-11.


KUONGEA LUGHA YA MUNGU!

Wanadamu wanatamani kupendwaa na kujaliwa. Lakini ni vigumu kwa njaa ya upendo kutimizwa, katika hali ya kibinadamu. Leo, Yesu anaongea kuhusu upendo unaozalisha furaha isiyo pimika, ambayo ni Baba na Yeye anayo tu kwa wale walio wake. Hatuwezi kumzidi Mungu kwa mapendo kwasababu anatupenda bila kipimo, kwa upendo unaotoa neema, uzima, Amani na furaha.

Upendo wa Mungu ni kamili na hauwezi kuingiliwa. Upendo wa Baba kwa Mwanae ni kamili katika nyanja zote. Hauna masharti na unakamilisha yote. Ni kamili na hauna ubinafsi. Kwa kupokea upendo wa Baba, Yesu alipokea yote aliyo hitaji. Upendo aliopokea Yesu kutoka kwa Baba yake hauwezi kuondolewa. Hauwezi kuwekwa kwa ubinafsi. Unatiririka kutoka katika moyo wa Yesu na kuja kwetu. Mtiririko huu wa upendo, tuliopewa sisi, hauwezi kufungwa ndani ya mioyo yetu bila kwenda kwa wengine. Hivyo kama tunataka kuwa wapokeaji wa zuri wa upendo wa Baba na Mwana, tunapaswa kuruhusu upendo huo uwatiririkie wengine bila “Kikomo” na bila “Masharti”. 

Leo tunaitwa kupenda kwa niaba ya upendo wenyewe, kwa niaba ya Kristo, ambaye ndiye msingi wa upendo wa kweli. Si kwasababu nyingine bali kwa upendo kamili ambao Yesu alitoa kwa ajili yetu. Maisha yetu kama wafuasi wa Yesu yanapaswa kuwa maisha ya kujitoa kwa upendo kwa wengine. Upendo wa Yesu ambao upo ndani yetu unapaswa kutambuliwa, kukukubali na kuupeleka kwa wengine. Hili ndilo lengo la maisha ya Kikristo: kubaki katika upendo wa Kristo na kujazwa furaha. Mimi na wewe tumebarikiwa kufahamu ukweli kwamba MUNGU ni UPENDO. Hivyo tutangaze ukweli huu bila wasi wasi na bila kujibakiza. Kama tutamruhusu Mungu atupende kwa upendo mkamilifu, tutaanza kuona mara moja kwamba upendo huu ukitiririka ndani mwetu kama vile mto wa neema na huruma.

Sala: Bwana, ninakupenda wewe na ninatambua napendwa na wewe. Nisaidie mimi niweze kuwa wazi kwa upendo wako. Nisaidie niweze kufanya upendo huo uzame ndani ili uweze kutiririka kutoka moyoni mwangu na kwenda kwa wengine pia. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 7, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 7, 2026
ALHAMISI YA 5 YA PASAKA

SOMO 1 
Mdo. 15:7-21

Wakati wa Mtaguso wa Yerusalemu, baada ya hoja nyingi Petro alisimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini. Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi; wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani. Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua. Bali twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu vile vile kama wao.

Basi mkutano wote wakanyamaza, wakawasikiliza Barnaba na Paulo wakiwapasha habari za ishara na maajabu, ambayo Mungu aliyafanya kwa ujumbe wao katika Mataifa. Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu, akisema, Ndugu zangu, nisikilizeni. Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake. Na maneno ya manabii yapatana na hayo, kama ilivyoandikwa.

Baada ya mambo haya nitarejea, nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, nami nitaisimamisha; ili wanada- mu waliosalia wamtafute Bwana, na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao; asema Bwana, ajulishaye hayo tangu milele.

Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwata- abishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa; bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu. Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 96:1-3, 10 (K) 3

(K) Wahubirini mataifa habari za utukufu wake.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Mwimbieni Bwana nchi yote.
Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake. (K) 

Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,
Na watu wote habari za maajabu yake. (K)

Semeni katika mataifa, Bwana ametamalaki;
Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, 
Atawahukumu watu kwa adili. (K)



SHANGILIO 
Lk. 24 : 25-26

Aleluya, aleluya, 
Ilimpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 15:9-11

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUONDOA MAJIVUNO NA UBINAFSI!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Mei 6, 2026
Juma la 5 la Pasaka


Mdo 15:1-6;
Zab 122:1-5 (R. 1);
Yn 15:1-8.


KUONDOA MAJIVUNO NA UBINAFSI!


Kupunguza matawi ni muhimu kwa mti kama unapenda uzae mataunda mazuri au maua mazuri. Kama, kwa mfano, mti wa maua ya waridi unakuwa bila kupunguzwa, unatoa vimaua vidogo vingi, amabavyo ni dhaifu. Lakini kwa mti mzuri ulio pruniwa unatoa maua mazuri yenye afya. Yesu anatumia mfano kama huu kutufundisha somo kama hilo katika kuzaa matunda mazuri kwa ufalme wake. Anataka maisha yetu yawe yenye matunda mema na anataka kututumia sisi kama vyombo vyake vyenye nguvu ulimwenguni. Lakini tusipo ingia katika maisha ya kiroho ya kujipruni mara kwa mara , hatutakuwa vyombo ambavyo Mungu anaweza kuvitumia.

Kujipruni kiroho unachukua ile hali ya kumruhusu Mungu aondoe maovu katika maisha yetu ili fadhila ziweze kungaa. Na hili lina fanikiwa hasa tunapo mruhusu atupe unyenyekevu na kutuondoa katika maringo yetu. Hili linaweza kuumiza, lakini maumivu yanayo tokana na kunyenyekeshwa na Mungu ni ufunguo wa kukuwa kiroho. Kwa kukuwa katika unyenyekevu, tunakuwa zaidi katika kujikita katika chanzo chetu kuliko katika kukuwa katika hali zetu wenyewe, mawazo yetu wenyewe na mipango yetu wenyewe. Mungu katika hali ya juu kabisa ana hekima kuliko sisi na kama tutaendelea kumwelekea kila mara kama chanzo chetu, tutakuwa wenye nguvu zaidi na kujiandaa yeye afanye mambo makubwa zaidi kwa njia yetu.

Kujiruhusu kupruniwa kiroho maana yake ni kuachia yaondoke mapenzi yetu wenyewe na mawazo yetu. Maana yake tunaachia kujitawala wenyewe na kumwachia aliye mkuu wa kukuza akuze na kuchukua nafasi. Ina maana tuna mwamini yeye zaidi kuliko tunavyo jiamini sisi wenyewe. Hili linahitaji kufa kwa nafsi zetu wenyewe na unyenyekevu wa kweli na kukiri kabisa kwamba Mungu ndiye tegemeo letu kwa kila kitu, kama tawi linavyo tegemea mti. Bila mti, tutaseka na kufa. Mwamini yeye na mipango yake na tambua kuwa hii ndio njia pekee ya kuzaa matunda mema, ambayo Mungu anayataka kupitia wewe.

Sala: Bwana, ninakuomba upruni majivuno yangu na kuyatupa mbali na pia uovu wangu. Nitakase mimi kutoka katika dhambi zangu nyingi ili niweze kujikabidhi kwako kwa kila kitu. Na ninapo jifunza kujikabidhi kwako, ninakuomba uanza kuzaa matunda mema katika maisha yangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com