“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila Jumapili
Jumapili,
Septemba 6, 2026
Dominika
ya 23 ya Mwaka
Ez
33: 7-9;
Zab
94: 1-2, 6-9;
Rom
13: 8-10;
Mt
18: 15-20
KUJENGA
JUMUIYA YENYE KUWA NA TAHADHARI!
Wakati
watu wameshakutana na ugumu fulani, wanakuwa wanatoa kiashirio kwa wengine
kwamba muelekeo sio mzuri, viashirio vyao mara nyingi wengi hawa vitilii
maanani. Lakini katika hali ya kweli, wengi hupenda kuwatazama wengine wakiwa
katika njia isio faa. Mara nyingi wanawachukia, kuwatania na kuwaona wajinga.
Mungu analinganisha kazi ya nabii Ezekieli na ya mlinzi. Alikuwa apewe onyo kutoka
kwa Mungu naye alipeleke onyo hilo kwa kila mtu. Kazi ya Kanisa na ya kila
mkristo ni sawa sawa. Ni kuwaongoza watu kwa ujumbe wa neno la Mungu. Siku hizi
tunatumia teknolojia yenye nguvu kuwapa watu ishara ya hatari ya kujisahau
kushika neno la Mungu. Tunachofanya leo na teknolojia kilifanyika katika
Biblia, ambapo waliwaweka walinzi katika sehemu Fulani ili aweze kutoa ishara
ya hatari wakati aduia anataka kukaribia.
"Mtu
mmoja alikuwa akishanga shangaa aliokota ufunguo bondeni karibu na mlima
mkubwa. Ulikuwa ni ufunguo wa ajabu, ufunguo ambao ulikuwa na uwezo wakufungua
kila aina ya nyumba yenye hazina ulimwenguni. Kwa ufunguo huu alikusanya
dhahabu na almasi kutoka katika sehemu mbali mbali alizopenda duniani. Akiwa
njiani akirudi alisikia sauti ikimwambia kutoka chini ya mlima: “kabla
haujatoka nje, hakikisha hausahau kitu muhimu kuliko vyote. Gafla mlango
ukafunga moja kwa moja. Alikuwa amesahau kuchukua ufunguo.”
Mwanadamu
daima anatafuta kupata ufunguo wa furaha, Amani na kujitosheleza. Sisi wote
tunatafuta ufunguo wa urafiki, kueleweka, kuwa na jina na uzuri, na kuwa na
kazi nzuri yenye kuvutia na faraja. Wengine wanatafuta furaha kwa fedha,
madaraka nk. Lakini hivi vyote vinatufunga na kujikuta tunapotelea huko.
Vinatufunga kiasi ambacho tunasahau kitu muhimu ziadi nacho ni ufunguo wa
maisha. Maisha ya Ukristo yanatufundisha kwamba dunia hii itapita, hiki ndicho
tunacho paswa kuzingatia kwa macho yetu na kutazama “maisha ya umilele”. Hii
inamaana kwamba maisha yetu hapa duniani yana lengo zaidi ya lengo la kawaida.
Furaha tulio nayo hapa sio kitu, ni kivuli tu cha furaha halisi ambayo tutakuwa
nayo huko mbinguni. Lakini ufunguo wa furaha ya maisha haya uko wapi?
Katika
somo la Injili ya leo Yesu anatuonesha picha nzuri ya jumuiya ya mapendo na yenye
kujali. Inatuonesha ni kwa jinsi ghani tunaweza kuanzisha jumuiya ya kweli ya
Kikristo na yenye kupendana.
1.
Kama mtu akikukosa, tunapaswa tumwendee kwa upendo wa Kimungu na kumrudisha
kundini. Tofauti kabisa na kumlaumu na kuanza kumlaumu, tunapaswa kumfuata kwa
mapendo na kumsihi katika mapendo yetu. Injili inatushauri kuwa na mazungumzo
ya moja kwa moja, kwa utulivu na katika hali ya upekee, katika hali ya
kurekebishana kindugu, ili kuanzisha tena urafiki uliyo vunjika. Kama hili
litashindikana inashauriwa kuchukuwa watu wenye hekima na kumfuata kumuonesha
kwamba jumuiya nzima inakuhitaji kurudi kundini katika mapendo yote.
2.
Yesu anasisitiza nguvu ya sala. Anasema “pale wawili au watatu walipokusanyika
kwa ajili yangu, Baba atakuwa katikati yao”. Huu ni uhakika anaotoa Yesu kwamba
wale wanaosali yeye atakuja katikati yao na kuwa kati yao na kushiriki katika
sala yao. Wayahudi walikuwa na Imani kubwa katika sala za pamoja. Iliandikwa
“wawili walipo kusanyika na wanajihusisha na kujifunza Torati, utukufu wa Mungu
upo katikati yao” sala za jumuiya huweka magomvi mbali na kuleta umoja. Agano,
jumuiya, ukarimu, msamaha hizi ni sifa za dini ya Kibiblia. Uzoefu wa haya yote
vinafanya maisha yetu kuwa na furaha, na kuishi vizuri. Haya yote yanawezekana
tu pale ambapo tuna upendo. Kwa mfano,
"Mfungwa
mmoja alikuwa anarudi nyumbani, kutoka katika mahabusu ya mbali akiwa kwenye
treni. Alikuwa akiona aibu kwa kufungwa kwake na alikuwa akidhani familia yake
itakuwa imemsamehe. Kwa ishara ya kuonesha kwamba wamemsamehe, walipaswa
wafunge riboni nyeupe kwenye mti ambao ulikuwa karibu na gari nyumbani kwake.
Hivyo kama hataona riboni nyeupe kwenye mti, yeye atapitiliza na treni aelekee
kokote atakapo kwenda. Wakati treni ilivyofika karibu na nyumbani, akawa na
wasi wasi mkubwa kiasi ambacho hakuthubutu kutazama kupitia dirishani. Marafiki
zake wakaamua kubadilisha nafasi wakisema tunafahamu tu ataangalia mti
uliokaribu na gari. Ghafla akanyanyua kichwa bila kujua na tazama sio roboni
moja iliyowekwa kwenye mti bali mti wote ulikuwa umejaa riboni"
Amani
na mshikamano unawezekana tu, pale ambapo watu wanaishi kwa roho ya upendo na
msamaha. Mungu ni upendo na penye upendo Mungu yupo. Upendo wa Mungu unabeba
pia upendo kwa jirani. Upendo tunaweza kuupata tu tunapo amua kuishi na
wenzetu, kwa mshikamano katika jumuiya. Hili halimuumizi mtu yeyote, bali
linakamilisha kila kitu na kufanya maisha yafikie katika kilele cha hali ya
juu.
Mungu
ametufanya sisi tuwe walinzi wa dunia sasa. Tunapaswa kuwa walinzi, kutangaza
kwa kila mmoja, jumuiya zetu, na ulimwengu wa ukweli katika Yesu Kristo.
Tunaitwa kusimama pamoja, bila kuachana katika Imani bila kuogopa kuitwa tusio
na maana au mafundisho potofu, bali tutangaze kwa jirani na jumuiya zetu, ili
watu wafahamu katika kutokufahamu kwao, kumuamini Yesu, na kukuwa katika neema
na utakatifu. Tunapaswa kuwasaidia wengine watambue makosa yao, hasa tukiwa na
kazi kama ya wazazi kwa mtoto, mwalimu kwa wanafunzi, wazee na vijana.
Tutumie
njia sawa ya kuwasaidia wengine watoke katika makosa yao bila ya kuwaumiza au
kuwadhalilisha na kuwaachia makovu. Badala ya kuponya tukakuza kidonda zaidi.
Katika vikao vyetu tuangalie njia njema ya kumsadia mtu na kumuonya badala ya
kumwanika hadharani mbele ya watu wote, kama kuna njia nzuri ya mtu mmoja
kumfuata kwa hekima utamsaidia zaidi, kuliko kumkosoa mtu mbele ya watu wengi
au katika kikao, hili haliponyi kwani mmoja hujisikia amedhalilishwa na utu
wake kudharauliwa. Mfano tusisubiri mpaka mtu afe ndio tupate muda wa kukaa
pamoja tuje kumrekebisha mtu mbele ya kikao cha ukoo, badala yake tutumie njia
mbadala ya kutuma mtu mwenye hekima amsaidie na kupatana kabla ya kukaa pamoja.
Kutangaza dhambi ya mtu mbele ya kikao, daima haina lengo la kuleta upatanisho
wa kweli badala yake humuachia mtu maumivu na kisasi moyoni. Hakuna hata mmoja
wetu angependa dhambi yake itajwe mbele ya watu. Ndio maana sakramenti ya
kitubio husaidia kweli. Tumuige Yesu aliyekuwa na huruma kwa wadhambi.
Sala:
Bwana, upo nasi katika jumuiya yetu, tukishikana pamoja kwa mapendo, huruma na
msamaha. Tunakuomba tuwe watu wakutafuta furaha, upendo na Amani. Tunakuomba
tuwe tayari kusamehe na kupatana na kila mtu. Yesu, ninakuamini wewe. Amina
------------------------
Copyright
©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.



