Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUWA MUWAJIBIKAJI!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Agosti 19, 2026, 
Juma la 20 la Mwaka 


Eze 34:1-11; 
Zab 22:1-6; 
Mt 20:1-16


KUWA MUWAJIBIKAJI!


Neno la Mungu linaongea nasi kuhusu kuwajibika, na kwanamna ya pekee, majukumu yaliowekwa juu yetu na Mungu. Katika somo la kwanza, Mungu anawakumbusha viongozi wa wana Waisraeli kuwa wao ni wawajibikaji wa matatizo na mateso ya watu. Walichaguliwa kuongoza watu, kuendana na amri zake. Lakini, wanawaongoza katika kuvunja uhusiano wao na Mungu kwakuharibu taratibu za kidini, nakuwachanganya kati yao ili waweze kujinufaisha binafsi kifedha na kisiasa. Na hili lime sababisha uharibifu na kupelekwa uhamishoni. Ezekiel anawaeleza kuhusu kushindwa kwao kuwa wachugaji wema wa watu.

Sisi wote pia, katika hali Fulani, tumewekwa kuwa wachungaji au wahudumu juu ya wengine. Kama Padre, Mtawa, Wazazi, Walimu, viongozi wa serikali, tunapaswa kutimiza majukumu yetu yakuwahudumia watu waliowekwa chini yetu au wanao tutegemea. Somo la kwanza linatueleza kwamba watu hawa hawapo chini yetu ili kuwahujumu au kuwaonea bali ni watu wa Mungu waliowekwa chini yetu na Mungu ili tuwahudumie. Hii inamaana kwamba sisi tupo na tutabaki kuwa wawajibikaji wa Mungu.

Somo la Injili ni juu ya mfano wa wafanyakazi wa shamba la mizabibu walio ajiriwa nakufanya kazi kwa masaa tofauti bali wanapewa mshahara sawa. Kitu kimoja cha kweli ambacho mfano huu unatufunulia ni kwamba, kwakuangalia majukumu yetu aliotupa Mungu, Mungu haangalii umefanya kazi muda mrefu kiasi ghani, bali anaangalia ni kwa jinsi ghani tumetenda kazi kwa uaminifu na kwa majitoleo. Hatimaye, hata kama tuna kazi ndefu na majukumu marefu katika maisha kama ya wazazi au kama ya mwalimu anayefundisha wanafunzi kwa kipindi kifupi, tunapaswa kuwa sawa katika kuitenda hiyo kazi kiaminifu na kwa majitoleo. Na majitoleo yetu ya kujitoa kwetu kutakuwa kwa hali ya juu na hapo tutaambiwa-“njooni kwangu mliobarikiwa na Baba yangu, muurithi ufalme mliotayarishiwa kabla ya kuumbwa misingi ya ulimwengu” (Mt 25:34).

Sala: Bwana, nakuomba unisaidie niweze kuwa mchungaji mwema wa kundi lililowekwa chini yangu, niweze kutimiza majukumu yaliowekwa chini yangu. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUMATANO, AGOSTI 19, 2026




MASOMO YA MISA 
JUMATANO, AGOSTI 19, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 34:1 – 11

Neno la Bwana likanijia, kusema, Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana Mungu asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo. Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala. Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama-mwitu, wakatawanyika. Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.

Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; kama mimi niishivyo, asema Bwana Mungu, kwa sababu kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu; kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana.

Bwana Mungu asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.

Maana, Bwana Mungu asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 23:1 – 6 (K) 1

(K) Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati aya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika. (K)

Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)


SHANGILIO
Zab. 119:34

Aleluya, aleluya,
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Aleluya.


INJILI
Mt. 20:1–16

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba, aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.

Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. Hata kama saa kumi na moja akatoka, akauta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.

Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia masimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.

Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unukia mwenye nyuma, wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa. Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari? Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe. Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUACHA YOTE NA KUMFUATA KRISTO!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Agosti 18, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 20 la Mwaka  Kanisa

Ez 28:1-10; 
Kumb 32:26-28, 30, 35-36; 
Mt 19:23- 30


KUACHA YOTE NA KUMFUATA KRISTO!


Kilele cha mwisho kabisa cha mwanadamu ni kujua, kupenda, kumtumikia Mungu na kufurahia maisha ya milele pamoja naye daima. Na Mungu anapenda kutushirikisha uzima huu wa milele. Ni zwadi kutoka kwa Mungu. Hatuwezi kupata uzima huu kwa nguvu za kibinadamu. Tungeachiwa sisi tu, ingekuwa vigumu sana kwetu sisi kuupata. Lakini kwa neema ya Mungu yote yanawezekana. Lakini, mali na utajiri vinaonekana viashiria vinavyo hatarisha kutokuupata ufalme huu wa milele. Katika ulimwengu huu wa sasa wenye mambo mengi inakuwa vigumu kwa wengine kukwepa hili. Ni jambo kubwa la kweli “kuacha yote” lakini kubwa zaidi “kumfuata Yesu”. 

Kumfuata Yesu ni kazi yetu.katika hili linabeba ukombozi wa mwanadamu, lakini hatuwezi kumfuata kristo kama hatutaacha yote yanayotufunga tushindwe kumfuata. Nabii Ezekiel katika somo la kwanza anatoa angalisho kwa mji wa Tiro na viongozi wake waliopata mafanikio makubwa na nguvu. Wamweka ulinzi wao na Imani yao katika utajiri na mali ambavyo vimegeuka kuwa miungu yao.

Lakini Petro anasema, “tumeacha yote” sio tuu vitu vya ulimwengu, lakini pia tamaa zinazopendwa na mioyo yetu. Wanaobaki wakiwa wameshikilia baadhi ya vitu, inakuwa hawajaacha yote. Kwa nini anatoa ujumbe mkali namna hiyo kwa matajiri? Kwanini Yesu anaongea sana kuhusu mali? Ni kwasababu mali inaweza kutufanya tusiwe huru au kutupa uhuru wa uongo. Wengine wameshindwa kumfuata Yesu kwasababu ina maana ya kuacha baadhi ya uhusiano, na wengine kama yule tajiri, ni kwasababu watapoteza nafasi yao ya heshima au njia zao za kupata mali. Wewe je? 
Sala: Bwana, naomba nikufanye wewe wa kwanza katika maisha yangu na nikuchague wewe kwa uhuru kamili hata kama kukufuata inagarimu.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 18, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 18, 2026
JUMANNE, JUMA LA 20 LA MWAKA

SOMO 1
Eze. 28:1 – 10

Neno la Bwana likanijia tena, kusema, Mwanadamu, mwambie mkuu wa Tiro, Bwana mungu asema hivi; Kwa kuwa moyo wako umeinuka, nawe umesema, Mimi ni mungu, nami nimeketi katika kiti cha Mungu, kati ya bahari; lakini u mwanadamu wala si Mungu, ujapokuwa umeweka moyo wako kama moyo wa Mungu. Tazama, una hekima kuliko Danieli; hapana neno la siri watu wawezalo kukuficha; kwa hekima yako na kwa fahamu zako umejipatia utajiri, nawe umepata dhahabu na fedha katika hazina zako; kwa hekima yako nyingi, na kwa biashara yako, umeongeza utajiri wako, moyo wako umeinuka kwa sababu ya utajiri wako.

Basi, kwa hiyo, Bwana Mungu asema hivi; Kwa kuwa umeweka moyo wako kama moyo wa Mungu; basi, tazama, nitaleta wageni juu yako, watu wa mataifa wenye kutisha; nao watafuta panga zao juu ya uzuri wa hekima yako, nao watautia uchafu mwangaza wako. Watakushusha hata shimoni; nawe utazidi kusema mbele yake huyo akuuaye, Mimi ni Mungu? Lakini u mwanadamu, wala si Mungu, mkononi mwake akutiaye jeraha. Utakufa kifo cha hao wasiotahiriwa, kwa mikono ya wageni; kwa maana mimi nimenena neno hili, asema Bwana Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Kum. 32:26 – 28, 30, 35 – 36 (K) 39

(K) Naua Mimi, nahuisha Mimi.

Nalisema, Ningewatawanyia mbali,
Ningekomesha kumbukumbu lao kati ya wanadamu;
Isipokuwa naliogopa makamio ya adui,
Adui zao wasije wakafikiri uongo. (K)

Wasije wakasema, Mkono wetu umetukuka,
Wala Bwana hakuyafanya haya yote.
Maana hawa ni taifa wasio shauri,
Wala fahamu hamna ndani yao. (K)

Mmoja angefukuzaje watu elfu,
Wawili wangekimbizaje elfu kumi,
Kama Mwamba wao asingaliwauza,
Kama Bwana asingaliwatoa? (K)

Mmoja angefukuzaje watu elfu,
Wawili wangekimbizaje elfu kumi,
Kama Mwamba wao asingaliwauza,
Kama Bwana asingaliwatoa? (K)

Maana siku ya msiba wao imekaribia,
Na mambo yatakayowapata yatafanya haraka.
Kwa kuwa Bwana atawaamua watu wake,
Atawahurumia watumwa wake. (K)


SHANGILIO
Zab. 25:4, 5

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.


INJILI
Mt. 19:23 – 30

Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka? Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.

Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi? Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli. Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele.

Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, Agosti 17, 2026
Juma la 20 la Mwaka


Ez 24: 15-24
Lumb 32:18-21;
Mt 19: 16-22


TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO 

Tunaishi katika ulimwengu ambao ni rahisi kuchukuliwa na mali au vitu na hivyo kupoteza muelekeo wetu na wa wengine. Sisi twaweza kuingia katika kujali mali kuwa ndio mwisho wa kila kitu. “kama unataka kuwa mkamilifu, uza vyote ulivyo navyo na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Alafu, njoo unifuate”. Wakati kijana huyu mdogo alivyo sikia hivyo alihuzunika sana kwani alikua na mali nyingi. 

Yesu anawaita baadhi ya watu katika hali ya kawaida wauze vyote walivyo navyo. Na wote wale wanao tambua wito huu na kujitoa katika kuacha kushikamana na mali, wanapata uhuru mkubwa. Wito wao ni alama ya ndani ya kila mmoja wetu, wito wa ndani ambao kila mmoja wetu amepewa. Lakini kwa wengine je, Bwana anawaitaje? Ni kwa kuwa maskini wa roho. Kwa kuwa “maskni wa roho” ni katika hali hiyo Bwana alikuwa anawaalika kuachilia yote ya malimwengu na kuacha kujifungamanisha nayo, kama hawa waliofanya katika hali ya vitendo. Tofati iliopo ni kwasababu wito wa mmoja ni wa ndani na wa njee, na wengine ni kwa ndani tu. Lakini inapaswa kuwa kamili. 

Umaskini wa roho ni kwamba tunatambua Baraka tunazozipata kwa kujinasua kwa kutokushikamana na mali za ulimwengu huu. Mali sio mbaya. Lakini ni rahisi kushikwa na vitu vya ulimwengu. Mara nyingi tunakuwa na vishawishi na kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa na mali nyingi ndivyo tunavyokuwa na raha zaidi. Lakini sio kweli, “aliye na vingi hatosheki”. 

Tafakari leo juu ya wito ulioitiwa wa kuishi huku Ulimwenguni bila kujifunganisha na mali. Mali na vitu vingine ni ishara tu ya njee ya kukusaidia kupata uzima wa milele katika malengo ya maisha. Na hili litakuwa na maana kwamba utapata unayo hitaji na kukwepa kuwa na vingi, na hasa kukwepa kujishika na malimwengu kutoka ndani. 

Sala: Bwana, ninatamani kuacha yote yanayo nifunga. Ninajitoa kwako kama sadaka ya kiroho. Pokea yote niliyonayo na nisaidie mimi niweze ku tumia katika hali ambayo wewe mwenyewe unatamani. Katika kuachilia huko niweze kuvumbua utajiri wa kweli ulioniwekea mimi. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 17, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 17, 2026
JUMATATU, JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 24:15 – 24

Neno la Bwana linanijia tena, kusema, Mwanadamu, tazama, ninakuondolea kwa pigo moja tunu, mteule wa macho yako; walakini hutaomboleza wala kulia, wala yasichuruzike machozi yako. Ugua, lakini si kwa sauti ya kusikiwa; usifanye matanga kwa ajili yake yeye aliyekufa; jipige kilemba chako, ukavae viatu vyako, wala usiifunike midomo yako, wala usile chakula cha watu.

Basi nalisema na watu asubuhi; na jioni mke wangu akafa; nami nalifanya asubuhi kama nilivyoagizwa. Watu hao wakaniambia, Je! Hutaki kutuambia maana ya mambo haya kwetu, hata umefanya kama vile ufanyavyo.

Nikawaambia, Neno la Bwana, lilinijia, kusema, Uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana Mungu asema hivi, Angalieni, nitapatia unajisi patakatifu pangu, fahari ya uwezo wenu, mahali pa kutamaniwa na macho yenu, ambapo roho zenu zinapahurumia; na wana wenu nab inti zenu, mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga. Nanyi mtafanya kama mimi nilivyofanya; hamtaifunika midomo yenu, wala kula chakula cha watu. Na vilemba vyenu vitakuwa juu ya vichwa vyenu, na viatu vyenu miguuni mwenu; hamtaomboleza wala kulia; lakini mtafifia katika maovu yenu, na kuugua kila mtu pamoja na mwenziwe. Basi ndivyo Ezekieli atakavyokuwa isahra kwenu; ninyi mtatenda sawasawa na yote aliyoyatenda yeye; litakapokuja jambo hili, ndipo mtakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Kum. 32:18 – 21 (K) 18

(K) Umemsahau Mungu aliyekuzaa.

Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa, 
Mungu aliyekuzaa umemsahau.
Bwana akaona, akawachukia,
Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe nab inti zake. (K)

Akasema, Nitawaficha uso wangu, 
Nitaona mwisho wao utakuwaje;
Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi,
Watoto wasio Imani ndani yao. (K)

Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu;
Wamenikasirisha kwa ubatili wao;
Nami nitawatia wivu kwa wasio watu,
Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo. (K)


SHANGILIO
1Sam. 3:9, Yn. 6:68

Aleluya, aleluya,
Nena, Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikia: Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Aleluya.


INJILI
Mt. 19:16 - 22

Mtu mmoja alimwendea Yesu akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hivi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KWA IMANI, SISI WOTE WATOTO WA MUNGU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Agosti 16, 2026
Juma la 20 la Mwaka
___________________

Is 56:1, 6-7; 
Zab 66:2-3, 5-6, 8;
Rom 11: 13-15, 29-32;
Mt 15:21-28
___________________

KWA IMANI, SISI WOTE WATOTO WA MUNGU


Masomo ya leo yanaonesha hali ya ajabu ya jinsi Mungu anavyotoa wokovu wake kwa watu wote. Yesu alikuja kuwapa watu wote mapendo na wote wanaitwa kuwa wafuasi wake. Kama Wakatoliki sisi tumejikita katika ukristo ambao unatolewa kwa wote, na unapatika kwa wote wale wanaopenda. Neno “Katoliki” ni neno walilopewa wakristo wa kwanza baada ya kutambulika kwamba wanakaribisha watu wote bila ubaguzi. Mt. Inyasi wa Antokia alisema “Sehemu yeyote alipo Kristo, kuna Kanisa Katoliki”.

Hofu ya kupoteza Taifa lao na utambulisho wa dini yao umeifanya Israeli kujitenga na watu wengine na kuwa na sheria kali kuhusu watu wa njee. Kitabu cha Kumbukumbu la Torati kinasema “usifanya agano na wao wala usiwe na huruma na wao…msioane nao, wala kuwapa mtoto wako aolewe nao wala kijana wako kuchukua mke huko kwasababu watafanya watoto wenu waabudu miungu mingine”(Kumb 7:2-4). Kinyume na hilo, somo la kwanza kutoka katika kitabu cha Nabii Isaya, “katika nyumba ya Mungu hakuna aliye mgeni”. Wimbo wa katikati unabeba maada hiyo hiyo kwakusema kwamba “Mkono wa Mungu wa kuokoa utaonekana na ‘mataifa yote’ ”. Paulo pia aliezea pia hili alipo Sali “mataifa yote watakuja kuuona utukufu wa Mungu uliofunuliwa na sura ya Yesu (1Kor 4:6). Katika somo la pili Paulo, ana wahakikishia wasomaji wake kwamba ‘Mungu anataka kuwaonesha watu wote huruma yake’(Rom 11:32).

Wakristo wa kwanza walikutana na hali ya utengano kuhusu Wayahuni na Wayunani. Na ilisemwa kuwa Injili ilikuwa ihubiriwe kwa wa Israeli tu. Ili kuongezea chumvi usemi wao wali rejea utume wa Yesu (Mt 10:5-6). Kwasababu ya muda mfupi Yesu alikita utume wake kwa “kondoo waliopotea wa nyumba Israeli.”

Katika somo la Injili Yesu anafuatwa na mwanamke Myunani, aliyeomba msaada kwa Yesu kwasababu ya mtoto wake aliyekuwa amepagawa na pepo mbaya. Jinsi, Yesu alivyo kabiliana na mwanamke huyu inaleta maana, kwamba Wayunani hawatatengwa na waisraeli. Mwanamke huyu amekuwa mfano wa Imani kuu. Kwasababu ya Imani yake Mama huyu ameweza kushinda jaribu la Yesu. Alishinda kwa kuwa na Imani kubwa. Alitambua kuwa hana sehemu nyingine zaidi ya Yesu. Na hivyo alijikita kwa mmoja tu amabaye angeweza kumsaidia. Hili lilikuwa ni tendo lake la Imani.
Ingaweje Yesu alijibu ombi lake katika hali ambayo ni ya kushangaza kidogo “Mimi nilitumwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”. Aliongea naye katika lugha ambayo Mwanamke yule aliweza kuelewa wengine hawakuweza kuielewa. Yesu anatumia picha ya “kundi la kondoo” ambapo neno hili lilitumika mara nyingi katika Agano la Kale. “Ni mimi mwenyewe nitawachunga kondoo wangu….nitawachunga kondoo wangu kwa haki” (Ez 34:11-16). Yesu kwakusema yeye ni Mchungaji wa Israeli, Yeye anakamilisha unabii huo na mwanamke huyu anaelewa. Anatambua kuwa yeye si mmoja wao kati ya wale waliochaguliwa. Lakini anajinyenyekesha magotini kwa Yesu, akiomba “Bwana, nisaidie” .

Yesu anajibu katika hali ya lugha ya ukali ya Wayahudi “sio vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwapa mbwa”. Waisraeli walikuwa ni kondoo. Kumuita mtu “mbwa” ni hali ya ukatili na dharau ambayo waisraeli waliwapa wapagani (Mt 7:6, Rev 22:15, FIl 3:2). Kutoka katika midomo ya Yesu, maneno haya yanashangaza, na hasa ikitegemea mwanamke huyu alimwendea Yesu kwa heshima kubwa. Mara tatu akimwita “Bwana”. 

Ufunguo wa kuelewa mazungumzo haya nikutazama matokeo ya mwisho. Yesu alimpa mwanamke huyu muda wakuonesha Imani yake kwa watu wote. Maneno yake yalimfanya yeye angare kwa wote. Mwanamke huyu alionesha Imani yake ndio maana hata sasa tunashuhudia Imani yake na unyenyekevu wake. Mwanake huyu hakuona shida kuitwa “mbwa”. Hakujisikia kwamba yeye asiye thaminika. Alidhihirisha kuwa “mbwa” mwaminifu anaye mpenda na kumtiii Bwana wake. Kwa kuonesha Imani hii, ilimfanya Yesu atende muujiza ule ambao alitaka kumtendea. Mwanamke huyu Mkananayo anachukuliwa kama kioo kizuri cha Imani. Alitambua kwamba yeye hastahili kitu, kuamini tu katika neno la Yesu aliingia katika wokovu. Alishikilia hilo na kuliweka kama zawadi.

Je, sisi ni watoto waaminifu wa Baba yetu wa mbinguni? Je, tupo tayari kusema kama yule mwanamke kwenye Injili,? Je sisi ni watii kama mbwa mbele ya bwana wao? Mara nyingi sisi tupo katikati na pia tunapenda kujitenga. Tujifunze kutoka katika hali hii ya Yesu kukutana na mwanamke huyu, na hivyo tuweze kuwa watoto wa Mungu. Kwani Mt. Paulo anasema wazi kwamba “Katika Kristo, sisi wote ni watoto wa Mungu kwa njia ya Imani…au sisi wote ni wamoja katika Kristo” (Gal 3:26-29).

Sala: Bwana, ninatambua kwamba mimi sistahili huruma yako kila siku katika maisha yangu. Lakini pia ninakiri kwamba wewe una huruma ambayo ni zaidi hata ya ile ninayo tamani uweke ndani mwangu, mimi maskini na mdhambi mkubwa. Ninakuomba huruma hiyo Bwana wangu, ninaweka Imani yangu yote kwako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 16, 2026



MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 16, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA 

________

SOMO I
Isa. 56:1, 6-7

Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatenda haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 67:1-2, 4-5, 7 (K) 5

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu, 
Watu wote na wakushukuru.

Mungu na atufadhili na kutubariki,
na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

mataifa na washangilia,
naam, waimbe kwa furaha.
Maana kwa haki utawahukumu watu,
na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

watu na wakushukuru, Ee Mungu,
watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)
________

SOMO 2
Rum. 11:13-15, 29-32

Nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa. Basi, naitukuza huduma iliyo yangu? Huenda nikapata kuwapatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao. Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa. Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake. Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao; kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema. Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

SHANGILIO
Mdo. 16:14

Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, Ee Bwana, 
Ili tuyatuze maneno ya Mwanao.
Aleluya
________

INJILI 
Mt. 15:21-28

Yesu aliondoka huko, akaenda kando pande za tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana unisaidie. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MALENGO YA JITIHADA ZETU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 15 2026
Juma la 19 la Mwaka

SIKUKUU YA KUPALIZWA BIKIRA MARIA MBINGUNI

Ufu 11:19, 12:1-6, 10;
Zab 45:9-11, 15 (K) 10;
1Kor 15:20-26;
Lk 1:39-56


MALENGO YA JITIHADA ZETU!


Katika sikukuu ya Kupalizwa Mbinguni kwa Mama wa Mungu, tunafanya sherehe ya Bikira Maria kutoka katika hali ya ubinadamu mpaka kufika hali ya mwenye heri. Kwa kumtafakari Bikira Maria katika utukufu wake, tunaelewa kuwa hapa duniani sio kwetu bali tu wapitaji, pia tunaelewa kuwa tunatakiwa kuishi hapa duniani tukiwa tumejawa na tamaa ya vitu vya mbinguni basi kwa kufanya hivyo tutarithi vivyo vitu katika ufalme wa milele. Kwa kusema hivyo basi tujitahidi kutunza amani na utulivu wa mioyo yetu, japokuwa tumesongwa na magumu ya maisha. Mwangaza wa Bikira Maria akiwa amechukuliwa mbinguni huendelea kuonekana japokuwa wingi zito la huzuni na mateso limetanda.

Katika sikukuuu ya Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria tunakumbuka kushiriki kwa Bikira Maria katika Ufufuko wa mwanae, kwa kupalizwa mbinguni mwili na roho, alipomaliza kile alichokijia hapa duniani. Kupalizwa Mbinguni kunatuonyesha kile kitakachotutokea pale tutakapofufuliwa siku ya mwisho. Kupalizwa mbinguni ndio lengo kuu la maisha yetu kama Wakristo.

Kama vile Mt. Paulo atuambiapo kuwa, tutafufuliwa na miili yetu iliyo tukuka kama ilivyokuwa kwa Kristo. Kwa ile nguvu ya Yesu mfufuka tutaweza kuungana na Baba katika utukufu wa Kristo, kama vile Bikira Maria anavyoshiriki katika muungano huo kwa sasa. Kupalizwa Mbinguni ni siku ambayo tunaitwa kutafakari kwa kina malengo ya maisha yetu, na urithi wa uzima wa milele.

Kwa kusema hivyo basi tujitahidi kuyawaza hayo kila siku. Inatulazimu kufikiria kuwa tumesimama na Bikira Maria na mwezi nchini ya miguu yake, akiwa wamevaa taji la jua na nyota kichwani mwake. Pia inatubidi kumwona yule joka limefungwa, na kila mmoja wetu kwa neema aliyopewa na Mungu na kwa msaada wa Bikira maria anatakiwa kumzaa Kristo katika maisha yake. kwa kufanya hivyo basi tutakuwa na uhakika wa kufufuliwa mwili na roho.kwa kufanya hivyo basi tunakuwa tumepata maana halisi ya maisha yetu, na kwamba ukweli unaoelezewa katika mafundisho ya kanisa juu ya kupalizwa Bikira Maria ndio utimilifu wa matamanio ya maisha yetu.

Sala: Ewe mama uliyejaa msamaha, utukufu wako unisaidie kuyabeza na kuyachukia yale yaliyo ya dunia na kutamani yale yaliyo ya mbinguni. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 15, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 15, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 19 LA MWAKA 

SHEREHE YA KUPALIZWA MBINGUNI BIKIRA MARIA


SOMO 1 
Ufu 11: 19, 12: 1-6, 10

Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake. Kukawa na umeme, na sauti, na radi, na tetemeko la nchi, na mnua ya mawe nyingi sana.

Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili. Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba. Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za muinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake. Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi. Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini.

Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 45: 9-11, 15 (K) 10 

(K) Mkono wako wa kuume amesimama malkia
       amevaa dhahabu ya Ofiri.

Binti za wafalme wamo
Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki.
Mkono wako wa kuume amesimama malkia, 
Amevaa dhahabu ya Ofiri.
Sikia, binti, utazame, utege sikio lako,
Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. (K)

Naye mfalme atautamani uzuri wako,
Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. 
Watapelekwa kwa furaha na shangwe,
Na kuingia katika nvumba va mfalme. (K)


SOMO 2  
1Kor 15: 20-26

Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watanuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja. Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Maria amepalizwa mbinguni majeshi yote ya malaika wanafurahi.
Aleluya.


INJILI 
Lk 1: 39-56

Mariamu aliondoka, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeth Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu; akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi? Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu. Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
Mariamu akasema,
Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Na roho yangu imemfurahia Mungu,
Mwokozi wangu;
Kwa kuwa ameutazama
Unyonge wa mjakazi wake.
Kwa maana, tazama, tokea sasa
Vizazi vyote wataniita mbarikiwa;
Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, 
Na jina lake ni takatifu.
Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi 
Kwa hao wanaomcha.
Amefanya nguvu kwa mkono wake;
Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; 
Na wanyonge amewakweza.
Wenye njaa amewashibisha mema
Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu. 
Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;
Ili kukumbuka rehema zake;
Kama alivyowaambia baba zetu,
Ibrahimu na uzao wake hata milele.
Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com