Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
‘MJINGA’ KWA AJILI YA KRISTO?
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, AGOSTI 28, 2026
KUWA TAYARI!
Juma la 21 la Mwaka
1Kor 1:1-9;
Zab 144:2-7;
Mt 24:42-51
KUWA TAYARI !
Injili ya leo inatangaza kuja sio kwa tufani bali ukombozi. Inatangaza kuja kwa Ufalme wa Mungu. Na hapo hapo tunaambiwa kwamba hatujui siku wala saa itakapokuja na kuja kwake kutakuwa kama ujio wa mwizi. Njia na silaha kubwa ya mwizi ni kuja kwakustukiza. Kuja kwa Ufalme wa Mungu hakutakuwa na kengele za tahadhari. Kuna silaha moja tuu ambayo tunaweza kuiandaa kwaujio wa ufalme wa Mungu nayo ni – kuandaa maisha yetu. Mungu ametupa sisi wanadamu uhuru wakuchagua. Kila mtu anauwezo wakuchagua jema na kutenda mema nakuishi vizuri na hapo ufalme wa Mungu ujapo atakuwa amejiandaa au mtu anauwezo wakuchagua kutenda dhambi na Mungu haingilii uhuru wake, lakini Mungu ameweka wazi njia yake kwamba kuchagua uovu sio kadiri ya sheria yake. Tuombee neema ya Mungu ili tuweze kutumia uhuru wetu vizuri tuchague kutenda mema kila wakati na tuwasaidie wengine waweze kuchagua kutenda mema ili ufalme wa Mungu ujapo kwa mara ya pili utukute tumejiandaa kila wakati.
Tuna mengi sana ya kutufundisha sisi, kila mara tunawaona vijana wadogo wanapoteza maisha wakiwa na umri mdogo kabisa, pengine kwa ajali au kwa magonjwa, tunajiuliza hivi walijua kwamba Mungu angewachukua wakiwa wadogo namna hii? Tunajiuliza hivi walikuwa wamejiandaa? Sio kazi yetu kuhukumu nakujua kuhusu wema wao lakini tunachojifuza ni kwamba siku ya mwisho ya mwanadamu hapa duniani ni Mungu mwenyewe anayepanga, lililo bora tena sana ni kuwa tayari kwa ujio wa Mungu muda wowote ule. Tukiishi kwa matumaini yetu yakiwa ndani ya Kristo, siku hiyo itakuwa ya furaha kwetu na hatutaishi kwa woga. Hofu inakuja kwasababu ya dhambi, lakini tukijipatanisha na Kristo kila mara matumaini yetu kwake ni makubwa na furaha yetu ya kuungana naye itakuwa kubwa zaidi.
Tuwasaidie ndugu zetu wote wamrudie Kristo, tukitambua kuwa hata jani la mwisho kabisa kwenye mti ni sehemu ya mti. Mkristo au ndugu unayemuona mdhambi sana bado ni sehemu ya mwili wa Kristo. Tuwasaidie ndugu zetu kwa kuwatia moyo ili wawe karibu zaidi na Kristo ili siku yake itakapokuja tuweze kupokea neema na kumlaki Kristo. Ni furaha yetu wote kwa pamoja kuuona uso wa Mungu.
Sala: Bwana, kwakupokea sakramenti kila wakati, kwanjia ya sala zangu na ndugu zangu, kwa kutembea katika mwanga wa neno lako, naomba niwe tayari daima kukupokea wewe. Amina.
MASOMO YA MISA ALHAMISI, AGOSTI 27, 2026
ALHAMISI, AGOSTI 25, 2022
1 Kor. 1:1 – 9
Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu, kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu. Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo yesu; kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika maneno yote, na maarifa yote; kama ushuhuda wa Kristo ulivyothibitika kwenu; hata hamkupungukiwa na karama yoyote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo; ambaye atawathibitisha hata mwisho, ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo. Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingine katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145:2 – 7 K (1)
(K) Ee Bwana, nitalihimidi jina lako milele na milele.
Kila siku nitakuhimidi,
Nitalisifu jina lako milele na milele.
Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana,
Wala ukuu wake hautambulikani. (K)
Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako,
Kitayatangaza matendo yako makuu.
Nitakufikiri fahari ya utukufu wa adhama yako,
Na matendo yako yote ajabu (K)
Watu watayajua matendo yako ya kutisha,
Nami nitausimulia ukuu wako.
Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu.
Wataiimba haki yako. (K)
SHANGILIO
Yn. 14:23
Aleluya, aleluya,
Mtu akinipenda, atalishika neno langu,
na Baba yangu atampenda,
na sisi tutakuja kwake.
Aleluya.
INJILI
Mt. 24:42 – 51
Yesu aliwambia wanafunzi wake: Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu. Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote. Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia; akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi; bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
KUONDOA UFARISAYO NDANI MWETU!
Jumatano, Agosti 26, 2026
Juma la 21 la Mwaka
___________________
2 The 3: 6-10, 16-18
___________________
KUONDOA UFARISAYO NDANI MWETU!
Katika somo la Injili leo Yesu analalamika na kusema ole juu ya Mafarisayo na Waandishi kwasababu ya hali yao ya unafiki. Walikuwa wamewabebesha watu mizigo ya sheria na mambo ya njee. Waliwatesa na kuwadhulumu manabii waliokuwa wajumbe wa Mungu na kukataa kusikiliza sauti ya Mungu waliokuwa nayo ndani yao juu yao na watu wote. Wamefana na makaburi yaliopakwa chokaa, yanayo onekana mazuri kwa njee lakini ndani yamejaa mifupa na uozo. Mafarisayo na waandishi walionekana wenye haki mbele za watu lakini hawakuweza kukukutana na mwenye haki Mwenyewe-Yesu.
Kitu kimoja muhimu ni kwamba Yesu ni mwaminifu mno. Wewe je? Upo tayari kufanya kila kitu kwa uaminifu wote? Je, upo tayari kuwa mwaminifu mbele ya Mungu na juu ya roho yako mwenyewe? Tatizo ni kwamba hatuoni hivyo. Daima tunajipitisha mbele ya watu tukijifanya kwamba ni wema na kukwepa ukweli wa mifupa na kila aina ya uchafu uliyo ndani mwetu. Hili sio jambo zuri na Yesu analipinga hili katika Injili.
Leo Injili inakualika utazame ndani ya moyo wako katika hali ya kweli, na ujiulize unaona nini? Natumaini utaona wema na fadhili na kuzifurahia. Lakini pia katika hali ya kweli utaziona dhambi. Pengine sio katika hali kama ya Mafarisayo, lakini kwa hakika utaona hali ya dhambi ambazo zinapaswa kusafishwa. Tafakari leo, ni jinsi ghani waweza kuzitazama dhambi zako katika hali ya kweli na jinsi ya kuziacha.
Sala: Bwana, nisaidie mimi niweze kuchukua hatua ya kujitazama mimi mwenyewe maisha yangu. Nisaidie nisione tuu fadhila nzuri ulizoweka ndani yangu, lakini pia nisaidie niweze kuona uovu au dhambi zilizo ndani ya moyo wangu. Ninakuomba unisafishe kutoka katika dhambi hiyo ili niweze kukupenda wewe zaidi. Yesu, nakuamini wewe. Amina
MASOMO YA MISA, JUMATANO, AGOSTI 26, 2026
JUMA LA 21 LA MWAKA
SOMO I
2 The 3: 6-10, 16-18
Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo,
jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata
mapokeo mliyoyapokea kwetu.
Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu
hatukuenda bila utaratibu kwenu; wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure;
bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu
wa kwenu awaye yote. Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi tufanye nafsi zetu
kuwa kielelezo kwenu, mtufuate.
Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza
neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.
Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa
njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.
Salamu zangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii
ndiyo alama katika kila waraka, ndio mwandiko wangu. Neema ya Bwana wetu Yesu
Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.
WIMBO WA KATIKATI
Zab 128: 1-2, 4-5 (K) 1
(K) Heri kila mtu amchaye Bwana.
Taabu ya mikono yake hakika utaila;
Utakuwa heri, na kwako kwema.
Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,
Vyumbani mwa nyumba yako. (K)
Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana.
Bwana akubariki toka Sayuni,
Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako. (K)
________SHANGILIO
nami nawajua, nao wanifuata.
INJILI
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
UHURU KWAKUACHANA NA UNAFIKI!
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, AGOSTI 25, 2026
NJOO NA UONE: KUKUTANA NA YESU!
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com






