Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, Agosti 17, 2026
Juma la 20 la Mwaka


Ez 24: 15-24
Lumb 32:18-21;
Mt 19: 16-22


TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO 

Tunaishi katika ulimwengu ambao ni rahisi kuchukuliwa na mali au vitu na hivyo kupoteza muelekeo wetu na wa wengine. Sisi twaweza kuingia katika kujali mali kuwa ndio mwisho wa kila kitu. “kama unataka kuwa mkamilifu, uza vyote ulivyo navyo na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Alafu, njoo unifuate”. Wakati kijana huyu mdogo alivyo sikia hivyo alihuzunika sana kwani alikua na mali nyingi. 

Yesu anawaita baadhi ya watu katika hali ya kawaida wauze vyote walivyo navyo. Na wote wale wanao tambua wito huu na kujitoa katika kuacha kushikamana na mali, wanapata uhuru mkubwa. Wito wao ni alama ya ndani ya kila mmoja wetu, wito wa ndani ambao kila mmoja wetu amepewa. Lakini kwa wengine je, Bwana anawaitaje? Ni kwa kuwa maskini wa roho. Kwa kuwa “maskni wa roho” ni katika hali hiyo Bwana alikuwa anawaalika kuachilia yote ya malimwengu na kuacha kujifungamanisha nayo, kama hawa waliofanya katika hali ya vitendo. Tofati iliopo ni kwasababu wito wa mmoja ni wa ndani na wa njee, na wengine ni kwa ndani tu. Lakini inapaswa kuwa kamili. 

Umaskini wa roho ni kwamba tunatambua Baraka tunazozipata kwa kujinasua kwa kutokushikamana na mali za ulimwengu huu. Mali sio mbaya. Lakini ni rahisi kushikwa na vitu vya ulimwengu. Mara nyingi tunakuwa na vishawishi na kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa na mali nyingi ndivyo tunavyokuwa na raha zaidi. Lakini sio kweli, “aliye na vingi hatosheki”. 

Tafakari leo juu ya wito ulioitiwa wa kuishi huku Ulimwenguni bila kujifunganisha na mali. Mali na vitu vingine ni ishara tu ya njee ya kukusaidia kupata uzima wa milele katika malengo ya maisha. Na hili litakuwa na maana kwamba utapata unayo hitaji na kukwepa kuwa na vingi, na hasa kukwepa kujishika na malimwengu kutoka ndani. 

Sala: Bwana, ninatamani kuacha yote yanayo nifunga. Ninajitoa kwako kama sadaka ya kiroho. Pokea yote niliyonayo na nisaidie mimi niweze ku tumia katika hali ambayo wewe mwenyewe unatamani. Katika kuachilia huko niweze kuvumbua utajiri wa kweli ulioniwekea mimi. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 17, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 17, 2026
JUMATATU, JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 24:15 – 24

Neno la Bwana linanijia tena, kusema, Mwanadamu, tazama, ninakuondolea kwa pigo moja tunu, mteule wa macho yako; walakini hutaomboleza wala kulia, wala yasichuruzike machozi yako. Ugua, lakini si kwa sauti ya kusikiwa; usifanye matanga kwa ajili yake yeye aliyekufa; jipige kilemba chako, ukavae viatu vyako, wala usiifunike midomo yako, wala usile chakula cha watu.

Basi nalisema na watu asubuhi; na jioni mke wangu akafa; nami nalifanya asubuhi kama nilivyoagizwa. Watu hao wakaniambia, Je! Hutaki kutuambia maana ya mambo haya kwetu, hata umefanya kama vile ufanyavyo.

Nikawaambia, Neno la Bwana, lilinijia, kusema, Uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana Mungu asema hivi, Angalieni, nitapatia unajisi patakatifu pangu, fahari ya uwezo wenu, mahali pa kutamaniwa na macho yenu, ambapo roho zenu zinapahurumia; na wana wenu nab inti zenu, mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga. Nanyi mtafanya kama mimi nilivyofanya; hamtaifunika midomo yenu, wala kula chakula cha watu. Na vilemba vyenu vitakuwa juu ya vichwa vyenu, na viatu vyenu miguuni mwenu; hamtaomboleza wala kulia; lakini mtafifia katika maovu yenu, na kuugua kila mtu pamoja na mwenziwe. Basi ndivyo Ezekieli atakavyokuwa isahra kwenu; ninyi mtatenda sawasawa na yote aliyoyatenda yeye; litakapokuja jambo hili, ndipo mtakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Kum. 32:18 – 21 (K) 18

(K) Umemsahau Mungu aliyekuzaa.

Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa, 
Mungu aliyekuzaa umemsahau.
Bwana akaona, akawachukia,
Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe nab inti zake. (K)

Akasema, Nitawaficha uso wangu, 
Nitaona mwisho wao utakuwaje;
Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi,
Watoto wasio Imani ndani yao. (K)

Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu;
Wamenikasirisha kwa ubatili wao;
Nami nitawatia wivu kwa wasio watu,
Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo. (K)


SHANGILIO
1Sam. 3:9, Yn. 6:68

Aleluya, aleluya,
Nena, Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikia: Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Aleluya.


INJILI
Mt. 19:16 - 22

Mtu mmoja alimwendea Yesu akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hivi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KWA IMANI, SISI WOTE WATOTO WA MUNGU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Agosti 16, 2026
Juma la 20 la Mwaka
___________________

Is 56:1, 6-7; 
Zab 66:2-3, 5-6, 8;
Rom 11: 13-15, 29-32;
Mt 15:21-28
___________________

KWA IMANI, SISI WOTE WATOTO WA MUNGU


Masomo ya leo yanaonesha hali ya ajabu ya jinsi Mungu anavyotoa wokovu wake kwa watu wote. Yesu alikuja kuwapa watu wote mapendo na wote wanaitwa kuwa wafuasi wake. Kama Wakatoliki sisi tumejikita katika ukristo ambao unatolewa kwa wote, na unapatika kwa wote wale wanaopenda. Neno “Katoliki” ni neno walilopewa wakristo wa kwanza baada ya kutambulika kwamba wanakaribisha watu wote bila ubaguzi. Mt. Inyasi wa Antokia alisema “Sehemu yeyote alipo Kristo, kuna Kanisa Katoliki”.

Hofu ya kupoteza Taifa lao na utambulisho wa dini yao umeifanya Israeli kujitenga na watu wengine na kuwa na sheria kali kuhusu watu wa njee. Kitabu cha Kumbukumbu la Torati kinasema “usifanya agano na wao wala usiwe na huruma na wao…msioane nao, wala kuwapa mtoto wako aolewe nao wala kijana wako kuchukua mke huko kwasababu watafanya watoto wenu waabudu miungu mingine”(Kumb 7:2-4). Kinyume na hilo, somo la kwanza kutoka katika kitabu cha Nabii Isaya, “katika nyumba ya Mungu hakuna aliye mgeni”. Wimbo wa katikati unabeba maada hiyo hiyo kwakusema kwamba “Mkono wa Mungu wa kuokoa utaonekana na ‘mataifa yote’ ”. Paulo pia aliezea pia hili alipo Sali “mataifa yote watakuja kuuona utukufu wa Mungu uliofunuliwa na sura ya Yesu (1Kor 4:6). Katika somo la pili Paulo, ana wahakikishia wasomaji wake kwamba ‘Mungu anataka kuwaonesha watu wote huruma yake’(Rom 11:32).

Wakristo wa kwanza walikutana na hali ya utengano kuhusu Wayahuni na Wayunani. Na ilisemwa kuwa Injili ilikuwa ihubiriwe kwa wa Israeli tu. Ili kuongezea chumvi usemi wao wali rejea utume wa Yesu (Mt 10:5-6). Kwasababu ya muda mfupi Yesu alikita utume wake kwa “kondoo waliopotea wa nyumba Israeli.”

Katika somo la Injili Yesu anafuatwa na mwanamke Myunani, aliyeomba msaada kwa Yesu kwasababu ya mtoto wake aliyekuwa amepagawa na pepo mbaya. Jinsi, Yesu alivyo kabiliana na mwanamke huyu inaleta maana, kwamba Wayunani hawatatengwa na waisraeli. Mwanamke huyu amekuwa mfano wa Imani kuu. Kwasababu ya Imani yake Mama huyu ameweza kushinda jaribu la Yesu. Alishinda kwa kuwa na Imani kubwa. Alitambua kuwa hana sehemu nyingine zaidi ya Yesu. Na hivyo alijikita kwa mmoja tu amabaye angeweza kumsaidia. Hili lilikuwa ni tendo lake la Imani.
Ingaweje Yesu alijibu ombi lake katika hali ambayo ni ya kushangaza kidogo “Mimi nilitumwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”. Aliongea naye katika lugha ambayo Mwanamke yule aliweza kuelewa wengine hawakuweza kuielewa. Yesu anatumia picha ya “kundi la kondoo” ambapo neno hili lilitumika mara nyingi katika Agano la Kale. “Ni mimi mwenyewe nitawachunga kondoo wangu….nitawachunga kondoo wangu kwa haki” (Ez 34:11-16). Yesu kwakusema yeye ni Mchungaji wa Israeli, Yeye anakamilisha unabii huo na mwanamke huyu anaelewa. Anatambua kuwa yeye si mmoja wao kati ya wale waliochaguliwa. Lakini anajinyenyekesha magotini kwa Yesu, akiomba “Bwana, nisaidie” .

Yesu anajibu katika hali ya lugha ya ukali ya Wayahudi “sio vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwapa mbwa”. Waisraeli walikuwa ni kondoo. Kumuita mtu “mbwa” ni hali ya ukatili na dharau ambayo waisraeli waliwapa wapagani (Mt 7:6, Rev 22:15, FIl 3:2). Kutoka katika midomo ya Yesu, maneno haya yanashangaza, na hasa ikitegemea mwanamke huyu alimwendea Yesu kwa heshima kubwa. Mara tatu akimwita “Bwana”. 

Ufunguo wa kuelewa mazungumzo haya nikutazama matokeo ya mwisho. Yesu alimpa mwanamke huyu muda wakuonesha Imani yake kwa watu wote. Maneno yake yalimfanya yeye angare kwa wote. Mwanamke huyu alionesha Imani yake ndio maana hata sasa tunashuhudia Imani yake na unyenyekevu wake. Mwanake huyu hakuona shida kuitwa “mbwa”. Hakujisikia kwamba yeye asiye thaminika. Alidhihirisha kuwa “mbwa” mwaminifu anaye mpenda na kumtiii Bwana wake. Kwa kuonesha Imani hii, ilimfanya Yesu atende muujiza ule ambao alitaka kumtendea. Mwanamke huyu Mkananayo anachukuliwa kama kioo kizuri cha Imani. Alitambua kwamba yeye hastahili kitu, kuamini tu katika neno la Yesu aliingia katika wokovu. Alishikilia hilo na kuliweka kama zawadi.

Je, sisi ni watoto waaminifu wa Baba yetu wa mbinguni? Je, tupo tayari kusema kama yule mwanamke kwenye Injili,? Je sisi ni watii kama mbwa mbele ya bwana wao? Mara nyingi sisi tupo katikati na pia tunapenda kujitenga. Tujifunze kutoka katika hali hii ya Yesu kukutana na mwanamke huyu, na hivyo tuweze kuwa watoto wa Mungu. Kwani Mt. Paulo anasema wazi kwamba “Katika Kristo, sisi wote ni watoto wa Mungu kwa njia ya Imani…au sisi wote ni wamoja katika Kristo” (Gal 3:26-29).

Sala: Bwana, ninatambua kwamba mimi sistahili huruma yako kila siku katika maisha yangu. Lakini pia ninakiri kwamba wewe una huruma ambayo ni zaidi hata ya ile ninayo tamani uweke ndani mwangu, mimi maskini na mdhambi mkubwa. Ninakuomba huruma hiyo Bwana wangu, ninaweka Imani yangu yote kwako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 16, 2026



MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 16, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA 

________

SOMO I
Isa. 56:1, 6-7

Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatenda haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 67:1-2, 4-5, 7 (K) 5

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu, 
Watu wote na wakushukuru.

Mungu na atufadhili na kutubariki,
na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

mataifa na washangilia,
naam, waimbe kwa furaha.
Maana kwa haki utawahukumu watu,
na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

watu na wakushukuru, Ee Mungu,
watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)
________

SOMO 2
Rum. 11:13-15, 29-32

Nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa. Basi, naitukuza huduma iliyo yangu? Huenda nikapata kuwapatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao. Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa. Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake. Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao; kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema. Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

SHANGILIO
Mdo. 16:14

Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, Ee Bwana, 
Ili tuyatuze maneno ya Mwanao.
Aleluya
________

INJILI 
Mt. 15:21-28

Yesu aliondoka huko, akaenda kando pande za tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana unisaidie. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MALENGO YA JITIHADA ZETU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 15 2026
Juma la 19 la Mwaka

SIKUKUU YA KUPALIZWA BIKIRA MARIA MBINGUNI

Ufu 11:19, 12:1-6, 10;
Zab 45:9-11, 15 (K) 10;
1Kor 15:20-26;
Lk 1:39-56


MALENGO YA JITIHADA ZETU!


Katika sikukuu ya Kupalizwa Mbinguni kwa Mama wa Mungu, tunafanya sherehe ya Bikira Maria kutoka katika hali ya ubinadamu mpaka kufika hali ya mwenye heri. Kwa kumtafakari Bikira Maria katika utukufu wake, tunaelewa kuwa hapa duniani sio kwetu bali tu wapitaji, pia tunaelewa kuwa tunatakiwa kuishi hapa duniani tukiwa tumejawa na tamaa ya vitu vya mbinguni basi kwa kufanya hivyo tutarithi vivyo vitu katika ufalme wa milele. Kwa kusema hivyo basi tujitahidi kutunza amani na utulivu wa mioyo yetu, japokuwa tumesongwa na magumu ya maisha. Mwangaza wa Bikira Maria akiwa amechukuliwa mbinguni huendelea kuonekana japokuwa wingi zito la huzuni na mateso limetanda.

Katika sikukuuu ya Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria tunakumbuka kushiriki kwa Bikira Maria katika Ufufuko wa mwanae, kwa kupalizwa mbinguni mwili na roho, alipomaliza kile alichokijia hapa duniani. Kupalizwa Mbinguni kunatuonyesha kile kitakachotutokea pale tutakapofufuliwa siku ya mwisho. Kupalizwa mbinguni ndio lengo kuu la maisha yetu kama Wakristo.

Kama vile Mt. Paulo atuambiapo kuwa, tutafufuliwa na miili yetu iliyo tukuka kama ilivyokuwa kwa Kristo. Kwa ile nguvu ya Yesu mfufuka tutaweza kuungana na Baba katika utukufu wa Kristo, kama vile Bikira Maria anavyoshiriki katika muungano huo kwa sasa. Kupalizwa Mbinguni ni siku ambayo tunaitwa kutafakari kwa kina malengo ya maisha yetu, na urithi wa uzima wa milele.

Kwa kusema hivyo basi tujitahidi kuyawaza hayo kila siku. Inatulazimu kufikiria kuwa tumesimama na Bikira Maria na mwezi nchini ya miguu yake, akiwa wamevaa taji la jua na nyota kichwani mwake. Pia inatubidi kumwona yule joka limefungwa, na kila mmoja wetu kwa neema aliyopewa na Mungu na kwa msaada wa Bikira maria anatakiwa kumzaa Kristo katika maisha yake. kwa kufanya hivyo basi tutakuwa na uhakika wa kufufuliwa mwili na roho.kwa kufanya hivyo basi tunakuwa tumepata maana halisi ya maisha yetu, na kwamba ukweli unaoelezewa katika mafundisho ya kanisa juu ya kupalizwa Bikira Maria ndio utimilifu wa matamanio ya maisha yetu.

Sala: Ewe mama uliyejaa msamaha, utukufu wako unisaidie kuyabeza na kuyachukia yale yaliyo ya dunia na kutamani yale yaliyo ya mbinguni. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 15, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 15, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 19 LA MWAKA 

SHEREHE YA KUPALIZWA MBINGUNI BIKIRA MARIA


SOMO 1 
Ufu 11: 19, 12: 1-6, 10

Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake. Kukawa na umeme, na sauti, na radi, na tetemeko la nchi, na mnua ya mawe nyingi sana.

Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili. Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba. Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za muinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake. Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi. Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini.

Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 45: 9-11, 15 (K) 10 

(K) Mkono wako wa kuume amesimama malkia
       amevaa dhahabu ya Ofiri.

Binti za wafalme wamo
Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki.
Mkono wako wa kuume amesimama malkia, 
Amevaa dhahabu ya Ofiri.
Sikia, binti, utazame, utege sikio lako,
Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. (K)

Naye mfalme atautamani uzuri wako,
Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. 
Watapelekwa kwa furaha na shangwe,
Na kuingia katika nvumba va mfalme. (K)


SOMO 2  
1Kor 15: 20-26

Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watanuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja. Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Maria amepalizwa mbinguni majeshi yote ya malaika wanafurahi.
Aleluya.


INJILI 
Lk 1: 39-56

Mariamu aliondoka, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeth Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu; akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi? Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu. Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
Mariamu akasema,
Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Na roho yangu imemfurahia Mungu,
Mwokozi wangu;
Kwa kuwa ameutazama
Unyonge wa mjakazi wake.
Kwa maana, tazama, tokea sasa
Vizazi vyote wataniita mbarikiwa;
Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, 
Na jina lake ni takatifu.
Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi 
Kwa hao wanaomcha.
Amefanya nguvu kwa mkono wake;
Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; 
Na wanyonge amewakweza.
Wenye njaa amewashibisha mema
Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu. 
Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;
Ili kukumbuka rehema zake;
Kama alivyowaambia baba zetu,
Ibrahimu na uzao wake hata milele.
Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

NDOA-AGANO LA UPENDO!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Agosti 14, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 19 la mwaka wa Kanisa

Ez 16: 1-15, 60, 63; 
Is 12: 2-6; 
Mt 19: 3-12


NDOA-AGANO LA UPENDO!


Katika somo la Injili leo tunaona tafakari na ukweli kuhusu ndoa na maisha ya kitawa. Yesu anaeleza kuhusu kifungo cha ndoa. Mtu yeyote asitenganishe- mtu anayeongelewa hapa ni mwanamume sio mtu mwingine wa tatu kama hakimu hivi. Katika ndoa za Wayahudi ilikuwa ni mkataba, ambao mwanamume alikuwa na uwezo wakuuvunja (Kumb 24:1). Mafarisayo waliichukua sheria hii kama sheria nzuri, bali Yesu katika Injili anaielewa kama sheria iliowekwa kwa wale waliokuwa na mioyo migumu. Anawaeleza akiwarudisha kabisa mwanzoni mwa mpango wa Mungu kuhusu ndoa aliokuwa nao tangu kuumbwa kwa Ulimwengu, “Kwahiyo Mwanamume atamuacha Baba yake na Mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja’” (Mwanzo 2:24) 

Siku hizi uelewa kuhusu ndoa, talaka na maisha ya usafi wa moyo unapata maana mbali mbali. Kizazi cha sasa imewawia vigumu kuelewa kwamba ndoa ni kifungo na Agano la maisha yote. Wakati watu wanapofikiria hivyo wanaona haifai na haiwezekani na wanamua kupeana talaka kama njia rahisi tu. Kuishi katika mahusiano bila ndoa inawavutia vijana wa leo zaidi kuliko kufunga ndoa kwani wanaona ni rahisi zaidi kuachana kama maisha hayaendi. Watu wanaishi uchumba sugu miaka baada ya miaka hata wengine wamefariki wakiwa katika hali hiyo. Leo tunaalikwa tusikie ujumbe wa Yesu ambao ni changamoto kwetu. Hakuna maisha ya majaribio katika ndoa, ndoa ni agano kati ya mume na mke, na linafanyika kwa uhuru kamili wa mke na mume bila shuruti, baada ya maamuzi yao hufanya agano hilo hadharani na kuamua kuishi pamoja siku zote za maisha yao. Tofauti na hilo sio ndoa ni maisha ya dhambi na kuigiza. 

Sala: Mungu Baba yetu, tunaomba ulichokiunganisha wewe Mwanadamu asikitenganishe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 14, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 14, 2026
IJUMAA, JUMA LA 19 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 16:59 – 63

Bwana Mungu asema hivi; Nitakutenda vile vile kama ulivyotenda, uliyekidharau kiapo kwa kulivunja agano. Walakini nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe, katika siku za ujana wako, nami nitaweka imara agano la milele pamoja nawe. Hapo ndipo utakapozikumbuka njia zako, na kutahayarika, hapo utakapowakaribisha maumbu yako, walio wakubwa wako na wadogo wako; nami nitakupa hao wawe binti zako, lakini si kwa agano lako. Nami nitaweka imara agano langu nawe; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; upate kukumbuka, na kufadhaika, usifumbue kinywa chako tena, kwa sababu ya aiba yako; hapo nitakapokusamehe yote uliyoyatenda, asema Bwana Mungu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Bwana.


WIMBO WA KATIKATI
Isa. 12:2 - 6 (K) 1

(K) Hasira yako imegeukia mbali, nawe unanifariji moyo.

Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu;
Nitatumaini wala sitaogopa;
Maana Bwana Yehova ni nguvu zangu
Na wimbo wangu;
Naye amekuwa wokovu wangu. (K)

Basi, kwa furaha mtateka maji 
Katika visima vya wokovu.
Na katika siku hiyo mtasema,
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake;
Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa,
Litajeni jina lake kuwa limetukuka. (K)

Mwimbieni Bwana; kwa kuwa ametenda makuu;
Na yajulikane haya katika dunia yote.
Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni;
Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako. (K)


SHANGILIO
Ebr. 4:12

Aleluya, aleluya,
Kwa kupenda kwake mwenyewe, Baba alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.
Aleluya.


INJILI
Mt. 19:3 – 12

Mafarisayo walimwendea Yesu wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu? Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha? Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. Nami nawambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.

Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa. Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumobni mwa mama zao; tena wak omatowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MSAMAHA KATIKA MAISHA YA MKRISTO!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Agosti 13, 2026, 
Juma la 19 la Mwaka


Eze 12: 1-12; 
Zab 77: 56-59, 61-62; 
Mt 18: 21-19:1


MSAMAHA KATIKA MAISHA YA MKRISTO!

Inasemwa kwamba kukosea ni ubinadamu lakini kusamehe ni Umungu. Kwa njia hii kusamehe imekuwa changamoto kwa mwanadamu. Katika Injili, jibu la Yesu lipo tofauti na mawazo aliyokuwa akiwaza Petro, kwamba kusamehe hakuna kikomo. Inapaswa kuendelea na kuwa hali halisi katika maisha ya mtu. 

Msamaha hautufanyi dhaifu, wajinga, kudhalilika, au wasio na thamani. Bali unatualika katika hali ya juu kabisa ya kuishi. Kwanza kabisa maisha ya Bwana yalikuwa maisha ya msamaha. Aliwasamehe wafuasi wake na adui zake. Zaidi sana, anatusamehe sisi na wale waliotukosea. Kwahiyo, huwa tunamuomba kila tusalipo sala ya Baba yetu, “atusamehe dhambi zetu kama tunavyo wasamehe waliotukosea”. Ulimwengu hauwezi kusitawi kama tutatafuta tu haki. Hamna Amani kama hamna haki kadhalika hamna haki kama hamna msamaha.

Ya pili, msamaha si sawa na kusahau; bali msamaha ni sawa na utakatifu. Msamaha hauwezekani bila neema ya Mungu. Naweza tu kuwasamehe adui zangu kama kuna neema ya Mungu ndani mwangu-maisha binafsi ya kuhisi msamaha wa Mungu ndani mwangu, na ile hamu ya kuwasamehe walionikosea. Kwahiyo, ninaposamehe sisahau kile alichofanya Mungu kwangu. 

Na mwisho kabisa, kusamehe sio ubinadamu, ni Ukristo. Leo, Yesu anatualika tufuate hatua alisowafundisha wafuasi wake: ongea na Baba kwanza, ungama sehemu yako, kabiliana na tatizo lenyewe sio kumshambulia mtu, ona huruma na wengine na kuwa muelewa, na baadae chukua hatua ya kuonana na aliyekukosea. Hakuna hatua rahisi katika msamaha. Yesu hakusema itakuwa rahisi katika kumfuata. Msamaha unatupa changamoto sisi wote. Lakini hiki ndicho kinacho tutambulisha sisi na Yesu. Tumuombe Yesu atupe neema yakuachia yote moyoni mwetu na kuwasamehe wote waliotukosea katika maisha yetu yote. Hata kama ni kosa kubwa kiasi ghani, tuachie yote ili Mungu aendelee kutusamehe na sisi na kutupatia Baraka zake.

Sala: Bwana nisaidie niweze kuwasamehe ndugu zangu wote. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA - AGOSTI 13, 2026



MASOMO YA MISA 
ALHAMISI, AGOSTI 13, 2026
JUMA LA 19 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 12:1 – 12

Neno la Bwana likanijia tena, kusema, Mwanadamu, wewe unakaa katika ya nyumba iliyoasi, watu ambao wana macho ya kuona, ila hawaoni, wana masikio ya kusikia, ila hawasikii; kwa maana ni nyumba iliyoasi. Basi, mwanadamu, funga tayari vyombo kwa uhamisho, ukahame wakati wa mchana mbele ya macho yao; nawe utahama toka mahali pako hapa mpka mahaoli pengine mbele ya macho yao; labda watafahamu, wajapokuwa ni nyumba iliyoasi. Nawe ukatoa vyombo vyako, wakati wa mchana, mbele ya macho yao, kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa; nawe mwenyewe utatoka, wakati wa jioni, mbele ya macho yao, kama watu watokavyo katika kuhamishwa. Toboa mahali ukutani mbele ya macho yao, kama watu watokavyo katika kuhamishwa. Toboa mahali ukutani mbele ya macho yao, ukachukue vitu kwa kuvipitisha pale. Mbele ya macho yao utajitwika begani pako, na kuvichukua nje gizani; utafunika uso wako, hata usiione nchi; kwa maana nimekuweka uwe ishara kwa nyumba ya Israeli.

Nikafanya vile vile kama nilivyoamriwa; nalitoa vyombo vyangu wakati wa mchana kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa, na wakati wa jioni nikautoboa ukuta kwa mkono wangu; nikavito agizani, nikavichukua begani, mbele ya macho yao.

Asubuhi neno la Bwana likanijia, kusema, Mwanadamu, nyumba ya Israeli, je! Nyumba ile iliyoasi, hawakukuambia, Unafanya nini wewe? Waambie Bwana Mungu asema hivi; Ufunuo huu wamhusu mkuu wa Yerusalemu, na nyumba yote ya Israeli walio kati ayo. Sema, Mimi ni ishara kwenu; kama mimi nilivyotenda, wao nao watatendwa vile vile; watahamishwa, watakwenda kufungwa. Naye mkuu aliye kati yao atachukua begani katika giza; naye atatoka kwenda zake; watatoboa mahali ukutani, wapate kuvichukua vyombo vyao nje; atafunika uso wake, kwa sababu hataiona nchi kwa macho yake.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 78:56 – 59, 61 – 62 (K) 7

(K) Usiyasahau matendo ya Mungu.

Walimjaribu Mungu Aliye juu wakamwasi.
Wala hawakuzishika shuhuda zake.
Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;
Wakaepea kama upinde usiofaa. (K)

Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,
Wakamtia wivu kwa sanamu zao,
Mungu akasikia, akaghadhibika,
Akamkataa Israeli kabisa. (K)

Akaziacha nguvu zake kutekwa,
Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;
Akaughadhibikia urithi wake. (K)


SHANGILIO
Kol. 3:16, 17

Aleluya, aleluya,
Neno la Kristu likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote; mkimshukuru Mungu Baba kwa Yeye.

Aleluya.


INJILI
Mt. 18:21 – 19:1

Petro alimwendea Yesu akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi. Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipowe ile deni. Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa waojli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. Ndipo bwana wake akamwita akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi; nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe? Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake. Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng’ambo ya Yordani.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.