Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
USIOGOPE
MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 9, 2026
1 Fal. 19:9, 11-13
Eliya alifika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia. Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi: na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu. Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi vake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango.
Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 85 :8-13, (K)7
(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.
Nisikie atakavyosema Mungu Bwana,
Maana atawambia watu wake amani.
Hakika wokovu wake u karibu na wamchao,
Utukufu ukae katika nchi yetu. (K)
Fadhili na kweli zimekutana,
Haki na amani zimebusiana.
Kweli imechipuka katika nchi,
Haki imechungulia kutoka mbinguni. (K)
Naam, Bwana atatoa kilicho chema,
Na nchi yetu itatoa mazao yake.
Haki itakwenda mbelc zake,
Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia. (K)
SOMO 2
Rum 9: 1-5
Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, ya
kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu. Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili; ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.
Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu
SHANGILIO
Lk. 19:38
Aleluya, aleluya,
Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana;
Aleluya.
INJILI
Ml 14:22-33
Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambe. wakati yeye alipokuwa akiwaaga makutano. Nave alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea. akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli, wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akanena, akawaambia, Jipeni movo; ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma. Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia wakisema, Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
IMANI KUBWA!
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 8 2026
Juma la 18 la Mwaka
Zab. 9 : 7-12 (K) 10;
Mt 17: 14-20.
Katika Injili ya leo,
baada ya wanafunzi wa Yesu kurudi katika utume wao, walishangaa kwanini
hawakuweza kumponya kijana aliyekuwa ana pepo mchafu. “kasababu ya Imani yenu
ndogo” Yesu aliwaambia. Mngekua na Imani ndogo kama chembe ya haradani”
aliwaambia, “hakuna chochote ambacho kingeshindikana kwenu”.Mwaliko huu wa Yesu
sio kiingiilio cha kumpa rushwa Mungu atafanyie maajabu, bali ni mwito wa
kuweka matumaini yetu yote kwake kwa chochote kitokeacho kwetu, yeye tayari
ajua lipi bora kwetu kulingana na mapenzi yake.Imani hii ikiwa ndani ya upendo
mkuu, ndio iletayo furaha na amani katika maisha yetu, hata katika kipindi
kigumu cha maisha yake.
Sala: Ee Bwana,
Nakutumainia wewe. Amina.
------------------------
Copyright ©2013-2026
©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, AGOSTI 8, 2026
SOMO 1
INJILI
Mt. 17: 14-20
Mtu mmoja alimjia
Yesu, akampigia magoti, akisema, Bwana, umrehemu mwanangu, kwa kuwa ana kifafa,
na kuteswa vibaya; maana mara nyingi huanguka motoni, na mara nyingi majini.
Nikamleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponva. Yesu akajibu, akasema. Envi
kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini?
Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu. Yesu akamkemea pepo, naye
akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo
KUPOTEZA MAISHA YA NAFSI ILI KUPATA YOTE!
MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 7, 2026
SOMO 1
Tazama juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema, atangazaye Amani. Zishike sikukuu zako, Ee Yuda, uziondoe nadhiri zako; kwa maana yule asiyefaa kitu hatapita kati yako tena kamwe; amekwisha kukatiliwa mbali.
Kwa maana Bwana anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.
Ole wake mji wa damu! Umejaa mambo ya uongo na unyang’anyi; mateka hayaondoki. Kelele za mjeledi, kelele za magurudumu yafanyayo kishindo; na farasi wenye kupara-para, na magari ya vita yenye kuruka-ruka; mpanda farasi akipanga, na upanga ukimeta-meta, na mkuki ukimemetuka; na wingi wa waliouawa, na chungu kubwa ya mizoga; mizoga haina mwisho; wanajikwaa juu ya mizoga yao. Nani nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dahrau. Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji?
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
WIMBO WA KATIKATI
Kum. 32: 35 – 36, 39, 41 (K) 39
(K) Naua Mimi, nahuisha Mimi.
Maana siku ya msiba wao imekaribia,
Na mambo yatakayowapata yatafanya haraka.
Kwa kuwa Bwana atawaamua watu wake,
Atawahurumia watumwa wake. (K)
Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye.
Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi;
Naua Mimi, nahuisha Mimi,
Nimejeruhi, tena naponya. (K)
Nikiuonoa upanga wangu wa umeme,
Mkono wangu ukishika hukumu,
Nitawatoza kisasi adui zangu,
Nitawalipa wanaonichukia. (K)
SHANGILIO
Lk. 8:15
Aleluya, aleluya,
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno la Mungu, na kulishika.
Aleluya.
INJILI
Mt. 16:24-28
Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo
KUITWA KWENYE UTUKUFU!
MASOMO YA MISA - TAREHE 6, AGOSTI, 2026
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
WOTE NI WATOTO WA MUNGU!
Sala: Bwana, naomba watu wote wahisi upendo wako kwao kwa kupitia mimi. Amina
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com





