Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

NINYI MNASEMA MIMI NI NANI?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Agosti 23, 2026
Juma la 21 la Mwaka

___________________

Isa 22: 19-23; 
Zab 137:1-3, 6, 8; 
Rum 11:33-36; 
Mt 16:13-20
___________________

NINYI MNASEMA MIMI NI NANI?

Picha ya Yesu inayotumika kwa tangu miaka 2000 iliyopita, anatumika kama rafiki wa waliotengwa, mwenye ujumbe ulioleta mapinduzi katika maisha ya Mwanadamu, mshindi wa falme mbali mbali na mlinzi wa viongozi. Yesu tabia yake ni tabia ambayo kila mmoja anapenda kufanana nayo au kuishi kama yeye. Sisi pia tuna picha ya Yesu ambayo tunabeba ndani mwetu tangu tukiwa wadogo. Baada ya miaka yote hiyo hajawahi kumuuliza mtu kama alivyo fanya karibu na Kaisaria Philipi, “Ninyi mnasema mimi ni nani?”

Katika somo la kwanza kutoka katika kitabu cha nabii Isaya, mfalme Hezekia amemchagua Shabna kama mkuu wa nyumba yake. Shabna, mtu wa kutafuta maslahi na mtu wa kupenda rushwa, aliye kinyume na ujumbe wa nabii Isaya anafanya njama na Wamisri. Shebna anaondolewa na Eliakimu, mtu mwaminifu, mwenye uwezo, wakutegemewa katika siasa. Eliakimu alikuwa mevikwa koti la mtangulizi wake, akapewa mamlaka yote na hatimaye akapewa ufunguo na kuwa na nguvu zote juu ya ufalme.

Katika somo la Injili, Yesu anawauliza mitume maswali mawili. La kwanza ni rahisi “Je, watu wanasema Mwana wa Adamu ni nani? Na swali la pili linalo leta changamoto ni “nyie mnasema mimi ni nani?” Yesu aliwaheshimu watu wote wa zama zote na muda wote. Amekuwa ni kiungo cha kupendwa na kutukuzwa. Lakini Yesu hakufuata ujanja wa kibinadamu na mitizamo yao. Aliyapa kipaumbele maisha ya Kimungu, taratibu huku akifunua mpango wake, na baadae kushinda werevu wa mwanadamu na ufahamu wake kwa katika maisha yake mwenyewe. Wafuasi wake hawakuwa wafuasi kwasababu tu walimfuata. Mfuasi wake ni yule aliye elewa kwamba yeye ni wa pekee, yeye ambaye amempenda kwa moyo wote, kumwamini kabisa na kuwa tayari kufanya chochote kwa ajili yake. Ni katika hali hii Petro anakuja na jibu la pekee. Alisema “wewe ni Masiha” Mwana wa Mungu aliye hai, ambaye Manabii walikutabiri na ambaye una tazamamiwa.”

“Wewe ni ambaye sisi tumeamua kujitoa maisha yetu kwa ajli yako.” Petro alitoa jibu zuri sana lakini katika maneno tu, lakini katika akili yake alikuwa na wazo tofauti. Alikuwa na hakika kwamba Yesu alikuwa anakaribia kuanzisha ufalme wake hapa duniani na hivyo angetumia nguvu, miujiza mikali na mambo mengi ya kushangaza ambayo yataleta mshangao na kuvuta hisia za watu. Haya pia yalikuwa ndio matazamio ya wafuasi wengine, licha ya wao kufahamu kitu tofauti na makutano wamefungwa na mawazo ya kizamani bado.

Katika sehemu ya pili ya Injili Yesu anamwambia Simoni Petro: “Wewe ni Petro na juu ya Mwamba huu nitalijenga kanisa…” . Maelezo ya maneno haya ni magumu zaidi ya jinsi tunavyo yatazama. Kwanini na kwasababu ghani Simoni Petro anaitwa Mwamba ambao juu yake atalijenga kanisa? Kwanza kabisa, tunatambua kuwa “mwamba” kama msingi wa kanisa umeongelewa pia sehemu nyingine katika Agano Jipya. Mwamba huu, ambao ni mgumu usio sogea, daima ni “Yesu Kristo” hakuna mwigine -Paulo anasema hakuna anayeweza kuweka msingi mwingine tofauti na ule ambao umewekwa, ambao ni “Yesu Kristo” (1 Kor 3:11). “ninyi ni nyumba ambayo misingi yake ni mitume na manabii, na jiwe kuu ni Kristo mwenyewe..” (Ef 2:19-21). Petro pia katika barua yake anawaalika wabatizwa wapya wasijitenge kabisa na Kristo kwani yeye ni “jiwe””mwamba” unao ishi, uliokataliwa na watu, lakini aliyechaguliwa na mwenye thamani machoni pa Mungu (1 Pet 2:4-6). Sehemu ya pili ni kwamba jina alilolopewa Simoni kama Kefa au Petro katika lugha ya Aramaiki katika hali zote halina maana ya “mwamba” bali jiwe la kujengea. Jiwe analosema Yesu ni Imani inayotangazwa na Petro. Imani ambayo imebeba msingi wa kanisa, ambayo inalifanya liunganike na “Kristo-Mwamba”, na kulifanya lisiharibiwe na kulifanya lisiguswe na nguvu za yule muovu. Wale wote kama Petro, wanao amini na kutangaza Imani hii, tumewekwa kama mawe hai, katika nyumba ya kiroho alioijenga Mungu mwenyewe.

Petro pia alipokea funguo za kufunga na kufungua. Kumpa mtu ufunguo ni kumwamini kwamba ataweza kazi unayompa. Marabii au walimu wa sheria walidhani kwamba wameshika “ufunguo wa Torati” kwasababu waliyafahamu maandiko. Waliamini kwamba kila mtu lazima alikuwa awategemee. Maamuzi yao. Yesu anachukua usemi huu katika hali ya ukali “lawama ipo juu yenu ninyi walimu wa sheria, kwani mmechukua ufunguo wa akili. Ninyi wenyewe mmeshindwa kuigia na mmewafungia wengine wasipate kuingia” (Lk 11:52). Badala ya kufungua milango ya wokovu watu waingie wameifunga watu wanashindwa kuingia badala ya kuwangulia watu ukweli kuhusu Mungu na mapenzi yake. Yesu anawa nyanganya ufunguo ambao wenyewe waliutumia vibaya. Na sasa ni hivi “Ufalme wa Mbinguni” ni wazi kwa wafuasi wote wanaopenda kuingia na ufunguo wa kuingia ni Imani iliotangazwa na kukiriwa na Petro. Kwa kumpa Petro ufunguo haina maana kwamba anamfanya Petro kuwa mlinzi wa mlango wa kuingia mbinguni. Bali Yesu anamwambia “yeye awe mfano kwa kundi” (1 Pet 5:3). Anamwamini yeye afungue zaidi akili ya ufahamu wa Kristo na Injili yake. Wanaopita kwa kutumia mlango uliofunguliwa na Petro kwa kutangaza imani anayo ikiri atapata wokovu, anaye ikataa basi anajifungia mwenyewe.

Wakti Yesu alivyo uliza “watu wanasema mimi ni nani” (Mt 16:13), si kwamba ni kwasababu alikuwa anataka kufahamu kuhusu sura yake. Ni kutaka kujua kama mtazamo wa watu unaendana na ukweli wenyewe kuhusu yeye –kama wanamfahamu kweli. Jibu linalo tolewa linaonesha kwamba watu hawakuwa sahihi. Lakini Yesu yeye anataka kubaki mwaminifu katika utume wake kama Kristo. Nia moja tu ambayo alitaka kutimiza ilikuwa ni nia ya Baba yake “chakula changu ni kutimiza mapenzi ya Baba yangu” (Yn 4:34).

Katika muda mmoja au mwingine, sisi pia tunapaswa tuelezee Yesu ni nani katika maisha yangu. Tujaribu kuelezea leo na kuangalia kuhusu Imani yetu na uelewa wetu kuhusu Kristo, Masiha. Tutafute kutambua “siri” ya utambulisho wake halisi tukisikiliza sauti ya Baba yetu anaye ongea nasi ndani ya mioyo yetu. Ni katika moyo huu tunaweza kuingia katika Imani ya kweli kuhusu Mwana wa Mungu. Tuvutwe katika hali ya kuwa na Imani na kumvaa Yesu Kristo, ili tuweze kutangaza Imani, kwani hili ndilo la maana katika wito wetu wa Ukristo tulio uvaa. Ni kwa njia ya Imani tu ndani ya Kristo tunaweza kungara na kuwa na nguvu dhidi ya yule muovu na kumshinda.

Sala: Bwana, nina amini kwamba wewe ni Kristo, Masiha, Mwana wa Mungu! Nisaidie kukosa Imani kwangu ili niweze kukuamini wewe na kukupenda kwa nafsi yangu yote. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 23, 2026



MASOMO YA MISA, JUMAPILI, AGOSTI 23, 2026
JUMA LA 21 LA MWAKA 
________

SOMO I
Isa. 22:19-23

Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi: Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nvumba ya Yuda. Na ufunguo wa nvumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga. Nami nitamkaza kanta msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 138: 1-3, 6, 9 (K) 9

(K) Ee Bwana, fadhili zako ni za milele, 
Usiziache kazi za mikono yako.

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,
Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu. (K)

Nitalishukuru jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Kuliko jina lako lote.
Siku ile niliyokuita ulinitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, 
Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)
________

SOMO 2 
Rum 11: 33-36

Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

SHANGILIO
Mt 11: 25

Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, 
kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye
hekima na akili. ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya
________

INJILI 
Ml 16:13-20

Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipo, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaa- mbia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia. Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikufunulia hili, bali Baba vangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Ndipo alipowakataza sana wanafunzi

wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

SALAMU, MALKIA !



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 22, 2026, 
Juma la 20 la Mwaka

Kumbukumbu ya Bikira Maria Malkia

Is 9: 2-7;
Zab 113: 1-8;
Lk 1: 26-38; 


SALAMU, MALKIA !

Baba Mtakatifu Pius XII katika waraka wake “Ad Caeli Reginam” alipendekeza kuwe na desturi na fundisho juu ya Umalkia wa Bikira Maria na alianzisha sikukuu hiyo katika Kanisa. Lakini Umalkia wa Mama una msingi kutoka katika maandiko Matakatifu. Alivyopashwa habari na malaika Gabriel, alitangaza kwamba Mwana wake atapokea kiti cha enzi cha Daudi na atatawala milele. Maria alivyomtembelea Elizabeth, Elizabeth alimwita Maria “Mama wa Bwana wangu” katika mafumbo yote ya maisha ya Maria, Maria anahusianishwa na Yesu. Umalkia wake ni ushiriki wake katika ufalme wa Kristo. Tunaweza kukumbuka pia katika Agano la Kale, Mama wa Mfalme alikuwa na nguvu sana katika mahakama. 

“Malkia yupo tayari kila wakati kumuomba Mfalme aliyemzaa” alisema Baba Mtakatifu Sixtus IV. Katika Karne ya nne, Mt. Efrem alimuita Maria kuwa ni “Malkia”. Baadae Mababa wa Kanisa na Walimu wa Kanisa wakawa wanatumia jina hilo. Utenzi wa karne ya 11 mpaka karne ya 13 unamuelezea Maria kama Malkia. Rozari ya Kidominiko na Wafransisko katika sala mbali mbali na litania wanamvika Maria taji kama Malkia. Sikukuu hii katika hali ya kufikirika inafuata baada ya sherehe ya Bikira Maria kupalizwa Mbinguni na ndio maana inaadhimishwa katika siku ya oktava ya sherehe hiyo.

Mungu anamimina neema zake kwao wote wanao muamini na anaonesha upendo wake kwa walio wadogo, wanyenyekevu na wote wanaopokea neno lake. Swali la Mama Maria “Itawezekanaje?” hakuuliza kwasababu alikuwa haamini au kwamba alikuwa na wasi wasi bali ni kwamshangao. Yeye ni mtekelezaji wa kweli wa neno la Mungu, aliyetayari kufanya mapenzi ya Mungu, hata inapo onekana kugharimu. Mungu anatupa neema na anategemea sisi tuweze kupokea kwa mapenzi hayo hayo, kwa utii, kwa moyo wote kama Maria alivyofanya. Wakati Mungu anaamuru, anatupa pia msaada wake, nguvu, na njia ya kupokea. Tunachohitaji ni “mapenzi mema” tuzame katika neema zake kwakusema “ndio” ya kweli kwa mapenzi yake na mipango yake juu ya maisha yetu. Tuache neno lake lichukue mwili katika maisha yetu. 

Sala: Salamu Malkia Mama mwenye huruma uzima tulizo  na matumaini yetu salamu, tunakusihi ugenini huku sisi wana wa Eva, tunakulalamikia na kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi, haya basi Mwombezi wetu utuangalie kwa macho yako yenye huruma, na mwisho wa ugani huu utuoneshe Yesu mbarikiwa wa tumbo lako, ee mpole, ee Mwema, ee mpendelevu Bikira Maria. Yesu nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, AGOSTI 22, 2026



MASOMO YA MISA, AGOSTI 22, 2026
JUMAMOSI  LA 20 LA MWAKA 

KUMBUKUMBU YA BIKIRA MARIA MALKIA


SOMO 1
Isa. 9:2 – 7

Watu wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu; wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewaangaza.

Umeliongeza taifa, umezidisha furaha yao; wanafurahi mbele zako, kama furaha ya wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.

Kwa maana umeivunja nira ya mzigo wake, na gongo la bega lake yeye aliyemwonea, kama katika siku ya Midiani. Maana silaha zote za mtu mwenye silaha wakati wa mshindo, na mavazi yaliyofiringirishwa katika damu, yatakuwa tayari kuteketezwa, yatakuwa kuni za kutiwa motoni.

Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa. Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani hayatakuwa na mwisho kamwe. Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; kuuthibitisha na kuutegemeza kwa hukumu na kwa haki, tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 113:1 – 8 (K) 2

(K) Jina la Bwana lihimidiwe tangu leo hata milele.

Aleluya.
Enyi watumishi wa Bwana, sifuni,
Lisifuni jina la Bwana.
Jina la Bwana lihimidiwe
Tangu leo na hata milele. (K)

Toka maawio ya jua hata machweo yake
Jina la Bwana husifiwa.
Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote,
Na utukufu wake ni juu ya mbingu. (K)

Ni nani aliye mfano wa Bwana,
Mungu wetu aketiye juu;
Anyenyekeaye kutazama,
Mbinguni na duniani? (K)


INJILI
Lk. 1:26 – 38

Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanawali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja nawe.

Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya maana gani? Malaika akamwambia, Usiogope. Mariamu kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.

Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Neno la Bwana.. Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

AMRI KUU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Agosti 21, 2026 
Juma la 20 la Mwaka 


Eze 37: 1-14; 
Zab 107: 2-9; 
Mt 22: 34-40


AMRI KUU


Injili ya leo inatualika tutafakari njia iliyo kuu ambayo kila mfuasi wa Kristo inapaswa kuwa msingi wake. Upendo kwa Mungu na upendo kwa jirani. Kwanza kabisa upendo kwa Mungu ni kushuhudia na kukiri upendo wa Mungu kwetu sisi. Sisi ni dhaifu sana na tunashindwa kumpenda Mungu kama inavyotupasa. Lakini ndani ya Yesu tunahisi upendo wa Mungu kwetu. Kwahiyo, kuhisi upendo wa Mungu, licha ya upweke wa mtu mwenyewe inamfanya mtu ampende Mungu kama matokeo ya kuhisi upendo huo. Huu ndio mwanzo wa kumpenda Mungu. Wakati mtoto anavyohisi upendo wa Mama, hafanyi kitu kinyume na Mama. Hii ndio maana ya kumpenda Mungu. Tukihisi upendo wa Mungu hatutafanya mambo kinyume na Mungu, hatujiingiza kwenye dhambi, bali tutafanya yote yenye kumpendeza. 

Inamfurahisha Mungu tukiwapenda wengine. Kwahiyo, wakati mtu anampenda Mungu, anaanza kumpenda jirani pia. Je, ni muda ghani upendo wangu juu ya jirani unapokuwa kamilifu? Tunapowapenda ndugu zetu tunakuwa tunatamani na wao kila wakati wawe washiriki kwenye uzima wa milele. Tunakuwa tunatamani na kuomba kwamba waishi maisha yao yote katika neema. Kwahiyo wanakuwa washiriki wa uzima wa milele zawadi tuliopewa na Yesu. Tunakumbuka alichosema Yesu ‘mlicho watendea wadogo hawa mme mtendea yeye’. Tutoke njee ya nafsi zetu, tuweze kukutana na watu waliowahitaji, tuwasaidie kadiri ya uwezo wetu. Huu ndio upendo kwa jirani zetu. 

Sala: Bwana nisaidiye niweze kukupenda wewe ili niweze kuwapenda wengine. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA IJUMAA, AGOSTI 21, 2026




MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 21, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 37:1 – 14

Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa; akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.

Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana Mungu, wajua wewe. Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana. Bwana Mungu aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, teteme3ko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake, lakini haikuwamo pumzi ndani yake. Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana Mungu asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi. Basi nikatabiri kama alivyoiamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.

Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa. Basi tabiri, uwaambie Bwana Mungu asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli. Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu. Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza asema Bwana.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 107:1 – 9 (K) 1

(K) Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele.

Waseme hivi waliokombolewa na Bwana,
Wale waliowakomboa na mkono wa mtesi.
Akawakusanya kutoka nchi zote,
Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini. (K)

Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika;
Hawakuona mji wa kukaa.
Waliona njaa, waliona na kiu,
Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. (K)

Wakamlilia Bwana katika dhiki zao,
Akawaponya na shida zao.
Akawaongoza kwa njia ya kunyoka,
Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.(K)

Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake,
Na maajabu yake kwa wanadamu.
Maana hushibisha nafsi yenye shauku,
Na nafsi yenye njaa huijaza mema. (K)


SHANGILIO
Zab. 111:7, 8

Aleluya, aleluya,
Maagizo yako yote, ee Bwana, 
ni amini, yamethibitika milele na milele.
Aleluya.


INJILI
Mt. 22:34 – 40

Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu; Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

SHEREHE YA HARUSI!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Agosti 20, 2026, 
Juma la 20 la Mwaka 

Eze 36:23-28; 
Zab 50:12-15, 18-19; 
Mt 22:1-14


SHEREHE YA HARUSI!

Inafarijisha sana, kufikiri mbinguni kama sehemu ya sherehe ya harusi/karamuni. Itakuwa Yesu aliipenda sherehe ya harusi na akaona ni kielelezo/mfano mzuri wa kutueleza sisi alicho tuandalia Mungu. 

Katika somo la injili, mfalme anashangazwa kwamba ameandaa sherehe kubwa ya harusi ya mtoto wake lakini wageni walioalikwa hawana muda wakuhudhuria karamu hiyo. Kuna mambo mengi katika mfano huu. Kwa hakika cha kwanza ni kuhusu kualikwa. Mungu anatualika na hatulazimishi anatupa uhuru. Tunaweza kukubali au kukataa. Tupo huru. Inavyoonekana alivyotendewa yule asiyevaa vazi la harusi inaweza kushangaza kidogo. Tuliangalie hili kwa ukaribu zaidi. Wakati mfalme anavyomtambua “alikaa kimya!” iko wazi kutoka kwenye somo kwamba huyu mtu hakuwa na vazi la harusi kitendo cha kukosa kuwa makini na heshima kwa mfalme. Si kwamba huyu mgeni alishindwa kuwa na vazi

Sisi tumealikwa kwenye urafiki na Mungu. Tumepewa neema ya utakaso kama zawadi, lakini ni zawadi inayohitaji kujishughulisha. Tunapaswa tuishi ujumbe wa Ukristo unaoweza kutulazimu kubadili mitizamo yetu, tabia na aina ya maisha. Huyu mtu aliyeelezwa kwenye injili hakuwa na lakusema. Hakuwa amejiandaa kuingia katika karamu. 

Mfano wa karamu unaoendana sambamba na mfano huu ni Ekaristi Takatifu- zawadi ambayo ni ya hali ya juu kabisa ambayo hatuwezi kujitetea kuwa haki yetu, zawadi tusio stahili. Je, tunamaanisha kweli maneno tunayo sema kabla ya komunyo; Ee Bwana sistahili uingie kwangu lakini sema neno tu na roho yangu itapona? Kwahiyo leo, tunaomba mfano huu, ututikise mioyo yetu nakututoa katika uvivu na hali ya kuridhika na hali yetu. Tusimchukulie Mungu kwa mizaha! Tumpende Mungu kweli tuwe tayari kutoa sadaka yote yanayotufanya tujifariji binafsi na kushindwa kujiweka tayari kwa karamu na hapo kiaminifu tuweze kusema kwa ujasiri “Kufanya mapenzi yako, Ee Mungu, ndio furaha yangu”.

Sala: Ee Mungu, ninakushukuru kwa kunialika kwenye karamu yako ya Mbinguni. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA ALHAMISI, AGOSTI 20, 2026



MASOMO YA MISA 
ALHAMISI, AGOSTI 20, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 36:23 – 28

Neno la Bwana linifikia hivi: Nitalitakasa jina langu kuu, lililotiwa unajisi katika mataifa, mlilolitia unajisi kati yao; nao mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mungu, nitakapotakaswa kati yenu mbele ya macho yao. Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe. Nami nitawanyunyizia maji safi, nayi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote.

Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama. Nami nitatia rohoyangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. Nayi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 51:10: - 13, 16 – 17 (K) Eze. 36:25

(K) Nitawanyunyizia maji safi, Nanyi mtakuwa safi, nitawatakaseni na uchafu wenu wote.

Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.
Usinitenge na uso wako,
Wala roho yako mtakatifu usiniondolee. (K)

Unirudishie furaha ya wokovu wako;
Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
Nitawafundisha wakosaji njia zako,
Na wenye dhambi watarejea kwako. (K)

Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,
Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau. (K)



SHANGILIO
Zab. 19:8

Aleluya, aleluya,
Amri ya Bwana ni safi, huyatia macho nuru.
Aleluya.



INJILI
Mt. 22:1 – 14

Yesu aliwaambia makuhani na makutano kwa mithali, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi. Akawatuma watumwa waake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja. Akatuma tena watumwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu, ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusi. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake; nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua. Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakin wale walioalikwa hawakustahili. Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini. Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.

Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi. Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa. Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUWA MUWAJIBIKAJI!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Agosti 19, 2026, 
Juma la 20 la Mwaka 


Eze 34:1-11; 
Zab 22:1-6; 
Mt 20:1-16


KUWA MUWAJIBIKAJI!


Neno la Mungu linaongea nasi kuhusu kuwajibika, na kwanamna ya pekee, majukumu yaliowekwa juu yetu na Mungu. Katika somo la kwanza, Mungu anawakumbusha viongozi wa wana Waisraeli kuwa wao ni wawajibikaji wa matatizo na mateso ya watu. Walichaguliwa kuongoza watu, kuendana na amri zake. Lakini, wanawaongoza katika kuvunja uhusiano wao na Mungu kwakuharibu taratibu za kidini, nakuwachanganya kati yao ili waweze kujinufaisha binafsi kifedha na kisiasa. Na hili lime sababisha uharibifu na kupelekwa uhamishoni. Ezekiel anawaeleza kuhusu kushindwa kwao kuwa wachugaji wema wa watu.

Sisi wote pia, katika hali Fulani, tumewekwa kuwa wachungaji au wahudumu juu ya wengine. Kama Padre, Mtawa, Wazazi, Walimu, viongozi wa serikali, tunapaswa kutimiza majukumu yetu yakuwahudumia watu waliowekwa chini yetu au wanao tutegemea. Somo la kwanza linatueleza kwamba watu hawa hawapo chini yetu ili kuwahujumu au kuwaonea bali ni watu wa Mungu waliowekwa chini yetu na Mungu ili tuwahudumie. Hii inamaana kwamba sisi tupo na tutabaki kuwa wawajibikaji wa Mungu.

Somo la Injili ni juu ya mfano wa wafanyakazi wa shamba la mizabibu walio ajiriwa nakufanya kazi kwa masaa tofauti bali wanapewa mshahara sawa. Kitu kimoja cha kweli ambacho mfano huu unatufunulia ni kwamba, kwakuangalia majukumu yetu aliotupa Mungu, Mungu haangalii umefanya kazi muda mrefu kiasi ghani, bali anaangalia ni kwa jinsi ghani tumetenda kazi kwa uaminifu na kwa majitoleo. Hatimaye, hata kama tuna kazi ndefu na majukumu marefu katika maisha kama ya wazazi au kama ya mwalimu anayefundisha wanafunzi kwa kipindi kifupi, tunapaswa kuwa sawa katika kuitenda hiyo kazi kiaminifu na kwa majitoleo. Na majitoleo yetu ya kujitoa kwetu kutakuwa kwa hali ya juu na hapo tutaambiwa-“njooni kwangu mliobarikiwa na Baba yangu, muurithi ufalme mliotayarishiwa kabla ya kuumbwa misingi ya ulimwengu” (Mt 25:34).

Sala: Bwana, nakuomba unisaidie niweze kuwa mchungaji mwema wa kundi lililowekwa chini yangu, niweze kutimiza majukumu yaliowekwa chini yangu. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUMATANO, AGOSTI 19, 2026




MASOMO YA MISA 
JUMATANO, AGOSTI 19, 2026
JUMA LA 20 LA MWAKA


SOMO 1
Eze. 34:1 – 11

Neno la Bwana likanijia, kusema, Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana Mungu asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo. Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala. Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama-mwitu, wakatawanyika. Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.

Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; kama mimi niishivyo, asema Bwana Mungu, kwa sababu kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu; kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana.

Bwana Mungu asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.

Maana, Bwana Mungu asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 23:1 – 6 (K) 1

(K) Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati aya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika. (K)

Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)


SHANGILIO
Zab. 119:34

Aleluya, aleluya,
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Aleluya.


INJILI
Mt. 20:1–16

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba, aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.

Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. Hata kama saa kumi na moja akatoka, akauta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.

Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia masimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.

Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unukia mwenye nyuma, wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa. Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari? Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe. Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.