Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
KUFANYA YASIOWEZEKANA!
MASOMO YA MISA, JUMATATU, AGOSTI 3, 2026
Hes. 11 :4-15
Wana wa Israeli walilia wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule? Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu; lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hi; mana tu.
Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtarna, na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola. Watu wakazunguka-zunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa nyunguni, na kuandaa mikate; na tamaa yake ilikuwa kama tamu ya mafuta mapya. Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao.
Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika.
Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? Je! ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote? je! ni mimi nilivewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto aamwaye, wende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? kwani wanililia, wakisema, Tupe nyama, tupate kula. Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.
Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 81 :11-16 (K) 1
(K) Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha.
Watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,
Wala Israeli hawakunitaka.
Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,
Waenende katika mashauri yao. (K)
Laiti watu wangu wangenisikiliza,
Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Ningewadhili adui zao kwa upesi,
Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu. (K)
Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake,
Bali wakati wao ungedumu milele.
Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano,
Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani. (K)
SHANGILIO
Zab. 119:34
Aleluya, aleluya,
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Aleluya.
INJILI
Mt. 14:22-36
Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na
kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga makutano.
Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba.
Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. Na kite chombo kimekwisha kufika
katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.
Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya
bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni
kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akanena, akawaambia, Jipeni moyo; ni
mimi; msiogope.
Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru
nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa
miguu juuya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo. akaogopa; akaanza
kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake,
akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Nao
walipopanda chomboni, upepo ulikoma. Nao waliokuwamo ndani ya chombo
wakamsujudia, wakisema, Hakika wewe u Mwana wa Mungu.
Na walipokwisha kuvuka, walifika nchi ya Genesareti. Na watu wa mahali pale walipomtambua, walituma watu kwenda nchi zile zilizo kandokando, wakamletea wote waliokuwa hawawezi; nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu; na wote waliogusa wakaponywa kabisa.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
MASOMO YA MISA JUMAPILI, AGOSTI 2, 2026
JUMAPILI, AGOSTI 2, 2026
SOMO 1
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145:8-9,15-18
(K) Bwana waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
SOMO 2
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Mt. 4:4
Aleluya, aleluya,
INJILI
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
UCHAGUZI SAHIHI!

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, AGOSTI 1, 2026
UDONGO WENYE RUTUBA ILI KUPOKEA BARAKA ZA MUNGU
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, JULAI 31, 2026
MFINYANZI MTAKATIFU!

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JULAI 30, 2026

ALHAMISI, JUMA LA 17 LA MWAKA
NGUVU YA YESU DHIDI YA MAUTI!





