Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

AGANO LA UPENDO


“ASALI ITOKAYO MWMABANI”
Tafakari ya Kwaresima
Alhamisi, Machi 26, 2026
Juma la 5 la Kwaresima

Mwa17: 3-9;
Zab 104: 4-9; 
Yn 8: 51-59.


AGANO LA UPENDO!

Lirtujia na Neno la Mungu linatualika sisi kukumbuka Agano la Mungu nasi kwa njia ya Yesu. Somo la kwanza linaonesha ukarimu wa Mungu akifanya Agano na Abram, na kuingia katika historia ya Mwanadamu. Ukuu wa Abramu umejikita katika Imani yake na utii kwa Mungu. Bila hata kujua Abram ana anza safari kwenda nchi asio ifahamu. Kwa kumuita Abram Mungu alibadilisha maisha yake yote. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Mwanadamu Mungu anabadilisha jina la mtu. Abram anaitwa Abrahamu. Ikiwa na maana kwamba Mungu anauwezo wa maisha yetu yote ya sasa na ya baadae. Agano la Mungu halifungwi tu kwa Abrahamu na familia yake tu. Kama mto unaotiririka daima limejaa ukarimu. Anacho taka Mungu kutoka kwetu ni kudumisha Agano hili daima. 

Katika somo la Injili, Yesu anawaita watu waheshimu Agano la Mungu. Kama watalishika Agano hili hawataona mauti. Kwani kifo ni matokeo ya dhambi. Kwasababu ya kutotii Mwanadamu alipoteza heri machoni pa Mungu lakini Agano la Mungu kwa njia ya Yesu ni kuirudisha tena ile neema iliyopotea.

Sala: Bwana, ninakuomba Moyo wako uweze kuchuja makosa yangu yote na kuruhusu mbegu ya ukweli kumea ndani ya akili na moyo wangu. Mungu wa Agano, tusaidie pia sisi tuweze kuwa waaminifu kwa maagano yetu nawe. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2026
ALHAMISI JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1
Mwa. 17:3-9

Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. Agano langu nitalifanya imara katia ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako, nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao.

Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzaqo wako kwa vizazi vyao baada yako.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 150: 4-9 (K) 8

(K) Analikumbuka agano lake milele.

Mtakeni Bwana na nguvu zake,
Utafuteni uso wake siku zote.
Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya,
Miujiza yake na hukumu za kinywa chake. (K)

Enyi wazao wa Ibrahimu, mtumishi wake;
Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu;
Duniani mwote mna hukumu zake. (K)

Analikumbuka agano lake milele;
Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
Agano alilofanya na Ibrahimu,
Na uapo wake kwa Isaka. (K)


SHANGILIO
2 Kor. 6:2

Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa, tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.


INJILI
Yn. 8:51-59

Yesu aliwaambia Wayahudi: Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele. Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele. Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Yesu akajibu, nikijutukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika. Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.

Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

HABARI KUU YA KIHISTORIA


“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumatano, Machi 25, 2026
Juma la 5 la kwaresima

Sherehe ya Kupashwa habari ya kuzaliwa Bwana

Isa 7:10-14, 8:10;
Zab 40:7-11;
Ebr 10:4-10;
Lk 1:26-38


HABARI KUU YA KIHISTORIA


Leo kanisa lina sheherekea tangazo la mapenzi ya Mungu ya kutaka kumuokoa mwanadamu. Kupashwa habari ni mwaliko wa kila mmoja kujazwa na furaha na shukrani, tunapo tafakari juu ya Upendo wa Mungu wakutuokoa sisi. Tunafurahi kuona kujitoa na kukubali kwa Maria. Inaonesha ni kwa jinsi ghani kusema ‘ndio’ kwa mapenzi ya Mungu inaweza kuleta tukio la pekee kabisa katika maisha yetu, kama Bikira Maria alivyosema ‘ndio’ na kuleta tukio la ukombozi wa wanadamu. Kwa ‘ndio’ hii sio kwamba tu mipango ya Mungu inafanya kazi, bali Mungu mwenyewe anakuja kukaa ndani yetu na kati yetu.

Maria alionesha ni kwa jinsi ghani ya kuwa mfuasi wa Kristo, kwa kujikabidhi kwenye mikono ya Mungu anaye tupenda sisi. Wakati tunatafakari kama tunaweza kufanya kitendo hicho cha kujitoa kabisa na kujiweka katika mikono ya Mungu, tutambue kuwa wakati Mungu anatuita anatupatia pia neema. Kujikabidhi kwa Mungu, na kuacha yote na kujiweka mikononi mwake sio kitu rahisi. Ina maana kuacha mengine yapite, na kama Maria kuyakabili yale tusio yatambua kwa akili zetu ambayo yanatutisha. Mungu awezi kutupa kitu kama mikono yetu sio mitupu ili tuweze kupokea. Tukiwa tumekumbatia au kushika vitu mikononi hatuwezi kupokea vitu kutoka kwa Mungu. Sababu kwa nini kuna watakatifu wachache ni kwasababu hatutaki kumwachia Mungu atupende. Kupendwa maana yake, kujikabidhi kwa Mungu, kujikabidhi kwa Mungu bila kutegemea nguvu tofauti, na kutegemea yote jinsi Mungu anavyotaka. Maana yake ni furaha ya kukubali utupu wetu, kumtazama tu Mungu anayetoa yote, bila kuhesabu ni mangapi tunayompa kama zawadi. Sisi wote tunakabiliwa na utayari na uamuzi wa Maria. Je, tupo tayari kujikabidhi kwa Mungu na kumwomba Mungu afanya yale yote ambayo kwa jicho la kibinadamu tunaona hayawezekani?

Sala: Mungu mwenyezi, tunakuomba sala za Maria zimlete Yesu kwa dunia. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2026
JUMATANO, JUMA LA 5 LA KWARESIMA


SHEREHE YA KUPASHWA HABARI YA KUZALIWA BWANA



SOMO 1
Isa. 7:10 – 14

Bwana alisema na Ahazi akinena, Jitakie ishara ya Bwana, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu Bwana. Naye akasema, Sikilizeni sana, enyi nyumba ya Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka kumchosha Mungu wangu pia? Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 40:6 – 10 (K) 7 , 8

(K) Tazama, nimekuja, Ee Bwana, kuyafanya mapenzi yako.

Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja. (K)

Katika gombo la chuo nimeandikiwa
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (K)

Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. (K)

Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha fadhili zako wala kweli yako
Katika kusanyiko kubwa. (K)



SOMO 2
Ebr. 10:4 – 10

Haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari; Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo; Ndipo niliposema, Tazama nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.

Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati), ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili. Katika mapenzi hayo tumepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Yn. 1:14

Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukaona utukufu wake.



INJILI
Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye ju, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

UHUSIANO WETU NA MUNGU


“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumanne, Machi 24, 2026
Juma la 5 la Kwaresima

Hes 21: 4-9;
Zab 101: 2-3, 16-21; 
Yn 8: 21-30.


UHUSIANO WETU NA MUNGU


Katika somo la kwanza tunasikia waisraeli wakimlalamikia Mungu na Musa. Hawa watu walikombolewa kutoka utumwani, lakini wanataka tu kurudi tena huko utumwani. Hawaku mfahamu Mungu, aliye wakomboa. Hawakuwa na uhusiano wa kweli naye. Katika somo la Injili tunamuona Yesu anavyo jali, na upendo wake kwa wanadamu. Karne baada ya karne waliwasikia manabii, na walitegemea Masiha. Lakini aliposimama kati yao walishindwa kumtambua. Uelewa wao kuhusu Masiha haukuwa kamili. Yesu anajaribu kuwaamsha kwa mafundisho yake. 

Baba ndiye aliye mtuma Yesu ulimwenguni kwa utume na Yesu anakiri kwamba Mungu hawezi kumwacha. Yesu anatambua hili na anafurahia Baraka za Kimungu kwa muunganiko huu. Tofauti na Waisraeli na mafarisayo, Yesu anatambua uhusiano wake na Baba.

Sisi tunaweza kuwa “Wakristo walio lala”. Tunafahamu kusali, tunafahamu ni muda ghani wa kusimama, wakati wa kupiga magoti, wakati wa kukaa tukiwa kanisani, lakini uhusiano wetu na Mungu ni wakati tu tukiwa na furaha. Tunaanza kuwa na wasi wasi na Mungu tunapo kumbani na Matatizo. Liturjia ya leo inatutaka tuwe wakristo tulio amka, kuwa na uelewa na uhsiano wetu na Mungu na pia kuelewa mambo ya ulimwengu. Yesu kwa sadaka yake msalabani ametukomboa kutoka katika utumwa wetu wa dhambi. Kipindi hichi cha kwaresima tunaitwa kuwa wapya katika mapendo na Mungu, kumgeukia Yesu msalabani na kutafuta upendo, msamaha na huruma kutoka kwake, na kuwa upendo na huruma kwa wengine. 

Tafakari leo juu ya utume aliopewa Yesu: maisha yake ya kujitoa sadaka. Tafakari jinsi Mungu anavyopenda tuishi utume huu kwa maisha ya sadaka ya upendo na kujitoa. Unaweza kuwa uyaishi kwa moyo wako wote, au unaweza kuwa unahitaji kuelekezwa upya. Sema “ndio” kwa mapenzi yake kwa ujasiri na ushujaa na Mungu atatembea nawe katika kila hatua ya maisha yako. 

Sala: Bwana, ninasema “ndio” kwa mpango kamili ulionao katika maisha yangu. Vyovyote itakavyokuwa ninakubali bila kuwa na mashaka, Bwana mpendwa. Ninatambua upo na mimi daima na sipo mwenyewe. Yesu nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MACHI 24. 2026



MASOMO YA MISA, MACHI 24, 2026
JUMANNE, JUMA LA 5 LA KWARESIMA


SOMO 1
Hes. 21:4-9

Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia. Watu wakamnung’unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.

Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa. Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa. Basi, Musa akawaombea watu. Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo, ataishi. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
 Zab. 102:1-2, 15-20 (K) 1

(K) Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, kilio changu kikufikie.

Ee Bwana, usikie kuomba kwangu,
Kilio change kikufikie,
Usinifiche uso wako siku ya shida yangu,
Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. (K)

Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana,
Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;
Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni,
Atakapoonekana katika utukufu wake,
Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa,
Asiyadharau maombi yao. (K)

Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo,
Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu,
Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa,
Na kuwafungua walioandikiwa kufa. (K)



SHANGILIO
Yn. 8:12

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye, atakuwa na nuru ya uzima.



INJILI
Yn. 8:21-30

Yesu aliwaambia Mafarisayo: Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja.

Basi, Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja?

Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu. Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.

Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia. Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake ndiyo ninenayo katika ulimwengu.

Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba. Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo. Naye aliyenipeleka yu pamoja nami; hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.
Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamwini.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

TAZAMA NINATENDA TENDO JIPYA


Tafakari ya Ukarimu
Jumatatu, Machi 23, 2026
Juma la 5 la Kwaresima

Dan 13:1-9,15-17,19-30,33-62; 
Zab 23: 1-6; 
Yn 8: 1-11


TAZAMA NINATENDA TENDO JIPYA


Katika injili, tunamkuta akinamama mmoja aliyesukumwa mbele ya Yesu. “Amefumaniwa alipokuwa akizini. Mwanaume yeye ametoweka lakini mwana mke huyo amekamatwa. Mafarisayo wamemleta mbeie yaYesu. Macho yao yana mhukumu sawasawa na maneno yao. Ha Yesu hamwangalii hata. Asiwe anamw aibisha, Yesu anatazama chini naye anawazungumzia kwanza wenye kumshtaki. Kitambo tu nao wameondoka kwa sababu wanaona kwamba hata wao wenyewe wangeweza kushtakiwa.

Yesu alifanya nini kwa ajili ya mwanamke huyo. Je, alisema kwamba alilo tenda si jambo baya? Je, alisema kwamba kwa vyo vyote si vibaya sana kulala na mtu asiye mumewe? Hata. Ha alimsaidia aende mbele. Asahau mambo ya zamani na kutazama siku za usoni

“Hakuna aliyekuhumu kuwa na hatia?
Wala mimi sikuhukumu.
Enenda zako; wala usitende dhambi tena.”

Yesu anasahau na kusamehe mambo yake ya zamani. Ndivyo Mungu alivyo Ndivyo alivyokuwa amefanya kwa ajili ya Taifa lake —taifa Ia Israeli - kabla ya Yesu kuja ulimwenguni petu. Mungu anawaita: “Wateule wangu”. Hata ikiwa taifa lake wamekuwa wanamkosea uaminifu mara nyingi sana. Hata ikiwa mara nyingi mno wamekwenda mbali naye wala hawakutii amri zake, Mungu anawaambia waya sahau mambo ya zamani na kuona “tendojipya”analowafanyia. Anawasamehe tena na kuwaokoa.

Ndivyo Mungu wetu alivyo: Mungu anayeangalia mambo yetu ya zamani ili kuyasamehe ikiwatunayasikitikia hayo tuliyotenda. Ndiye Mungu mwenye kuele keza macho na mioyo yetu kwa siku za usoni. kwa hayo anayotuandalia Yeye

Ndio hasa ujumbe wa injili - Habari Njema ambayo sote twahitaji kuisikia. Mungu hataki kutuona tunasukuma makosa yetu ya zamani na kushindwa kwetu kama mzigo mzito. Mungu haoni furaha kutuona tunatembea tukiwa na nyuso zenye huzuni na mioyo mizito kwa ajili ya mzigo wa dhambi zetu za zamani.

Makumbukumbu mabaya, masikitiko, na hall mbaya mno ya kujisikia kuwa hawawezi kuyafuta kabisa mambo ya zamani. Mambo hayo yote yawalemeza watu. Wanajisikia wamepondwa na mzigo wa namna hii. Wangependa kuwekwa huru kutoka kwa mzigo huo, ila upo nao siku zote, mchana na usiku.

Lakini yupo Mmoja awezaye kutuweka huru kutoka kwa mziço wetu Mzigo wa dhambi na hatia. Mzigo wa makumbukumbu mabaya na masikitiko. Mungu ndiye atakaye kufanya hivi. Mwanaye Yesu amekuja kwetu kwa kusudi hilo hasa. Anangoja tu tuwe tunamgeukia. Pengine, hata ndiye Mwenyewe anayetugeukia akituomba tuukubali msaada wake.

Kama ilivyomtokea mwanamke yule aliyegunduliwa katika kuzini. Aliachwa na mpenzi wake. Sasa wenye kumshtaki wameondoka naye yupo peke yake mbele ya Yesu akiogopa Yesu alimsamehe mwanamke naye alimwachia Yesu mambo yake ya zamani

Sisi vile vile mara nyingi twajisikia tumeachwa tu peke yetu na kuogopa Lakini sisi pia twaweza kusamehewa. Na tukiwa tumesamehewa, Mungu anatu omba tumwachie mambo yetu ya zamani. Lililo Ia maana hasa siyo hayo tuli yosema na kutenda. Lililo a maana ndiyo afanyayo Mungu na hayo atakayotuwe zesha kufanya na sisi wakati ujao

Tukimruhusu Mungu ayashughulikie mambo yetu ya zamani, hapotutajisikia kama Wayahudi. Katika Zaburi ya leo, tumewasikia wakisema: “Bwana alipoture jeza, tulikuwa kama waotao ndoto. Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko.” Jambo tile tile laweza kututokea sisi, ikiwa tutamruhusu Mungu atufanye tuwe wapya kwa msamaha wake.

Maisha mapya - Juma hililija uchukue muda na uone jambo gani maishani mwako ni zito kubebwa. Ujiulize kwa nini unasukuma mzigo huo. Halafu, umgeukie Bwana na umwachie jambo lo lote lenye kukulemeza tangu zamani.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2026


MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2026
JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA


SOMO 1
Dan.13:41-62

Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, akikaa Babeli, naye ameoa mke jina lake Susana binti Helkia, mwanamke mzuri sana na mcha Mungu. Wazee wake nao walikuwa wenye haki, pia wamemfundisha binti yao sawasawa na Torati ya Musa. Basi Yoakimu alikuwa mwungwana tajiri, na karibu na nyumba yake alikuwa na bustani nzuri; hivyo Wayahudi humwendea, maana alikuwa ni mwenye heshima kupita wengineo wote. Mwaka ule ule wakaamriwa wawili miongoni mwa wazee wa watu ili kuamua, watu wa namna ile ambao Bwana aliwanena, ya kama ufisadi ulitoka Babeli kwa wazee waamuzi waliohesabiwa kuwa wanatawala watu. Hao walikuwa wakienda mara nyingi kuzuru kwenye nyumba yake Yoakimu; na wote wenye mashtaka yoyote desturi yao wakawajia huko. Basi watu walipoondoka kwenda zao panapo saa sita, Susana huingia katika bustani ya mumewe ili kutembea. Nao wale wazee humwona kila siku anakwenda kutembea; hata wakawaka tamaa kwa sababu yake. Ndipo walipozipotosha nia zao, wakayageuza upande macho yao wasiweze kutazama mbinguni wala kukumbuka hukumu za haki. Ikawa walipongoja wakati wa kufaa, yeye aliingia bustanini kama ilivyokuwa desturi yake pamoja na wajakazi wawili, naye alitaka kuoga kwa sababu kulikuwa na joto. Wala hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa wale wazee wawili, ambao wamejificha wakimvizia. Basi akawaambia wajakazi wake, Nileteeni mafuta na sabuni, mkaifunge milango ya bustani ili nioge . Mara wale wajakazi walipokwishas kutoka, wale wazee wawili waliondoka wakamwendea mbio, wakasema, Tazama, milango ya bustani imefungwa asiweze kutuona mtu yeyote nasi tunakupenda sana; haya! Basi, utukubali na ulale nasi. La! Hutaki tutakushuhudia ya kuwa hapa palikuwapo na kijana pamoja nawe, ndiyo sababu uliwaruhusu wajakazi wako. Basi Susana aliugua akasema, Nimesongwa pande zote, maana nikilitenda hilo ni mauti yangu; nisipolitenda siwezi kuokoka mikononi mwenu. Ni afadhali niangukie katika mikono yenu na kukataa, kuliko kutenda dhambi machoni pa Mungu. Mara Susana akapiga kelele kwa sauti kuu; nao wale wazee wawili wakampigia kelele pia. Kisha mmoja wao akakimbia, akaifungua milango ya bustani. Hivyo watumishi wa nyumbani waliposikia kelele bustanini, wao waliingia kwa kasi kwa mlango wa nyuma ili waone ni nini iliyompata. Lakini wale wazee waliisimulia hadith yao nao watumishi wakaona aibu kabisa, kwa maana Susana hakuchongelewa habari ya namna hiyo wakati wowote.

Ikawa kesho yake watu walipokusanyika kwa Yoakimu mumewe, wale wazee wawili wakaja nao, wamejaa kusudi lao ovu juu ya Susana la kumfisha. Wakasema mbele ya watu, "Mwiteni Susana binti Helkia, mkewe Yoakim, aje hapa". Basi akaenda kuitwa; naye akaja pamoja na baba yake na mama yake, na watoto wake, na jamaa zake wote. Naye huyo Susana alikuwa mwanamke mwenye adabu, mzuri wa uso; basi hao watu wabaya waliamuru afunuliwe uso, maana alifunikwa utaji, ili washibe uzuri wake. Kwa hiyo rafiki zake na wote waliomtazama wakasikitika. Ndipo wale wazee wawili waliposimama katikati ya watu, wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. Naye akatoka machozi, akatazama juu mbinguni, kwa maana moyo wake ulimtumaini Mungu. Wale wazee wakasema, Sisi tulipokuwa tukitembea bustanini peke yetu, huyu aliingia pamoja na wajakazi wawili, wakaifunga milango ya bustani, naye mara akawaruhusu wajakazi. Kisha kukatokea kijana, ambaye amejificha humo, akamwendea akalala naye. Walakini sisi tungaliko pembeni mwa bustani, tuliona ubaya huo, tukamwendea mbio. Hata tukiwa tumewaona pamoja, yule kijana hatukuweza kumkamata, maana alikuwa mwenye nguvu kuliko sisi, akifungua milango akaepuka. Bali huyu tulimkamata, tukauliza yule kijana yu nani, asikubali kutuambia. Hayo basi, tunashuhudu. Basi waliohudhuria wakawasadiki, wakiwa wazee wa watu na waamuzi; hivyo wakahukumu auawe. Mara Susana akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Mungu wa milele, Wewe wajua yaliyositirika, wajua mambo yote yasijekuwako, Wewe wajua ya kwamba wananishuhudia uongo, na tazama, imenipasa kufa; walakini sikufanya mambo kama hayo, ambayo watu hawa wameyabuni juu yangu kwa ukorofi.

Naye Bwana akaisikia sauti yake. Kwa hiyo, alipochukuliwa huyo kwenda kuuawa, Mungu alimchocheleza roho kijana mmoja, jina lake Danieli; naye akapaza sauti akasema, Mimi simo; mimi sina hatia kwa habari ya damu yake mwanamke huyu. Mara wote wakamgeukia, wakasema, Maneno hayo uyasemayo, maana yake nini? Akasimama katikati, akasema, Enyi bani Israeli, mmekuwa wapumbavu, hata kumhukumu binti Israeli bila kuhoji wala kupata hakika ya kweli? Rudini hukumuni; mradi hao wanamshuhudia uongo.

Basi watu wote walirejea kwa haraka, nao wale wazee wakamwambia, Njoo uketi kati yetu, utujulishe habari hiyo, endapo Mungu amekupa wewe heshima yam zee. Hapo Danieli aliwaambia, Watu hawa wawili watengwe, nami nitawahoji. Basi wakiisha kutengwa, akamwita mmoja wao akamwambia, Ewe uliyepata kuwa mzee katika uovu, sasa dhambi zako zimekukalia, ulizozitenda zamani kwa kuhukumu isivyo haki, kumpatiliza asiye na hatia na kumwachilia mwovu; lakini Bwana asema, Asiye na hatia, mwenye haki, usimwue. Haya! Basi, wewe ulimwona kwa macho; useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya msandarusi. Danieli akasema, Hakika umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana sas hivi malaika wa Mungu amepokea hukumu ya Mungu, akukate vipande viwili. akamtenga huyo tena, akaamuru kumleta yule mwingine, akamwambia, Ewe mzao wa Kanaani, wala si wa Yuda, uzuri umekudanganya, na tamaa imeupotosha moyo wako. Hivyo ndivyo ulivyowafanyia binti za Israeli, na kwa hofu walitembea nawe; bali huyu binti Yuda hakuweza kuustahimili uovu wako. Haya! Basi, nawe useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya mkwaju. Danieli akamwambia, Hakika wewe nawe umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana malaika wa Mungu yu tayari, anakungoja mwenye upanga, akukate vipande viwili; ili awaangamize nyote wawili.

Mara hiyo makusanyiko yote wakapaza sauti kwa nguvu, wakamhimidi Mungu awaokoaye wamtumainio. Wakawaondokea wale wazee wawili, kwa maana Danieli ameuhakikisha ushuhuda wao wa uongo hata vinywani mwao wenyewe. Wakawatenda kwa Torati ya Musa kama vile walivyokusudia kwa ukorofi kumfanyia jirani yao; wakawaua; na mwenye damu isiyo na hatia aliokolewa siku ile.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 23 (K) 4

(K) Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami.

Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza,
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati aya bonde la uvuli wa mauti
Sitaogopa mabaya; kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe change kinafurika. (K)

Hakika wema na fadhili zinanifuata,
Siku zote za maisha yangu,
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)



SHANGILIO
Yn. 6:64, 69

Maneno yako, Ee Bwana, ni roho, tena ni uzima, Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.



INJILI
Yn. 8:1-11

Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni. Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.

Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Basi katiak torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? Nao wakasema neno hili wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki.

Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

WATU WA UFUFUKO



“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumapili, Machi 22, 2026
Juma la 5 la Kwaresima

Eze 37: 12-14;
Zab 130: 1-8;
Rum 8: 8-11;
Yn 11: 1-45.


WATU WA UFUFUKO


Giza, na ukimya, vilifunika kifo kadiri ya tamadunii za Wayahudi. Ni vigumu kupata maelezo kuhusu kutoharibika kwa roho au ufufuko wa wafu katika Agano la Kale. Ayubu alisema “kuna matumaini kwa mti; kama ukikatwa unaweza kuchipua tena, machipukizi mapya yatatokea tena. Lakini mwanadamu anavyokatwa, huanguka chini na huvuta pumzi yake ya mwisho-atakuwa wapi? Maji ya bahari yanaweza kutoweka, mito kukauka, lakini yule anayelala chini hawezi kuamka tena; mbingu zitaisha kabla hajaamka, kabla hajaamka usingizini.” (Ayubu 14:7-12). Biblia ilihifadhi kumbukumbu ya jinsi jambo lilivyokuwa gumu ili kutukumbusha ni kwa jinsi ghani giza lilitisha katika kaburi, kabla ya ufufuko na mwanga wa Pasaka duniani. Lakini pia mzaburi analeta matumaini. “Nijapopita katika giza la mauti, sintaogopa mbaya, kwani wewe Bwana wa uhai utakuwa pamoja nami”

“Kifo” kinaonekana kutisha kwa watu wengi, lakini ni wazi kwamba hakuna kitu tulicho na uhakika nacho katika maisha zaidi ya kifo. Wengi wetu tunazungukwa na hofu, baada ya kifo kuna nini? Wafuasi hawakuwa na tofauti. Hali yote inayo wazunguka inaonekana kutisha, na kwa upande mwingine Yesu anatabiri kuwa kifo chake kipo karibu na kwa upande mwingine wanawaogopa Wayahudi amabao walitaka kumpiga Yesu mawe mpaka afe. Kwa kipindi hichi tunaona jibu laTomasi lilivyo na mashaka “twende na sisi tukafe pamoja naye”. Ni hakika kwamba hofu ya kifo iliwakumba wafuasi. Yesu kwa kumfufua Lazaro kutoka wafu anataka kuwafunulia mitume na watu wengine kwamba yeye ni nani “YEYE NI UFUFUO NA UZIMA”.

Kifo ni nini?
Katika Injili ya leo, Yesu anakwepa kutumia neno ‘kufa’ badala yake anatumia ‘kupumzika’ akionesha kifo cha Lazaro. Kifo kilionekana kuwa ni kitu hasi na pia mwisho wa kitu. Lakini Yesu kwa kutumia neno “kupumzika’ anataka kuwaambia wafuasi kwamba kifo sio mwisho wa kila kitu, bali njia ya kupitia kutoka hali moja kwenda hali nyingine ya maisha. Kifo ni njia ya kupitia kutoka maisha haya ya duniani kuelekea maisha ya milele, njia ambayo imefunguliwa kwa ufufuko wa Yesu.

Ufufuko ni nini?
Wayahudi waliamini kwamba ni Mungu mwenyewe anaweza kurudisha uhai. Yesu anatumia kifo cha Lazaro kuonesha kweli yeye ni mwana wa Mungu, kwa kumfufua kutoka wafu. Lazaro ambaye alikuwa amekufa kwa siku nne, sasa anakuwa hai. Lazaro aliyekuwa amekufa sasa anatembea kutoka kaburini. Wayahudi waliamini kuhusu ufufuo wa wafu lakini ilikuwa mpaka dunia itakapopita. Na hapa wanaona kitu ambacho kina washangaza, mtu ambaye alikuwa amekufa kwa siku nne, anakuwa hai tena. Walio shuhudia waliamini kabisa Yesu sio nabii wa kawaida wala mwalimu wa kawaida bali Mungu mwenyewe. Yesu anaendelea kuonesha kwamba ufufuko sio tukio baada ya kifo, bali linaanza duniani kwa kuishi ukiwa umeunganika na Yesu.

Katika somo la kwanza katika kitabu cha nabii Ezekieli, anatangaza tukio ambalo Mungu anaenda kulitenda, muujiza wa ajabu. Mungu analeta uhai katika mifupa iliokauka. Mungu atafunua makaburi ambayo walikuwa wamefungwa, atawafanya watoke katika makaburi yao na kuwaongoza tena katika Nchi yao. Roho wa Mungu aliingia kila mahali na maisha yakaanza. Yalianza wakati wa mwanzo wa dunia, wakati Mungu anamuumba mwanadamu kutoka mavumbini, alimpulizia pumzi ya uhai na mwanadamu akaishi (Mwa 2:7). Hakuna kinacho shindikana kwa Roho wa Mungu. Anaweza kuleta maisha pia hata katika mifupa iliyo kauka kabisa.

Katika somo la pili, Paulo anatuambia, Yesu akiwa mtu kama sisi, alikufa. Lakini alifufuka. Yesu ana Roho kamili wa Mungu, ni kwamba ana ndani yake uhai wa Kimungu ambao hauwezi kufa. Yesu alikuwa na uhai huu wa Kimungu ndani yake. Roho wa Mungu alimfufua, na kumtambulisha katika utukufu wa Baba. Wale walio batizwa katika roho wake, katika maisha yake, hawafi tena. Maisha yetu katika ulimwengu huu yataisha, yatafika mwisho, lakini haitakuwa mwisho wa kila kitu. Roho aliye mfufua Yesu atatufua na kuipatia uzima wa milele miili Yetu inayo kufa.

Mkristo haamini katika kifo na ufufuko kama kitu ambacho kitatokea mwisho wa dunia. Ana amini kwamba mtu aliyekombolewa na Yesu hafi. Yesu alitangaza kwa Martha kwamba “kila anaye niamini mimi hatakufa kamwe”(Mtari wa 26). Pasaka inakaribia ni majuma mawili tu yajayo, na waliyo wengi tunatazama ufuko kama tukio litakalo tokea baadae. Tunashindwa kuishi kama watu wa ufufuko. Kwaresima inaonekana kama maombolezo, kujinyima, toba, lakini kwa hakika kwaresima ni kipindi cha kujifunza jinsi ya kuishi maisha ya ufufuko. Yesu amekuja kutukomboa sisi, sio tu baada ya kifo chetu bali pia tukiwa hai. Tukiwa na matumaini na tukiishi Imani katika ufufuko tuishi kama watu wa ufufuko kuanzia leo. Na yeye aliyempa Lazaro uhai kwa hakika atatupa sisi uhai, uhai tele.

Sala: Bwana, wewe ni ufufuo na uzima. Nisaidie niondokane a muonekano wangu mbaya kuhusu uzima na kifo. Ninaomba nikuwe katika Imani ya roho wa uzima aliye ndani mwangu. Ninakuomba niweze kutambua Uzima wa Kimungu ndani mwangu. Ninaomba nitoke katika hofu zangu, na kwenda katika maisha ya ufufuo. Yesu, nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.