Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MOYO UNAO WAKA MAPENDO!



⁠⁠⁠⁠⁠“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila Siku
Ijumaa, Juni 12, 2026,
Juma la 10 la Mwaka wa Kanisa

Sherehe ya Moyo Mtakatifu wa Yesu

Kumb 7: 6-11;
Zab 103: 1-4;
1 Yn 4: 7-16;
Mt 11: 25-30


MOYO UNAO WAKA MAPENDO!


“Huu ni upendo si kwamba sisi tulimpenda Mungu kwanza bali yeye alitupenda sisi kwanza akamtuma mwanaye ulimwenguni kama sadaka kwaajili ya dhambi zetu” (1 Yn 4: 10). Sherehe ya Moyo Mtakatifu wa Yesu ni sherehe ya upendo wa ukombozi wa Mungu wetu. Mungu anayetupenda alimtoa mwanaye aje ulimwenguni kama sadaka kwaajili ya ukombozi wa Ulimwengu. Upendo huu unaoneshwa katika moyo wa mwana wa Mungu. Neno “moyo” linasimama kama upendo wa mtu. Na hivyo watu husema “Nakupenda kwa moyo wangu wote” na wakati tunapo sheherekea sikukuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu kanisa linatuhimiza kutafakari juu ya upendo wa Mungu, upendo uliofunuliwa ndani ya mwili wa Mwanaye Yesu Kristo.

Ni Mungu aliyewachagua wa Israeli kuwa watu wake. Aliwabariki na akawachagua kuwa watu wake kati ya mataifa mengi. Si kwasababu walikuwa na nguvu kuliko wengine lakini kwasababu ya upendo wake. Hili ndilo Musa alilowafundisha watu wa Israeli. Anawakumbusha juu ya upendo wa Mungu juu yao. Upendo wa Mungu kwa watu wake hauna mwisho na hauna masharti. Aliwapenda watu wake pamoja na mapungufu yao na makosa yao. Na hata hivyo ubinadamu uliponaswa na dhambi alimtoa mwanaye wa pekee kwajili yetu. Kwahiyo tunapaswa kuuzoea nakuupenda upendo huu ili tuweze kuuelewa zaidi na kuwa watu wakweli wanotamani kuwa na Mungu daima. Ili tuweze kumpenda kwa moyo wetu wote na akili yetu zote.

Kwahiyo katika sikuu hii ya moyo Mtakatifu wa Yesu, tunamshukuru Mungu kwa upendo wake mkubwa kwetu anaotuonesha kila siku. Tuupende na kuushi upendo huu ndani mwetu ili tuweze kuwashirikisha na wengine.

SALA: Moyo Mtakatifu wa Yesu, utuhurumie. Ninakushukuru Bwana wangu kwa kunipa yote hayo. Hakuficha kitu kwangu na unaendelea kunigawia maisha yako kwa ajili yangu na kwa ajili ya ulimwengu mzima. Ninaomba nipokee yote unayonipa bila kubakiza chochote kutoka kwako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 12, 2026




MASOMO YA MISA, JUNI 12, 2026
IJUMAA, JUMA LA 10 LA MWAKA

SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU


SOMO 1
Kum. 7:6 - 11

Musa aliwaambia makutano: Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa Bwana Mungu wako; Bwana, Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.

Bwana hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote; bali kwa sababu Bwana anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu, ndiyo sababu Bwana akawatoa kwa mkono wa nguvu, akawakomboa katika nyumba ya utumwa katika mkono wa Farao, mfalme wa Misri.

Basi, jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu; naye huwalipa wamchukiao mbele ya uso wao, ili kuwangamiza. Hatakuwa mlegevu kwake yeye amchukiaye, atamlipa mbele ya uso wake. Basi zishike amri, na sheria, na hukumu ninazoamuru leo, uzitende.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 103:1 – 4, 6 – 8, 10 (K) 17

(K) Fadhili za Bwana zina wamchao, tangu milele hata milele.

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Naam, vyote vilivyo ndani yangu
Vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Wala usizisahau fadhili zake zote. (K)

Akusamehe maovu yako yote,
Akuponya magonjwa yako yote,
Aukomboa uhai wako na kaburi,
Akutia taji ya fadhili na rehema. (K)

Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki,
Na hukumu kwa wote wanaoonewa.
Alimjulisha Musa njia zake,
Wana wa Israeli matendo yake. (K)

Bwana amejaa huruma na neema,
Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.
Hakututenda sawasawa na hatia zetu,
Wala hakutulipa kwa kadiri ya maovu yetu. (K)



SOMO 2
1Yoh. 4:7 – 16

Wapenzi na tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye. Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. Wapenzi, ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake. Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu. Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu. Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Mt. 11:29

Aleluya, aleluya,
Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu, kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo.
Aleluya.



INJILI
Mt. 11:25-30

Wakati ule Yesu alijibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndiyvo ilivyopendeza mbele zako. Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.

Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

PEANENI MOYO!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Juni 11, 2026 
Juma la 10 la Mwaka

Kumbukumbu ya Mt. Barnaba Mtume.


Mdo 11: 21-26, 13: 1-3; 
Zab 98: 1-6; 
Mt 5: 13-16


PEANENI MOYO!


Barnaba alikuwa mtu muhimu katika kanisa la mwanzo, ingawaje sio mmoja wa wale mitume kumi na mbili aliyokuwa nao Yesu katika karamu ya mwisho, yeye alipata cheo cha mtume. Uwepo wake unaonekana kuwa muhimu katika sura kumi na tano za mwanzo za kitabu cha Matendo ya mitume. Aliuza mali zake zote na akaleta yote kwa mitume (Mdo 4: 37). Alikuwa akijulikana kama Yosefu kutoka Cyprus, lakini mitume walimpa jina la Barnaba ( maana yake mwana wa kutia moyo), ukweli uliopo katika jina hii, aliwatia moyo watu wa Yerusalemu wa mpokee Saulo kwasababu sio tena mtesi wa kanisa baada ya kuongoka (Mdo 9: 27). Wakati idadi kumbwa ya Wasamaria ilipo ongoka nakupokea Ukristo katika Antokia ya Siria, Jumuiya ya Yerusalemu walimtuma kwenda Antokia kuhakikisha na kuangalia hali halisi. Barnaba aliijua neema ya Mungu alipoona na kuwatia moyo jumuiya hii mpya kwa maendeleo mazuri (Mdo 11: 19-26).

Jumuiya ya Antokia waliwachagua Paulo na Barnaba kuwa watu wakwanza kwa safari ya kimisionari, kutoka kati ya “manabii na walimu” ili wafanye kazi ya Roho Mtakatifu (Mdo 13 na 14). Katika utume Barnaba alifuatana na Paulo mtu wa haki. Ingawaje baadae kulikuwa na mgongano kati yao. Waligawa jumuiya walizo zianzisha. Katika hili tunaona ubinadamu kama sisi katika nguvu na madhaifu. Tukijikita wenyewe katika kazi ya Mungu, Roho Mtakatifu atatutumia mpaka mwisho wa kilele cha nguvu zetu, licha ya madhaifu yetu.


Mt. Barnaba anatufundisha kitu katika maisha yetu kama wafuasi wa Kristo, tuwe na moyo wa kushirikisha yale aliyotujalia Mungu pasipo choyo. Tuwe tayari kuwatazama jirani zetu kwa yale aliotujalia Mungu. Barnaba aliuza yote aliokuwa nayo akaleta kwa Mitume ili jumuiya yote ya waumini iweze kufaidika kwa majitoleo yake. Katika jumuiya zetu ndogo ndogo wakati mwingine tunasali pamoja, tunacheka pamoja baada ya sala na kupanga mipango mbali mbali. Pengine tujiulize katika mipango yetu tunapata muda wa kuwajali maskini na wasio jiweza walio kati yetu? Na pengine tumesali nao? Au tunafurahi kucheka nao bila kujali wanaishi je? Na pengine mnapotofautiana katika mawazo mnatafuta njia sahihi ya kurudisha tena upendo kati yenu? Au mnaishi kwakununiana ili mradi nimekuja tuu jumuiya nimeonekana ili na wao waje kwangu kipindi kingine? Ndugu zangu, mipango yetu katika jumuiya zetu isimtenge mtu au kumuona mmoja kati yetu ni bora zaidi ya mwingine. Tufanye yote kwa umoja tukiwajali wale wasio nacho kama jumuiya ya kwanza ya Yerusalemu. Tuwe kama Barnaba tuwafariji wengine na kuona uzuri pia ndani ya wengine, tuwape moyo ili wasikate tamaa. Mungu amatupa vipaji tofauti tuviunganishe vyote kwa pamoja ili vikamilishane vijenge jumuiya yenye nguvu, mmoja asijione kuwa yeye ndio kila kitu. Tushirikiane kwa upendo tukichukuliana kwa furaha na Amani ili ufalme wa Mungu uwe kati yetu.


Sala: Nisaidie mimi Bwana, niwatie moyo na kushirikiana na wenzangu katika kujenga kanisa lako. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, ALHAMISI, JUNI 11, 2026



MASOMO YA MISA, 
ALHAMISI, JUNI 11, 2026
JUMA LA 10 LA MWAKA

KUMBUKUMBU YA MTUME BARNABA


SOMO 1
Mdo 11:21-26, 13:1-3

Watu wengi waliamini, wakamwelekea Bwana. Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Baranaba, aende hata Antiokia. Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote wawaambatane na Bwana kwa kusudi la moyo. Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na Imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.

Kasha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli; hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.

  Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-6 (K) 2

(K) Bwana ameufunua wokovu wake machoni pa mataifa.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Bwana ameufunua wokovu wake,
Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)

Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi,
Kwa kinubi na sauti ya zaburi.
Kwa panda na sauti ya baragumu.
Shangilieni mbele za Mfalme, Bwana. (K)


SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Ee Mungu, tunakusifu, tunakukiri kuwa Bwana.
Jamii tukufu ya mitume inakusifu.
Aleluya.


INJILI
Mt 5:13-16

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

SHERIA YA UPENDO!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Juni, 10, 2026, 
Juma la 10 la Mwaka wa Kanisa

1Fal 18:20-39; 
Zab16: 1-2, 4-5, 8, 11; 
Mt 5:17-19.


SHERIA YA UPENDO!


Katika Injili ya leo, Yesu kwa hakika anawahakikishia wanaomsikiliza kwamba, “hakuja kutengua sheria na manabii. Nimekuja si kutengua bali kuikamilisha”. Yesu alikuja si kuifuta sheria bali aiinue katika hali ya juu ya ukamilifu. Mtazamo wa Yesu unatusaidia tuione sheria katika mwanga mpya. Maneno yake ni kwa ajili ya kufariji lakini pia yanaleta changamoto, akionesha njia inayoenda juu sana kuliko sheria mpaka kwenye sheria ya Upendo. Sheria isiyo na upendo haiwezi kulinda utu na maisha ya mwanadamu. Inamfanya mwanadamu awe kama aina fulani ya kitu kisicho na uhai. Yesu anatutaka tuwe na upendo zaidi. Pengine wakati mwingine tunasisitiza mno sheria kiasi cha kushindwa kuonesha upendo na msamaha kwa wengine.

Katika maisha yetu, tunapaswa kuwa tayari kusonga mbele tukiwa wabunifu wa njia mpya za kuweza kutufanya tuelewe na kuishi Imani yetu zaidi. Tamaduni zetu na mapokeo yetu ni mazuri na tusiyapoteze lakini pia tutumie hali hiyo hiyo katika kuelewa na kuangalia hitaji la sasa. 

Sala: Bwana Yesu, ifanye imani yetu iwe mpya kila siku katika mwanga wa sheria zetu na mapokeo yetu na katika njia ya sheria ya Upendo. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 10, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 10, 2026
JUMATANO, JUMA LA 10 LA MWAKA


SOMO 1
1 Fal. 18:20-39

Ahabu akapeleka watu kwa wana wa Israeli wote, akawakusanya manabii pamoja katika mlima wa Karmeli. Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasitasita katikati ya mawazo mawili hata lini? Bwana akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno.

Ndipo Eliya akawaambia watu, Mimi nimesalia, mimi peke yangu, nabii wa Bwana; lakini manabii wa Baali ni watu mia nne na hamsini. Kwa hiyo na watutolee ng’ombe wawili; wao na wajichagulie ng’ombe mmoja, wamkatekate na kumweka juu ya kuni, wasitie moto chini; name nitamtengeza huyo ng’ombe wa pili, na kumweka juu ya kuni, wala sitatia moto chini. Nayi ombeni kwa jina la mungu wenu, name nitaomba kwa jina la Bwana; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu. Watu wote wakajibu wakasema, Maneno haya ni mazuri.

Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng’ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini. Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya. Ikawa, wakati wa adhuhuri, Eliya akawafanyia dhihaka, akasema, Mwiteni kwa sauti kuu; maana ni mungu huyo; labda anazungumza, au ana shughuli, au anasafiri, au labda amelala, sharti aamshwe. Wakapiga kelele, wakajikatakata kwa visu na vyembe kama ilivyo desturi yao, hata damu ikawachuruzika. Ikawa, wakati wa adhuhuri ulipopita, walitabiri hata wakati wa kutoa dhabihu ya jioni; lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu, wala aliangalia.

Kisha Eliya akawaambia watu wote, nikaribieni mimi. Watu wote wakamkaribia. Akaitengeneza madhabahu ya Bwana iliyovunjika. Eliya akatwaa mawe kumi na mawili, kwa hesabu ya kabila za wana wa Yakobo, aliyejiliwa na neno la Bwana na kuambiwa, Jina lako litakuwa Israeli. Naye akaijenga madhabahu kwa mawe hayo katika jina la Bwana; akafanya mfereji, kama wa vipimo viwili vya mbegu, ukiizunguka madhabahu. Kasha akazipanga zile kuni, akamkata yule ng’ombe vipande vipande, akaviweka, juu ya kuni. Akasema, Jazeni mapipa manne maji, mkayamwage juu ya sadaka ya kuteketezwa, juu ya kuni. Akasema, Jazeni mapipa mnne maji, mkayamwage juu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya kuni. Akasema, Fanyeni mara ya pili. Wakafanya mara ya pili. Akasema, Fanyeni mara ya tatu. Wakafanya mara ya pili. Akasema, Fanyeni mara ya tatu. Wakafanya mara ya tatu. Yale maji yakaizunguka madhabahu; akaujaza mfereji maji.
Ikawa, wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, Eliya nabii akakaribia, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo ya kuwa wewe ndiwe Mungu katika Israeli, nay a kuwa mimi ni mtumishi wako, nay a kuwa nimefanya mambo haya yote kwa neno lako. Unisikie, Ee Bwana, unisikie, ili watu hawa wajue ya kuwa wewe, Bwana, ndiwe Mungu, nay a kuwa wewe umewageuza moyo wakurudie.
Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji. Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 16:1-2, 4-5, 8-11 (K) 1

(K) Mungu, unihifadhi mimi, kwa maana nakukimbilia Wewe.

Mungu, unihifadhi mimi, 
Kwa maana nakukimbilia Wewe.
Nimemwambia Bwana, ndiwe Bwana wangu,
Sina wema ila utokao kwako. (K)

Huzuni zao zitaongezeka
Wambadilio mungu kwa mwingine;
Sitazimimina sadaka zao za damu,
Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu. (K)

Bwana ndiye fungu la posho langu,
Na la kikombe changu;
Wewe unaishika kura yangu.
Nimemweka Bwana mbele yangu daima,
Kwa kuwa yako kuumeni kwangu sitaondoshwa. (K)

Utanijulisha njia ya uzima,
Mbele za uso wako ziko furaha tele.
Na katika mkono wako wa kuume,
Mna mema ya milele. (K)


SHANGILIO
Zab. 27:11

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unifundishe njia yako, na kuniongoza katika njia iliyonyoka.
Aleluya.


INJILI
Mt. 5:17-19

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, mpaka mbingu nan chi zitakapoondoka, yodi moja wala nukata moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

CHUMVI NA MWANGA

 

ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Jumanne, Juni 9, 2026,
Juma la 10 la Mwaka


1 Fal 17: 7-16;
Zab 4: 1-4,6-7;
Mt 5: 13-16

CHUMVI NA MWANGA
 
Yesu anawaambia Wafuasi wake: ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Ninyi ni mwanga wa ulimwengu. Maneno haya ni utangulizi wa maneno ambayo Yesu atayasema katika hutuba ya mlimani. Wafuasi wa Yesu wanatakiwa maneno ya Yesu yapenye ndani yao, ya watawale na wayaishi.

Katika Agano la Kale, WaisraelI walipewa Amri kumi na Agano likafanywa kati yao likiwataka waishi kitakatifu na kwa haki kama wanavyotakiwa na Agano. Je, walitambua wao ni chumvi ya ulimwengu?. Walisisitiza sana kuhusu sheria, mpaka wakaua ile roho. Yesu anaonesha hili kwa wafuasi wake kwakuwaambia, wema wao usipozama ndani nakuushinda ule wa Walimu wa sheria na Mafarisayo, hawawezi kuwa chumvi ya ulimwengu. Yesu aliwataka Wafuasi wake wawe chumvi ya ulimwengu, si kwakusimama na kuonekana kama watakatifu machoni pa watu bali kwa maadili mema na utu ambao umevishwa taji ya upendo kwa Mungu na kwa jirani. Kwa wema, maadili na utu huu uliovishwa taji, na kungarishwa na Imani, matumaini na mapendo, wakristo wanaalikwa kuwa mwanga wa Ulimwengu. Hawahitaji kujitangaza kwamba wao ni Wakristu. Wataonesha kwamba wao ni Wakristo “kwanjia hii wote watajua ya kuwa ninyi ni wafuasi wangu, kama mna pendana ninyi kwa ninyi” (Yn 13: 35).

Kama tunavyoweza kufikiri mlo bila chumvi, au kupotelea msituni wakati wa usiku, tutatambua ni kitu ghani Yesu anatuambia. Kiasi kidogo cha chumvi au kiasi kidogo cha mwanga kina badili kila kitu. Mt. Fransisko wa Assis anatuambia giza lote la ulimwengu mzima haliwezi kuzima hata mwanga wa mshumaa mmoja. Ulimwengu tunaoishi upo gizani katika hali mbali mbali. Mungu anatuita mimi na wewe tuweze kuwa chumvi na mwanga na kuwaonesha watu njia. Mungu anataka kungara kupitia wewe na mimi, na anakutaka wewe uangaze. Jukumu letu ni kuwa wawazi.

Sala: Bwana, ninataka kutumiwa na wewe. Ninataka kuwa chumvi na mwanga. Ninataka kufanya mabadiliko ulimwenguni. Ninajitoa kwako kwa huduma yako. Yesu, ninakuamini wewe. Amina.

------------------------
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUNI 9, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 9, 2026
JUMANNE, JUMA LA 10 LA MWAKA


SOMO 1 
l Fal. 17:7-16

Baada ya siku kupita, kite kijito kikakauka, kwa sababu mvua haikunya katika nchi. Neno la Bwana likamjia Eliya, kusema, Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe. Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa.

Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi
mwako. Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili nilngie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.

Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ilc chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi.

Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya.



WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 4 :1-4, 6-7 (K) 6

(K) Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; 
Umenifanyizia nafasi wakati wa shida;
Unifadhili na kuisikia sala yangu.
Enyi wanadamu,
hata lini utukufu wangu utafedheheka? (K)

Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa;
Bwana atasikia nimwitapo.
Mwe na hofu wala msitende dhambi,
Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. (K)

Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mcma?
Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.
Umenitia furaha moyoni mwangu,
Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai. (K)


SHANGILIO 
Zab. 27:11

Aleluya, alcluya, Ee Bwana, unifundishe njia yako, na kuniongoza katika njia iliyonyoka. Aleluya.


INJILI
Mt. 5:13-16

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

HERI WALIO…..!




“ASALI ITOKAYO MWAMBENI”
Tafakari ya kila Siku
Jumatatu, Juni 8, 2026
Juma la 10 la Mwaka


1 Fal 17 :1-6;
Zab 121: 1-8;
Mat 5: 1-12


HERI WALIO…..!

Yesu leo anaanza mazungumzo yake kwa maneno ya pekee ya heri. Zipo heri nane, kila moja ikianza kwa “heri walio..”. Yesu anatumia neno hili la heri ambalo kwa Kigirini ni Makarios ambalo ndani yake halibebi tuu furaha bali linabeba neno bahati nzuri ya kupata baraka maalumu. Kwahiyo tunaweza kusema, “heri walio…” au “Wanabahati kweli walio….”

Ufalme wake ni ufalme uliojaa huruma na msamaha. Na kama tutakavyokuwa tayari kuwasamehe wenzetu tutajikuta pia wenzetu wanatusamehe tunapo wakosea. Katika sala ya Bwana, ambayo ni sala ya Ufalme, huwa tunaomba hili, “tusamehe dhambi zetu kama na sisi tunavyo wasamehe waliotukosea”. Kwa kawaida ni vigumu sana kwa wale walio katika ufalme huu kutokusamehe, wao kawaida ni wepesi kusamehe na kukaribisha amani. Hii haimaanishi kwamba tuwatendee kila ubaya. Haki pia lazima iwepo. Kupinga na kukataa uovu haina maana ya kuacha kusamehe na kuponya vidonda vilivyo sababishwa na wengine.

Na huruma inayoeleweka katika nyanja ya kujali wengine ndio inayojenga Ufalme huu ndani ya mtu. Mtu huyu sio kwamba anaona huruma kwa wanaoteseka tuu bali anajua pia jinsi yakujiingiza katika matatizo ya wengine na kuhuzunika nao katika hali yao. Hii ndio sifa aliokuwa nayo Yesu katika hali zote. Aliingia katika maisha ya watu na kukaa nao na kuleta furaha na matumaini mapya.

Sala: nisaidie niweze kuwa mpole na mwenye huruma, maskini wa roho, mwenye kuleta Amani na mtu mwenye kukubali mateso. Nisaidie mimi niweze kupokea kwa shauku na kwa furaha ufalme wako. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2026



MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2026
JUMATATU, JUMA LA 10 LA MWAKA


SOMO 1 
1 Fal. 17 :1-6

Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.

Neno la Bwana likamjia, kusema, Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani. Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko. Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani. Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 121:1-8 (K) 2

(K) Msaada wangu u katika Bwana, aliyezifanya mbingu na nchi.

Nitayainua macho yangu niitazamc milima;
Msaada wangu utatoka wapi?
Msaada wangu u katika Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi. (K)

Asiuache mguu wako usogezwe;
Asisinzie akulindaye;
Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,
Yeye aliye mlinzi wa Israeli. (K)

Bwana ndiye mlinzi wako;
Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.
Jua halitakupiga mchana,
Wala mwezi wakati wa usiku. (K)

Bwana atakulinda na mabaya yote,
Atakulinda nafsi yako.
Bwana atakulinda utokapo na uingiapo,
Tangu sasa na hata milele. (K)


SHANGILIO 
Zab. 119:34

Aleluya, aleluya, Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote. Aleluya.


INJILI
Mt 5:1-12

Yesu alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia; akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema, 

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.
Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.
Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.
Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.
Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com