Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MAISHA YETU YANATOKA KWA KRISTO!

 


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Aprili 24, 2026
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 9:1-20;
Zab 117:1-2 (K. Mk 16:15);
Yn  6:52-59.


MAISHA YETU YANATOKA KWA KRISTO!


Mt. Paulo ambaye tunamsikia katika somo la kwanza la leo alikuwa mtu mwenye Elimu ya juu/ busara aliyesoma chini ya mwalimu mkuu Gamaliel. Uongofu wake wa ghafla ulitokea  barabarani akielekea Dameski. Paulo ambaye alikuwa na mambo mengi, lakini akikosa jambo muhimu zaidi ambalo alilipata kupitia ndani ya tukio hili la wongofu. Alimpata Yesu Kristo. Baada ya uzoefu huo Paulo anatangaza, "Kwangu mimi, kuishi ni Kristo"; kama nilivyo, maisha ni Yesu Kristo" au "Naweza kufanya  yote katika Yeye anitiaye nguvu." "Naishi sasa si kwa maisha yangu mwenyewe bali kwa maisha ya Kristo anayeishi ndani yangu."

Mara baada ya Paulo kukutana na Yesu, maisha yake hayakubaki kamwe jinsi yalivyo kuwa mwanzo. Alibadilika kabisa. Alikuwa kiumbe kipya katika Kristo. Nasi pia tunampokea Kristo katika Ekaristi Takatifu. Ni kwa kiasi gani Ekaristi inabadilisha maisha yetu? Ni kwa kiasi gani najitoa mwenyewe kwa Kristo pale anapojitoa mwenyewe kwangu?

Katika somo la Injili, Yesu anasema “msipo ula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake hamna uzima ndani yenu”. Wengi wao walichukizwa na kuanza kuuliza uliza juu ya maneno yake. Inavutia kwamba wakati Yesu anapokutana na maneno makali ya wengine, anajibu tena kwa ujasiri mkubwa zaidi na uwazi zaidi. Hili linamuonesha kuwa mtu wa ujasiri mkubwa, mwenye nguvu na kuelewa. Unafunua pia kwetu sisi ujasiri ambao sisi tunapaswa kuwa nao katika ulimwengu huu. Ulimwengu tunaoishi ni ulimwengu unao kataa ukweli. Unakataa ukweli wa maadili, lakini pia unapinga ukweli wa ndani wa kiroho pia. Ukweli huu wa ndani ni kama uwepo wa uzuri wa Ekaristi Takatifu, umuhimu wa sala za kila siku, unyenyekevu, na kumtegemea Mungu, kuweka mapenzi ya Mungu mbele kuliko kitu chochote nk. Tunapaswa kutambua kuwa kila mara tunapo sogea karibu zaidi na Mungu, ndivyo tunavyozidi kujikabidhi kwake zaidi, na tutakapo hubiri ukweli wa Mungu ndivyo tunavyo upa ulimwengu shinikizo uache kutuiba kutoka kwa Mungu.

Sasa tufanye nini? Tunajifunza kutoka katika ujasiri na nguvu ya Yesu. Tunapojikuta sisi wenyewe tukiwa katika changamoto au tunapo hisi kana kwamba Imani yetu inashambuliwa, ndivyo tunavyo takiwa tuzame ndani zaidi na kuwa waaminifu zaidi na zaidi. Hili litatufanya tuwe na nguvu zaidi na kufanya vishawishi vinayokuja kuwa nafasi ya neema! Chagua kuiga ujasiri na ushupavu wa Bwana wetu na utakuwa chombo chenye kuonekana cha neema na huruma.

Sala: Bwana, ninaomba unipe ujasiri wa nguvu zako . Ninaomba unipe mwangaza katika utume wangu na unisaidie kukutumikia kiaminifu katika kila kitu. Ninaomba nisiwe muoga ninapo kutana na changamoto za maisha bali nitazame hamu yangu ya kukutumikia kwa moyo wangu wote. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 24, 2026





MASOMO YA MISA, APRILI 24, 2026
IJUMAA, JUMA LA 3 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 9:1-20

Siku zile, Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kwenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.

Hapo alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda. Na wale watu waliosafiri pamoja naye wakasimama kimya, wakiisikia sauti, wasione mtu. Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.

Basi palipokuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.

Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu; hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maan ahuyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu. Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani, akamwekea mikono akisema, Ndugu, Sauli, Bwana amenituma, Yesu yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu. Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa, akala chakula, na kupata nguvu.

Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski. Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 117 (K) Mk. 16:15

(K) Enendeni ulimwenguni mwote,
mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

Enyi mataifa yote, msifuni Bwana,
Enyi watu wote, mhimidini. (K)

Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu,
Na uaminifu wa Bwana ni wa milele. (K)



SHANGILIO
Rum. 6:9

Aleluya, aleluya,
Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Aleluya.



INJILI
Yn. 6:52-59

Siku ile, Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule?

Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.

Maneno hayo aliyasema katika sinagogi, alipokuwa akifundisha, huko Kapernaumu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KUVUTWA KWA YESU!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Aprili 23, 2026
Juma la 3 la Mwaka

Mdo 8:26-40;
Zab 66:8-9,16-17,20 (K. 1);
Yn 6:44-51.


KUVUTWA KWA YESU!

Karl Rahner anasema, “kila ninapo ongea kuhusu mimi najikuta nikiongelea kuhusu Mungu, na kila ninapo ongelea kuhusu Mungu najikuta naongea kuhusu mimi”. Safari ya maisha yetu pia karibia ni kuvuta kila kitu na kila mtu kwangu. Katika ulimwengu huu ambao kila mtu yupo na shughuli zake ni rahisi sana kuruhusu sauti mbali mbali zituharibu. Ni rahisi kusikia kusukumwa huku na kule katika ulimwengu na mambo yake yote. Ulimwengu umekuwa mzuri sana ukiteka mipango yetu yote na kutupatia kuridhika kwa haraka lakini utatuacha bila kitu.

Lakini sauti ya Mungu na mwaliko wake ni tofauti. Unapatikana katika ukimya wa ndani. Lakini haina maana kwamba unapaswa kuwa katika monasteri ili kupata ukimya huu wa ndani. Unapatika katika uaminifu mkubwa katika sala kila siku, na tabia ya kurudi kwa Mungu kila wakati katika vitu vyote. Unapatikana tunapo jibu wito wa Mungu, na kuifuata, na kurudia tena kila mara. Hili linajenga tabia ya kuvutwa karibu, kusikia, na kuitika na kuvutwa karibu na kusikiliza na kuitika tena na tena.

Katika Injili ya leo, tunatambua kuwa tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, na tunavutwa daima kwa Mungu. Ndani kabisa mwa moyo wa Mwanadamu, ana mtamani Mungu. Ndio maana Yesu anasema wazi kwamba “hakuna ajaye kwangu asipovutwa na Baba yangu” (Yn 6: 44). Katika somo la kwanza tunamuona Ofisa wa Ethiopia wakati akisoma chuo cha nabii Isaya, anakutana na ukweli katika Maandiko Matakatifu kwa msaada wa Filipo, na baadae anamkubali Yesu kama Mkombozi na Bwana.

Tutenge muda tuvutwe kwa Yesu. Tenga muda mchache au zaidi kila siku wa ukimya. Funga macho na jisikilize. Msikilize Mungu akiongea na wewe. Wakati akikuvuta kwake itika kwa ukarimu. Huu ndio uchaguzi mzuri kabisa ambao waweza kufanya kila siku!

Sala: Bwana, naomba univute karibu ili niweze kutambua sauti yako. Ninapo kusikia ukiita, nisaidie niweze kukuitikia kwa ukarimu. Maisha yangu ni yako, Bwana mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 23, 2026




MASOMO YA MISA, APRILI 23, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 3 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 8:26-40

Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa. Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu, akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya. Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo. Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma? Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye. Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake. Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine? Filipo akafunua kinywa chake, naye, akakianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Lakini Filipo akaonekana katika Azoto, na alipokuwa akipita akahubiri Injili katika miji yote, hata akafika Kaisaria.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 66:8-9, 16-17, 20 (K) 1

(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote.

Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu,
Itangazeni sauti ya sifa zake;
Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai,
Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe. (K)

Njoni sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Nalimwita kwa kinywa changu,
Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulinzi wangu. (K)

Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu;
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)



SHANGILIO
Yn. 20: 29

Aleluya, aleluya,
Wewe Toma, umesadiki kwa kuwa umeniona, wa heri wale wasioona, wakasadiki.
Aleluya.



INJILI
Yn. 6:44-51

Yesu aliwaambia Wayahudi: Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho. Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.

Si kwamba mtu amemwona Baba, ila yeye atokaye kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba. Amin, amin, nawaambia, Yeye aaminiye yuna uzima wa milele.

Mimi ndimi chakula cha uzima. Baba zenu waliila mana jangwani; wakafa. Hiki ni chakula kishukacho kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

JE, MATESO YANA KUVUNJA MOYO?




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Aprili 22 2026
Juma la 3 la Pasaka


Mdo 8:1-8;
Zab 66:1-7 (K. 1);
Yn 6:35-40.


JE, MATESO YANA KUVUNJA MOYO?


Kifo cha Stefano ni mwanzo wa mateso kwa jumuiya ya Kikristo. Lakini mbali na kujaribu kuupunguza ujasiri wa wanafunzi wa Yesu, kifo cha Stefano kinatia chachu na nguvu ya kuendelea kuhubiri. Kutawanyika kwa Wakristo kulikuwa na maana ya kuhubiri neno la Mungu sehemu mbali mbali na sio kukimbia kwa sababu ya hofu.

Injili ya leo inaendelea kufundisha jinsi gani Ekaristi itafanya kazi, ina maana gani, na kuna umuhimu gani kwa mpokeaji wa sakramenti kama anataka imsaidie. “hakuna hata mmoja atakaye kuja kwangu atakayeona njaa au kuona kiu” Yesu alisema. Lakini watu walikuwa na ugumu wakumuamini Yesu analalamika kwa upole “Ingawaje mmeniona hamtaki kuamini”. Sio kwamba walikuwa wamemuona tu bali walikuwa wameshaona mambo wakuu aliokuwa ametenda, kutembea juu ya maji, kuongeza mikate na samaki, kuwaponya wagonjwa na kufufua wafu. Lakini Yesu hakatishwi tamaa na mtu. Anawahakikishia; Yote alionipa Baba yatakuja kwangu, hakuna ambaye atakuja kwangu nimkatae. 

Maneno ya Yesu ni muhimu kwani yanatuhakikishia sisi kwamba ni wakuaminika. Ni kweli kwamba tunaweza kuja kwake na kumuamini yeye, kumkabidhi mioyo yetu, yeye atatutendea vyema, kutujali na kututunza. Yesu anauwezo wakutujali zaidi ya hata sisi tunavyojijali wenyewe. Tunapokumbwa na dhoruba tusikate tamaa na kuogopeshwa na majaribu tukashindwa kumwamini.

Mt. RosemarĂ­a Escriva anasema, "dhoruba ya mateso ni nzuri. Ina hasara gani? Kwani jambo ambalo limekwisha kupotezwa haliwezi kupotezwa tena. Mti ukiwa na mizizi iliyojishika chini sana, hakuna upepo uwezao kuungoa mti wa Kanisa, labda tu matawi yake makavu yataanguka”. Basi leo tuangalie maisha yetu kama tu matawi mabichi yaliojishika na kanisa au makavu yategemeayo kuanguka kutoka mtini muda wowote kutokana na upepo!

Sala: Ee Bwana, Utusaidie kuishuhudia Injili na kukubali mateso yoyote yatokanayo na shughuli hiyo. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 22 2026



MASOMO YA MISA, 
APRILI 22 2026
JUMA LA 3 LA PASAKA, JUMATANO

SOMO 1
Mdo 8:1-8

Siku ile kulitukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. 

Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu. Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.

Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno. Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo. Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifanya. Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na watu wengi waliopooza, na viwete wakaponywa. Ikawa furaha kubwa katika mji ule.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 66:1-7 (K) 1

(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote.

Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote, 
Imbeni utukufu wa jina lake,
Tukuzeni sifa zake.
Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini. (K)

Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, 
Naam, italiimbia jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu;
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)

Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tulikomfurahia.
Atawala kwa uweza wake milele;
Macho yake yawaangalia mataifa;
Waasio wasijitukuze nafsi zao. (K)



SHANGILIO
Yn. 10:27

Aleluya, aleluya,
Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata.
Aleluya.



INJILI
Yn. 6:35-40

Yesu aliwaambia: Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe. Lakini naliwaambia ya kwamba mmeniona wala hamwamini. Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe. Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka. Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmjoja, bali nimfufue siku ya mwisho. Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com