Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 3, 2026
Juma la 5 la Pasaka


Mdo 6: 1-7;
Zab 32: 1-5, 18-19;
1 Pet 2: 4-9;
Yn 14: 1-12.


MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA


Je umekombolewa? “ndio” tumekombolewa kwa njia tatu: tumekombolewa kwa njia ya neema ya Ubatizo, tunaendelea kukombolewa kwa njia ya neema za Mungu na huruma tunapo amua kumfuata kwa uhuru kamili, na tunatumaini kokombolewa na kuingia katika utukufu wa Mbinguni.

Imekuwaje tumepokea zawadi ya thamani ya ukombozi? Kwa njia ya maisha, mateso kifo na ufufuko wa Yesu Kristo ambaye ndiye pekee aliye njia ya kwenda kwa Baba. Njia pekee ya Ukombozi ni Yesu. Hivyo Yesu Kristo anapaswa kuwa kiini cha maisha yetu, na tunapaswa kumuona kama njia, ukweli na uzima. Yeye ni njia pekee ya Mbinguni, yeye ni utimilifu wa ukweli wote ambao tunapaswa kuuamini, na yeye ni uzima ambao tunapaswa kuuishi na yeye ndiye chanzo cha maisha mapya ya neema. Bila yeye sisi si kitu, bali kwa njia yake unapata maisha makamilifu.

Katika somo la pili, Petro analifananisha Kanisa na jengo la kiroho ambalo mjenzi ni Mungu na mawe yanayoishi ni watu. Msingi ulianza kwa mawe imara kwa jengo lote, Kristo ambaye juu yake Mungu ameweka pia mawe mengine, wale wanao mwamini yeye. Wakiwa wameunganika na Yesu, wanatengeneza hekalu moja la Mungu.

Injili inamuonesha Yesu kama kielelezo cha maisha ‘njia, ukweli na uzima’. Kiini cha ukristo ni Kristo mweyewe. Kazi yetu kwa Yesu na upendo wetu kwa watu, haijalishi tumeitwa katika maisha ya namna ghani, maisha yetu yanatiririka kutoka katika chanzo hiki. Mama Teresa aliulizwa kwanini alifanya aliokuwa akifanya, na alijibu tu “ni kwa ajili ya Yesu”. Hiki ndicho kiini kinacho shikilia ili kusiwe na mtikizo au usumbufu wowote. Ni muunganiko wa ndani na Yesu. Kusoma maisha yake, kupata muda wa kutambua mazingira yake na matukio ya maisha yake, kuwa familia na Injili na kumfahamu katika moyo wa sala, njia yetu ya kuweka msingi wetu na ujasiri wetu kuwa imara kwa Yesu. Hivyo mchague yeye katika hali zote za maisha kama Bwana wako na mkombozi. Kwa unyenyekevu jitambue kuwa bila yeye wewe si kitu, na jikabidhi kwake ili yeye aweze kukuongoza salama kwa Baba yetu wa mbinguni.

Sala: Bwana na Mkombozi, ninakukubali wewe katika maisha yangu kama Bwana na Mkombozi. Ninakushukuru kwa zawadi ya ubatizo iliyo anzisha maisha ya neema ninaomba nibadilishe maisha yangu niendelee kukufuata kikamilifu, leo na siku zote, ili uweze kuingia zaidi ndani ya maisha yangu. Ninaomba matendo yangu yote yaongozwe nawe ili niweze kuwa sadaka ilyio unganika na wewe milele, Yesu mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026


MASOMO YA MISA, MEI 3, 2026
JUMAPILI, JUMA LA 5 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3

(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)


SOMO 2
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 14 : 6

Aleluya, aleluya,
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14: 1-12

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia, maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaa ndalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendakt mwaijua njia. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia? Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MUNGU KUDHIHIRIKA NDANI YA MAISHA YETU!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Mei 2, 2026
Juma la 4 la Pasaka


Mdo 13:44-52;
Zab 98:1-4 (R. 3);
Yn 14:7-14.


MUNGU KUDHIHIRIKA NDANI YA MAISHA YETU!


Mara nyingi, hatujui ni kwa jinsi ghani Mungu anajifunua mwenyewe katika maisha yetu kama Filipo, anayetaka kumuona Baba. Alikuwa mbele ya Yesu, na bado anamtafuta Mungu. Sisi pia katika maisha yetu. Mungu yupo nasi daima lakini kwasababu ya mawazo yetu na mitizamo yetu tunamtafuta. Sisi nasi tunamtafuta Mungu na baadae tuna mtambua Yesu mbele yetu.

Paulo na Baranabas walitambua utambulisho wa kweli wa Yesu na wanamhubiri kwa ujasiri mkubwa, kwa mataifa licha ya mateso na vipingamizi. Kama sisi tunajiita wakristo, Kristo anapaswa kudhihirika katika maisha yetu. Kama kumuona Yesu ni kumuona Mungu Baba ni wazi kwa matumaini na katika sala, kutuona sisi ni kumuona Yesu pia.

Injili ya Yohane inatumia lugha hii mara nyingi kuonesha umoja mkamilifu wa Yesu na Baba yake. Ni jambo zuri namna ghani sisi nasi kusema sisi hatuseme wenyewe bali ni Kristo anasema ndani yetu? Hili ndilo linalopaswa kuwa lengo letu la kila mara. Kama tutaongea maneno kwa wengine, tukiwa tumejikita katika hekima yetu wenyewe na uelewa wetu wenyewe, ni lazima tuji nyenyekeshe na kutambua kwamba maneno yetu hayawezi kuwa na nguvu. Lakini kwa upande mwingine, lakini kama tunaweza kusema maneno yaliyo jaa Kristo, maneno ambayo yanasemwa kutoka ndani ya moyo wake, tutaanza kuona maneno hayo yanakuwa na manufaa katika maisha ya watu. Maneno yana maana sana, na tunapaswa kuwa makini katika kuongea na kuwa na ujasiri na kile tunachosema, jinsi ya kusema na tunasemaje. Kumruhusu Baba aongee ndani mwetu na kupitia sisi maneno yetu yanakuwa na ujasiri na nguvu. Yanakuwa maneno ambayo Mungu alitaka kuongea kwa wengine ambayo yanamfanya Mungu afanye mabadiliko katika maisha yao.

Sala: Bwana, nipe maneno yako ya kuongea. Nisaidie mimi nikurudie wewe ndani ya moyo wangu kwa ujasiri ili uweze kuwa chanzo cha ukweli na uzuri. Ninaomba ukweli huo utoke ndani mwangu kila siku. Ninaomba wote wakuone wewe kwa njia ya maisha yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 2, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 2, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 4 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 13:44-52

Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,

Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.

Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3

(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)

Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)



SHANGILIO
Rum. 6:9

Aleluya, aleluya.
Kristo akiisha kufufuka katika wafu, hafi tena wala mauti haimtawali tena.
Aleluya.



INJILI
Yn. 14:7-14

Yesu aliwambia wanafunzi wake: Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.

Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.

Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Minisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MT. YOSEFU MFANO WA WAFANYA KAZI





“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Mei 1, 2026.
Juma la 4 la Pasaka

Kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi


Mwa 1:26-2:3; 
Zab 90:2-4, 12-14, 16 (K. 17);
Mt 13:54-58.


MT. YOSEFU MFANO WA WAFANYA KAZI


Injili  ya leo inaongelea kuhusu lile kundi la watu wanaomtafuta Yesu, siku baada ya kuongeza ile mikate. Kumtafuta huku haikuwa kwasababu ya upendo kwake, bali kufaidika kutoka kwake. Yesu, anawaambia wazi kwamba wanamtafuta kwasababu walikula mikate, Yesu anawaeleza wawe na lengo lingine la kumtafuta. Sababu iwe ni kwasababu anataka kuwapa chakula cha kiroho.

“Je, unamtafuta Yesu kwasababu njema?” pengine mara nyingi tunamtafuta Yesu kwasababu ya faida fulani, pengine ili kupata gari, nyumba, mchumba, uponyaji wa ugonjwa. Yesu anatuonya tuangalie tusimtafute kwasababu ya vitu vinavyo haribika tu, bali tutafute uzima wa milele.

Kanisa leo lina adhimisha kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi. Mungu alimwamini na kumpa jukumu la kumtunza Mama wa Mungu na Mwana wa Mungu, na kuwa mlinzi wa nyumba ya Mungu. Hakuna mtu mwingine yeyote aliyekuwa na nafasi hii pekee. Kupenda kwake kazi ilionesha unyenyekevu wake, aliishi kwa kadiri ya matakwa ya Mungu. Alikuwa mtu mwenye haki. Kilicho mfanya akubalike machoni pa Mungu ilikuwa kwasababu ya Imani yake na utii wake. Kujitoa kwake kulionesha unyenyekevu na kumtegemea Mungu. Na hata baada ya kupata upendeleo kutoka kwa Mungu, hakuacha kufanya kazi.

Katika hali hii tunaweza kusema kwamba yeye ni somo wa wale wote wanaofanya kazi, kazi ambayo ni kuonesha unyenyekevu na tegemeo letu kwa Mungu. Leo tunawakumbuka watu wote duniani wanao fanya kazi kwa manufaa ya uzuri wa wanadamu wote. Tuwaombee kazi zao zisiharibu mpango wa Mungu kwa mwanadamu bali zilinde utu na uhai wa kila mwanadamu kama Mt. Yosefu alivyo linda uhai wa Yesu dhini ya Herode.

Sala: Asante, Mt. Yosefu kwa kumfundisha Yesu kufanya kazi yako. Tunakushukuru kwa kuzipa kazi za mikono thamani na utakatifu. Tunaomba tuweze kuzipa heshima kazi na kuwa tayari kwa ajili ya wengine kama wewe. Mt. Yosefu, mlinzi wa nyumba ya Mungu. Utuombee.



Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com


MASOMO YA MISA, MEI 1, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 1, 2026
IJUMAA, JUMA LA 4 LA PASAKA,

KUMBUKUMBU YA MT. YOSEFU, MFANYAKAZI

SOMO 1
Mwa. 1 : 26-2 : 3

Mungu alisema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu; kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote. Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 90:2-4, 12-14, 16 (K) 17

1. Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba duma,
Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.

(K) Kazi ya mikono yetu uithibitishe, Ee Bwana.

2. Wamrudisha mtu mavumbini,
Usemapo, Rudini, enyi wanadamu.
Maana miaka elfu machoni pako
Ni kama siku ya jana ikiisha kupita,
Na kama kesha la usiku. (K)

3. Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu,
Tujipatie moyo wa hekima.
Ee Bwana, urudi, hata lini?
Uwahurumie watumishi wako. (K)

4. Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako,
Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote. 
Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako.
Na adhama yako kwa watoto wako. (K)



INJILI
Mt. 13:54-48

Yesu alipofika nchi yake, akawafundisha maku tano katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe. Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Neno la Bwana
Sifa kwako Ee Kristo



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

TUME BAHATIKA KUWA “WATUMWA”



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Aprili 30, 2026.
Juma la 4 la Pasaka

Mdo 13:13-25;
Zab 89:2-3,21-22,42:225,27 (K. 2);
Yn 13:16-20.


TUME BAHATIKA KUWA “WATUMWA”


“Nawaambieni, hakuna Mtumwa aliye mkubwa kuliko Bwana wake, na wala hakuna mjumbe aliye mkuu kuliko yule aliye mtuma”. Yesu anajaribu kutuambia vitu viwili. Cha kwanza, ni vizuri kujiona sisi wenyewe kama watumwa na wajumbe wa Mungu na pili tunapaswa kumpa Mungu utukufu wote. Hili ni jambo muhimu la kuishi katika maisha ya kiroho.

Kawaida habari ya kuwa “mtumwa” haitamaniki sana. Na kilicho kibaya kuhusu utumwa ni kutendwa vibaya na Bwana wao. Wanatendwa vibaya na kuonekana kama vitu tu tofauti na utu wao wa kibinadamu. Lakini chukulia hali nyingine ambapo mmoja ni mtumwa alafu Bwana wake anampenda na jambo lake la kwanza kabisa la Bwana huyu ni kumsaidia huyu “mtumwa” ili atambue talanta zake ili aweze kukamilisha malengo yake ya maisha. Katika hali hii, “Bwana” huyu anamfanya mtumwa kuwa na upendo na furaha na wala hata haribu utu wake wa kibinadamu.

Hali hii ndivyo ilivyo kwa Mungu. Hatupaswi kukataa habari ya kuwa watumwa wa Mungu. Katika hali ya kweli, tunapaswa tutamani Mungu awe Bwana wetu zaidi kuliko hata tunavyo tamani kuwa mabwana sisi wenyewe. Kwani Mungu atatutenda vizuri zaidi kuliko hata sisi wenyewe. Kwani atatupa maisha ya utakatifu na furaha na kwa unyenyekevu kutuweka katika mapenzi yake. Atatupa vyote tunavyo hitaji kwa ajili ya kutenda yale anayo tuamuru. Kuwa “Mtumwa wa Mungu” ni kitu kizuri na tunapaswa kutamani mpango huo katika maisha.

Sala: Bwana, ninajikabidhi katika kila unacho niamuru. Ninaomba mapenzi yako yakamilike kwangu, mapenzi yako tu. Ninakuchagua wewe kuwa Bwana wangu katika kila kitu na ninaamini upendo wako mkamilifu kwangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com