Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MUNGU KATIKA UTATU

 



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya kila Jumapili
Jumapili, Mei 31, 2026 
Sherehe ya Utatu Mtakatifu

Kut. 34 : 4-6, 8-9;
Dan. 3:52-56. (K) 52;
2 Kor. 13 :11-14;
Yn. 3:16-18.


MUNGU KATIKA UTATU


Wakatoliki, duniani kote, sio kwamba wanaamini Mungu tu, bali wanaamini Mungu mmoja. Lakini Mungu wetu yupo katika Utatu- Utatu katika umoja na umoja katika Utatu. Kila mmoja ni Mungu kwa asili na wote ni Mungu mmoja. Sawa katika Nguvu, ni wa milele na wana utukufu. Fumbo hili kuu linaweza kuchukuliwa kama fumbo lililo kuu kabisa katika Biblia Takatifu. Wakristo tunaamini fumbo hili kuu ndani ya mamlaka ya Yesu Kristo na Agano Jipya. Ni moja wapo ya fumbo kubwa la ndani kabisa lililofunuliwa na lililopo juu kabisa kupita akili ya mwanadamu. Yesu mara nyingi ameongea kuhusu Mungu kama Baba yake. Sauti ya Baba ilisikika wakati wa ubatizo wa Yesu; “Huyu ni mwanangu mpendwa niliye pendezwa naye msikilizeni yeye”. Yesu alipo ngara sura, pia, sauti hiyo hiyo ilisikika ikisema maneno hayo hayo. Katika matukio yote uwepo wa wingu jeupe ilionyesha uwepo wa Roho Mtakatifu, ambaye Yesu aliwaahidia wakati alipokuwa akipaa kwenda kwa Baba, “nitawapa msaidizi Mwingine-Roho wa kweli anayetoka kwa Baba”. 

Yesu anatuambia kwamba, Mungu aliupenda sana ulimwengu mpaka akamtuma mwanaye ulimwenguni, ili wote watakao muamini wasipotee bali wawe na uzima wa milele (Yn 3:16). Anaelezea uhusiano wake ndani ya Mungu mmoja wa kweli na anawataka mitume na wafuasi watambue na wakubali kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, na kwamba Mungu ni Baba yake, na kwamba Roho Mtakatifu alitumwa kwao na Baba na Mwana. Wakristo wa kwanza walisadiki ndani ya Utatu Mtakatifu bila kupinga. Baada ya kuamini, kinachofuata ni Upendo. “Kama mtu akinipenda mimi” Yesu anasema, “Baba yangu atampenda. Nasi tutakuja kwake nakufanya makao ndani yake.”

“…(Wana ndoa) matunda ya wana ndoa yanakuwa ishara ya kuelewa na kuelezea fumbo la Mungu mwenyewe, kwasababu kwa mtazamo wa Kikristo wa Utatu mtakatifu, Mungu anatafakariwa kama Baba, na Mwana na Roho Upendo. Utatu Mtakatifu ni umoja wa upendo, na familia ndiyo inayoishi kuonesha umoja huu. Mtakatifu Papa Yohane Paulo wa Pili, alitoa mwanga kwa hili alivyosema ‘Mungu wetu katika undani wake sio upweke bali ni familia, kwani ndani yake ana Ubaba, mwana na undani wa familia ambaye ni Upendo. upendo huo ndani ya familia ya Kimungu ni Roho Mtakatifu’”. (Baba Mtakatifu Fransisko katika Furaha ya upendo, Amoris Laetitia, 11)

Tutafakari leo juu ya sherehe hii ya Utatu Mtakatifu, ni mara ngapi nina enzi upendo huu wa Utatu Mtakatifu katika mahusiano yangu? Tujaribu kufanya jitihada tusonge mbele zaidi, katika mapendo yetu, na kumruhusu Mungu akupe matokeo mazuri ya tokanayo na upendo wako kwake na kwa jirani. 

Sala: Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, nisaidie mimi niweze kuku fahamu wewe na kukupenda. Nisaidie niweze kuelewa upendo unaoshiriki na Mwanao. Kwa kuelewa upendo huo, nisaidie na mimi niweze kushirikisha upendo huo kwa wengine. Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAPILI MEI 31, 2026

 



MASOMO YA MISA, JUMAPILI MEI 31, 2026
SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU

JUMAPILI BAADA YA PENTEKOSTE - MWAKA A


SOMO 1 
Kut. 34 : 4-6, 8-9

Musa aliinuka na mapema asubuhi, naye akakwea katika mlima wa Sinai, kama Bwana alivyomwamuru, akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake.

Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka, akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema, Ikiwa sasa nimepata neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.


WIMBO WA KATIKATI 
Dan. 3:52-56. (K) 52

(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

Umehimidiwa, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu: 
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. 
Limehimidiwa jina lako takatifu, tukufu;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)

Umehimidiwa katika hekalu la fahari yako takatifu; 
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. 
Umehimidiwa juu ya kiti cha ufalme wako;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)

Umehimidiwa utazamaye vilindi, uketiye juu ya makerubi;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa katika anga la mbinguni 
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)


SOMO 2 
2 Kor. 13 :11-14

Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfariji- ke, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. Sali- mianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu. na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.


SHANG1LIO 
Ufu. 1 :8

Aleluya, Aleluya, Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, Mungu ambaye yupo, aliyekuwako, na atakayekuja. Aleluya.


INJILI 
Yn. 3:16-18

Yesu alimwambia Nikodemu: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhu- kumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.



Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

KUMUONA MUNGU KATIKA MAISHA YETU!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Mei 30, 2026, 
Juma la 8 la Mwaka wa Kanisa

Yud 17:20-25; 
Zab: 62: 2-6; 
Mk 11: 27-33


KUMUONA MUNGU KATIKA MAISHA YETU!

Yesu sasa yupo Yerusalemu. Katika Injili ya leo, wakati Yesu akiwa anatembea hekaluni, walimuendea viongozi na wazee Wawayahudi, Makuhani, walimu wa sheria na Wazee. “nikwa mamlaka ya nani unatenda haya?” walimuuliza Yesu. Hii ikimaanisha kwamba hafanyi katika hali ambayo inaonesha kujali mamlaka yao. Kama ilivyo ada kwa Yesu, anawauliza swali na wao. Aliuliza kama kazi ya Yohane Mbatizaji ilitoka kwa wanadamu au kwa Mungu.

Wakatambua mara moja kujibu Swahili la Yesu ingewaletea matatizo. Kwa udhaifu mkubwa wanajibu, “hatujui”. Jibu lisilo lakawaida kabisa tena lisiloridhisha na ajabu kabisa tena kutoka kwa viongozi wakubwa wa kiroho wa watu. Hapo Yesu akakataa kuwajibu swali lao walilokuwa wameuliza awali. Hali ya Yesu inafanana na ile ya Yohane Mbatizaji. Watu waliomsikia Yesu akiongea (“hakuna aliyewahi kuzungumza namna hii”) na kuona anavyoponya watu (“Mungu amewajia watu wake”), hawakuwa na wasiwasi wowote juu ya mamlaka yake. “Watu walishangazwa na mafundisho yake, kwani alifundisha kwa mamlaka sio kama Walimu wa sheria” (Mk 1:22). Swali la viongozi wa Wayahudi ilidhirisha kabisa udhaifu wao na upofu wao kwenye jambo ambalo lipo wazi lisiloweza kufichika machoni pa watu wote. 

Sisi pia tunaweza kuwa na upofu huo. Tunaweza tukakataa kuona uwepo wa kazi ya Mungu katika hali ambazo sisi wenyewe hatutaki kuona, katika watu ambao hatutaki kuwaona, au kuwadharau baadhi ya watu na kuwaona kama hawana chochote chakuweza kuniambia pengine kwasababu ya elimu yao au udhaifu wao. Lakini tutambue Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote, jambo lolote, zuri au lisiloonekana zuri machoni petu, ili kuleta ujumbe wake. 

Sala: Nisaidiye Bwana, kukutafuta na kukupata na nitende yale yote unayotaka nitende katika Maisha yangu. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 30, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 30, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 8 LA MWAKA

SOMO 1
Yud. 1:17,20-25

Wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele. Wahurumieni wengine walio na shaka, na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.

Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu; Yeye aliye Mungu pekee, Mwokozi wetu kwa Yesu Kristo Bwana wetu; utukufu una yeye, na ukuu, na uwezo, na nguvu, tangu milele, na sasa, na hata milele. Amina.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 63:1-5 (K) 1

(K) Nafsi yangu inakuonea kiu, Ee Bwana.

Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yangu inakuonea kiu,
Mwili wangu wakuonea shauku,
Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji. (K)

Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu,
Nizione nguvu zako na utukufu wako.
Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai;
Midomo yangu itakusifu. (K)

Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai;
Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono;
Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha. (K)


INJILI 
Mk. 11:27-33

Yesu na wanafunzi walifika Yerusalemu; alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee, wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya? Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya. Ubatizo wa Yohane ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Nijibuni.

Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini? Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu. Waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohane kuwa nabii halisi. Wakamjibu Yesu, wakasema, Hatujui. Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MATUNDA YENYE KUWAVUTA WATU




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Mei, 29, 2026 
Juma la 8 la mwaka wa Kanisa

1 Pet 4: 7-13; 
Zab 95: 10-13; 
Mk 11: 11-26


MATUNDA YENYE KUWAVUTA WATU

Yesu alivyo ulaani mtini baada ya kuuona hauna matunda, kitendo hiki kinaweza kuonekana cha ajabu kidogo na cha kutisha. Yesu alijua kabisa ilikuwa sio kipindi cha matunda ya mti ule. Mt. Bede katika maelezo yake akiongelea kuhusu muujiza huu wa Yesu, anatuambia kwamba, muujiza huu wa Yesu ulikuwa na lengo maalumu. Yesu alikuja kati ya watu wake, Wayahudi, akiwa na njaa yakutaka matunda ya utakatifu, wao hawakuupokea ujumbe wake na matunda ya kazi yake. Lakini yote aliyo yakuta ni msisitizo wakushika dini, matendo ya njee yasioendani na kilicho ndani, na katika hali hii wamekuwa kama majani ya miti bila matunda. Wakati alivyo ingia Hekaluni alikuta wamepageuza kuwa pango la biashara. Kitu ambacho kilimfanya hata halitakase kwakutumia nguvu. “Kwahio wewe” anasema Mt. Bede kwakumalizia, “unapaswa ujilinde usiwe kama mti usio zaa matunda, jitoe kwa Yesu, aliyejifanya mwenyewe maskini, anategemea uwe tunda la utakatifu” 

Fadhili zinaongeza furaha ya maisha ya sala na sala inapaswa ionekane katika matendo ya fadhila. Sala ya kweli inapaswa utuongoze taratibu katika mabadiliko ya kweli ya maisha yetu, tukikua katika fadhila na madiliko ya ndani. Vinginevyo tutakuwa kama Wayahudi, mtini uliyo na majani pekee usio zaa matunda.

Sala: Bwana nijaliye neema, ili kwa maisha yangu niweze kutoa matunda mema. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 29, 2026

 



MASOMO YA MISA, MEI 29, 2026
IJUMAA, JUMA LA 8 LA MWAKA

SOMO 1 
1 Pet. 4:7-13

Mwisho wa mambo yote umekaribia; basi iweni na akili, mkeshe katika sala. Zaidi ya yote iweni na juhudi, mkeshe katika sala. Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi. Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika; kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio katik yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 149:1-6,9 (K) 4

(K) Bwana awaridhia watu wake. au: Aleluva.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,
Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao. (K)

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, 
Huwapamba wenye upole kwa wokovu. (K)

Watauwa na waushangilie utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. (K)


SHANGILIO 
Lk. 8 :15

Aleluya, aleluya, 
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao, hulisikia neno la Mungu na kulishika. 
Aleluya.


INJILI 
Mk. 11:11-26

Yesu aliingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara.

Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipouiikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.

Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza na wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa; wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu. Akafundisha, akasema, Je! haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi. Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote walishangaa kwa mafundisho yake. Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.

Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mtini umenyauka toka shinani. Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. Yesu akajibu, akawaambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.

Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, ntkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KUONA TENA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Mei, 28, 2026,
Juma la 8 la Mwaka


1Pet 2: 2-5, 9-12; 
Zab 100:2-5; 
Mk 10:46-52.


KUONA TENA!

Leo, wakati Yesu akiuacha mji, akiwa anafuatana na wafuasi wake na umati mkubwa wa watu, kulikuwa na kipofu mmoja muombaji anayeitwa Batimayo mwana wa Timayo, akiwa amekaa pembeni ya barabara. Wakati kipofu huyu alivyosikia sauti za umati kama ilivyokawaida alitaka kujua nikitu ghani kinaendelea na anaambiwa kuwa ni Yesu Mnazareti anapita katika njia ile, mara moja baada ya kusikia hilo anapaaza sauti yake “Yesu Mwana wa Daudi unirehemu”. Ni aina ya sala tunayoiita sasa “Sala ya Yesu”. Sala tunayopaswa kuisali kila mara; ni sala ambayo tunaweza kuisali kwa uaminifu wakati tunapokubali kwamba sisi tunahitaji msaada wa Yesu na kuongozwa naye, na wakati tunapotambua nakukubali kwamba tupo mbali sana na kile alichotuitia Yesu tukiishi.

Maelezo ya yule kipofu ni maneno ambayo yanamfaa kila mmoja wetu anayemtambua Yesu. Sisi bila Yesu, ni vipofu, hatuwezi kuona vizuri ingawaje tunaweza kujiona wenye akili na maarifa mengi, tuliyosoma sana. Sisi ni waombaji. Tunaweza kumfuata Yesu kweli kama tutatambua kwamba, hata tuwe na akili ya namna ghani, maadili ya namna ghana au mali nyingi kiasi ghani, sisi kwa hakika ni masikini. Yule kipofu alikuwa amekaa kando ya barabara, sio barabarani. Na hii ndio maana halisi ya anaye kaa kando ya barabara, kwamba ni mwombani na kipofu kweli. Barabara au njia kwenye habari iliopo kwenye Injili ni ishara inayoonesha kwamba Kristo ni njia. Aliye na ukweli na uzima wote. Kwahiyo mwishoni mwa ujumbe wa Injili, baada ya yule kipofu kukutana na Yesu sasa anaweza kuona tena, yeye sio muombaji tena, na anafuatana na Yesu barabarani, njiani. Nasi tuliokutana na Yesu katika ubatizo, tutembee katika njia yake. 

Sala: Yesu Mpendwa, naomba niweze kuona vyema katika wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.



Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 28, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 28, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 8 LA MWAKA


SOMO 1 
1 Pet. 2:2-5,9-12

Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.

Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima. Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo. Ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri. ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 100 :2-5 (K) 2

(K) Njoni mbele za Bwana kwa kuimba kwa furaha

Mtumikieni Bwana kwa furaha;
Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)

Jueni kwamba Bwana ndiyc Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)

Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru;
Nyuani mwake kwa kusifu;
Mshukuruni, lihimidini jina lake. (K)

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)


SHANGILIO 
Yn. 14 21

Aleluya, aleluya, Mtu akinipenda, atalishika neno langu, na Baba yangu atampenda, na sisi tutakuja kwake. Aleluya.


INJILI 
Mk. 10:46-52

Walifika Yeriko; Yesu alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia. Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.

Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita. Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu. Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia, Mwalimu wangu, nataka nipate kuona. Yesu akamwambia. Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

NJIA AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUSHIKILIA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Mei, 27, 2026
Tafakari ya kila siku 
Juma la 8 la Mwaka wa Kanisa

1Pet 1: 18-25; 
Zab 147: 12-15, 19-20; 
Mk 10:32-45

NJIA AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUSHIKILIA!


“Walikuwa njiani wakielekea Yerusalemu.” Yesu ndiye njia, na njia yake inamleta Yerusalemu, kubeba msalaba wake, kwakukubali kuachia maisha yake kwa upendo wa Baba nakutupenda sisi, akituongoza kwenye ushindi wa mwisho. Wote wanaopenda kuwa wafuasi wake wanapaswa wawe tayari kutembea katika njia hiyo pamoja naye. Wafuasi bado hawajafikia hali hii ya ufuasi. Wakati Yesu akisonga mbele kiaminifu kuelekea Yerusalemu, wafuasi wake wanaonekana kubaki nyuma kidogo. Walikuwa katika hali ya kutoelewa na wote walio wafuata walikuwa katika hali ya woga. Kwajinsi walivyofikiri wao walidhani Yesu hayupo katika mawazo yao. Kwenda Yerusalemu kipindi hiki, ilikuwa nikujitakia matatizo, tena makubwa. Yerusalemu palikuwa ni Sehemu ya mwisho kabisa kwenda.

Yesu kwa upole kabisa anawapa somo jingine, kuhusu nini maana halisi ya kuwa mkubwa katika hali ya ufalme wake. Katika dunia kuwa “mkubwa” ni kuwa na nguvu juu ya wengine, kutawala, kuwa na uwezo wakuwafanya watu wakubaliane na kile unachopenda, kuwatumia watu ili ufikie lengo lako. Lakini katika ulimwengu wa Yesu, ukubwa nikujiweka chini kwaajili ya kuwahudumia wengine, ndugu zetu, majirani, na zaidi sana wale waliowahitaji. Na watu wote kuwatumikia bila kuharibu utu wao. Mamlaka sio kuamrisha, bali kujitoa. Baada ya miaka zaidi ya 2000 ya Ukristo bado ni jambo kubwa sana kwetu kujifunza hili “Mwana wa mtu hakuja kutumikiwa bali kutumikia”. 

Sala; Bwana, badilisha mioyo yetu ya ubinafsi iwe mioyo ya kuwahudumia wengine. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 27, 2026



MASOMO YA MISA, MEI 27, 2026
JUMATANO, JUMA LA 8 LA MWAKA

SOMO 1 
1 Pet. 1 :18-25

Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo. Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hataimani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.

Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo. Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu ienye uzima, lidumulo hata milele. Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka; Bali Neno la Bwana hudumu hata milele. Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 147 :12-15,19-20

(K) Msifu Bwana, ee Yerusalemu. au: Aleluya.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Ndiye afanyaye amani mipakani mwako,
Akushibishaye kwa unono wa ngano.
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lo lote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua.
Aleluya. (K)


SHANGILIO 
Yn. 14:5

Aleluya, aleluya, 
Bwana anasema: mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. 
Aleluya.


INJILI 
Mk. 10:32-45

Walikuwako njiani, huku wakipanda kwenda Yerusalemu; na Yesu alikuwa akiwatangulia; wakashangaa, nao katika kufuata wakaogopa. Akawatwaa tena wale Thenashara, akaanza kuwaambia habari za mambo yatakayompata, akisema, Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi, nao watamhukumu afe, watamtia mikononi mwa Mataifa, nao watamdhihaki, na kumtemea mate, na kumpiga mijeledi, na kumwua; na baada ya siku tatu atafufuka.

Na Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, wakamwendea, wakamwambia, Mwalimu, twataka utufanyie lo lote tutakalokuomba. Akawaambia, Mwataka niwafanyie nini? Wakamwambia, Utujalie sisi tuketi, mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika utukufu wako. Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi? Wakamwambia, Twaweza. Yesu akawaambia, Kikombe ninyweacho mimi mtakinywea, na ubatizo nibatizwao mimi mtabatizwa; lakini habari ya kuketi mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto si langu kuwapa, ila wao watapewa waliowekewa tayari.

Hata wale kumi waliposikia wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohane. Yesu akawaita,  akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote. Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.