Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
ISHARA YA UTUKUFU YA JUA LA HAKI !
MASOMO YA MISA, JUNI 24, 2026
MASOMO YA MISA, JUNI 23, 2026

JUMANNE, JUMA LA 12 LA MWAKA
SOMO 1
2 Fal. 19 : 9-11,
14-21, 31-36
Senakeribu alituma
wajumbe kwa Hezekia mara ya pili, kusema, Mwambieni Hezekia, mfalme wa Yuda,
maneno haya, mkisema, Asikudanganye Mungu wako unayemtumaini, akisema,
Yerusalemu hautatiwa katika mikono ya mfalme wa Ashuru. Tazama, umesikia ni
mambo gani wafalme wa Ashuru waliyozitenda nchi zote, kwa kuziangamiza kabisa;
je! utaokoka wewe?
Basi Hezekia
akaupokea waraka katika mikono ya wale wajumbe, akausoma; kisha Hezekia akapanda,
akaingia katika nyumba ya Bwana, akaukunjua mbele za Bwana. Naye Hezekia
akaomba mbele za Bwana, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya
makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia; wewe
ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi. Tega sikio lako, Ee Bwana, usikie; fumbua
macho yako, Ee Bwana, uone; uyasikie maneno ya Senakeribu, ambayo amemtuma mtu
aje nayo ili kumtukana Mungu aliye hai.
Ni kweli, Bwana,
wafalme wa Ashuru wamewaharibu mataifa na nchi zao, na kuitupa miungu yao motoni;
kwa maana haikuwa miungu, bali ni kazi ya mikono ya wanadamu; ilikuwa miti na
mawe tu, ndiyo sababu wakaiharibu. Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe na
mkono wake, nakusihi, ili kwamba falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe
ndiwe Bwana Mungu, wewe peke yako.
Ndiyo Isaya. mwana wa
Amozi, akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akisema, “Bwana, Mungu wa Israeli, asema
hivi, Kwa kuwa umeniomba juu ya Senake- ribu, mfalme wa Ashuru, mimi
nimekusikia. Tamko alilolitamka Bwana katika habari zake ndilo hili, Bikira,
binti Sayuni, amekudharau, na kukudhihaki sana; binti Yerusalemu ametikisa
kichwa chake juu yako. Maana mabaki yatatoka katika Yerusalemu, na, wao watakaookoka
katika mlima wa Sayuni; wivu wa Bwana utatimiza jambo hilo.
Basi Bwana asema hivi
katika habari za mfalme wa Ashuru, Yeye hatauingia mji huu, wala hatapiga mshale
hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake.Njia ile ile aliyojia, kwa njia iyo hiyo atarudi
zake, wala hataingia ndani ya ya mji huu, asema Bwana. Maana nitaulinda mji
huu, niuokoe, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.
Ikawa usiku uo huo
malaika wa Bwana alitoka. akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na
themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! hao
walikuwa maiti wote pia. Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda
zake, akarudi akakaa Ninawi.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 48 :1-3,9-10 (K)
8
(K) Mungu ataufanya
imara hata milele.
Bwana ndiye aliye
mkuu,
Na mwenye kusifiwa
sana
Katika mji wa Mungu
wetu,
Katika mlima wake
mtakatifu. (K)
Mlima Sayuni pande za
kaskazini,
Mji wa Mfalme mkuu.
Mungu katika majumba
yake
Amejijulisha kuwa
ngome. (K)
Tumezitafakari
fadhili zako, Ee Mungu,
Katikati ya hekalu
lako,
Ndivyo na sifa yako
hata miisho ya dunia.
Mkono wako wa kuume
umejaa haki. (K)
SHANGILIO
Zab. 130:5
Aleluya, aleluya, Roho
yangu inamngoja Bwana, na neno lake nimelituaminia. Aleluya.
INJILI
Mt. 7:6,12-15
Yesu aliwaambia wanafunzi wake; Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua. Basi yoyote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeeni vivyo hivya hiyo” maana hiyo ndiyo torati na manabii. Ingieni kwa kupitia mlango uliyo mwembamba, maana, mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
NJIA NYEMBAMBA!
Jumanne, Juni 23, 2026
Juma la 12 la Mwaka
2 Fal. 19 : 9-11, 14-21, 31-36;
Zab. 48 :1-3,9-10 (K) 8;
Mt 7: 6, 12-14
NJIA NYEMBAMBA!
Katika Injili ya leo Bwana wetu anatuambia, “tuingie kupitia mlango mwembamba, maana mlango mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo” (Mt 7:13). Tukiangalia maisha yetu kwa ujumla, si kitu zaidi ya msururu wa matokeo ya chaguzi zetu. Kuna wakati tumehuzunikana sana kwa kufanya uchaguzi mbaya na pia kuna wakati tumefurahi sana kwa kufanya uchaguzi au uamuzi sahihi.
Leo Yesu anaongelea kuhusu uchaguzi kati ya njia rahisi na njia iliyongumu. Tuna shawishika kuchagua njia pana na iliyo rahisi na kukwepa njia nyembamba. Lakini katika maisha ya kiuzoefu ya mwanadamu yanatuambia kwamba hakuna njia iliorahisi inayopelekea mafanikio mazuri ya maisha ya mwanadamu. Ukuu/mafanikio mara nyingi ni matokeo ya kazi ngumu. Njia inayoelekea kwenye Ufalme wa Mungu ni nyembamba. Ina mambo yake, inatuhitaji tujitoe, kujikatalia na sadaka.
Kutenda dhambi ni rahisi na inaonekana kuwa kawaida kwa mwanadamu, lakini kubaki bila dhambi ni ngumu kwasababu inatutaka kupingana na matamanio yetu. Inatutaka tujikatalie. Na Injili ya Leo inatuambia kwamba ni wachache sana wanaochagua njia nyembamba, walio wengi wanachagua njia iliopana na iliyo rahisi. Ni wachache sana wanao ipokea Injili na kuishi kadiri ya ujumbe wake. Tuombe neema ya Mungu itusaidie tuweze kuchagua njia nyembamba yakutuchukua kwenye ufalme wa Mungu, inatugarimu sisi wakati mwingine kwenda kinyume na matakwa ya wengi, unaweza kuchukiwa nakutopendwa lakini kwakuujua ukweli wa Yesu katika Injili, ishi kadiri yake.
Sala: Bwana, nioneshe njia nyembamba inayo niongoza kwako. Nisaidie niwatendee wengine yale ambayo natamani wanitendee. Nisaidie nitumie upendo ulio ndani yangu kuhusu mimi mwenyewe niweze kuutumia kuwapenda wengine. Katika kujitoa kwangu, nisaidie niweze kupata ukamilifu katika majitoleo hayo. Yesu, nakuamini wewe. Amina.
USIHUKUMU!

MASOMO YA MISA, JUNI 22, 2026
YESU YUPO PAMOJA NASI KUTUOKOA!
Katika somo la kwanza tunakutana na Yeremia aliyeishi katika kipindi katika historia ya mwenendo usio kuwa mzuri wa watu wake. Jeshi la Nebukadneza limeizunguka Yerusalemu na kuichukua mateka. Mfalme na majeshi yake wamefanya maamuzi yasio kuwa sahihi ya kuleta maangamizi. Badala ya viongozi wa dini kutambua yanayo wapata watu, wanamsifia Mfalme na jeshi lake. Katika hali hii ngumu, Yeremia kijana mdogo, mwenye aibu, na mtu wa amani anaitwa na Mungu kufanya utume hatarishi juu ya “Mfalme wa Yuda na viongozi wake, makuhani wake na watu wote katika nchi”. Ana imarishwa na Bwana kwa maneno haya “watapigana nawe lakini hawata kushinda, kwani nipo nawe kukuokoa” (Yer 1:17-19). Yeremia anakutana na upinzani. Maadui wa Yeremia hawaja jifunga tu katika makundi bala wanamtafuta ili wamtundike na kumuua. Yeremia anaona utume wake umeshindwa, anajisikia kukataliwa na watu wake na watu wote. Anakata tamaa, na kujiuliza kama kweli wito wake pengine haukuwa wa kweli. Anaeleza hisia zake kwa Mungu. Sala yake alioifanya kwa mkazo, lakini katika uaminifu, inaleta matokeo kwake ya ukweli wa uamini fu wa Mungu. Ujasiri wake na matumaini yake yana amka tena. Anatangaza: “Yahweh Bwana wa majeshi yupo nami” (mstari. 11). Ana ujasiri na uhakika kwamba Mungu, Mungu atamshindia, anafanya ukweli utawale na kumfanya mwenye kutetea haki kungara.
Katika somo la pili kutoka barua kwa Warumi, Paulo anamlinganisha Adamu na Yesu: analinganisha matokeo ya dhambi ya mtu wa kwanza na matokeo ya ukombozi ulioletwa na Kristo. Tangu awali mwanadamu alitenda dhambi, kwa kufuata mfano wa Adamu aliyekosa utii na kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu, lakini, Yesu alifanya kinyume chake. Yeye ni mtii kwa Baba, ametimiza mapenzi yake mpaka kufa. Matokeo ya dhambi ya Adamu ni kifo. Neema inayo patika kwa utii wa Kristo, ni mkuu sana. Kwa njia ya Kristo, Mungu amewapa uhai wote.
Katika Injili ya Mathayo iliyo andikwa kipindi cha Mfalme Domitian wa Kirumi, aliye amuru kuabudiwa kama Mungu. Wakristo hawakuweza kumpa mfalme sifa za Mungu. Kwa njia hiyo, matatizo yalianza, kupigwa, kutengwa, mali zao kuchukuliwa yalianza juu yao. Walio wengi hawakuweza kuvumilia unyanyasaji wa namna hii. Walikuwa katika hali ngumu ya kufanya uamuzi. Hivyo, ili kuwafariji wakristo wa jamii yake, Mathayo ana andika maneno hayo ya Yesu, ya kihistoria, ambayo aliyaweka katika Injili, maneno ya Yesu kuhusu kupatwa na magumu na mateso kwa wafuasi wake. Kwa Wakristo mateso sio ajali; haya kwepeki: “wale wote wanaotaka kumtumikia Mungu kwa njia ya Kristo, watateseka”. (2 Tim 3:12).
Katika Injili ya Leo, Yesu anasisitiza mara tatu “msiogope!” na kila wakati ameongeza motisha ili kuonesha msisitizo wa ujumbe wake. Yesu ana tuhakikishia kwamba licha ya magumu na mateso, Injili itaenea ulimwenguni na kuubadilisha. Yesu anatuita pia tutafakari: ni madhara ghani adui wa Injili anaweza kuleta? Kusingiziwa, kuhukumiwa bila haki, kupigwa, kuchukua mali, kuuwawa! Ndio, lakini hamna zaidi! Hakuna vita vyenye uwezo wakuweza kuchukua thamani ya uzima: uzima aliotoa Mungu hakuna anaye weza kuuchukua. Lakini kuna mtu-Yesu anaendelea-ambaye anapaswa kuogopwa. Ni “yule ambaye ana nguvu ya kuangamiza mwili na roho kwa pamoja”. Hali hii sio hali ya nje, bali niuovu ambao tangu kuzaliwa, tunauchukua ndani mwetu. Hii ni msukumo mbaya unao tuongoza kwenye njia tofauti na njia ya Kristo. Hivyo tunapaswa pia kujiogopa sisi wenyewe na hofu yetu. Yesu anatuita kutegemea nguvu ya Mungu. Anatupa uhakika kwamba Mungu atatambua uzuri wetu kama tutakuwa jasiri na kubaki waaminifu.
Sala: Baba wa Mbinguni, ninakushukuru kwa upendo wako katika maisha yangu. Ninakushukuru kwa kuniita mimi na kunibadili ili niweze pia kubadili ulimwengu. Nisaidie mimi nitegemee upendo wako na kujikabidhi kwako. Katika nyakati za mateso, kuwa nguvu yangu na tumaini. Ninawaombea pia wakristo wote wanao onewa ulimwenguni, ili waweze kuvumilia mpaka mwisho. Yesu nakuamini wewe. Amina
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JUNI 21, 2026
JUMAPILI YA 12 YA MWAKA
Nimesikia mashutumu ya watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki; huenda akahahadaika; nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake. Lakini Bwana yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe. Lakini Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo. nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.
Mwimbieni Bwana; msifuni Bwana;
Kwa maana ameiponya roho ya mhitaji
Katika mikono ya watu watendao maovu.
(K) Kwa wingi wa fadhili zako unijibu.
Kwa ajili yako nimestahimili laumu,
Fedheha imenifunika uso wangu.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila,
Na laumu yao wanaokulaumu zimenipata. (K)
Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana,
Wakati ukupendezao; Ee Mungu,
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu,
Katika kweli ya wokovu wako.
Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema,
Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. (K)
Walioonewa watakapoona watafurahi;
Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yetu ihuishwe.
Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji,
Wala hawadharau wafunga wake.
Mbingu na nchi zimsifu
Bahari na vyote viendavyo ndani yake. (K)
Kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia uli mwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria; walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, alive mfano wake yeye atakayekuja. Lakini karama ile haikuwa kama lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi.
Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, ee Bwana,
Ili tuyatunze maneno ya Mwanao.
Aleluya.
Yesu aliwaambia mitume wake: Msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba. Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum, Je! mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu; lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi; bora nyinyi kuliko mashomoro wengi. Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
BWANA WANGU NINANI- MUNGU AU PESA?

MASOMO YA MISA, JUNI 20, 2026






