Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

FURAHA NA TUMAINI LA UFUFUKO!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Mei, 15, 2026 
Juma la 6 la Pasaka


Mdo 18: 9-18;
Zab 47: 2-7 (K. 8);
Yn 16: 20-23.


FURAHA NA TUMAINI LA UFUFUKO!

Kila tukio katika maisha yetu linaleta matokeo fulani katika maisha yetu. Wakati matokeo yakiwa mazuri tunakuwa na furaha. Na wakati tukiwa tunazamia mazuri yatokee hilo tunaita kuwa tumaini. Kama matokeo ni mabaya tunakuwa na huzuni na tunakuwa na hofu na mashaka. Hali hizi zinabadilika kadiri ya hisia zetu, na hayabakii kuwa yale yale. Injili inayaweka yote haya katika mfano wa kuzaliwa kwa mtoto. Kunakuwepo na maumivu, hofu lakini furaha huja baadae. Tunapaswa kuwenda zaidi ya haya tunayo yaona ulimwenguni ili tuweze kwenda kufuhia furaha ya ufalme wa Mungu. Kama Yesu alivyokufa juu ya vitu vyote ili afufuke katika utukufu wa Mungu, hivyo hivyo nasi tunapaswa tufe juu ya mambo yanayoleta furaha ya muda na kwa kufanya hivi lazima tuhizi uchungu wa kuacha baadhi ya mambo ili tuweze kufufuka ndani Yake. Maisha yanakuwa kwa kuyatoa, lakini yanaharibika kwa kujitenga na kujifariji binafsi.

Je, mateso yana maana kwamba upo mbali na Mungu? Au hauna neema ya Mungu? Ina maana kwamba Mungu amekuacha? Au ina maana kwamba unafanya kitu kibaya? Hakika sio hivyo, tunachopaswa kufanya nikuangalia maisha ya Yesu na tutatambua kwamba hili halipo hivyo. Alikuwa katika hali ya misuko suko na kupingwa na viongozi kila wakati lakini alijikita zaidi katika utume wa Baba yake. Alikuwa akisali kwa siku arobaini jangwani. Katika utume wake alikutana na vipingamizi vingi sana. Alitukanwa na kupingwa, kutokueleweka, kutemewa mate, na zaidi hata mpaka alivyokufa msalabani. 

Mama yetu Bikira Maria alipatwa na “uchungu kama upanga” ukampenya moyo wake. Alikuwa na upendo kamili kwa mtoto wake. Aliwaona wengi waliokuwa wakimpenda mwanae na wale wasiompenda mwanae. Aliwaona wale waliokuwa wakimsulubisha na kumbebesha msalaba. 

Lakini fikiria juu ya maisha yao. Wanafurahi sasa Mbinguni kama watakatifu, na Mama yetu kama Malkia wa mbinguni na watakatifu wote, na Yesu kama Mfalme wa Mbingu na Nchi. Wanaishi katika utukufu milele. Huzuni zao zimebadilika na kuwa furaha kamili. Kama unafikiri umetendewa vibaya au wamekuonea, furahi upo salama. Tambua kuwa unapo bakia mwaminifu na kutembea katika njia ya uaminifu ya Mungu aliokuwekea, mwisho ni kwamba utafurahia! Shikilia katika tumaini hilo na elekeza macho yako katika njia ya Mungu. Hakika utafanikiwa. 

Sala: Bwana, ninakabidhi mizigo yangu yote na uchungu wote kwako. Ninaunganisha na msalaba wako nikitumaini kuwa utakuwa nami katika yote katika njia yangu ya maisha. Ninaomba niweke moyo wangu katika lengo langu nikiwa na furaha katika upendo wako kamili. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 15, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 15, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, IJUMAA

SOMO 1 
Mdo. 18: 9-18

Bwana alimwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze, kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu. Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu.

Hata Galio alipokuwa liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya kiti cha hukumu, wakisema, Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sheria. Na Paulo alipotaka kufunua kinywa chake, Galio akawaambia Wayahudi, Kama lingekuwa jambo la dhuluma au la hila mbaya, enyi Wayahudi, ingekuwa haki mimi kuchukuliana nanyi; bali ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo.

Akawafukuza waondoke mbele ya kiti cha hukumu. Nao wote wakamshika Sosthene, mkuu wa sinagogi, wakampiga mbele ya kiti cha hukumu. Wala Galio hakuyaona mambo hayo kuwa ni kitu. Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 47:1-6 (K) 7

(K) Mungu ndiye mfalme wa dunia yote. 
Au: Aleluya.

Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe,
Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya, 
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. (K)

Atawatiisha watu wa nchi chini yetu,
Na mataifa chini ya miguu yetu.
Atatuchagulia urithi wetu,
Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda. (K)

Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti ya baragumu.
Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;
Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. (K)


SHANGILIO 
Yn- 10:14

Aleluya, aleluya, 
Mimi ndimi mchungaji mwema, nao walio wangu nawajua, nao walio wangu wanijua mimi. 
Aleluya.

INJILI
Yn. 16:20-23

Siku ile Yesu aliwaambia wanafunzi wake; Amin, amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha. Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika, lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni. Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye. Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

VYOMBO VYA UPENDO!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Mei, 14, 2026, 
Juma la 6 la Pasaka

Sikukuu ya Mtakatifu Matia, Mtume

Mdo 1: 15-17, 20-26;
Zab,113: 1-8 (k.8);
Yn 15: 9-17.


VYOMBO VYA UPENDO!

“Hakuna upendo uliyo mkuu kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwaajli ya rafiki zake”. Upendo wa Yesu ni wa pekee na unajifunua kwa majitoleo yake pale msalabani. Upendo wa Yesu ni sadaka na hauna masharti. Yuda hakuutambua upendo huo, lakini sisi tunaitwa kuutambua kama wafuasi wa Kristo.

Kuwa mfuasi wa Kristo kuna mambo matatu yanayo jitokeza katika Injili ya leo, kwanza kabisa, kila Mkristu ana wito wa pekee wakupendana na mwezake. Na pili kila Mkristu ana wajibu wakumfuata Kristo na kutembea katika njia yake ya utakatifu na upendo. Na mwisho kabisa kila Mkristo anapaswa kujiunga na Mungu daima kwa njia ya sala. 

Tumuombe mtakatifu Matia mtume tunae muadhimisha leo atuombee kwa Mungu tuweze kuyashika hayo kama yeye alivyofanikiwa kuyashika kama mtume wa Kristo aliyechukuwa ile nafasi ya Yuda Iskariote.

Sala: Yesu, naomba unisaidie mimi niweze kuwa chombo cha upendo kama mtakatifu Matia mtume. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 14, 2026




MASOMO YA MISA, MEI 14, 2026
ALHAMISI YA 6 YA PASAKA
SIKUKUU YA MT. MATHIA, MTUME


SOMO 1
Mdo. 1:15-17, 20-26

Siku zile Petro alisimama kati ya ndugu zake (jumala ya majina ilipata mia na ishirini), akasema, Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi. katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu, kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii. Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa,

Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo; tena, Usimamizi wake autwae mwingine. Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, kuanza tangu ubatizo wa Yohane, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.


W1MBO WA KATI KATI 
Zab. 113:1-8 (K) 8

(K) Amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake. au: Aleluya.

Aleluya.
Enyi watumishi wa Bwana, sifuni,
Lisifuni jina la Bwana.
Jina la Bwana lihimidiwe 
Tangu leo na hata milele. (K)

Toka maawio ya jua hata machweo yake 
Jina la Bwana husifiwa.
Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote,
Na utukufu wake ni juu ya mbingu. (K)

Ni nani aliye mfano wa Bwana,
Mungu wetu aketiye juu;
Anyenyekeaye kutazama,
Mbinguni na duniani? (K)

Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,
Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
Amketishe pamoja na wakuu,
Pamoja na wakuu wa watu wake. (K)


SHANGILIO 
Yn. 15 :16

Aleluya, aleluya, Ni mimi niliyewachagua ninyi, nikawaweka mwende mkazae matunda, na matunda yenu yapate kukaa. Aleluya.


INJILI 
Yn. 15:9-17

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.

Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu. Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni. Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.


Neno la Bwana.........sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MUNGU ASIYE JULIKANA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Mei 13, 2026 
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 17: 15, 22-18:1;
Zab 148: 1-2,11-14;
Yn 16:12-15.

MUNGU ASIYE JULIKANA!

Katika somo la kwanza, Mt. Paulo anawavuta watu wa Atheni katika utambuzi kuhusu altare zao walizojenga kwa “Mungu asiye julikana”. Anawaeleza kwamba amekuja kuwafunulia ukweli juu ya huyu Mungu asiye julikana wanaye mwabudu waweze kumtambua yeye ni nani. Wakati mwingine tunamtazamia Mungu ambaye tunataka kumuona au kumshika. Wakati mwingine tunajikuta tunakimbilia mara nyingi sehemu ambazo tunaona Mungu amechorwa katika picha ya kibinadamu. Lakini tunapaswa kutambua kwamba Mungu wetu ni Mungu aliyefichika (Is 45: 15). Amefichika katika ufahamu wetu. Katika wimbo wa kuabudu tunaimba ‘Yafichika machoni Imani yaona’, fahamu haiwezi kutambua fumbo hili bali Imani inatusaidia.

Katika Injili Yesu anatufunulia kuhusu Utatu Mtakatifu. “Roho atakayekuja atachukua kila kilicho changu” (Yn 16:14). “kila alicho nacho Baba ni changu” (Yn 16: 15). Hapa umoja wa Utatu Mtakatifu na asili ya nafsi tatu unafunuliwa.

Hii inamaana kwamba tunapaswa kuwa wazi katika maisha yetu juu ya nguvu na uwepo wa Roho Mtakatifu, yeye aliyebeba ukweli wote. Roho Mtakatifu anapaswa kuwa hai ndani mwetu, akifunua ukweli. Na tukiwa wazi kiakili na mioyo yetu kwa Roho Mtakatifu, tutakuwa watu wakutamani ukweli. Tutakuwa na hamu ya kuelewa vitu ambavyo vitafungua mioyo yetu. Tutakuwa na uwezo wakutazama mambo katika hali ya upya. 

Wewe ni wazi kiasi ghani katika uweli? Ni mara ngapi katika hali ya kweli unakumbatia yote ambayo Mungu ameyafunua kwako? Jifungue zaidi kwa Roho Mtakatifu na tafuta yote ambayo anayafunua kwako. 

Sala: Roho Mtakatifu, ninaomba uje utawale maisha yangu. Nifundishe na kuniongoza katika ukweli wote. Roho Mtakatifu, Bwana Mtakatifu, Baba mwenyewe huruma, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 13, 2026


MASOMO YA MISA, MEI 13, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMATANO

SOMO 1 
Mdo. 17 :15, 22-18:1

Siku zile, wale waliomsindikiza Paulo wakampeleka mpaka Athene; nao wakiisha kupokea maagizo kuwapelekea Sila na Timotheo, ya kwamba wasikawie kumfuata, wakaenda zao. Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini. Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, kwa Mungu asiyejulikana.

Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua. Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono; wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote. Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu. Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wetu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu. Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu. Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo. Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha. Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, Mwareopago, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao. Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 148:1-2, 11-14

(K) Utukufu wako unajaza mbingu na ulimwengu. 
Au: Aleluya.

Aleluya. 
Msifuni Bwana kutoka mbinguni;
Msifuni katika mahali palipo juu.
Msifuni. enyi malaika zake wote;
Msifuni, majeshi yake yote. (K)

Wafalme wa dunia, na watu wote,
Wakuu, na makadhi wote wa dunia.
Vijana waume, na wanawali,
Wazee, na watoto. (K)

Na walisifu jina la Bwana,
Maana jina lake peke yake limetukuka;
Adhama yake i juu ya nchi na mbingu. (K)

Naye amewainulia watu wake pembe,
Sifa za watauwa wake wote;
Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. (K)


SHANGILIO 
Ufu. 1 : 5

Aleluya, aleluya, 
Ee Kristo, yu shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. 
Aleluya.

INJILI 
Yn. 16:12-15

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Bado ningali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa. Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza mimi; kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari. Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasha habari.

Neno la Bwana... Sifa kwako ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MAISHA NDANI YA ROHO MTAKATIFU

 


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Mei 12, 2026
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 16: 22-34;
Zab 138: 1-3,7-8 (K.7);
Yn 16:5-11.


MAISHA NDANI YA ROHO MTAKATIFU


Katika somo la kwanza, tunakutana na Paulo akiwa amejazwa na Roho Mtaktifu akisifu na kumshukuru Mungu kwa kumpa yeye pamoja na ndugu zake kushiriki katika mateso ya Kristo. Hii ni neema kamili ya Roho Mtakatifu ilikuwa ikifanya kazi ndani mwao. Akiwafundisha wafanye mema na kwa wakati muafaka. Hata milango ya gereza ilipo funguka yeye na wenzake hawakukimbia. Ushuhuda huu na wa wenzake ulimfanya yule mlinzi wa gereza kubadili maisha yake yeye na familia yake. Wanaongozwa na Roho Mtakatifu kuokoa maisha ya yule mlinzi wa Gereza, aliyekuwa sababu ya mateso yao pia.

Katika somo la Injili, mioyo ya wafuasi ilijazwa na huzuni, lakini pia walikuwa wakijitahidi kuamini kile ambacho Yesu alikuwa akiwaambia.Yesu aliwaambia kwamba atapaa kwenda kwa Baba yake na kwamba ilikuwa ni vizuri yeye aondoke. Kwasababu akiondoka atamtuma Msaidizi kwao.

Katika hali yya kibinadamu, ilikuwa vigumu kwa wafuasi kumwacha Yesu aondoke tu kwasababu ya wao kumzoea na kuongea naye kila wakati. Ni hakika kwamba walimkosa sana kuendelea kumuona kwa macho yao kama walivyo zoea kumuona, kumshika na kumsikia akiongea. Lakini Yesu aliweka wazi kwamba hata kama anaondoka bado atakuwa nao daima. Na kwamba atamtuma Msaidizi Roho Mtakatifu ambaye atakuwa pamoja nao na kuwaongoza katika ukweli wote, akiwapa nguvu, na kuwafundisha ukweli wote. Watakuwa wawakilishi wake sasa ulimwenguni kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Hatukuwa na bahati ya kumuona Yesu kama wanafunzi wake walivyokuwa. Lakini tuna bahati ya kuwa nasi kila siku. Na tuna bahati ya kupokea utimilifu wa Roho Mtakatifu. Tumepokea kipaimara, lakini tunaweza kushindwa kumruhusu Roho Mtakatifu akae ndani yetu na kutufanya wapya. Tunapo karibia sikukuu ya Pentekoste, kubali na jinyenyekeshe na kukiri kwamba unamhitaji Roho Mtakatifu aweze kuwa ndani ya maisha yako. Amini kwamba Yesu anataka umpokee yeye katika Utimilifu. Na wala usiwe na wasi wasi kuruhusu muunganiko huu utokee kwako. Tunapaswa kuisikiliza sauti ya Roho Mtakatifu ambaye yupo ndani mwetu na ambaye anajaribu daima kutuelekeza kwenye ukweli.

Sala: Roho Mtakatifu, naomba uje ndani mwangu. Ninaomba unisaidie kuwasha moto wako katika maisha yangu. Ninakuomba nikupokee wewe ambaye uliahidiwa na Yesu katika utimilifu wote. Roho Mtakatifu, Yesu mwana wa Mungu, Mungu Baba mwenye huruma, najiaminisha chini yako. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, MEI 12, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 12, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMANNE

SOMO 1
Mdo. 16:22-34

Siku ile, pale Filipi, wenyeji waliwakamata Paulo na Sila, wakawaendea, makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora. Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana. Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale. Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.

Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati huo huo. Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 138; 1-3, 7-8 (K) 7

(K) Utanyosha mkono, Ee Bwana, utaniokoa. aur Aleluya.

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,
Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, (K)

Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Siku ile niliyokuita uliniitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu,
Na mkono wako wa kuume utaniokoa.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)


SHANGILIO 
Kol 3:1

Aleluya, aleluya, 
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, amcketi mkono wa kuume wa dunia. 
Aleluya.


INJILI 
Yn 16:5-11

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi? Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu. Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi; kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

ROHO MTAKATIFU: MSAIDIZI




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Mei 11, 2026.
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 16: 11-15;
Zab 149: 1-6, 9;
Yn 15:26 - 16:4.

ROHO MTAKATIFU: MSAIDIZI

Kanisa lenye msingi wake kwa Yesu linaongozwa na Roho Mtakatifu tangu Pentekoste. Mtakatifu Paulo na wengine walihubiri Injili ya Yesu. Sehemu yeyote lilipo hubiriwa neno la Mungu, Roho Mtakatifu ndiye aliyesababisha wongofu wa mioyo ya watu. Lidia alimsikia Paulo na wengine wakihubiri Injili ya Yesu. Alifungua moyo wake kwa Bwana. Ina maana kwamba kwanza kabisa alifungua masikio yake akamsikiliza Yesu, naye Roho Mtakifu akamtia nguvu. Moyo wake na utayari wake wakukaribisha ujumbe wa Kristo moyoni mwake haukuwa tuu kwaajili yake binafsi bali ulibadilisha nyumba yake yote. 

Wafuasi walimsikiliza Yesu akiwaambia kwamba watafukuzwa katika masunagogi na hata kuuwawa, maneno haya hawakuyaelewa. Huenda iliwasumbua kidogo, lakini mara moja kwenda kwa mambo mengine ili wasiyawaze zaidi na kuwasumbua. Na bila shaka mitume walipo adhibiwa na Mafarisayo na waandishi, waliyakumbuka maneno haya ya Yesu. Walitambua walipaswa wawaongoze kwenda kwa Mungu, wana sababisha adha katika maisha yao. Watakuwa walijaribiwa katika hali ya kutaka wapoteze Imani yao. Lakini Yesu alitabiri jaribu hili kuu litakuja, lakini akawaonya na kuwaambia kuwa yatakuja. 

Lakini kinacho vutia ni kile ambacho Yesu hakusema. Hakuwaambia kwamba watapigana na kurudisha, kuanza fujo, au mapinduzi yeyote nk. lakini tunamuona Yesu akiwaaambia Roho Mtakatifu ndiye atakaye shughulika na hayo. Atawaongoza na kuwawezesha kumshuhudia Yesu. Kuwa mkristo maana yake umekubali mateso.
Roho Mtakatifu anaitwa “Msaidizi”, huwafariji waamini, hasa wakati wauhitaji na mateso. Pia, wakati mwingine kile tunacho dhani ni ukweli kinaweza kisiwe ni ukweli kabisa, kinaweza kuchanganywa na uongo. Yeye pia ni “Roho wa Ukweli”, anayetuonyesha ukweli- kwamba ni Yesu aliyesema ‘mimi ni ukweli, njia na uzima’ (Yn 14:6). Leo tujiulize kama maisha yetu yanaongozwa na Roho Mtakatifu?

Sala: Bwana, ninapo elemewa na mzigo wa ulimwengu au mateso nipe Amani ya mwiili na Roho. Ninaomba unipe nguvu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili niweze kuwa shahidi wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, MEI 11, 2026





MASOMO YA MISA, MEI 11, 2026
JUMA LA 6 LA PASAKA, JUMATATU

SOMO 1
Mdo. 16:11-15

Tuling’oa nanga kutoka Troa, tukafika Samothrake kwa tanga moja, na siku ya pili tukafika Neapoli; na kutoka hapo tukafika Filipi, mji wa Makedonia, mji ulio mkuu katika jimbo lile, mahali walipohamia Warumi; tukawa katika mji huu, tukikaa siku kadha wa kadha. Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.

Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambave moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo. Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 149 :16, 9 (K) 4

(K) Bwana awaridhia watu wake. au Aleluya.
Au: Aleluya.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,
Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba wenye upole kwa wokovu. (K)

Watauwa na waushangilic utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wote. (K)


SHANGILIO 
Rum. 6 : 9

Aleluya, aleluya, 
Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena wala mauti haimtawali tena. 
Aleluya.


INJILI 
Yn. 15:26-16:4

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia. Nanyi pia mnashuhudia, kwa kuwa tangu mwanzo mmekuwapo pamoja nami.

Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.