“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya kwaresima
Alhamisi, Februari 19, 2026
Alhamisi baada ya Jumatano ya majivu
Kum 30: 15-20;
Za 1: 1-4, 6;
Lk 9: 22-25
KUIPATA ROHO KWA KUPOTEZA ULIMWENGU!
Somo la kwanza kutoka katika kumbukumbu la Torati linatufundisha kushika
Amri za Mungu kwa kumpenda Mungu, kwa kumtii na kutembea katika njia zake. Kama
tutafanya hivyo, tutapokea ahadi zake, ambazo ni uhai na mafanikio. Kwa upande
mwingine yule ambaye hamtafuti Mungu anakuwa amechagua kifo na uovu.
Injili inaongelea kuhusu kuchukuwa misalaba yetu na kumfuata Yesu kila
siku. Luka anasisitiza “KILA SIKU”, kuonesha umuhimu wakujikita kila siku na
kukumbutia misalaba inayopitia katika njia zetu kwa uaminifu na mapendo.
Kukumbatia kile ambacho kinaleta uchungu, kisicholipa, kilicho chukiwa na
ulimwengu sio rahisi. Hili ndilo alilolifanya Yesu kwa njia ya mateso yake, na
kifo juu ya msalaba kwa ajili yetu, akashinda kwa ajili ya wokovu wetu.
Kuchagua maisha ya Imani na ukombozi wa roho zetu inatupasa kuacha mengi
ulimwenguni humu. Tunapaswa kuishi katika hali ambayo inatuweka tayari “kuachia
yote” hata kama yalikuwa kwa ajili ya faida yetu au kwa ajili ya ukombozi wa
wengine. Hili ni ngumu kulifanya na linahitaji mapendo makubwa kwa Mungu.
Inatakiwa tuwe tumeridhia wenyewe kutoka ndani, kiasi kwamba kuona utakatifu ni
zaidi ya kitu kingine chochote. Usisite kumfanya Mungu kuwa kiini na lengo la
maisha yako. Kipindi cha kwaresima ni kipindi muhimu sana cha kuingia ndani na
kutazama mitazamo yako na tamaa yako na lengo la maisha yako katika hali ya juu
kabisa. Mchague Mungu awe zaidi ya yote na wala hutajutia kufanya kufanya
hivyo.
Sala: Bwana, tunapoingia katika kipindi hiki cha kwaresima, nipe neema
niweze kutazama juu ya malengo yangu. Nisaidie niweze kuchagua kile kilicho cha
muhimu kabisa na kiini cha maisha yangu. Nisaidie nikuchague wewe zaidi ya yote
katika maisha yangu ili unisaidie kuendana na mapenzi yako matakatifu. Yesu,
nakuamini wewe.
Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki:
see www.fur-kat.blogspot.com.




