Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MFUASI WA KRISTO!




"ASALI ITOKAYO MWAMBANI"
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, Julai 13, 2026,
Juma la 15 la Mwaka

KUMBUKUMBU YA MT. BONAVENTURE


Isa. 1:10 – 17
Zab. 50: 8 – 9, 16 – 17, 21, 23 (K) 23
Mt 10: 34 - 11: 1.



MFUASI WA KRISTO!

          
Injili haina lele mama, hakuna cha nusu njia, wala njia fupi katika kumfuata Yesu. Injili yake inatualika tuwe na msimamo mmoja tu. Kifungu cha Injili ya leo kimegawanyika katika sehemu kuu mbili, zote zikiwa na mitazamo mbalimbali juu ya utume.

Sehemu ya kwanza inaonesha masharti ya Yesu kwa yeyote yule anayetaka kumfuata. Yesu anahitaji mtu ajikane kwa hali ya juu kabisa, na kama haitoshi, anamalizia masharti hayo akirudia mara tatu maneno, “hanistahili”. Yeyote atakaye kumfuata Yesu anapaswa ajikane mwenyewe kutoka mambo yote ayapendayo na mvuto wa upendo wa asili kama vile, kuwapenda zaidi wazazi na watoto. Yesu haipingi amri ya kuwapenda na kuwaheshimu baba na mama, bali anaweka wazi kuwa hawapokei watu ambao wanajitoa kwake nusu nusu na kwa muda tu. Wafuasi wanapaswa, si tu kuwa tayari kupoteza chochote, bali kupoteza hata uhai wenyewe. Yesu anahitaji mtu awe jasiri kuacha vyote ikiwemo vitu na vitegemewa vyote kwa ajili ya, apendo. Kinachohitajika ni msimamo mmoja na kumpokea na kumkubali kwa moyo mmoja.

Sehemu ya pili ya Injili hii inahusu ahadi yake kuu – zawadi yake na utimilifu wake. “Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake.”

Sala: Ee Yesu nisaidie niweze kukufuata kwa moyo wote. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 13, 2026



MASOMO YA MISA, JULAI 13, 2026
JUMATATU, JUMA LA 15  LA MWAKA


SOMO 1
Isa. 1:10 – 17

Lisikieni neno la Bwana, enyi waamuzi wa Sodoma; tegeni masikio msikie sharia ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora. Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani? Asema Bwana. Nimejaa mafuta ya kafara za kondoo waume, na mafuta ya kafara za kondoo waume, na mafuta ya wanyama walionona; name siifurahi damu ya ng’ombe wala ya wanakondoo wala ya mbuzi waume. Mjapo ili kuonekana mbele zangu, ni nani aliyetaka neno hili mikononi mwenu, kuzikanyaga aliyetaka neno hili mikononi mwenu, kuzikanyaga nyua zangu?

Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. Sikukuu zenu za mwezi mpya na karama zenu za mwezi mpya na karama zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo haya yanilemea; nimechoka kuyachukua.

Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengu, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.

Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; achene kutenda mabaya; jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 50: 8 – 9, 16 – 17, 21, 23 (K) 23

(K) Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,
Na kafara zako ziko mbele zangu daima.
Sitatwaa ng’ombe katika nyumba yako,
Wala beberu katika mazizi yako. (K)

Una nini wewe kuitangaza sharia yangu,
Na kuliweka agano langu kinywani mwako?
Maana wewe umechukia maonyo,
Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. (K)

Ndivyo ulivyofanya, name nikanyamaza,
Ukadhani ya kuwa Misri ni kama wewe.
Atoaye ya kuwa Misri ni kama wewe.
Atoaye dhabihu za kushukuru ndiye anayenitukuza.
Nitamwonyeshsa wokovu wa Mungu. (K)



SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Ee Bwana unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.



INJILI
Mt 10: 34 - 11: 1.

Yesu aliwafundisha mitume wake: Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta Amani duniani; la! Sikuja kuleta Amani, bali upanga. Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, nab inti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.

Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki. Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake.

Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MBEGU NI NENO LA MUNGU


"ASALI ITOKAYO MWAMBANI"
Tafakari ya kila siku
Jumapili, Julai 12, 2026, 
Juma la 15 la Mwaka
           
Isa. 55: 10-11
Ps. 64:10-14
Rom. 8:18-23
Mt 13:1-23


MBEGU NI NENO LA MUNGU

Neno liwe, limezungumzwa au kuandikwa, lina ushawishi mkubwa kwetu sisi sote. Kwa mfano: Mwalimu anaposema kitu, wanafunzi hufanya. Wazazi wanaposema kitu, watoto hutii.wazee huzungumza na vijana, husikiliza, na kathalika. Yale tunayoyaona au kusikiliza kupitia TV, Redio au kwenye magazeti yana ushawishi mkubwa sana kwetu sote. Hakuna anayeweza kukataa hili. 

Lakini swali linabaki, kama maneno ya mwanadamu, yana ushawishi mkubwa namna hiyo kwetu, je, ni kwa nini maneno ya Mungu, yanachukua muda mrefu katika kutushawishi? Au, ni kwa nini yanachukua muda mrefu, kuingia mioyoni mwa watu? Jibu linapatikana katika mfano wa mpanzi, anaoutoa Bwana Yesu katika Injili ya leo.

Katika mfano huu, Bwana Yesu anajulishwa kwetu kama mkulima, na mbegu ni neno la Mungu. Mbegu hizo, zilizoanguka kwenye njia, miamba, miiba, na penye udongo mzuri, zinawakilisha makundi ya watu wa aina mbalimbali, ambao husikiliza neno la Mungu. Wengine walilipokea hilo neno, na kulikataa mara moja. Wengine walilipokea, lakini baadaye wakalisahau, na wengine walilipokea, wakalikubali na kulistawisha. Katika makundi yote haya, neno la Mungu lilipokelewa kwa furaha, isipokuwa kundi moja tu, ambalo lililikataa mara moja. Kwa hiyo, tatizo haliko kwenye kupokea neno la Mungu, bali tatizo lipo ni jinsi gani ya kulitunza na kuliishi. Kwa hakika, tunaweza kusema kwamba, kuna hatua tatu za kulienzi neno la Mungu, ambazo ni kulipokea, kulihifadhi na kuliishi.

Hatua ya kwanza, ni kulipokea neno la Mungu, hapo ndipo akili inaposhirikishwa, hii ni kwa njia ya kusikiliza kwa makini kile kinachosemwa na kufafanuliwa.

Hatua ya pili, kulihifadhi hilo neno la Mungu hii inashirikisha moyo, ambao huangalia matumizi ya hilo neno katika maisha yetu, na jinsi gani linaweza kustawisha maisha yetu ya kila siku. Hii inatakiwa kufanyika kwa wiki nzima mara baada ya neno la jumapili.

Hatua ya tatu, ni jinsi gani ya kuliishi hilo neno la Mungu ambalo akili imelipokea na moyo kulihifadhi. Yaani, roho zetu!

Hatua zote hizi tatu, zinaweza kuelezeka kwa kusikiliza mfano ufuatao. Kuna hadithi inayomuhusu mtu mmoja aliyeitwa Ndg. Bill, ambaye alikuwa ni Contracta wa kudumu. Katika muda Fulani, hali ya biashara yake ilimfanya awe mlevi. Hivyo, alifilisika kibiashara na kutengana na familia yake. Siku moja, alipokuwa anatembea mitaani, aliona msumari wenye kutu na uliojikunja. Bill aliwaza moyoni mwake ‘maisha yangu ni kama huu msumari! Mimi nami ninakutu na kupinda, mimi si chochote, na si lolote ni wakutupwa nje kama huu msumari’.

Lakini aliokota ule msumari na kuweka mfukoni mwake. Alipofika nyumbani alichukua nyundo na kuanza kuunyoosha na baadaye alichukua msasa na kuusugua. Halafu akachua msumari mpya na kuchanganya pamoja na ule aliouokota. Ilikuwa vigumu sana kwake kuitofautisha. Ndipo, alipoanza kuyafikiria maisha yake, kwamba yanaweza kunyoka na kutu iliyomo ikaondoka kama ule msumari. Lakini inawezekana? Je, alikuwa tayari kuvumilia mapigo ya nyundo pamoja na msasa? Aliamua kujaribu! Hivyo, alijikuta maisha yake yakibadilika na akaungana tena na familia yake na kurudi kwenye kazi yake ya ukontracta.

Katika hadithi hii, tumeona hatua tatu. Hatua ya kwanza ni ushirikishwaji wa akili, ambapo ni pale Bill, alipogundua kwamba yeye hana tofauti na ule msumari uliopinda. Hatua ya pili, ni ushirikishwaji wa moyo, ambapo Bill, aliamua kuunyoosha na kuusugua, ule msumari na kutambua kwamba yeye naye anaweza akayanyoosha maisha yake. Na hatua ya tatu, ni ushirikishwaji wa moyo/roho, ambapo Bill, anaamua kubadilisha mwendo wa maisha yake.
 
Kama somo la kwanza, linavyotuasa kwamba neno litazaa matunda iwapo tu tutalipokea, kuliifadhi na kuliishi. Ndw, ni rahisi kulisikiliza neno la Mungu. Lakini, je, ni rahisi kuliishi? Hivyo kama alivyofanya Bill, nasi tunaalikwa kujaribu. Kwani kwa kujaribu ndipo mabadiliko hutokea, kwa hiyo katika ibada hii tumwombe Mkombozi wa dunia Bwana Yesu, atupe neema ili tuweze kuliishi neno lake analotulisha kila siku.

Sala: Bwana nisaidie mimi niweze kuwa udongo mzuri wa neno lako. Ninakuomba nisikilize yote unayoniambia ili niweze kupanda mbegu ya imani ndani mwangu. Ninakuomba Imani hii ikuwe na kuleta Baraka unazotaka. Yesu nakuamini wewe. Amina 


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, JULAI 12, 2026

 


MASOMO YA MISA, JUMAPILI, JULAI 12, 2026
JUMA LA 15 LA MWAKA


SOMO 1
Isa 55:10-11

Kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 65:9-13

(K) Mbegu nyingine zikaanguka penye udongo mzuri zikamea, zikazaa.

Umeijilia nchi na kuisitawisha,
Umeitajirisha sana;
Mto wa Mungu umejaa maji;
Wawaruzuku watu nafaka Maana ndiwe uitengenezaye ardhi.

Matuta yake wayajaza maji; Wapasawazisha palipoinuka,
Wailainisha nchi kwa manyunyu; Waibariki mimea yake.

Umeuvika mwaka taji ya wema wako;
Mapito yako yadondoza unono.
Huyadondokea malisho ya nyikani,
Na vilima vyajifunga furaha.

Na malisho yamevikwa kondoo,
Na mabonde yamepambwa nafaka,
Yanashangilia, naam, yanaimba.



SOMO 2
Rum 8:18-23

Ndugu, nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu. Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa. Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Efe 1:17, 18

Aleluya, aleluya
Baba wa Bwana wetu Yesu Kristu, Ayatie nuru macho ya mioyo yetu, Ili tujue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo.
Aleluya.



INJILI 
Mt 13:1-23

Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari. Wakamkusanyikia makutano mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani. Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda. Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila; nyingine zikaanguka penye miamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara zikaota, kwa udongo kukosa kina; na jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka. Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga; nyingine zikaanguka penye udongo mzuri, zikazaa, moja mia, moja sitini, moja thelathini Mwenye masikio na asikie. Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano? Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa. Kwa maana ye yote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini ye yote asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa. Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa. Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. Lakini, heri macho yenu, kwa kuwa yanaona; na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia. Kwa maana, amin, nawaambia, Manabii wengi na wenye haki walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi, wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi, wasiyasikie. Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi. Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia. Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha; lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa. Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai. Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

USIOGOPE!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Julai 11, 2026 
Tafakari ya kila siku
Juma la 14 la Mwaka wa Kanisa


Is 6: 1- 8; 
Zab 92: 1-5; 
Mt 10: 24 -33


USIOGOPE!


Tunaishi katika ulimwengu uliojawa wasiwasi tukiwa na hakika pia ya matukio ya kweli yanayotokea katika maisha. Tuna wasiwasi nini kitatokea kwetu tukumbanapo na ajali, au tukifilisika kifedha, au kama kutakuwa na vita, migomo au machafuko na mengine mengi. Kwa mawazo haya yaliopo mbele yetu huwa tunayaweka maisha yetu katika wasiwasi na pia kujijengea ulinzi mkubwa, pia wakati huo huo tuanasema tumeyaweka matumaini yetu kwa Yesu.

Woga na hofu tunayoiona katika maisha ya nabii Isaya, ndio hiyo hiyo inayotukumba sisi kutokana na matokeo ya maumivu ya dhambi tunazopalilia ndani mwetu. Kukabiliana na hali kama hiyo, Yesu anatutia moyo kwakusema “usiogope”. Na anatupa nguvu tunayohitaji ya kuachana na wasiwasi na hofu ya kujijengea ulinzi, na anatutaka tuweke matumaini yetu kwa Mungu ili tuweze kufurahia neema anazotujalia. 

Ni Mungu mwenyewe anayetawala kiu ya roho zetu akiwasha ndani mwetu mwali wa matumani ili tumpende yeye na kumuamini yeye peke yake. Sisi tukiwa na matumaini yetu ya kweli yaliojikita kwa Mungu tunapokea fadhila na tunu za nguvu yakukabiliana na changamoto za ulimwengu na ndipo tutatangaza neno la Mungu ulimwenguni bila woga na wasiwasi. Tunu hii ya matumani inayotawala ndani mwetu inatufanya tuwe kama Kristo mwenyewe na kwa moyo wa furaha tutaitika na kujibu kwakusema “Nipo hapa Bwana, nitume mimi!”. Tukijua kwamba kazi ya kumtangaza Kristo ni kazi ya kila mbatizwa, sio kazi ya wachache. Tujitahidi sasa sisi wote kumfanya Kristo ajulikane Ulimwenguni bila kuwa na hofu na wasiwasi na tuendelee kumuomba ili tuweze kustahili kupokea kile alicho tuandalia Mbinguni. 

Sala: Bwana, nisafishe dhambi yangu na ifanye safi dhamira yangu, ondoa hofu na woga moyoni mwangu, nijaze mapendo, ili niweze kuwa mfuasi wako mwaminifu. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 11, 2026



MASOMO YA MISA, JULAI 11, 2026
JUMAMOSI, JUMA LA 14 LA MWAKA

SOMO 1
Isa. 6: 1 – 8

Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, nap indo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.

Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.

Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, name ninakaa katik aya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.

Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa change kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na hdambi yako imefunikwa.

Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 93: 1 – 2, 5 (K) 1

(K) Bwana ametamalaki, amejivika adhama.

Bwana ametamalaki, amejivika adhama,
Bwana amejivika, na kujikaza nguvu. (K)

Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;
Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani;
Wewe ndiwe uliye tangu milele. (K)

Shuhuda zako ni amini sana;
Utakatifu ndio uifaao nyumba yako,
Ee Bwana, milele na milele. (K)


SHANGILIO
1 Thes. 2:13

Lipokeeni neno la Mungu, siyo kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu.
Aleluya.


INJILI
Mt. 10:24 – 33

Yesu aliwafundisha mitume wake: Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake. Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli; je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake?

Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba. Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum. Je! Mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu; lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi; bora nyinyi kuliko mashomoro wengi.

Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbel za Baba yangu aliye mbinguni. Basil mtu yeyote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

KONDOO NA MBWA MWITU!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Julai, 10, 2026
Tafakari ya kila siku
Juma la 14 la Mwaka wa Kanisa

Hos 14: 2-10; 
Zab 50: 3-4, 8-9, 12-14, 17; 
Mt 10: 16-23


KONDOO NA MBWA MWITU!

“Mti unaozaa matunda mazuri hupigwa mawe mengi”; vile vile Mkristo anayeshika kiaminifu tunu za Injili anapata mateso mengi. Katika Injili ya leo Yesu anatupa maelekezo nini cha kufanya wakati wa mambo kama hayo yanapotokea kwetu. “Nina watuma kama kondoo kati ya mbwa mwitu”. Yesu anatuita kondoo kwasababu hatutumii fujo wala vita, bali tunatumia ujumbe wa upendo, msamaha, Amani na haki kama silaha ya kuwatibia maadui na watesi wetu. Tunu hizi za kiroho mara nyingi kwao zinakuwa sumu na wanakuwa na hasira zaidi nakutaka kutuangamiza, lakini Yesu anatuambia ndio njia sahihi kabisa yenye tabia za Kimungu. 

Pili, “Muwe na busara kama nyoka wenye upole kama njiwa”. Tunapaswa kuwa wabunifu na wenye kuzaa matunda mema kawasababu tutakukumbana na mambo ya ulimwengu bila hivyo tunaweza kutekwa na kuanza kuwa kama wa ulimwengu pia. 

Tatu, “msiwe na wasiwasi mtasema nini au mtasema namna ghani”. Roho Mtakatifu aliyewashukia Mitume siku ile ya Pentekoste na kuwajaza nguvu wakatao ushuhuda juu ya Kristo atawaimarisha na ninyi pia. Sisi pia tumempokea Roho Mtakatifu kwa ubatizo wetu, atatuongoza na ataongea ndani mwetu wakati tunavyo ulizwa maswali na mamlaka ya ulimwengu huu, kama tuta shirikiana naye. Kwa nguvu zetu wenyewe bila msaada wake tutashindwa.

Neno la Kristo linatutia nguvu na kututia moyo katika hali ya vitisho na misukosuko yahusuyo Imani yetu. Kama Wafuasi wa Yesu mmoja wetu anaweza kupatwa na changamoto katika maisha, labda kuhukumiwa bila hatia, kuvunjika kwa familia, au kuonewa na kutengwa na jamii na mengine mengi. Katika nyakati hizi mmoja hapaswi kuwa kama mbwa mwitu (hasira, kulaumu na kulaani) , bali anapaswa kuwa kama kondoo akiendelea kuzishika tunu za Injili na kutoa ushuhuda wa Yesu kwa ujasiri na hekima. Yote yakiwa yametimilika katika mapendo ya Kristo, lengo la maisha yetu litakuwa limetimilika na tutapata tuzo katika maisha ya umilele. 

Sala: Bwana wangu, nifanye mimi nitambue njia yako na uniongoze katika njia hiyo ili niweze kufuata kiaminifu neno lako na kuwa shuhuda wako. Amina.


Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 10, 2026



MASOMO YA MISA, JULAI 10, 2026
IJUMAA , JUMA LA 14 LA MWAKA

SOMO 1
Hos. 14: 2 – 9

Bwana anasema: Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo tutakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe. Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema. Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha. Nitakuwa kama umande kwa Israeli; naye atachanua maua kama nyiroro, na kuieneza mizizi yake kama Lebanoni.
Matawi yake yatatandaa, na uzuri wake utakuwa kama uzuri wa mzeituni, na harufu yake kama Lebanoni. Na wao wakaao chini ya uvuli wake watarejea; watafufuka kama ngano, na kuchanua maua kama mzabibu; harufu yake itakuwa kama harufu ya divai ya Lebanoni.
Efraimu atasema, Mimi nina nini tena na sanamu? Mimi nimeitika, name nitamwangalia. Mimi ni kama mberoshi wenye majani mabichi. Kwangu mimi yamepatikana matunda yako.
Ni nani aliey na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliey na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 51: 1 – 2, 6 – 7, 10 – 11, 15 (K) 15

(K) Ulimi wangu utaiimba haki yako.

Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako. 
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu. (K) 

Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni,
Nawe utanijulisha hekima kwa siri,
Unisafishe kwa hisopo name nitakuwa safi,
Unioshe, name nitakuwa mweupe kuliko theluji. (K)

Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.
Usinitenge na uso wako,
Wala roho yako mtakatifu usiniondolee. (K)

Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,
Na kinywa change kitazinena sifa zako. (K)

SHANGILIO
1 Pet. 1:25

Aleluya, aleluya,
Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu. 
Aleluya.

INJILI
Mt. 10: 16 – 23

Yesu aliwaambia mitume wake: Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.
Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa. Lakini hapo watakapowapeleka, msifikirifikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema. Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu ndani yenu.
Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwafisha. Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka. Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

UWEZO KATIKA UTUME!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Julai 9, 2026, 
Tafakari ya kila siku
Juma la 14 la Mwaka wa Kanisa


Hos 11:1-4, 8-9; 
Zab 79:2-3, 15-16; 
Mt 10:7-15


UWEZO KATIKA UTUME!


Yesu mwana wa Mungu, alitumwa Ulimwenguni kwa Upendo wa Baba, alitangaza Ufalme wa Mungu ndani ya ufalme wa mwanadamu, ili watoke kutoka katika utawala wa yule mwovu. Akitutaka wadhambi kama mimi na wewe, tuache dhambi tushirikiane naye katika kuokoa ulimwengu kutoka katika giza la kifo na mauti, aliwachagua wafuasi kumi na wawili akawaita mitume mwazoni kabisa mwa utume wake. Kwa hawa aliwapa mafundisho maalumu kwaajili ya utume wao, akawapa uwezo wakutoa pepo, kufufua wafu na kuponya magonjwa mbali mbali.

Injili inomuonesha Yesu kama daktari mkuu, akiwaponya wenye ukoma, waliopooza, vipofu na viziwi, na hata kuwafufua wafu. Yesu, sasa anawashirikisha mitume wake nguvu hizi, ambao watakuwa mawakili wa kutangaza ufalme wa Mungu. Kama ilivyo katika elimu, mafunzo ya kijeshi, au mafunzo yeyote., inawapa watu ujuzi wa maisha, pia mitume wa Yesu walihiitaji mafundisho ili waweze kuwa na kiwango cha kutangaza Ufalme wa Mungu. Ufukara ulipaswa kuwa silaha yao dhidi ya hekima ya ulimwengu, na Amani ilipaswa kuwa matunda ya hekima yao. Walipaswa wamtegemee Mungu na pia kwa msaada wa waliowapa watu. Hii ni jinsi ghani Yesu alivyojua vizuri pesa ni chanzo cha maovu mengi. 

Ni kwa jinsi ghani wakati mwingine Kanisa limedhoofishwa katika utume wake kwasababu ya kuwa dhaifu katika pesa, pengine utajiri na tamaa. Uwezo wa Kanisa unakuja kwa ufukara wake na misaada ambapo unyenyekevu wa kweli ndio msingi wake. Chanzo kingine cha uwezo wa utume ni Amani ya ndani na utulivu unaotoka katika dhamira iliyo safi na yenye unyenyekevu wa kweli. Mtume wa kweli anabaki mtulivu pale anapo kubaliwa au kukataliwa. 

Sala: Roho Mtakatifu, tunaomba utufanye Wakristo wapya, na zaidi sana watumishi wako makleri waweze kuwa mitume wa kweli siku zote. Amina.

Copyright ©2013-2026 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JULAI 9, 2026






MASOMO YA MISA, JULAI 9, 2026
ALHAMISI, JUMA LA 14 LA MWAKA


SOMO 1
Hos. 11:1, 3 -4, 8 – 9

Bwana anasema: Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misrei. Lakini nalimfundisha Efraimu kwenda kwa miguu; naliwachukua mikononi mwangu; hawakujua ya kuwa naliwaponya. Naliwavuta kwa Kamba za kibinadamu, kwa mafungo ya upendo; name nalikuwa kwao kama hao waondoao kongwa tayari mwao, nikaandika chakula mbele yao.

Niwezeje kukuacha, Efraimu? Niwezeje kukuponya, Israeli? Niwezeje kukufanya kama Adma? Niwezeje kukuweka kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zimewaka pamoja. Sitatumia ukali wa hasira yangu, sitarudi kumwangamiza Efraimu; kwa maana mimi ni Mungu, si mwanadamu mimi; mimi ndiye aliye Mtakatifu katikati yenu; wala sitaingia ndani ya mji.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 80: 1 – 2, 14 – 15 (K) 3

(K) Uangazishe uso wako, Ee Bwana, nasi tutaokoka.

Wewe uchungaye Israeli, usikie,
Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi;
Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru.
Uziamshe nguvu zako.
Uje, utuokoe. (K)

Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi,
Utazame toka juu uone, uujilie mzabibu huu.
Na mche ule ulioupanda
Kwa mkono wako wa kuume;
Na tawi lile ulilolifanya
Kuwa imara kwa nafsi yako. (K)


SHANGILIO
Yak. 1:18

Aleluya, aleluya,
Kwa kupenda kwake mwenyewe, Baba alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.
Aleluya.


INJILI
Mt. 10: 7 – 15

Yesu aliwaambia mitume wake: Katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takasene wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. Msichukue dhahabu, wala fedha wala mapesa mishipini mwenu; wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake.

Na mji wowote au kijiji chochote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; make kwake hata mtakapotoka. Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni. Na nyumba ile ikistahili, Amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, Amani yenu na iwarudie ninyi. Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu. Amin, nawambia, Itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2026, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com