MASOMO
YA MISA, NOVEMBA 19, 2020
ALHAMISI,
JUMA LA 33 LA MWAKA
SOMO
1
Ufu.
5:1 – 10
Mimi,
Yohane, niliona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha
enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na nyumba, kimetiwa muhuri saba. Nikaona
malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, N’nani astahiliye kukifungua
kitabu, na kuzivunja muhuri zake? Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya
nchi, wa la chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama.
Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kukifungua hicho
kitabu, wala kukitazama. Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama,
Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye aliye na kabila ya Yuda,
Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri
zake saba.
Nikaona
katikati ya kiti cha enzi na wale wenye uhai wane, na katikati ya wale wazee,
Mwanakondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na
macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote. Akaja,
akakitwaa kile kitabu katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile
kiti cha enzi. Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wane na wale wazee
ishirini na wane wakaanguka mbele za Mwanakondoo, kil ammoja wao ana kinubi, na
vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.
Nao
waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua
muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila
kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu
wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.
Neno
la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO
WA KATIKATI
Zab.
149:1 – 6, 9 (K) Ufu. 5:10
(K)
Ulitufanya kuwa wafalme na makuhani.
Aleluya.
Mwimbieni
Bwana mwimbo mpya,
Sifa
zake katika kusanyiko la watauwa.
Israeli
na amfuhie Yeye aliyemfanya,
Wana
wa SAyuni na wamshangilie mfalme wao. (K)
Na
walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa
matari na kinubi wamwimbie.
Kwa
kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba
wenye upole kwa wokovu. (K)
Watauwa
na waushangilie utukufu,
Waimbe
kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa
kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Hiyo
ndiyo heshima ya watauwa wake wote.
Aleluya.
(K)
SHANGILIO
Yn.
17:17
Aleluya,
aleluya,
Neno
lako ndiyo kweli, Ee Bwana, ututakase kwa ile kweli.
Aleluya.
INJILI
Lk.
19:41-44
Yesu
alipofika karibu ya Yerusalemu aliuona mji, akaulilia, akisema, Laiti
ungalijua, hata wewe, katika siku hii, yapasayo Amani! Lakini sasa yamefichwa
machoni pako. Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma,
likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote; watakuangusha chini wewe
na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua
majira ya kujiliwa kwako.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.
-------------------------
Copyright
© 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment