NOVENA YA HURUMA YA MUNGU
SIKU YA TATU: DOMINIKA YA
PASAKA
NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA
HURUMA YA MUNGU
Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi
zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi
sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako,
Amina.
Nia ya sala za leo:
SIKU YA TATU
Maneno ya Bwana Yesu: “Leo niletee roho za watu wenye uaminifu na uchaji wa Mungu, na uwazamishe
katika Bahari Kuu ya Huruma yangu. Roho za watu hawa ndizo zilizonifariji
katika njia ya Msalaba. Wao ndio waliokuwa tone lile la faraja nilipokuwa
katikati ya bahari ya uchungu na mateso.”
Tuwaombee watu wote waaminifu
na wenye ibada ambao walimtuliza Yesu katika mateso yake.
W. Ee Yesu mpole na mwenye huruma sana, Wewe huchota neema kwa wingi kutoka
katika hazina Yako, na kuzigawa kwa ukarimu kwa kila mmoja wetu na kwa watu
wote. Tunakuomba utupokee katika makao ya Moyo wako mpole na wenye huruma
nyingi, na usituache tutoroke humo kamwe. Tunakuomba neema hii, kwa ajili ya
mapendo ya ajabu, yawakayo moyoni mwako kwa Baba yako wa mbinguni. Amina.
Baba yetu ……. Salamu Maria …… Atukuzwe
……
W. Baba wa Milele, elekeza macho yako yenye huruma, kwa watu wote walio
waaminifu, kama vile kwenye hazina na urithi wa Mwanao. Kwa ajili ya mateso
yake ya kuhuzunisha, uwajalie Baraka zako, na ulinzi wako daima. Kwa njia hii,
waweze kuimarika katika upendo, na wala wasije wakapoteza hazina bora ya Imani
Tashi Takatifu, bali, pamoja na majeshi yote ya malaika na watakatifu, waweze
kuisifu na kuitukuza huruma yako isiyo na mwisho, kwa milele yote. Amina.
Rozari ya Huruma ya
Mungu
(Tumia chembe za rozari ya kawaida)
Baba yetu
… Salamu Maria ….
x3 Nasadiki
kwa Mungu Baba Mwenyezi …….
Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea
Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu,
kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso
makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Mwisho wa Rozari sali mara
tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu
mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Litania ya Huruma ya Mungu
No comments:
Post a Comment