NOVENA YA HURUMA YA MUNGU
SIKU YA NNE: JUMATATU BAADA YA
PASAKA
NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA
HURUMA YA MUNGU
Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi zangu, kwani ndiwe mwema,
ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena,
nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako, Amina.
Nia ya sala za leo:
SIKU YA NNE
Maneno ya Bwana Yesu: “Leo niletee wale wote wasioniamini na
wale wasionijua bado. Wao pia niliwafikiria wakati wa mateso yangu makali, na
juhudi watakayokuwa nayo baadaye ilinituliza Moyo wangu. Uwaingize katika
Bahari Kuu ya Huruma Yangu.”
Tuwaombee watu wote
wasiomwamini Kristu, pamoja na wale wasiomjua bado.
W. Ee Yesu mwema, Wewe ni Mwanga wa dunia nzima, uzipokee katika makao ya Moyo
wako wenye huruma sana, roho za wale wote wasiokuamini na wale wasiokujua bado.
Achia mionzi ya neema yako iwaangazie, ili nao pia pamoja nasi sote. Waweze
kuitukuza huruma yako ya ajabu, na usiwaache wakatoroka makao hayo, ambayo ni
Moyo wako uliojaa huruma. Amina.
Baba yetu ……… Salamu Maria …….
Atukuzwe ………
W. Baba wa Milele, elekeza macho yako yenye huruma, kwa roho za watu wale
wasiomwamini Mwanao, na za wale ambao hawajakujua Wewe bado, ambao tumewaingiza
ndani ya Moyo wa Yesu uliojaa huruma tele. Uwavute kwenye mwanga wa Injili,
watu hawa hawajui Ukuu wa furaha iliyopo katika kukupenda Wewe. Uwajalie nao
pia waweze kuitukuza hisani ya huruma yako, kwa miaka isiyo na mwisho. Amina.
Rozari ya Huruma ya
Mungu
(Tumia chembe za rozari ya
kawaida)
Baba yetu
… Salamu Maria ….
x3 Nasadiki
kwa Mungu Baba Mwenyezi …….
Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea
Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu,
kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso
makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Mwisho wa Rozari sali mara
tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu
mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Litania ya Huruma ya Mungu
No comments:
Post a Comment