Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

NOVENA YA HURUMA YA MUNGU SIKU YA PILI: JUMAMOSI KUU




NOVENA YA HURUMA YA MUNGU
SIKU YA PILI: JUMAMOSI KUU

NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA HURUMA YA MUNGU

Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako, Amina.

Nia ya sala za leo:
SIKU YA PILI

Maneno ya Mwokozi: “Leo niletee mapadri wote na watawa. Uwazamishe katika kilindi cha huruma yangu isiyo na mwisho. Ni wao hasa walionipa nguvu ya kuweza kuyavumilia mateso yangu makali mno. Kwa njia yao, kama vile mifereji, huruma yangu humiminika na kuwatiririkia wote. Tuwaombee watawa wote wanawake ili wadumu kiaminifu katika utumishi wao na wakfu wa maisha yao kwa Yesu Kristu Bwanaharusi wao.”

W. Ee Yesu mwenye huruma tele, kwako hutoka mema yote. Uwazidishie neema yako watawa wanawake waliojitolea na kuwekwa wakfu katika utumishi wako, ili watekeleze utumishi wao kwa huruma na kwa jinsi inayofaa, na kwamba wale wanaowaona na kuzishuhudia kazi zao bora, waweze kumtukuza Baba wa Huruma aliye mbinguni. Amina.

Baba yetu ……. Salamu Maria …… Atukuzwe ……

Tuwaombee mapadri na watawa wote ambao ni vyombo vya huruma ya Mungu.

W. Baba wa Milele, elekeza macho yako yenye huruma, juu ya jeshi teule la wafanyakazi shambani mwako. Uzitazame kwa wema roho zao mapadre na watawa wote. Uwajalie wingi wa Baraka zako. Kwa njia ya upendo wa Moyo wa Mwanao, humo ambamo wameingizwa, uwape nguvu na mwanga, ili waweze kuwaongoza wengine katika njia ya wokovu, na kwa sauti moja, waihimidi huruma yako kwa nyimbo za sifa bila mwisho. Amina.


Rozari  ya Huruma ya Mungu
(Tumia chembe za rozari ya kawaida)
Baba yetu …       Salamu Maria …. x3            Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi …….

Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.

kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.

Mwisho wa Rozari sali mara tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.


Litania ya Huruma ya Mungu



No comments:

Post a Comment