Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

WATOTO WA MWANGA


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumanne, Septemba 5, 2023,
Juma la 22 la Mwaka wa Kanisa

Kumbukumbu ya Mt. Teresia wa Kolkota.

1 Thes 5: 1-6, 9-11;
Zab 27: 1, 4, 13-14;
Lk 4: 31-37


WATOTO WA MWANGA

Yesu ambaye aliweza kuonesha “mvuto mkubwa wa ndani sana” wakati anafundisha. Na walifananisha na mamlaka aliyo ongelea. Yesu hakuwa kuhani wa kipindi hicho, wala Mfarisayo au mwalimu wa sheria. Hawa ndio watu waliokuwa na mamlaka ya kufundisha na kufafanua neno la Mungu. Watu waliuliza “ni kitu ghani kilichopo katika mafundisho yake”, neno lake lilikuwa na mvuto na msukumo mkubwa kwasababu ya uhusiano wake na Baba yake. Maneno ya Yesu yalibeba mamlaka na msukumo mkubwa.

Mamlaka hayo hayo tumepewa sisi wote, kila Mkristo. Tunaitwa kutoa ushuhuda na kuhubiri. Furaha ya Injili tunayo hubiri au kuongea juu yake inabeba nguvu zaidi tunapokuwa na msukumu wa Yesu katika maisha yetu. Maneno yetu yanagusa mioyo ya watu yanapo toka katika chemchem hii ya furaha. Paulo akitumia mfano wa kulala na kuamka, anatuambia kwamba tutambue kwamba sisi ni watoto wa Mwanga, tunaojiandaa kwa ajili ya utukufu wa mbinguni, hivyo tunapaswa kuishi kama mwanga ulivyo. Sisi tunaitwa kutoa maisha ya ushuhuda, hatupaswi kuwa wakristo wa uvuguvugu, wavivu na walio lala, bali wachangamfu, wenye uhai na furaha, tuliojazwa na neno la upendo wa Kristo na Injili yake. Moto huu ndio ule moto alio udhihirisha Yesu wakati akihubiri neno, na kutoa pepo. Hili ndilo Kristo anapenda na sisi tufanye pia.

Leo tunasherekea , kumbukumbu ya Mt. Teresa wa Kolkota. Huyu mtakatifu alijazwa na upendo na msukumo wa Kristo. Aliongea kwa matendo yake, kuwalisha wenye njaa, kuwapa maji wenye kiu, akiwahudumia wagonjwa na wanao teseka, na kujali utu wao waliokuwa katika kufa. Alikuwa ni shuhuda wa upendo, katika jamii ambayo upendo ulikuwa umetelekezwa. Na akaanza kuleta mwanga katika giza kwa wale waliokuwa wamepotea, kunyanyaswa na kutengwa. Tujifunze leo katika liturjia ya leo jinsi ya kuwa watu wa mwanga.

Sala: Asante Bwana Yesu, kwa upendo wako na huruma yako. Umetubariki sisi na kutushirikisha katika mamlaka yako na msukumo wako, tuwe mwanga katika ulimwengu uliojazwa giza. Nipe nguvu mimi niweze kuwa karibu nawe na niwe mtoto wa mwanga. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2023 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

1 comment: