Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA DESEMBA 9, 2022


MASOMO YA MISA DESEMBA 9, 2022
IJUMAA, JUMA LA 2 LA MAJILIO


SOMO 1
Isa. 48:17-19

Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi: Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu! Ndipo Amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari; tena wazao wako wangalikuwa kama mchanga, na hao waliotoka katika tumbo lako kama chembe zake; jina lake lisingali katika, wala kufutwa mbele zangu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 1:1-4,6 (K) Yn. 8:12

(K) Akufuataye, Bwana, atakuwa na nuru ya uzima.

Heri mtu yule asiyekwenda,
Katika shauri la wasio haki,
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. (K)

Naye atakuwa kama mti uliopandwa,
Kandokando ya vijito vya maji.
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa. (K)

Sivyo walivyo wasio haki,
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea. (K)



SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Bwana atakuja, nendeni kumlaki, Yeye ni mfalme wa Amani.
Aleluya.



INJILI
Mt. 11:16-19

Siku ile, Yesu aliwaambia makutano: Lakini nitakifananisha na nini kizazi hiki? Kimefanana na watoto wanaokaa sokoni, wanaowaita wenzao, wakisema, Tuliwapigia filimbi, wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.

Maana Yohane alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo. Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment