“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Novemba 8, 2022
Juma la 32 la Mwaka wa Kanisa
Tit 2:1-8, 11-14;
Zab 36:3-4, 18, 23, 27, 29;
Lk 17:7-10
MTUMISHI MWAMINIFU!
Katika somo la kwanza tunamuona Paulo akiendelea
kumwambia Tito, aendelee kunena maneno ya uzima yenye kuwaelekeza watu wa rika
mbali mbali katika maisha ya ufuasi wa Kristo. Na zaidi sana wanadamu wote
wanaongozwa na neema ya Mungu ili waweze kupingana na yote duniani yasio endana
na mapenzi ya Mungu. Wazee, wa kike na wakiume na vijana wawe watu wakiasi,
wazima katika Imani, upendo na saburi, wazee wawe mfano kwa watoto wao. Hizi ni
sifa za mtumishi mwaminifu wa Kristo anayetambua kuwa yeye ni mtumishi tu, na
kwamba kila afanyalo linapaswa kuwa kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu.
Katika hali hiyo hiyo, somo la Injili leo Yesu
anatutaka tutambue ya kuwa sisi ni watumishi tu tulioko duniani. Kila tulicho
nacho,pamoja na maisha yetu ni zawadi ya bure kutoka kwa Mungu na kama viumbe
vyake sisi ni mali yake. Nguvu zetu, muda na vyote tulivyo navyo ni mali ya
Mungu ni kwa ajili ya sifa na utukufu wake. Kama Yesu alivyokuja, “si kutumikiwa
bali kutumikia” tunapaswa kuwa watumishi wanyenyekevu wa Mungu, tukimtumikia
Mungu na jirani zetu kwa uhuru kamili. Kila zawadi tutakayo pokea itakuwa ni
neema na sio kama kutafuta faida, na hatimaye mwisho wa nyakati kwa watumishi
wa aminifu, Bwana atawaambia “vyema mtumishi mwema na mwaminifu”(Mt 25:21)
Sala: Bwana, nisaidiye
nibaki mnyenyekevu ili niweze kukutumikia wewe na jirani zangu bila kutaka
faida. Amina
No comments:
Post a Comment