Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

JE, TUNAPATA UTUKUFU KATIKA YERUSALEMU YA ZAMANI AU KATIKA YERUSALEMU MPYA?


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Novemba 17, 2022
Juma la 33 la Mwaka wa Kanisa

Ufu 5:1-10;
Zab 149:1-6, 9;
Lk 19:41-44


JE, TUNAPATA UTUKUFU KATIKA YERUSALEMU YA ZAMANI AU KATIKA YERUSALEMU MPYA?


Mji wa Yerusalemu, na hekalu lake, ilikuwa ni alama ya dini ya Wayahudi, na kila Myahudi alijitambulisha kwa kutumia alama hiyo. Yesu, anatamani kufikisha ujumbe wake kwa wafuasi wake kwamba, sio Hekalu la duniani la mji wa Yerusalemu walilokuwa wakisemea manabii, bali Yerusalemu mpya, mji wa kiroho wa utawala wa Mungu. Somo la kwanza kutoka katika kitabu cha Ufunuo linaongelea kuhusu mji huu mpya wa Yerusalemu. Mwana-kondoo (Yesu Mwenyewe) kwa kumwaga damu yake, amewaokoa na kujipatia watakatifu wengi wa Mungu kutoka katika kila taifa, na sasa wanatawala katika Ufalme wa Mungu, Yerusalemu mpya. Je, unataka kuwa katika Yerusalemu ipi?

Sala: Bwana, nisadie nisipoteze macho yakutazama Yerusalemu mpya ulio iandaa kwa ajili yangu. Amina


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment