Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

26th APRIL 2024



 

MBINGUNI NI NYUMBANI KWETU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Aprili 26, 2024, 
Juma la 4 la Pasaka

Mdo 13: 26-33; 
Zab 2: 6-11; 
Yn 14: 1-6.


MBINGUNI NI NYUMBANI KWETU!

Mara kwa mara ni muhimu kuweka jitihada kuelekea kwenye utukufu wa Mbinguni! Mbingu ipo na ni mapenzi ya Mungu sisi wote siku moja tufurahi na Utatu Mungu mmoja. Kama tunatambua kwa hakika kuhusu mbingu, tunakuwa tunaitamani kwa moyo wote na tunawaka mapendo na kuitazamia kwa nguvu kubwa, tukiwa tumejazwa na Amani na furaha kila wakati tuki ifikirie. Kwa bahati mbaya, habari za kuacha ulimwengun huu na kwenda kukutana na Muumba wetu kwa wengi zina ogopesha. Pengine ni hofu ya mambo yasio julikana, utambuzi wa kwamba tutawaacha wapendwa wetu, au hofu ya kwamba huenda tusiende mbinguni.

Kama Wakristo, ni vizuri kujishughulisha tukitambua upendo wetu mkubwa mbinguni kwa kupata utambuzi mkubwa wa sio mbinguni pekee, bali kutambua jukumu la maisha yetu hapa duniani. Mbingu inasaidia sisi tuweze kupanga maisha yetu kwa kupitia ile njia inayo tuongoza kwenye heri hiyo. Katika Injili, tunapewa picha nzuri sana yenye kufariji kuhusu Mbinguni, ambayo ni “Nyumba ya Baba”. Nyumbani ni sehemu salama. Ni sehemu ambayo tunaweza kufurahia na kuishi bila kujifanya, kuwa na wapendwa wetu, kupumzika, na kujisikia ni sehemu ya familia. Sisi ni watoto wa Mungu na hivyo Mungu anapenda sisi tuwe nyumbani pamoja naye. 

Kwa kutafakari juu ya picha hii, inapaswa pia iwe faraja kwa wale wote waliopoteza wapendwa wao. Hali ya kusema kwaheri, ni ngumu. Na inapaswa kuwa ngumu. Ugumu wa kupoteza wapendwa wetu inaonesha uwepo wa upendo wa kweli katika mahusiano. Lakini Mungu anapenda hali ya hisia za kupoteza wapendwa wetu ichanganyike na furaha tunapo tafakari ukweli wa wapendwa wetu kuwa wapo na Baba nyumbani milele. Wana furaha kule zaidi ya jinsi tunavyo weza kudhania, na siku moja nasi tutaitwa kushiriki furaha hiyo. 

Sala: Bwana, natamani daima kuwa nawe. Nisaidie daima niweke lengo hili daima akilini mwangu, na kukuwa nalo siku zote kwa tamaa ya kufurahi nawe milele. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 26, 2024



MASOMO YA MISA, APRILI 26, 2024
JUMA LA 4 LA PASAKA, IJUMAA


SOMO 1
Mdo. 13:26-33

Paulo alisimama akawapungia mkono, akasema: Ndugu zangu, wana wa ukoo wa Ibrahimu, na hao miongoni mwenu wanaomcha Mungu, kwetu sisi neno la wokovu huu limepelekwa. Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu. Na ijapokuwa hawakuona sababu ya kumfisha wakamwomba Pilato auawe. Hata walipokwisha kumaliza yote aliyoandikiwa, wakamtelemsha katika ule mti, wakamweka kaburini. Lakini Mungu akamfufua katika wafu; akaonekana siku nyingi na wale waliopanda naye kutoka Galilaya hata Yerusalemu, ambao sasa ndio walio mashahidi wake mbele ya watu.

Na sisi tunawahubiri habari njema ya ahadi ile waliyopewa mababa, ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili, Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 2:6-11 (K) 7

(K) Ndiwe Mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.
Au: Aleluya.

Nami nimemweka mfalme wangu
Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.
Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia,
Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. (K)

Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako,
Na miisho ya dunia kuwa milki yako.
Utawaponda kwa fimbo ya chuma,
Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi. (K)

Na sasa, enyi wafalme, fanyeni akili,
Enyi waamuzi wa dunia, mwadibiwe.
Mtumikieni Bwana kwa kicho,
Shangilieni kwa kutetemeka. (K)


SHANGILIO
Yn. 20: 29

Aleluya, aleluya,
Wewe Toma, umesadiki kwa kuwa umeniona, wa heri wale wasioona, wakasadiki.
Aleluya.


INJILI
Yn. 14:1-6

Siku ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yngu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia, maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendako mwaijua njia.

Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?

Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo. 

Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

25th APRIL 2024

 




KUJAZWA NEEMA NA KUTANGAZA NENO LA MUNGU KWA MAPENDO



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Aprili 25, 2024 
------------------------------------------------
ALHAMISI, JUMA LA 4 LA PASAKA
SIKUKUU YA MT. MARKO, MWINJILI

Somo la 1: 1 Pet 5:5-14 Somo linaongelea kuhusu Marko, ambaye Patro alimchukua kama mtoto wake. 

Wimbo wa Katikati : Zab 89: 2-3, 6-7, 16-17 Maisha yote midomo yangu itatangaza ukweli wako. 

Injili: Mk 16: 15-20 Yesu anawambia wale kumi na mmoja waende ulimwenguni kote; wakahubiri kwa mataifa yote. 
------------------------------------------------

KUJAZWA NEEMA NA KUTANGAZA NENO LA MUNGU KWA MAPENDO 

Leo kanisa linasheherekea sikukuu ya Mt. Marko Mwinjili. Yohane Marko anatokea katika kitabu cha Matendo ya mitume (Mdo 12:12), na mara nyingi ametajwa katika katika barua za Petro na Paulo. Katika barua fupi ya filemoni Marko ananukuliwa kama rafiki wa karibu wa Paulo…’.. Marko Mwanangu”. Kuna mapokeo pia kwamba Marko alikuwa ni mwanzilishi wa kanisa la Alexandria, kaskazini mwa Misri. Mwandishi wa Injili ya Pili pia inasemekana pia ya Marko. Mapokeo yanasema pia wakristo wa Roma alimuomba Marko aandike maneno ya Petro. Na Injili inaoneakana kuandikwa kama utume wa Yesu kama alivyo uona Petro na hivyo Marko kuandika. Inasemekana ni Injili ya kwanza kuandikwa, na Mathayo na Luka inaonekana kupata kutoka kwake. Injili yake imejaa matendo ya Yesu, ambapo Yesu anafundisha zaidi yale anayotenda kuliko yale anayosema. 

Katika Injili ya leo Yesu anawapa mamlaka kutangaza Injili kwa kila kiumbe na kuna ahadi kwamba waamini watakuwa na uwezo wakutenda makuu-kutoa pepo, kunena kwa lugha, kukingwa na mabaya na kuponya wagonjwa. Na mwishoni somo linaonekana kuwa na maelezo kidogo kuhusu kupaa ambapo Bwana wetu alikuwa akirudi kwa baba yake, na kukaa mkono wa kuume wa Mungu. Marko anaelezea changamoto za wafuasi wa Kristo na katika kutimiza hali yao ya umisionari na kuanzisha Ufalme ambao mapenzi ya Mungu yatatendwa duniani. 

“Enendeni ulimwenguni mote mkahubiri Injili kwa kila kiumbe” (Mk 16:15). Amri iliyo ya kawaida kabisa. Na wimbo wa katikati unasema hivi “nitaimba daima sifa zako, ee Bwana, muda wote nitatangaza uaminifu wako…ni nani aliye kama Bwana.” Yesu aliwatuma wanafunzi wake ambao walikuwa watu wakawaida lakini wakiwa wamejaa nguvu ya ajabu ili kutangaza Injili yake na kuikomboa dunia. Cha muhimu haikuwa msingi wa wafuasi kuhubiri bali msingi wa kutegemea neema yake inayofanya kazi ndani yao na hivyo kwa namna tulivyo wawazi kwa neema ya Mungu, ndivyo neema yake inavyotiririka ndani yetu. Uwazi wetu kwa Mungu utasababisha matunda makubwa zaidi ya jinsi tusivyoweza kutegemea. 

Sala: Yesu, nisaidie mimi niweze kuwa wazi kwa neema yako. Tunakuomba utupe neema tuweze kumuiga Mt. Marko Mwinjili katika roho ya kutangaza Ufalme wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2024



MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2024
JUMA LA 4 LA PASAKA, ALHAMISI
SIKUKUU YA MTAKATIFU MARKO, MWINJILI


SOMO 1 
1 Pet 5: 5-14

Ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika ¡mani, mkijua ya kuwa mateso yale yaie yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika «risto, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu. Uweza una yeye hata milele na milele. Amina. 

Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo. Mwenzenu mteule hapa Babeli awasalimu, na Marko mwanangu. Salimianeni kwa busu la upendo. Amani na iwe kwenu — nyote, mlio katika Kristo. Amina.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI 
Zab. 89: 1-2, 5-6, 15-16

(K) Fadhili zako nitaziimba milele, Ee Bwana 
au: Alleluya

Fadhili za Bwana nitaziimba milele;
kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, fadhili zitajengwa milele;
katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Ee Bwana, mbingu zitayasifu maajabu yako,
uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.
Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na Bwana?
Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika? (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe,
Ee Bwana, huenenda katika nuru ya uso wako.
Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,
Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

SHANGILIO 
1 Kor. 1:23-24

Aleluya, aleluya,
Sisi tunamhubiri Kristu, aliyesulibiwa, ni nguvu na hekima ya Mungu.
Aleluya.

INJILI 
Mk 16: 15-20

Yesu aliwaambia wale Kumi na mmoja, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hatawakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya. Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na ulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristu. 



Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

YESU, MWANGA KWA ULIMWENGU!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatano, Aprili 24, 2024. 
Juma la 4 la Pasaka


Mdo 12:24-13:5;
Zab 67:2-3,5-6,8 (K. 4);
Yn 12:44-50.


YESU, MWANGA KWA ULIMWENGU!


Kumfahamu Yesu ni kumfahamu Baba pia. Ukweli ni kwamba uwepo wa Baba umefunikwa kama Umungu wa Kristo ulivyo funikwa. Ingawaje hatuna uzoefu wa kumuona Yesu akitembea kama wale wafuasi wa kwanza walivyo muona, tunakutana na ukweli huo huo katika Ekaristi Takatifu. Wakati tunapo ingia kanisani na kupiga goti kuelekea Tabernakulo, ni vizuri kuwa na uelewa na kufahamu kuwa tupo mbele ya uwepo wa Mungu Mwana. Na kwa njia hiyo tupo pia mbele ya uwepo wa Mungu Baba! Uwepo wao ni wazi na hakika. Ni kwasabau tu wamefichwa kutoka katika milango yetu mitano ya fahamu. 

Katika Injili, Yesu anakuja kama nuru ili tusiwe tena kwenye giza. Anakuja kwa lengo hili: tumuamini yeye na kuwa na ukweli na uzima. Zaburi ya 27 mstari wa 1, unasema “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu”. Kama ilivyo mwanga wa kawaida hufunua kile kilicho fichwa kwanye giza, vivyo hivyo Neno la Mungu huleta nuru ili tuweze kutambuaa ukweli ulio fichika ndani ya Ufalme wa Mungu. Kama nuru, huleta furaha na uzima kwa wengine. Inafanya mbegu ya imani ikue ndani yetu, ili tuweze kushiriki furaha ya Mungu na uzima na wengine. Sisi mara nyingi tunachagua kubaki kaburini kama Mafarisayo bila kufufuka. Lakini Yesu ni mlango wa uzima wa milele. Kwani Yesu ni uzima na ufufuo na wote wale wanao mwamini watakuwa na uzima wa milele. 

Sala: Bwana, nisaidie niweze kukuelewa wewe na kukupenda wewe na katika uhusiano huo niweze kumfahamu na kumpenda Baba na Roho Mtakatifu. Bwana, ninaomba wewe uwe mwanga ambapo kwa njia yako niweze kukuona wewe na ulimwengu. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 24, 2024



MASOMO YA MISA, APRILI 24, 2024
JUMATANO, JUMA LA 4 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 12:24-13:5

Siku zile, Neno la Bwana likazidi na kuenea. Na Barnaba na Sauli, walipokwisha kutimiza huduma yao, wakarejea kutoka Yerusalemu, wakamchukua pamoja nao Yohane aitwaye Marko.

Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.

Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro. Na walipokuwa katika Salami waklihubiri neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 67:1-2, 4, 5, 7 (K) 3

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu,
Watu wote na wakushukuru. au Aleluya.

Mungu na atufadhili na kutubariki,
Na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
Wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

Mataifa na washangilie,
Naam, waimbe kwa furaha,
Maana kwa haki utawahukumu watu,
Na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

Watu na wakushukuru, Ee Mungu,
Watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
Miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)


SHANGILIO
Yn. 10:14

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi mchungaji mwema,
Nao walio wangu nawajua, nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.


INJILI
Yn. 12:44-50

Siku ile Yesu alipaza sauti, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka. Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenipeleka. Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani. Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu. Yeyey anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumu siku ya mwisho. Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema. Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

24th APRIL 2024