“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumma
Desemba 17, 2021
Juma
la 3 la Majilio
Mwa
49: 2, 8-10;
Zab
71: 1-4, 7-8, 17;
Mt
1: 1-17
JE,
UNATAMBUA MPANGO WA MUNGU JUU YAKO?
Leo,
tunaingia kwenye ‘oktava’ ya kujiandaa kwa karibu kabisa kwa ujio wa Kristo.
Kwa siku hii, tunasikia historia ya ukoo wa Yesu. Matayo anatueleza katika
mtiririko wa hali tatu ya vizazi kumi na nne. Anaanza na Abrahamu na kumalizia
na Yesu. Injii inaanza kwa kumwita Yesu kuwa ni Mwana wa Daudi, Mwana wa
Abraham. Hii inaonyesha muunganiko kutoka tangu ahadi za Mungu kwa Abraham,
mpaka utimilifu wake katika nafsi ya Bwana wetu Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Katika
kutimiza ahadi hii, tunaona kwamba Mungu ni mwaminifu. Inachukua karne na
karne, ili ahadi yake kwa Abraham itimie, lakini kwa hakika ilitimia. Hili
linatueleza wazi kwamba muda wa Mungu na mpango wake juu yetu anajua muda wake
wakutimiza ahadi zake, tofauti na jinsi tunavyoweza kufikiri. Tunaweza kuja na
mawazo mazuri tukidhani kwamba yatapita. Lakini mara yasipopita mara moja kwa
jinsi tunavyodhani na kutumaini, tunaanza kukata tamaa.
Tutafakari
juu ya mipango alionayo Mungu juu ya maisha yetu. Inaweza isiwe kama
tunavyodhani na kutabiri au kadiri ya jinsi tunavyoomba katika sala. Lakini
inaridhisha kwamba ni kwa ajili ya uzuri wetu, ni kwasababu ya muunganiko wetu
naye Mbinguni. Yesu alizaliwa ili atuvute karibu zaidi nae. Leo Yesu anatutaka
mimi na wewe tuweke mipango yetu kwake na mitazamo yetu kwake. Anahitaji haya
na mengine mengi. Anataka tujikabidhi sisi wenyewe kwenye mpango wake mkamilifu
ndani ya moyo wa Baba yetu wa Mbinguni.
Sala:
Bwana, natambua kwamba njia zako ni kamilifu na kwamba mipango yako ni
mikamilifu sio yangu. Nisaidie niachane na tamaa zangu na nijikabidhi zaidi
kwako, na kukuamini kabisa, na kwa yote uliopanga kwa ajili yangu. Bwana,
hekima yako ni kamilifu. Nisaidie niweze kuamini hilo kwa moyo wangu wote. Yesu
nakuamini wewe. Amina
Copyright ©2013-2020 ©FurKat,
Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment