MASOMO YA MISA, JUMAMOSI, 23, 2021
SOMO 1.
Warumi 8:1-11
Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu
yao walio katika Kristo Yesu.
Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule
ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.
Maana yale yasiyowezekana kwa sheria,
kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwanawe
mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi,
aliihukumu dhambi katika mwili;
ili maagizo ya torati yatimizwe ndani
yetu sisi, tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali mambo ya roho.
Kwa maana wale waufuatao mwili
huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.
Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia
ya roho ni uzima na amani.
Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu
ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza
Mungu.
Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani
yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote
asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu
umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.
Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua
Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu
ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa
ndani yenu.
Neno la Bwana......Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI.
Zaburi 24:1-2.3-4ab.5-6 (R. see 6)
(K)Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,
Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya
BWANA,
Dunia na wote wakaao ndani yake.
Maana ameiweka misingi yake juu ya
bahari,
Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.
(K)
Ni nani atakayepanda katika mlima wa
BWANA?
Ni nani atakayesimama katika patakatifu
pake?
Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,
Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili,
(K)
Atapokea baraka kwa BWANA,
Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.
Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,
Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa
Yakobo.
(K)
SHANGILIO.
Ezekieli 33:11
Aleluia Aleluia!!
sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali
aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi.
Aleluia!!
INJILI.
Luka 13:1-9
Na wakati uo huo walikuwapo watu
waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na
dhabihu zao.
Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya
kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata
wakapatwa na mambo hayo?
Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu,
ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.
Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na
mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko
watu wote waliokaa Yerusalemu?
Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu,
ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.
Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na
mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu
yake, asipate.
Akamwambia mtunzaji wa shamba la
mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu,
nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?
Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka
huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
nao ukizaa matunda baadaye, vema! La,
usipozaa, ndipo uukate.
Neno la Bwana......Sifa kwako ee kristo.
Copyright © 2020, "MASOMO YA
MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings
reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment