MASOMO
YA MISA SEPTEMBA 25, 2021
JUMAMOSI,
JUMA LA 25 LA MWAKA
SOMO
I
Zek.
2:1-5, 10-11
Niliinua
macho yangu, nikaona, na atazama, mtu mwenye Kamba ya kupimia mkononi mwake.
Ndipo nikasema, Unakwenda wapi? Akaniambia, Ninakwenda kuupima Yerusalemu,
nione upana wake ulivyo na urefu wake ulivyo. Na tazama, yule malaika aliyesema
nami akasimama karibu, na malaika mwingine akatoka ili kuonana naye; naye
akamwambia, Piga mbio, kamwambie kijana huyu, na kusema, Yerusalemu utakaliwa
na watu, kama vijiji visivyo na kuta, kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo
iliyomo ndani yake. Kwa maana mimi, asema Bwana, nitakuwa ukuta wa moto
kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utufukuf ndani yake.
Imba,
ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa, kati yako,
asema Bwana. Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa
watu wangu.
Neno
la Mungu… Tumshukuru Bwana.
WIMBO
WA KATIKATI
Yer.
31:10-13 (K) 10
(K)
Bwana atatulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.
Lisikieni
neno la bwana, enyi mataifa,
Litangazeni
visiwani mbali,
Mkaseme,
aliyemtawanya Israeli atamkusanya,
Na
kulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake. (K)
Kwa
maana Bwana amemweka huru Yakobo,\
Amemkomboa
mkononi mwake
Aliyekuwa
hodari kuliko yeye.
Nao
watakuja, na kuimba katika mlima Sayuni,
Wataukimbilia
wema wa Bwana. (K)
Ndipo
bikira atafurahi katika kucheza,
Na
vijana na wazee pamoja,
Maana
nitageuza masikitiko yao kuwa furaha,
Nami
nitawafariji,
Na
kuwafurahisha waache huzuni zao. (K)
SHANGILIO
Zab.
19:8
Aleluya,
aleluya,
Amri
ya Bwana ni safi, huyati amacho nuru.
Aleluya.
INJILI
Yn.
1:47-51
Yesu
alipomwona Nathanaeli anakuja kwake akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli
kweli kweli, hamna hila ndani yake. Nathanaeli akamwambia, Umepataje
kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwa chini
ya mtini nilikuona. Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe
Mfalme wa Israeli. Yesu akajibu, akamwambia, kwa sababu nilikuambia, Nilikuona
chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya. Akawaambia, Amin,
amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na
kushuka juu ya Mwana wa Adamu.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.
-------------------------
Copyright © 2020,
"MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment