MASOMO YA MISA,
JUMATATU, SEPTEMBA 13,
2021
JUMA LA 24 LA MWAKA
SOMO I
1 Tim 2: 1-8
Kabla ya mambo yote,
nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani,
katika utauwa wote na ustahivu. Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu
Mwokozi wetu, ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.
Kwa sababu, Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja,
Mwanadamu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya
wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake. Nami kwa ajili ya huo naliwekwa niwe
mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa Mataifa katika imani
na kweli. Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono
iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.
Neno la
Bwana...Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 28: 2, 7-9
(K.) Na ahimidiwe Bwana,
maana ameisikia sauti ya
dua yangu.
Uisikie sauti ya dua
yangu
nikuombapo,
nikipainulia mikono yangu
patakatifu pako. (K.)
Bwana ni nguvu zangu na
ngao yangu
moyo wangu umemtumaini
nami nimesaidiwa; basi,
moyo wangu unashangilia,
na kwa wimbo wangu
nitamshukuru. (K.)
Bwana ni nguvu za watu
wake,
naye ni ngome ya wokuvu
kwa masiya wake.
Uwaokoe watu wako,
uubariki urithi wako,
Uwachunge, uwachukue
mileke. (K.)
SHANGILIO
Yn. 3: 16
Aleluya, aleluya,
Kwa maana jinsi hii Mungu
aliupenda ulimwengu,
hata akamtoa Mwanawe
pekee,
ili kila mtu amwaminiye
asipotee,
bali awe na uzima wa
milele.
Aleluya.
INJILI
Lk. 7: 1-10
Yesu alipokwisha
kuyamaliza maneno yake yote masikioni kwa watu, aliingia Kapernaumu. Na mtumwa
wake akida mmoja alikuwa hawezi, karibu na kufa; naye ni mtu aliyempenda sana.
Aliposikia habari za Yesu, alituma wazee wa Wayahudi kwake kumwomba aje amponye
mtumwa wake. Nao walipofika kwa Yesu, walimsihi sana wakisema, Amestahili huyu
umtendee neno hili; maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi.
Basi Yesu akaenda pamoja nao.
Hata alipokuwa si mbali
na nyumba yake, yule akida alituma rafiki kwake, akamwambia, Bwana,
usijisumbue, maana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; kwa hiyo
nilijiona sistahili mwenyewe kuja kwako; lakini, sema neno tu, na mtumwa wangu
atapona. Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari
chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa
wangu, Fanya hivi, kufanya. Yesu aliposikia hayo alimstaajabia, akaugeukia
mkutano uliokuwa ukimfuata, akasema, Nawaambia, hata katika Israeli sijaona
Imani kubwa namna hii. Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani, wakamkuta yule
mtumwa ni mzima.
Neno la Bwana...Sifa
kwako, ee Kristo
-------------------------
Copyright © 2020,
"MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see
www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment