“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila siku
Jumatano,
Septemba 22, 2021.
Juma
la 25 la Mwaka
Ezra:
9: 5-9;
Tob
13: 2,4,6-8;
Lk
9: 1-6
KUNGUTA
MAVUMBI: NAKUACHA MAMBO YA ZAMANI
Karibuni
sana wapendwa wa Bwana kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Tafakari
ya neno la Bwana katika somo la kwanza, Ezra anatoa sala ya kuukiri wema wa
Mungu aliowatendea wana wa Israeli licha ya makosa yao. Aliwatendea wema bila
ya wao kustahili kwani walikuwa wametenda dhambi. Ezra anamshukuru Mwenyezi
Mungu kwa kuwahurumia, na kuwawezesha kutoka utumwani na kuweza kupata hekalu
tena kwani kwa muda mrefu walikuwa bila hekalu, walikosa mahali pa kusali na
kutoa dhabihu. Lakini sasa wemebarikiwa kwa kuweza kupapata mahali hapo na
hivyo wanamshukuru Mungu kwa kuwatendea hili.
Na
pia anatambua kwamba wao wamepatiwa ukombozi na kurudi katika nchi ya ahadi ili
wamtumikie Mungu, ili waifanye kazi ya Bwana, ili watengeneze makao ya Bwana.
Ujumbe
huu utufariji na sisi pia ndugu zangu. Tutambue kwamba Mwenyezi Mungu
anapotupatia ukombozi, ni ili tuifanye kazi ya yake. Hatupatii ukombozi ili
tukatukane watu, au tukajivune, au kudharau wenzetu au kutumia kwa anasa na kwa
ulafi. Mwenyezi Mungu akitukomboa katika umaskini anafanya hivi ili wenzetu nao
watumikiwe. Tujifunze kutoa kwa ajili ya kuwatumikia wenzetu na si kwa ajili ya
kuwatesa au kunyanyasa.
Tusitumie
kipaji, elimu, ujuzi au mali yetu kuinyanyasa jamii. Yote tunayopewa na Bwana
yatumike kwa ajili ya Bwana.
Katika
somo la injili, Bwana Yesu anatoa mamlaka kwa wanafunzi wake ya kwenda
kuutangaza ufalme wa Mungu. Ufalme huu wahusu kuwaletea wenzetu matumaini na
kuwaganga jeraha zao. Sisi tutambue kwamba kila mfuasi wa Kristo amepewa
mamlaka haya. Hivyo tutumike katika kuutangaza ufalme wa mbinguni. Tunao uwezo:
tuna vipaji mbalimbali, tunao muda mwingi pia, tunao ulimi wa kuwafariji
wenzetu na masikio ya kusikia shida za wenzetu na pia macho ya kuona shida za
wenzetu.
Hivyo
tutumie nyenzo hizi kuona kweli ufalme huo wa Mungu na kuutangaza. Tuepuke
tabia za hasira na kukunguta mavumbi kwa haraka na kuwa watu wa laana. Lazima
tusiwe wepesi wa kukunguta mavumbi kama ishara ya kuwalaani wenzetu. Tumeumbwa
ili tuvumilie na hivyo kila mmoja wetu avumilie kweli.
------------------------
Copyright ©2013-2020
©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment