“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila siku
Alhamisi,
Septemba 23, 2021.
Juma
la 25 la Mwaka
Hag
1: 1-8;
Zab
149:1-6, 9;
Lk
9: 7-9
KUKUWA
KIUNDANI ZAIDI NDANI YA KRISTO!
Karibuni
sana wapendwa wa Bwana kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Neno la
Bwana katika somo la kwanza Nabii Hagai ananyanyuka kuwahimiza watu wajenge
hekalu la Bwana. Hiki ni kizazi ambacho wazazi wao walikuwa uhamishoni, sasa
wamerudi tena katika nchi ya Yuda na kuanza kupata maisha bora. Walitumia
rasilimali za nchi ile wakajenga majumba yao makubwa, na kumbi za starehe na za
biashara. Lakini cha ajabu ni kwamba hakuna aliyehangaika na hekalu la Bwana.
Watu
walikuwa wakiridhika kwenda kusali kwenye hekalu lilolo gofu, lililobomoka,
linalovuja. Hagai anawahimiza waijenge nyumba ya Bwana. Wasifikirie kwamba
wakitoa kwa ajili ya Bwana watakuwa maskini. Badala yake watambue ubaya uliopo katika
kuhifadhi ya dunia, kuweka moyo wao kwa ya dunia kwa kuvaa nguo, kwa
kuhangaikia chakula, na majengo. Watanunua na kuvaa nguo labda wakitegemea
wapendeze lakini muda sio mrefu watajiona kwamba hawapendezi tena kwani nguo
hutoka na fashion. Baada ya mwaka fashion hiyo hupita na unapoivaa hupendezi
tena.
Hata
vitu kama simu fashion yao hupita. Kwa sasa yaweza kuonekana kuwa nzuri naya
kisasa lakini baada ya mwaka fashion inapitwa na wakati. Hata vitu kama
majengo, kwa sasa yataonekana kuwa mazuri lakini baada ya muda yataonekana
kupungua kwa uzuri wake pia. Hivyo wanachoweza kujivunia ni kumtumikia Bwana.
Hivyo watoe vitu vyao kwa ajili ya Bwana.
Ujumbe
huu ututie moyo hasa kwa baadhi yetu tusiojali sehemu zetu za ibaada. Wapo
baadhi tunaoridhika kukalia mkeka kila tujapo kanisani au sehemu ya ibaada
lakini nyumbani mwetu tunakalia vitu vyema. Wapo tunaovaa mavazi mazuri,
tunavaa tai na nguo nzuri na kumbe tunasali kwenye kigango kisichokuwa na bati.
Lazima tubadilike na kulipenda kanisa, nyumba yetu ya ibada. Usiridhike nguo za
Padre zimechakaa na wewe unabadilisha suti kila siku, mtazame kuhani wako pia,
anakula nini, wanapolala, nyumba yao ipoje?
Katika
somo la injili, Herode anapata mshtuko kutokana na yote yanayotendwa na Yesu.
Herode anaishi kwa wasiwasi kwa sababu ya dhambi yake aliyoitenda ya kumwua
Yohane. Nasi tuogope ubaya wa dhambi. Hakika tutaitenda sasa lakini itatufanya
tubabaike kwa mwaka mzima.
Tujifunze
kuomba msamaha kwa pale tutendapo dhambi kwani tukiishi na dhambi bila kuomba
msamaha, ni mzigo kwa maisha yetu, ni mzigo kwa nafsi zetu na wale
wanaotutunza. Tujitahidi kuishi kwa ajili ya Bwana na kupenda mema.
------------------------
Copyright ©2013-2020
©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment