Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUKABILIANA NA KUKATALIWA!

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Tafakari ya Kila siku

Jumanne, Septemba  28, 2021,

Juma la 26 la Mwaka

 

Zek 8: 20-23;

Zab 86: 1-7;

Lk 9: 51-56

 

 

KUKABILIANA NA KUKATALIWA!

 

Karibuni sana wapendwa wa Bwana kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Neno la Bwana leo katika somo la injili ambapo Yesu anakataliwa na Wasamaria. Yesu alipokuwa anakwenda huku Samaria, alikuwa haendi kuomba kwao bali alitaka kuwahuburia ufalme wa mbinguni. Wao ndio wangalifaulu, magonjwa yao yangaliponywa na kuishi kwa amani zaidi. Lakini wanatokea wachache wanaopinga hili na kumfanya Yesu ashindwe kufanya utume huu.

 

Wanafunzi wake wanamshauri ashushe moto lakini Yeye anakataa kutumia mamlaka haya. uamuzi alioufanya Yesu unakuwa fundisho kwetu. Yesu alikuwa na mamlaka lakini anakataa kuyatumia kwani alitambua kwamba yeye hakuja ili watu walaaniwe bali watu wapate baraka. Yesu alikuja kuvunja vichaka vya fujo, na chuki na laana na hivyo alijiepusha sana na kulaani yeyote.

 

Nasi ndugu zangu tuwe na moyo wa kubariki wenzetu. Tusipende kulaani, tumetumwa ili tuvunje laana, usipende watu waumwe, wafe au wapate ajali. Mtu anayelaani ni mtu mwenye chuki, na pia kulaani laani ni dalili ya kuishiwa pesa. Watu wanapoanza kufilisika ndio wanaanza kulaani. Tuepuke na tabia za namna hii, tusipende kufurahia misiba ya wenzetu, au maumivu au matatizo ya wenzetu.

 

Katika somo la kwanza, Zekaria anazidi kumweleza Israeli juu ya faida iliyopo pale Bwana atakapokuja kati yao. Ni kwamba watakuwa na hekima, na watu watatoka mbali ili kupata hekima hii kwao. Hii ni kwa sababu kumcha Bwana ni msingi wa hekima. Moyo wa mwanadamu hauwezi kutulizwa na maneno ya hekima au elimu ya kibinadamu. Mt. Augustino anasema kwamba mioyo yetu haitatulia hadi itakapotulia katika wewe ee Bwana.

 

Sisi tunapaswa kusali, kusafisha uovu wetu, tupate kuwa watu wenye hekima zaidi ili basi wenzetu wapate kutulizwa na maneno na matendo yetu. Tusiposali kabla ya kumshauri mwezetu maneno yetu hubadilika na kuwa umbea. Tujitahidi kupambana na maneno yetu ya kimbea kwa njia ya kusali. Tumsifu Yesu Kristo.

 

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment