Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UKUBWA MACHONI MWA MUNGU

 

ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Tafakari ya kila siku

Jumatatu, 26 Julai, 2021,

Juma la 17 la Mwaka

 

Kut 32:15-24,30-34

Zab 106:19-23 (k) 1

Mt 13:31-35

 

 

UKUBWA MACHONI MWA MUNGU

Karibuni sana ndugu zangu kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Leo tunaadhimisha kumbukumbu ya Mt. Marta. Mtakatifu huyu anafahamika sana katika Biblia kwa upendo wake kwa Yesu. Ndiye aliyemkaribisha Yesu nyumbani mwake akiwa na Maria dada yake. Alionesha ukarimu wa hali ya juu kwa Yesu.

Alitaka kumtumikia kwa nguvu zake zote kwa kumpatia mahitaji yake ya kimwili. Kosa la Martha ni kwamba alitumia karibu muda wake wote kufanya haya, na mwishowe alishindwa kupokea ujumbe Yesu aliomletea kwa kuja kwake. Alipomuona tu Yesu, alihangaikia kutumikia bila hata kuuliza au kufuatilia kilichomleta. Hakika Yesu hakuja kwa akina Maria na Martha hivihivi-alikuwa na ujumbe maalumu kwao lakini Martha hakuhangaika kusikiliza ujumbe huu bali alikimbilia kukazania kutumikia. Yesu anamwambia kwamba kwa kufanya hivi, anapoteza sehemu kubwa ya kupata ujumbe toka kwake. Angalipaswa amsikilize Yesu kwanza. Yawezekana vile alivyokuwa anaandaa, Yesu hakuvihitaji.

Kilichomtokea Martha kinatutokea na sisi pia. Mara nyingi tunatumia muda wetu karibu wote katika kuwahudumia wazazi wetu, watoto na wanafamilia wetu. Lakini hatupaswi kutumia muda wetu wote katika kufanya kazi hizi tuu. Pawepo pia muda wa kukaa karibu na Yesu, ili atufundishe namna ya kutumikia.

Tunaweza kutumia nguvu zetu kutumikia lakini ikatokea kwamba kile tunachotumikia hakifai chochote, au tunatumikia kwa namna isiyofaa, au tunatumikia lakini hakuna faida ipatikanayo kwa sisi kutumika. Sisi tujitahidi kwenda mbele ya Yesu atufundishe namna ya kutumikia ili basi huduma zetu zileta manufaa na matunda zaidi kwa wale wanaotumikiwa.

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

No comments:

Post a Comment