MASOMO YA MISA, JULAI 8,
2021
ALHAMISI, JUMA LA 14 LA
MWAKA
SOMO 1
Mwa. 44:18-21, 23-29;
45:1-5
Yuda alimkaribia Yusufu
akasema, Tafadhali, bwana wangu, mtumwa wako na aseme neno moja masikioni mwa
bwana wangu, wala hasira yako isimwakie mtumwa wako, maana wewe u kama FArao.
Wewe, bwana wangu, ulituuliza watumwa wako, ukisema, Je! Mnaye baba, au ndugu?
Tukakuambia wewe, bwana wangu, Tunaye baba, naye ni mzee, na mwana wa uzee wake
ni mdogo, na nduguye amekufa; amebaki yeye peke yake wa katika tumbo la mamaye,
na baba yake anampenda. Ukatuambia watumwa wako, Mleteni kwangu, ili macho
yangu yamwangalie. Asiposhuka ndugu yenu mdogo pamoja nanyi, hamtaniona uso
wangu tena. Ikawa tulipokwenda kwa mtumwa wako, baba yangu, tukamwarifu maneno
yako, bwana wangu. Kisha baba yetu akanena, Rudini huko, mkatununulie chakula
kidogo. Tukasema, Hatuwezi kwenda; ndugu yetu mdogo akiwapo pamoja nasi,
tutashuka; maana hatutaweza kuuona uso wa mtu huyo, ndugu yetu mdogo asipokuwa
pamoja nasi. Mtumwa wako, baba yangu, akatuambia, Mnajua ya kuwa mke wangu
alinizaliwa wana wawili; mmoja alitoka kwangu, nikasema, Bilas haka
ameraruliwa, wala sikumwona tangu hapo. Na mkiniondolea huyu naye, na madhara
yakimpata, mtashusha mvi zangu na msiba kaburini.
Hapo Yusufu hakuweza
kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema,
Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu
alipojitambulisha kwa nduguze. Akapaza sauti yake akalia, nao WAmisri
wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia.
Yusufu akawaambia ndugu
zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake hawakuweza
kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake. Yusufu akawaambia ndugu zake,
Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye
mliniuza kwenda Misri. Basi sasa, msihuzunike, wal amsiudhike nafsi zenu, kwa
kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watu.
Neno la Bwana… Tumshukuru
Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 105:16-21 (K) 5
(K) Zikumbukeni ajabu
Bwana alizozifanya.
Au: Aleluya.
Bwana aliita njaa iijilie
nchi,
Akakiharibu chakula chote
walichokitegemea.
Alimpeleka mtu mbele yao,
Yusufu aliuzwa utumwani.
(K)
Walimwumiza miguu yake
kwa pingu,
Akatiwa katika minyororo
ya chuma.
Hata wakati wa kuwadia
neno lake,
Ahadi ya Bwana
ilimjaribu. (K)
Mfalme alituma watu
akamfungua,
Mkuu wa watu akamwachia.
Akamweka kuwa bwana wa
nyumba yake,
Na mwenye amri juu ya
mali zake zote. (K)
SHANGILIO
Ebr. 4:12
Aleluya, aleluya,
Neno la Mungu li hai tena
li na nguvu, li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10: 7 – 15
Yesu aliwaambia mitume
wake: Katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takasene wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure,
toeni bure. Msichukue dhahabu, wala fedha wala mapesa mishipini mwenu; wala
mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi
astahili posho lake.
Na mji wowote au kijiji
chochote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; make kwake
hata mtakapotoka. Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni. Na nyumba ile
ikistahili, Amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, Amani yenu na
iwarudie ninyi. Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo
katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu. Amin,
nawambia, Itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya
hukumu, kuliko mji ule.
Neno la Bwana… Sifa kwako
Ee Kristo.
Copyright © 2020,
"MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment