MASOMO YA MISA, JULAI 7,
2021
JUMATANO, JUMA LA 14 LA
MWAKA
SOMO 1
Mwa. 41:55-57; 42:5-7,
17-24
Nchi yote ya Misri
ilipoona njaa, watu walimlilia Farao awape chakula. Farao akawaambia Wamisri
wote. Enendeni kwa Yusufu; atakavyowaambia, fanyeni. Njaa ikawa katika dunia
yote pia. Yusufu akazifungua ghala zote, akawauzia WAmisri. Njaa ikawa nzito
katika nchi ya Misri. Watu wa nchi zote wakaja Misri kwa Yusufu; ili wanunue
nafaka; kwa sababu njaa imekuwa nzito katika dunia yote.
Wana wa Israeli wakaja
wanunue chakula miongoni mwao waliokuja, kwa kuwa kulikuwa na njaa katika nchi
ya Kanaani. Naye Yusufu alikuwa ni liwali juu ya nchi, ndiye aliyewauzia watu
wote wa nchi. Nao ndugu zake Yusufu wakaja, wakainama kifudifudi mbele yake.
Yusufu akawaona nduguze, akawatambua, lakini alijifanya kama mgeni kwao.
Akasema nao kwa maneno makali, akawaambia, Mmetoka wapi ninyi? Wakasema,
Tumetooka nchi ya Kanaani, ili tununue chakula.
Akawatia wote gerezani
siku tatu. Yusufu akawaambia siku ya tatu, Fanyeni hivi, mkaishi, maana mimi
namcha Mungu. Kama ni wa kweli ninyi, ndugu yenu mmoja na afungwe gerezani,
nanyi nendeni mkachukue nafaka kwa njaa ya nyumba zenu, mkamlete ndugu yenu
mdogo kwangu; hivyo maneno yenu yatahakikishwa, wala hamtakufa. Ndivyo
walivyofanya. Wakaambiana, Kweli sisi tuliomkosa ndugu yetu, kwa kuwa tuliona
shida ya roho yake alipotusihi, wal ahatukusikia; kwa hiyo shida hii imetupata.
Reubeni akajibu, akawaambia, Sikuwaambia, nikisema, msimkose kijana? Wala
hamkusikia; kwa hiyo damu yake inatakwa tena. Wal ahawakujua ya kwmba yusufu
anawasikia, kwa sababu alikuwapo mkalimali kati yao. Akajitenga nao akalia.
Kisha akawarudia, na kusema nao, akamtwaa Simeoni miongoni mwao, akamfunga
mbele ya macho yao.
Neno la Bwana… Tumshukuru
Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 33:1-2, 10-11, 18-19
(K) 22
(K) Ee Bwana fadhili zako
zikae nasi, kama vile tulivyokungoja Wewe.
Mpigieni Bwana
vigelegele, enyi wenye haki,
Kusifu kunawapasa wanyofu
wa moyo.
Mshukuruni Bwana kwa
kinubi,
Kwa kinanda cha nyuzi
kumi mwimbieni sifa. (K)
Bwana huyabatilisha
mashauri ya mataifa,
Huyatangua makusudi ya
watu.
Shauri la bwana lasimama
milele,
Makusudi ya moyo wake
vizazi na vizazi. (K)
Tazama jicho la Bwana li
kwa wamchao,
Wazingojeao fadhili zake.
Yeye huwaponya nafsi zao
na mauti
Na kuwahuisha wakati wa
njaa. (K)
SHANGILIO
Kol. 3:16,17
Aleluya, aleluya,
Neno la Kristu likae kwa
wingi ndani yenu katika hekima yote, mkishukuru Mungu Baba kwa Yeye.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10:1 – 7
Yesu aliwaita wanafunzi
wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza
magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na majina ya hao mitume kumi na wawili
ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa
Zebedayo, na Yohane nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza
ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo; Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye
ndiye mwenye kumsaliti. Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema.
Katika njia ya Mataifa
msiende, wala katika mji wowote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia
kuwaendea kodnoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu,
hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
Neno la Bwana… Sifa kwako
Ee Kristo.
Copyright © 2020,
"MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment