Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUZAMA KATIKA KRISTO!

 

“ASALI ITOKAYO MWMABANI”

Tafakari ya kila Siku

Alhamisi, Julai 22, 2021.

Juma la 15 la Mwaka

Sikukuu ya Mt. Maria Magdalena

Wimbo 3:1-4 or 2Cor 5:14-17;

Zab 63: 1-5, 7-8;

Yn 20:1-2, 11-18.

KUZAMA KATIKA KRISTO!

 

*Mungu aweza badili Historia yako na kuwa Bora zaidi*

Karibuni ndugu wapendwa kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Bwana ametuchagua tangu tumboni mwa mama zetu, ametupatia nguvu, baraka na neema na kila kifaachi kwa ajili ya kuendesha uwepo wetu hapa duniani. Magumu na dhoruba zitajitokeza lakini katika kila dhoruba, ipo nguvu na neema ya kushindana na dhoruba hizo. Hivyo, tunapaswa kujipa moyo ili tuweze kuziona nguvu za neema hiyo. Mungu ana mipango bora na kila mmoja wetu. Ndivyo ilivyotokea kwa Maria Magdalena. Mungu ana mpango na kila mmoja wetu. Yeye atupatiapo utume, hakika anatupatia na nguvu za kuutekeleza pia.

Alimmiminia neema hizo Mt. Maria Magdalena, yeye alikuwa na pepo wengi, waliokuwa kikwazo kwake katika kuifanya kazi ya Bwana. Lakini aliweza kutakaswa na Bwana na kuwa kiumbe cha kutangaza habari za Kristo mfufuka. Aliweza kuwa mtume kwa mitume wa Yesu, Yeye alitumwa na Yesu kuwapasha habari mitume kwamba Yesu amefufuka. Sisi nasi tukimtegemea Bwana, hakika atatubadilisha na kutufanya tutende mambo bora zaidi. Tusitumie historia zetu mbaya kujihukumu, tumtegemee Bwana na hakika aweza kugeuza historia zetu na kuwa historia bora na za mafanikio. Tumtegemee Yesu; amewabadilisha wengi, atatubadiisha na sisi pia.

Tumuombe Mt. Maria Magdalena, atuombee tupate ujasiri wa kubadili historia dhaifu za maisha yetu na kuwa historia zenye kuniletea mafanikio zaidi.

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

No comments:

Post a Comment