“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Juni 3, 2021.
Juma la 9 la Mwaka
Tob 6:10-11, 7:1, 9-14,
18:4-9;
Zab 127: 1-5;
Mk 12: 28-34.
PENDA KAMA UNAVYOPENDWA
NA MUNGU!
Kwakusoma Injili tunaweza
kufanya muktasari wa nafsi ya Yesu kwa neno moja tu, nalo ni UPENDO. Yesu
anatuambia kwamba sheria zote zinaweza kufupishwa katika sheria mbili tuu. Ya
kwanza kabisa ambayo ni muhimu sana ni upendo kwa Mungu usio na masharti, ya
pili ni matokea ya hiyo ya kwanza, kwasababu wakati mwanadamu anapendwa, Mungu
anapendwa, kwasababu mwanadamu ameumwa kwa sura na mfano wa Mungu
Upendo ulimsukuma Yesu
aweze kuwanyanyua wanyonge, kuwasaida waliotengwa, kuponya walioumizwa,
kuwafanya huru wafungwa na akatoa maisha yake msalabani ili kutukomboa sisi
kutoka utumwa wa dhambi. Upendo wa Mungu hauna masharti. Yesu kwa maneno na
matendo yake anatuhimiza kutimiza na kutenda “UPENDO huu” kwaajili ya ukombozi
wetu na ukombozi wa ulimwengu mzima. Na hiki ndicho kitambulisho chetu kama
Wakristo wanaomfuata Yesu kwa uaminifu. Kwa namna hiyo tutakuwa Wakristu wa kweli
“kama Kristo”. Pengine tujiulize swali lingine ambalo hatujazoea sana
kujiuliza, tunajua Mungu anatupenda wote bila ubaguzi. Je, ninampenda
mwenzangu/jirani yangu kama Mungu anavyompenda?
Kumpenda Mungu ni kitu
cha muhimu kabisa tunacho weza kufanya na hivyo ni ufunguo wa kujipenda sisi
wenyewe. Kumpenda jirani kama nafsi zetu maana yake kila tunachofanya kinapaswa
kimsaidie mtu kuweza kumpenda Mungu zaidi kwa moyo wote, akili zote na nguvu
zote. Haya yanafanywa na maneno yetu lakini zaidi kwa misaada yetu kwao.
Tukimpenda Mungu kwa kila kitu, upendo wetu kwa Mungu unakuwa unasambaa kwa
wengine. Wengine wataona upendo wetu kwa Mungu, tamaa yetu kwa Mungu na
majitoleo yetu kwa Mungu. Wataona na kuvutwa. Kwa kutoa ushuhuda huu wa upendo
unakuwa kivutio kwa wengine kumfuata Mungu.
Sala: Bwana, nisaidie
niweze kufuata amri hii ya mapendo. Nisaidie nikupende wewe kwa jinsi nilivyo
bila kubakiza kitu. Na katika mapendo haya yako, nisaidie kushirikisha wengine.
Yesu, nakuamini wewe. Amina.
------------------------
Copyright ©2013-2020
©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment