“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatano, Juni 2, 2021.
Juma la 9 la Mwaka
Tob 3: 1-11, 16-17;
Zab 24: 2-9;
Mk 12: 18-27.
MPE YESU KITI CHA DEREVA
WA MAISHA YAKO!
Leo Masadukayo wanataka
kumtega Yesu. Lakini jibu la Yesu linakata kiini cha tatizo lenyewe. Anaanza
kwa kuonesha kwamba Masadukayo hawayafahamu Maandiko Matakati wala nguvu ya
Mungu. Masadukayo walijigamba na aina Fulani ya maisha ambayo iliwafanya wawe
na majivuno na hali ya kuji halalisha wao wenyewe kuwa ni wenye haki. Yesu
anawaongoza katika hali ya kufikiri vizuri.
Yesu pia leo anatupa
changamoto kuhusu uelewewa wetu wa Maandiko Matakatifu na nguvu ya Mungu. Yesu
anatusaidia kutambua kuwa mara nyingi tumekuwa na uelewa tofauti kuhusu maisha
yajayo. Hisia zetu na hali ya kufikiri kimakosa vinatupeleka kiasi kwamba
tunajikuta kwenye njia au mtazamo tofauti usio wa kweli. Wakati tunapojikuta
kuwa tumepotea au wakati tunatambua kuwa hatuelewi nguvu ya Mungu ikiwa kazini,
tunapaswa kuacha, na kusali kutafuta kile ambacho Mungu anataka kutuambia.
Tunapaswa kushuka chini kwa unyenyekevu na kukiri kwa Mungu na nafsi zetu
kwamba hatufahamu njia zake na mapenzi yake. Tunapaswa kumsikiliza Mungu
achukue nafasi ya kuongoza maisha yetu.
Sala: Bwana, ninatamani
kufahamu ukweli. Wakati mwingine najikuta mwenyewe nikijiongoza kwenye njia
isio sawa. Nisaidie mimi niweze kujinyenyekesha mwenyewe chini yako ili uweze
kuniongoza. Yesu, nakuamini wewe. Amina
------------------------
Copyright ©2013-2020
©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment