Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2021

 

MASOMO YA MISA, JUNI 8, 2021

JUMANNE, JUMA LA 10 LA MWAKA

 

KUMBUKUMBU YA MT. ANTONI WA PADUA

 

SOMO 1

2Kor. 1:18 – 22

 

Kama Mungu alivyo mwaminifu, neno letu kwenu si Nidyo na siyo. Maana Mwana wa Mungu, Kristo Yesu, aliyehubiriwa katikati yenu na sisi, mimi na Silwano na Timotheo, hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo. Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi. Basi Yeye atufanyaye imara pamoja nanyi katika Krito, na kututia mafuta, ni Mungu, naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.

 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 119:129 – 133, 135 (K) 135

 

(K) Umwangazie mtumishi wako uso wako.

 

Shuhuda zako ni za ajabu,

Ndiyo maana roho yangu imezishika.

Kufafanusha maneno yako kwatia nuru,

Na kumfahamisha mjinga. (K)

 

Nalifunua kinywa changu nikatweta,

Maana naliyatamani maagizo yako.

Unigeukie, unirehemu mimi,

Kama iwahusuvyo walipendao jina lako. (K)

 

Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako,

Uovu usije ukanimiliki.

Umwangazie mtumishi wako uso wako,

Na kunifundisha amri zako. (K)

 

SHANGILIO

Zab. 19:18

 

Aleluya, aleluya.

Amri ya Bwana ni safi, huyatia macho nuru.

Aleluya.

 

INJILI

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

-------------------------

Copyright © 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment