Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUJIBU WITO WA YESU!

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Tafakari ya kila siku

Jumatatu, Mei 24, 2021.

Juma la 8 la Mwaka wa Kanisa

 

YbS 17: 20-24;

Zab 32: 1-2, 5-7;

Mk 10: 17-27

 

KUJIBU WITO WA YESU!

 

Karibuni sana ndugu wapendwa kwa adhimisho la Misa Takatifu asubuhi ya leo. Leo neno la Bwana katika somo la kwanza linatueleza juu ya kumrudia Mwenyezi Mungu, hakika ipo raha kubwa katika kumrudia Mwenyezi Mungu, kwa sababu wanaomsifu Mungu ni sisi, na ni kwa wakati huu ndio tunapopaswa kumsifu huyu Mwenyezi Mungu. Huu ndio wakati pia wa kumrudia, hakuna wakati mwingine, ni wakati tukiwa vijana, tukiwa na afya tumsifu Mwenyezi Mungu.

Na katika Zaburi yetu ya wimbo wa katikati, mzaburi anatueleza kwamba ana heri yule aliyesamehewa kosa na Mwenyezi Mungu. Sisi tukazane, tuungame makosa yetu ili tupate kuionja hii furaha, dhambi hutufanya tupoteze muda na rasilimali zetu kwa mambo ambayo kwa hakika hayatupatii msaada wowote. Dhambi hukwamisha mpango wa Mungu alionao kuhusu maisha yetu. sisi tuziungame dhambi zetu na hakika tutaweza kuionja furaha zaidi.

Katika somo la injili, tunakutana na kijana anayeshindwa kuwa mkamilifu kwa sababu ya mali zake. Anaalikwa kuwa mkamilifu lakini kwa sababu ya kuzipenda mali zake, mali zilimzuia. Sisi ndugu zangu tujifunze kutambua hatari iliyopo katika kungangania kitu. Hakika tukiwa watu wa kungangania, hatutaweza kuingia katika ufalme wa Mungu.

Tuhakikishe hatunganganii chochote, hata kama ni rafiki au mali hakika tusimnganganie na kushindwa kuuona ufalme wa Mungu.

Baadhi yetu tumekubali kungangania marafiki hata wakatuharibu na kuwa watenda dhambi. Tupo tayari kusema kwamba afadhali niende motoni kuliko kumwacha huyu rafiki. Sisi tusifanye hivyo, ni lazima tuwe tayari kuachia kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

 

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

No comments:

Post a Comment