“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Februari
4, 2021, Alhamisi
JUMA
LA 4 LA MWAKA
Ebr.
12:18-19, 21-24
Zab.
48:1-2, 8-10 (K) 9
Mk
6:7-13
SAFARI
ISIYO HITAJI MIZIGO
Karibuni
ndugu zangu kwa tafakari ya neno la Mungu asubuhi ya leo katika adhimisho la
Misa Takatifu. Zaburi yetu ya wimbo wa katikati leo inatuambia juu ya
kutafakari fadhili na upendo wa Bwana katikati ya hekalu lake. Hii ni zaburi
inayoimbwa na roho iliyotulia na yenye shukrani, inayokaa chini kutafakari
namna jinsi baraka za Mungu zilivyo kuu.
Zaburi
hii inatumika kusisitizia ujumbe wa somo la kwanza toka katika waraka kwa
Waebrania. Hapa tunakutana na ujumbe juu ya ukaribu na upendo kati yetu na
Mungu. Kristo ndiye aliyefanikisha yote haya. Mwandishi wa waraka huu anasema
kwamba sisi tumekuja sehemu takatifu, ambapo hatuogopi, sasa tupo katika
urafiki mkuu na Mungu wetu.
Analinganisha
na lile kutaniko kati ya Mungu na wana wa Israeli pale mlimani Sioni. Hapa,
wana wa Israeli waliogopa hata kusikia sauti ya Mungu. Wakiwa na Mungu waliona
hofu. Lakini cha ajabu ni kwamba sisi tukiwa na Mungu, ni urafiki, amani na
utulivu. Kristo ndiye aliyefanikisha yote haya. shukrani kwa Kristo wetu.
Zamani za Agano la kale, hata aliyelikaribia sanduku la Agano kama hastahili,
alikufa palepale.
Lakini
Kristo amekwisha tuleta karibu na Baba yake. Sisi tusitumie vibaya huu ukaribu
unaoletwa na Kristo. Wengi wetu tunautumia kumdharau au kufikiri kwamba Mungu
hana tena nguvu siku hizi. Tusitake kumjaribu Mwenyezi Mungu. Tutumie huu
urafiki vizuri. Hasa wakati wa kupokea Ekaristi-tuje kwa adabu. Tusitake Mungu
arudie zile zama za sanduku la Agano-hakuna aliyethubutu kulikaribia hivihivi.
Tusitumie
huruma ya Mungu vibaya. Tuviheshimu vitakatifu. Biblia, rozari na misalaba
iwekwe sehemu safi. Isiachwe katika vumbi. Tusitake laana hivihivi.
Katika
injili yetu, Yesu anawatuma wanafunzi wake kulihubiri neno lake. Anawaeleza
wakiingia mjini kama hawakaribishwi au kusikilizwa, basi wakungute mavumbi
miguuni mwao. Kukunguta mavumbi ni alama ya laana kwa wale wanaoikataa injili.
Wanafunzi wa Yesu hawapaswi kuwa wepesi wa kukunguta mavumbi. Wanapaswa kufanya
bidii sana ya kuongoa, wawe na upendo. Wasikungute mavumbi kabla hata ya kuanza
utume. Sisi ndugu zangu tunakunguta mavumbi kirahisi mno, ndio shida yetu. Tunapaswa
kuzidisha bidii zaidi.
Copyright
©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment