Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 3, 2021

 

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 3, 2021

JUMATANO, JUMA LA 4 LA MWAKA

 

SOMO 1

Ebr. 12;4 – 7, 11 – 15

 

Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi. Tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, wala usizimie moyo ukikemewa naye; maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, naye humpiga kil amwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimi; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi aisyerudiwa na babaye?

Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye Amani. Kwa hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza, mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kipnywe.

Tafuteni kwa bidii kuwa na Amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia kana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.

 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 103:1 – 2, 13 – 14, 17 – 18

 

(K) Fadhili za Bwana zina wamchao tangu milele hata milele

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana

Naam, vyote vilivyo ndani yangu

Vilihimidi jina lake takatifu.

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,

Wala usizisahau fadhili zake zote. (K)

 

Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake,

Ndivyo Bwana awahurumia wamchao.

Kwa maana yeye anatujua umbo letu

Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. (K)

 

Fadhili za Bwana zina wamchao

Tangu milele na milele,

Na haki yake ina wana wa wana;

Wale washikao agano lake. (K)

 

SHANGILIO

Yn. 8:12

Aleluya, aleluya,

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye hatakwenda gizani na kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.

Aleluya.

 

INJILI

Mk. 6:1-6

 

Yesu alitoka huko, akafika mpaka nchi ya kwao, wanafunzi wake wakamfuata. Na ilipokuwa sabato, alianza kufundisha katika sinagogi; wengi waliposikia wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake? Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake. Yesu akawaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jaama zake, na nyumbani mwake. Wala hakuweza kufanya mwujiza wowote huko; isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya. Akastaajabu kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

 

 

-------------------------

Copyright © 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment