Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 15, 2021

 

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 15, 2021

JUMATATU, JUMA LA 6 LA MWAKA

 

Mwa 4: 1-15, 25;

 

Adamu alimjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana. Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi. Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyma dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. Kaini akamwambia Habili nduguye, twende uwandani. Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua.

Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoto na mtu asiye na kikao duniani. Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami niakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua. Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo yeyote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.

Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pia Habili; kwa sababu Kaini alimwua.

 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 50:1, 8, 16 – 17, 20 – 21 (K) 14

 

(K) Umtolee Mungu dhabihu za kushukuru.

 

Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi,

Toka maawio ya jua hata machweo yake.

Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,

Na kafara zako ziko mbele zangu daima. (K)

 

Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia,

Una nini wewe kuitangaza sheria yangu,

Na kuliweka agano langu kinywani mwako?

Maana wewe umechukia maonyo,

Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. (K)

 

Umekaa na kumsengenya ndugu yako,

Na mwana wa mama yako umemsingizia.

Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza,

Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe.

Walakini nitakukemea;

Nitayapanga hayo mbele ya macho yako. (K)

 

SHANGILIO

1Sam. 3:9

 

Aleluya, aleluya,

Nena, Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikia: Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.

Aleluya.

 

INJILI

Mk. 8:11 – 13

Walitokea Mafarisayo, wakaanza kuhojiana na Yesu; wakitafuta kwake ishara itokayo mbinguni; wakimjaribu. Akaugua rohoni mwake, akasema, Mbona kizazi hiki chatafuta ishara? Amin, nawaambieni, Hakitapewa ishara kizazi hiki. Akawaacha akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

 

-------------------------

Copyright © 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

No comments:

Post a Comment