“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila siku
Jumamosi,
Februari 13, 2021,
Juma
la 5 la Mwaka wa Kanisa
Mwa
3:9-24;
Zab
90: 2-6, 12-13;
Mk
8: 1-10.
JE
UNA NJAA YA MUNGU?
Karibuni
ndugu zangu kwa tafakari ya neno la Mungu katika ashimisho la Misa Takatifu.
Neno la Bwana leo katika zaburi yetu ya wimbo wa katikati tunakutana na maneno
yasemayo “Ee Bwana umekuwa msaada wetu kizazi hata kizazi.” Kabla hata ya
misingi ya dunia kuumbwa huyu Bwana amekuwa msaada wetu. Na akimueleza
mwanadamu siku zake zimekwisha, yeye hurudi mavumbini alimotoka. Hivyo
mwanadamu anapaswa aishi kinyenyekevu mbele ya Bwana kwani hatma yake ipo
mikononi mwa Bwana.
Zaburi
hii inatumika kusisitizia kwa undani ujumbe wa somo la kwanza. Hapa mwanadamu
anadanganywa na kupewa adhabu kali. Adhabu hii lengo lake ni kumnyenyekesha,
ajue nafasi yake ili apate kurudi kwa Mungu, amtumainie Mungu zaidi, akae
miguuni kwa Mungu. Kwa namna hii, mwanadamu ataweza tena kupokea baraka na
neema toka kwa Mwenyezi Mungu na kubarikiwa. Hivyo, adhabu hii isitufanye
tuhuzunike sana, hii ni adhabu ya kutufanya tumrudie Mungu, tuanguke miguuni
mwake, tujue kwamba bila yeye sisi si kitu. Hivyo tumpatie Mungu utukufu wake,
tupige magoti, tumueleze kwamba bila wewe sisi si kitu, twende kwake kila siku
kuomba huruma yake. Tumtumainie.
Katika
somo la injili, tunakutana na Yesu akiwalisha makutano chakula. Yesu
anajionesha kuwa Baba wa huruma, anawaonea wengi huruma, anajali hata mahitaji
yao ya mwili. Alionesha kujali zaidi kabisa ya wanafunzi wake. Ukweli ni kwamba
Yesu ajua shida zetu zaidi, pia tutambue kwamba kabla ya Yesu kuwalisha,
aliwaeleza waeleze walichonacho, na pale walipokitoa alikibariki na kuwafanya
wengi wale na kushiba.
Sisi
tujapo kwa Bwana, lazima tukubali kuonesha sehemu yetu, twende na juhudi yetu
ili Bwana azibariki na hapa atatuwezesha kupata na kushiba. Wengi wetu ni
maskini kwa sababu hatuoneshi sehemu yetu, hatuoneshi sehemu yetu kwa Bwana,
tunataka yeye atufanyie kila kitu bila kuonesha sehemu yetu. Hii ni sababu ya
wengi wetu kushindwa kupata kile tuombacho. Ni lazima kukubali kuonesha kilicho
chetu mbele ya Bwana. Tukionesha uvivu na uchoyo hakika hatutaweza kufaulu
mbele ya Bwana.
------------------------
Copyright
©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment