Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

CHAGUA KULINDA MAISHA!

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Tafakari ya kila siku

Ijumaa, Februari 5, 2021,

Juma la 4 la Mwaka wa Kanisa

 

KUMBUKUMBU YA MT. AGATHA (MSHAHIDI)

 

Ebr 13: 1-8;

Zab 27: 1, 3, 5, 8-9;

Mk 6: 14-29.

 

CHAGUA KULINDA MAISHA!

 

 

Ndugu zangu wapendwa, karibuni kwa tafakari ya neno la Mungu asubuhi ya leo katika adhimisho la Misa Takatifu. Neno la Bwana leo katika somo la kwanza, mwandishi wa waraka kwa Waebrania anaanza kuhitimisha kitabu chake kwa kutoa mashauri mbalimbali.

Anawaeleza wakristo wake kwamba wawe watu wa kujali, waepukane na tabia ya kutojali. Watambue kwamba katika jamii kuna watu wenye mahitaji mbalimbali-watambue kwamba kuna watu tofauti-kuna wagonjwa, wazee, wageni, wengine ni washamba, wasiojua vitu, kuna vichaa, wengine akili haziko vizuri, wengine wanapata hasira kiurahisi basi wanapaswa kutambua hilo na kuweza kuishi na kila mmoja kama rafiki.

Anawaeleza kwamba Yesu huonekana ndani ya watu kama hawa. Hivyo wajitahidi kuishi na kila mmoja kwa hekima. Ikikosekana hili hatuwezi kutumikiana ndani ya jamii. Hekima ndio inayokosekana ndani ya jamii zetu ndugu zangu. Wenzetu hatuwajali kama ni tofauti, wanahitaji kutendewa tofauti. Kuna wagonjwa labda wa kisukari, wengine ni vilema-lakini tunataka wale kama sisi, watembee kama sisi, na kila kitu atende kama sisi. Hapana, watu ni fofauti. Kuna mwingine ni mshamba au mgeni-amekuja Dar es salaam kwa mara ya kwanza-hawezi kuelewa mji kama wewe. Akikuuliza kitu usicheke. Wengine wanahamaki haraka au hasira za ajabu-tuishi nao tukijua hili. Hapa ndipo tunapoweza kumwalika Yesu nyumbani kwetu.

Tukikosa hekima ya namna hii tutaishia kugombana na wenzetu kila kukicha.

Kwenye somo la injili, tunakutana na Herode akihofia juu ya Yesu akifikiri kwamba ni Yohane mbatizaji amefufuka. Pia tunapata maelezo juu ya namna Herode alivyomkata kichwa Yohane Mbatizaji. Yeye kabla ya kuamuru Yohane akatwe kichwa-alikuwa katika raha, mwili wake ukisisimka kwa vionjo vya raha vikamfanya hata kuwa tayari kutoa hukumu iliyokuja kumgharimu kwa maisha yake yote.

Hii linatokea kwa sababu kipindi mwili wako ukiwa katika raha, wakati vionjo vyote vya mwili vikiwa vimeamshwa ndio shetani humkuta karibu. Na hapa tunakamatwa kirahisi. Dhambi nyingi au maamuzi mabaya hutolewa kwa vipindi kama hivi. Hivyo tujitahidi kuthibiti vionjo vyetu ndugu zangu ili visitumiwe na shetani.

Kikitokea kipindi cha furaha, tupambane na vionjo vyake. Tumsifu Yesu Kristo.

 

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

 

No comments:

Post a Comment