“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi,
Januari 14, 2021,
Juma
la 1 la Mwaka wa Kanisa
Ebr
3: 7-14;
Zab
94: 6-11;
Mk
1: 40-45
KUMTAFUTA
YESU KWA MOYO WOTE!
Karibuni
ndugu zangu kwa adhimisho la Misa Takatifu asubuhi ya leo, ujumbe mkuu wa leo
ni 'Msiifanye Migumu mioyo yenu'.
Leo
kwenye somo la kwanza, mwandishi anasisitiza kwamba tusiifanye migumu mioyo
yetu kamwe mbele ya Mwenyezi Mungu; yaani tusiwe watu wa kiburi, watu
wanaotendewa miujiza na Mwenyezi Mungu bila kuruhusu miujiza hiyo itubadilishe;
watu tunalishwa sakramenti kila siku lakini hazitubadilishi. Kwa sababu
tunaifanya migumu mioyo yetu.
Mzaburi
wetu katika wimbo wa katikati leo anatupatia mfano wa walioifanya migumu mioyo
yao. Hawa ni wazee wa Israeli kule jangwani. Walioonyeshwa miujiza mikubwa na
Mungu, wakalishwa mana na kunywa maji katika mwamba. Mungu akawapigania,
akawaongoza kwa nguzo ya moto usiku na wingu mchana. Akawaokoa na mataifa mabaya
lakini wao wakaendelea kuwa wakaidi. Wakakosa imani, wakadiriki hata
kutengeneza sanamu na kuiabudu kama Mungu. Mungu alikasirika sana na kuwapa
adhabu kubwa.
Sisi
tusiige mifano ya babu zetu hawa. Turuhusu Mungu azungumze nasi, halafu tuwe
tayari kumwona Mungu kwenye matukio mbalimbali maishani mwetu. Kuna wakati
Mungu anatutendeaga miujiza-kuna mambo yanatutukia na tunaona kwamba hakika huu
ni mkono wa Mungu. Matukio kama haya yanapaswa kutubadilisha. Tusikaze mioyo na
kuona kana kwamba hakuna kitu kimetokea.
Mkoma
tunayekutana naye katika injili ya leo alionyesha unyenyekevu, aliufungua moyo
wake, hakuufanya kuwa mgumu na kwenda kwa Yesu na kweli aliponywa. Yesu
anawapenda wasioifanya migumu mioyo yao. Tukumbuke kwamba waliokuwa na ukoma ni
wengi nyakati za Yesu lakini walioponywa ni wachache. Waliokuwa na unyenyekevu
kama wa huyu mkoma wa leo walifaidi. Sisi tuepuke kuifanya migumu mioyo yetu.
Tuungame pia na dhambi zetu. Hizi hufanya mioyo yetu kuwa migumu na kushindwa
kuona nguvu ya Mungu ndani yetu. Tuikimbie dhambi!
Copyright
©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment