MASOMO
YA MISA, NOVEMBA 21, 2020
JUMAMOSI,
JUMA LA 33 LA MWAKA
KUMBUKUMBU
YA KUTOLEWA BIKIRA MARIA HEKALUNI
SOMO
1
Zek.
2:10-13
Imba,
ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa, kati yako,
asema Bwana. Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile,, nao
watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa
majeshi amenituma kwako. Na Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi
takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena. Nyamazeni, ninyi nyote wenye mwili,
mbele za Bwana; kwa maana ameamka, na kutoka katika maskani yake takatifu.
Neno
la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO
WA KATIKATI
Lk.
1:46-55 (K) 46
(K)
Mwenye nguvu amenitendea makuu, na jina lake ni takatifu.
Moyo
wangu wamwadhimisha Bwana,
Na
roho yangu imemfurahia Mungu,
Mwokozi
wangu. (K)
Kwa
kuwa ameutazama,
Unyonge
wa mjakazi wake.
Kwa
maana, tazama, tokea sasa
Vizazi
vyote wataniita mbarikiwa;
Kwa
kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,
Na
jina lake ni takatifu. (K)
Na
rehema zake hudumu vizazi hata vizazi
Kwa
hao wanaomcha.
Amefanya
nguvu kwa mkono wake;
Amewatawanya
walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao. (K)
Amewaangusha
wakuu katika viti vyao vya enzi;
Na
wanyonge amewakweza.
Wenye
njaa amewashibisha mema,
Na
wenye mali amewaondoa mikono mitupu. (K)
Amemsaidia
Israeli, mtumishi wake;
Ili
kukumbuka rehema zake;
Kama
alivyowaambia baba zetu,
Ibrahimu
na uzao wake hata milele. (K)
SHANGILIO
Lk.
1:28
Aleluya,
aleluya,
Salamu,
uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Umebarikiwa katika wanawake.
Aleluya.
INJILI
Lk.
11:27 – 28
Yesu
alipokisema maeno hayo, mwanamke mmoja katika mkutano alipaza sauti yake,
akamwambia, Heri tumbo lililokuzaa, na matiti uliyonyonya. Lakini yeye alisema,
Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.
-------------------------
Copyright
© 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment