“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumanne, Mei 6, 2025,
Juma la 3 la Pasaka
Mdo 7:51-8:1;
Zab 31:3-4,6-8,17,21 (K. 6);
Yn 6:30-35.
YESU ANATOSHA KABISA
Leo, Yesu anatumia njaa na kiu kutufundisha
kwamba tunapaswa kuwa na njaa na kiu ya kiroho. Kuna njia moja tu ya kutuliza
na kumaliza kiu hii… ni kwa njia yake tu.
Mara nyingi tunapatwa na njaa na kiu.
Tunakula na kunywa, lakini baada ya masaa kadhaa tunahisi tena njaa na kiu. Huu
mzunguko hatuwezi kuukwepa. Miili yetu daima inadai chakula na kinywaji. Hii ni
sawa pia katika maisha ya kiroho. Hatuwezi kusali mara moja na kusema basi
inatosha na kumaliza kiu ya kiroho milele. Hatuwezi tu kusema namwamini Yesu
mara moja na kubaki tu. Hii ni kwasababu sala na muunganiko na Yesu ni kitu
ambacho kinapaswa kuchukua nafasi kila siku.
Ekaristi, “mkate wa uzima” unaridhisha kiu
yetu na njaa yetu. Ekarisi ni zawadi ambayo tunapaswa kuitamani na kuipokea
daima. Ukweli kwamba tunapaswa kuhudhuria misa na kupokea Ekaristi kila wakati
ni ukweli kwamba maisha yetu ya Kikristo yanapaswa kufanywa mapya kila
siku.
Kumpenda Yesu na kumfuata yeye ni uamuzi
ambao haupaswi tu kufanywa upaya kila siku, bali kufanywa upya kila wakati.
Unapaswa kufanywa upya kama unavyo sikia njaa ya kimwili na kiu. Yesu ni mkate
wa uzima wa Kiroho na kinywaji cha kweli cha kiroho. Yeye yupo kwa ajili yako.
Muache yeye akamilishe hamu ya maisha.
Sala: Bwana, ninakutamani wewe. Natamani
umalize kiu yangu. Nisaidie nikugeukie wewe katika kila kitu. Nisaidie daima
nitambue kuwa wewe ni yule ambaye namuhitaji na unatosha. Yesu, nakuamini wewe.
Amina
No comments:
Post a Comment