Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUELEWA NENO LA MUNGU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Mei 11, 2024 
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 18: 23-28
Zab 47: 2-3, 8-10 (k. 8);
Yn 16: 23-28.


KUELEWA NENO LA MUNGU!

Katika somo la kwanza kutoka katika kitabu cha matendo ya Mitume, kina muongelea mtu mmoja ambaye anaitwa Apollo ambaye ni mfano kwa wakristo wote. Alifahamu maandiko na alikuwa na ujasiri wa kuhubiri habari njema. Alifanya watu wengi wabadilishe maisha yao na kuongoka, kwa kutangaza Neno la Mungu. Sio wote walio na uweze wa kufafanua Neno la Mungu. Tunahitaji msaada wa Mungu na uongozi wa Roho Mtakatifu. Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo umefungua milango ya neema. Tunaweza kuomba kwa Mungu kwa jina la Kristo na nguvu ya Roho Mtakatifu. 

Maandiko Matakatifu, na hasa mafundisho ya Kristo yapo katika lugha ambayo imefunikwa kiasi kikubwa, ambayo sio wote waweza kuelewa. Kwahiyo kwanini Yesu anaongea katika lugha ambayo imefunikwa au kufichwa na asiongee kwa wazi wazi moja kwa moja? Jibu linahusika na sisi ukosefu wetu wa kutokuwa wazi katika ukweli. Kama tunakuwa wazi katika ukweli, na kuwa tayari kukumbatia ukweli bila kujali ni namna ghani, Yesu angeongea nasi na sisi kuitika mara moja. Lakini sivyo ilivyo. Ufunguo wa kuelewa haya ni kuelewa na kutambua elimu ya mapenzi ya Mungu na utayari wa kutimiza mapenzi hayo. Mara nyingi sisi tunataka Yesu atuambie mapenzi yake, tufikirie juu yake, na kuangalia, alafu sisi tunakuja na majibu yetu wenyewe. Lakini kama tunataka Yesu aongee nasi wazi wazi, tunapaswa kusema ndio kwa Yesu hata bila kutambua anataka tufanye nini. Utayari wa kukubali mapenzi yake ni mwanzo wa kuelewa mapenzi yake. 

Mfano kamili wa hili ni Mama yetu Bikira Maria. Kabala ya Malaika kuja kwake yeye alikuwa akiyashika mapenzi ya Mungu. na Malaika alipofika na kumwelezea nini kitacho tokea, yeye aliuliza uelewa zaidi. Na kweli alipata kuelewa zaidi kwa kupata jibu kwa swali lake. Lakini sababu moja ya malaika, kama mjumbe wa Mungu, aliongea wazi wazi kwasababu alishafahamu wazi moyo wa Maria kuwa unamtegemea Mungu bila kujali kutatokea nini. 

Je, unataka Mungu aongee nawe katika hali ya uwazi? Je, unataka kuelewa Neno la Mungu? kama ndivyo, sema ndio kwa kile ambacho Mungu anapenda wewe utende daima. Kwa kujenga hali hii ya kusema ndio kwa mapenzi ya Mungu, itamfanya Mungu kukufungulia mlango mara moja kuelewa yale yote anayotaka uyatende katika kutimiza mapenzi yake. 

Sala: Bwana, ninachagua mapenzi yako leo na daima. Sichagui kitu kingine ni mapenzi yako tu. Ninavyosema ndio kwako, nisaidie niweze kukuwa katika hali ya uwazi wako unaopenda. Yesu, ninakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment