MASOMO YA MISA OKTOBA 4,
2023
JUMATANO JUMA LA 26 LA
MWAKA
KUMBUKUMBU YA MT.
FRANSISKO WA ASIZI
________
SOMO 1
Neh. 2:1-8
Ikawa katika mwezi wa
Nisani, mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta, na divai imewekwa mbele yake,
nikaishika ile divai, nikampa mfalme. Name mpaka sasa sikuwa na huzuni mbele ya
mfalme wakati wowote. Basi mfalme akaniambia, Mbona umesikitika uso wako, nawe
huna ugonjwa? Nini hii, isipokuwa ni huzuni ya moyo? Ndipo nikaogopa sana.
Nikamwambia mfalme, Mfalme na aishi milele; kwani uso wangu usiwe na huzuni,
iwapo mji, ulio mahali pa makaburi ya baba zangu, unakaa ukiwa, na malango yake
yameteketezwa kwa moto? Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka
kuniomba?
Basi nikamwomba Mungu wa
mbinguni. Nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na ikiwa mimi, mtumishi wako,
nimepata kibali machoni pako, tafadhali unipeleke mpaka Yuda, niuendee mji wa
makaburi ya baba zangu, nipate kuujenga. Mfalme akaniuliza, (malkia naye
ameketi karibu naye), Safari yako itakuwa ya siku ngapi? Nawe utarudi lini?
Hivyo mfalme akaona vema kunipeleka; nami nikampa muda.
Tena nikamwambia mfalme,
Mfalme akiona vema, na nipewe nyaraka kwa maliwali walio ng’ambo ya Mto, ili
waniache kupita mpaka nifike Yuda; nipewe na waraka kwa Asafu, mwenye kuutunza
mwitu wa mfalme, ili anipe miti ya kufanyizia boriti kwa malango ya ngome ya
nyumba, na kwa ukuta wa mji; na kwa nyumba ile nitakayoingia mimi. Naye mfalme
akanipa, kama mkono mwema wa Mungu wangu ulivyokuwa juu yangu.
Neno la Bwana…
Tumshukuru Mungu
________
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 137:1-6
(K) Ulimi wangu na
ugandamane na kaakaa la kinywa change, nisipokukumbuka.
Kando ya mito ya Babeli
ndipo tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka
Sayuni.
Katika miti iliyo
katikati yake
Tulivitundika vinubi
vyetu. (K)
Maana huko waliotuchukua
mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka
furaha;
Tuimbieni baadhi ya
nyimbo za Sayuni. (K)
Tuimbeje wimbo wa Bwana
Katika nchi ya ugeni?
Ee Yerusalemu,
nikikusahau wewe,
Mkono wangu wa kuume na
usahau. (K)
Ulimi wangu na
ugandamane
Na kaakaa la kinywa
change, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu
iliyo kuu. (K)
________
SHANGILIO
Zab. 147:12
Aleluya, aleluya,
Msifu Bwana, Ee
Yerusalemu, huipeleka amri yake juu ya nchi.
Aleluya.
________
INJILI
Lk. 9:57-62
Yesu na wanafunzi wake
walipokuwa wakienda njiani, mtu mmoja alimwambia, Nitakufuata kokote
utakakokwenda. Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana
vioto, lakini Mwana wa Adamu hana pa kujilaza kichwa chake.
Akamwambia mwingine,
Nifuate. Akasema, Bwana, nipe ruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu.
Akamwambia, Waache wafu wawazike wafu; bali wewe enenda ukautangaze ufalme wa
Mungu.
Mtu mwingine pia
akamwambia, Bwana, nitakufuata; lakini, nipe ruhusu kwanza nikawaage watu wa
nyumbani mwangu. Yesu akamwambia, Mtu aliyetia mkono wake kulima, kisha
akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa Mungu.
Neno la Bwana… Sifa
kwako Ee Kristo.
________
Copyright © 2023,
"MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see
www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment