Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Aprili 20, 2024
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 9: 31-42;
Zab 116: 12-17;
Yn 6: 60-69.


UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!


Yohane anataka kutuonesha kwamba Yesu ndiye anayetulisha chakula cha uzima wa Kimungu, kwakutupa sisi maisha yake mwenyewe na mwili wake. Kula mkate na samaki aliowapa Yesu ilikuwa rahisi lakini kusikiliza maneno yake ilikuwa vigumu, baada ya haya Injili inasema wazi kwamba wafuasi wengi walimwacha na wengine waliacha kuambatana naye. Lakini wakati Yesu alipowauliza wale kumi na wawili, kama na wao wanataka kuondoka pia, Petro alijibu, “Bwana tuende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele” Ndio, Petro anatambua japo kuwa si kwahakika sana kipindi hicho, kwamba “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu”

Swali hili la Yesu kwa Mitume wake ni muhimu sana. Kwa kuwauliza wao moja kwa moja, Yesu anawapa uhuru kamili wa kuchagua. Hawashinikizi kukubali au kuamini alichokuwa amefundisha mara. Hili lilikuwa muhimu kwa sababu kwa kiasi ambacho Yesu anatoa cha kuachia yote ni mwaliko wa kuwa na uhuru kamili, kwa upande wa mitume, kwa mafundisho yake ya utukufu juu ya Ekaristi. Wapo huru kabisa kukubali au kukataa. Ni uhuru huu utawafanya wazame katika Imani yao juu ya Yesu.

Tutafakari leo, juu ya kujikabidhi kwetu kwa Yesu. Tupo huru kabisa kumfuata yeye au kumkataa. Yesu hapendi tumchague na kumfuata nusu nusu. Maneno ya Yesu yana nguvu, yana changamoto na yanahitaji sadaka. Anataka tumwamini yeye na kumfuata kwa moyo wote na kujikabidhi kweli. Ni Yesu mwenyewe mwenye maneno ya uzima wa milele na tunapaswa tukubali maneno yake na kuamini kwa nguvu zetu zote.

Ni neno la Mungu kweli linalo tutakasa na kutuburudisha. Linatupa uzima; kwahiyo kinachotupa uzima ni Neno la Mungu, kwani maneno anayosema Yesu ni roho tena ni uzima. Jumuiya ya Wakristo kama tunavyosikia katika Somo la kwanza leo, walijenga msingi wao juu ya uzima huu walioupokea kutoka kwa Yesu na faraja ya Roho Mtakatifu. Sisi tuna uhai na uzima, ila uzima wetu na maisha yetu tuyaweke ndani ya Bwana wa uzima Yesu Kristo mwenyewe. Ni maneno haya yenye uzima ya Yesu yalioweza kumrudishia uzima Dorcasi kama tunavyosikia katika somo la kwanza.

Sala: Bwana Yesu, ni wewe pekee ninaye kuchagua kukuamini na kukufuata. Nisaidie nikumbatie yote uliyo fundisha na nisaidie kukuchagua kwa uhuru katika maisha yangu ya kila siku. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment