“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumatatu, Mei 1, 2023
Juma la 4 la Pasaka
Kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi
Mdo 11:1-18;
Zab 42:2-3,43:3-4 (R. 42:3);
Yn 10:11-18.
Au masomo ya kumbukumbu
Mwa 1:26-2:3; au Kol 3:14-15, 17, 23-24
Zab 90:2-4, 12-14, 16 (K. 17);
Mt 13:54-58.
MT. YOSEFU MFANO WA WAFANYA KAZI
Injili ya leo inaongelea kuhusu lile
kundi la watu wanaomtafuta Yesu, siku baada ya kuongeza ile mikate. Kumtafuta
huku haikuwa kwasababu ya upendo kwake, bali kufaidika kutoka kwake. Yesu,
anawaambia wazi kwamba wanamtafuta kwasababu walikula mikate, Yesu anawaeleza
wawe na lengo lingine la kumtafuta. Sababu iwe ni kwasababu anataka kuwapa
chakula cha kiroho.
“Je, unamtafuta Yesu kwasababu njema?” pengine mara nyingi tunamtafuta Yesu
kwasababu ya faida fulani, pengine ili kupata gari, nyumba, mchumba, uponyaji
wa ugonjwa. Yesu anatuonya tuangalie tusimtafute kwasababu ya vitu vinavyo
haribika tu, bali tutafute uzima wa milele.
Kanisa leo lina adhimisha kumbukumbu ya Mt. Yosefu Mfanyakazi. Mungu
alimwamini na kumpa jukumu la kumtunza Mama wa Mungu na Mwana wa Mungu, na kuwa
mlinzi wa nyumba ya Mungu. Hakuna mtu mwingine yeyote aliyekuwa na nafasi hii
pekee. Kupenda kwake kazi ilionesha unyenyekevu wake, aliishi kwa kadiri ya matakwa
ya Mungu. Alikuwa mtu mwenye haki. Kilicho mfanya akubalike machoni pa Mungu
ilikuwa kwasababu ya Imani yake na utii wake. Kujitoa kwake kulionesha
unyenyekevu na kumtegemea Mungu. Na hata baada ya kupata upendeleo kutoka kwa
Mungu, hakuacha kufanya kazi.
Katika hali hii tunaweza kusema kwamba yeye ni somo wa wale wote wanaofanya
kazi, kazi ambayo ni kuonesha unyenyekevu na tegemeo letu kwa Mungu. Leo
tunawakumbuka watu wote duniani wanao fanya kazi kwa manufaa ya uzuri wa
wanadamu wote. Tuwaombee kazi zao zisiharibu mpango wa Mungu kwa mwanadamu bali
zilinde utu na uhai wa kila mwanadamu kama Mt. Yosefu alivyo linda uhai wa Yesu
dhini ya Herode.
Sala: Asante, Mt. Yosefu kwa kumfundisha Yesu kufanya kazi yako.
Tunakushukuru kwa kuzipa kazi za mikono thamani na utakatifu. Tunaomba tuweze
kuzipa heshima kazi na kuwa tayari kwa ajili ya wengine kama wewe. Mt. Yosefu,
mlinzi wa nyumba ya Mungu. Utuombee.
No comments:
Post a Comment