MASOMO YA MISA, MEI 1, 2023
JUMATATU JUMA 4 LA PASAKA
KUMBUKUMBU YA MT. YOSEFU, MFANYAKAZI
SOMO 1
Mwa. 1 : 26-2 : 3
Mungu alisema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu;
kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama,
na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambacho juu ya nchi. Mungu akaumba
mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke
aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze
nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila
kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila
mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda
yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; na chakula cha kila mnyama wa
nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi,
chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo. Mungu
akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa
asubuhi, siku ya sita.
Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake
lote. Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe
siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia
siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha
kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 90:2-4, 12-14, 16 (K) 17
1. Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba
duma,
Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.
(K) Kazi ya mikono yetu uithibitishe, Ee Bwana.
2. Wamrudisha mtu mavumbini,
Usemapo, Rudini, enyi wanadamu.
Maana miaka elfu machoni pako
Ni kama siku ya jana ikiisha kupita,
Na kama kesha la usiku. (K)
3. Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu,
Tujipatie moyo wa hekima.
Ee Bwana, urudi, hata lini?
Uwahurumie watumishi wako. (K)
4. Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako,
Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote.
Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako.
Na adhama yako kwa watoto wako. (K)
INJILI
Mt. 13:54-48
Yesu alipofika nchi yake, akawafundisha maku
tano katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima
hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? mamaye si yeye aitwaye Mariamu?
Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo
hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? Wakachukizwa naye. Yesu
akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na
nyumbani mwake mwenyewe. Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya
kutokuamini kwao.
Neno la Bwana
.........................Sifa kwako Ee Kristo
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of
Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha
ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment