MASOMO YA MISA, JANUARI 16, 2023
JUMATATU, JUMA LA 2 LA MWAKA
SOMO 1
Ebr. 5:1 – 10
Kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu
amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ilia toe matoleo
na dhabihu kwa ajili ya dhambi; awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na
wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; na kwa sababu
hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake
mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. Na hapana mtu alitwaliaye mwenyewe
heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni.
Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake
kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye yaliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo
nimekuzaa, kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani milele kwa mfano wa
Melkizedeki. Yeye siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na
kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi,
akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu; na, ingawa ni Mwana, alijifunza
kutii kwa mates ohayo yaliyompata; naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu
ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; kisha ametajwa na Mungu kuhani
mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 110:1 – 4 (K) 4
(K) Ndiwe kuhani hata milele, kwa mfano wa
Melkizedeki.
Bwana atainyosha toka Sayuni
Fimbo ya nguvu zako.
Uwe na enzi kati ya adui zako. (K)
Watu wako wanajitoa kwa hiari,
Siku ya uwezo wako;
Kwa uzuri wa utakatifu,
Tokea tumbo la asubuhi,
Unao umande wa ujana wako. (K)
Bwana ameapa,
Wala hataghairi,
Ndiwe kuhani hata milele,
Kwa mfano wa Melkizedeki. (K)
SHANGILIO
Lk. 8:15
Aleluya, aleluya,
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa
mioyo yao hulisikia neno la Mungu na kulishika.
Aleluya.
INJILI
Mk. 2:18-22
Siku moja wanafunzi wake Yohane na Mafarisayo
walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohane na
wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje
kufunga maadamu bana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi
pamoja nao hawawezi kufunga. Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi,
ndipo watakapofunga siku ile. Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika
vazi kuukuu; ikiwa ashona, kile kipya kilichotiwa huliharibu lile vazi kuukuu,
na pale palipotatuka huzidi. Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba
vikuukuu; ikiwa atia, ile divai mpya itavipasua viriba vile, divai ikamwagika,
vile viriba vikaharibika. Bali hutia divai mpya katika viriba vipya.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora
- Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are
published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora –
Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings
are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment