Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA ALHAMISI, 29 DESEMBA 2022


MASOMO YA MISA 
ALHAMISI, 29 DESEMBA 2022
OKTAVA YA KUZALIWA BWANA

SOMO 1
1Yoh. 2:3-11

Wapenzi, Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua Yesu, ikiwa tunashika amri zake, Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.

Wapenzi, siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Na hiyo amri ya zamani ni neno lile mlilolisikia.

Tena nawaandikia amri mpya, neno lililo kweli ndani yake na yenu; kwa kuwa giza linapita na vile nuru ya kweli imekwisha kung’aa. Yeye asemaye kwamba yumo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa. Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala ndani yake hamna kikwazo. Bali yeye amchukiaye ndugu yake, yu katika giza, tena anakwenda katika giza, wala hajui aendako, kwa sababu giza imempofusha macho.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 96:1-3,5-6 (K) 11a

(K) Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Mwimbieni Bwana, nchi yote,
Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake. (K)

Tangazeni wokovu wake siku kwa siku,
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,
Na watu wote habari za maajabu yake. (K)

Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu,
Heshima na adhama ziko mbele yake,
Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake. (K)


SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Siku takatifu imetung’aria: Enyi mataifa, njoni mkamwabudu Bwana: Kwa sababu mwanga mkubwa umeshuka duniani.
Aleluya.


INJILI
Lk. 2:22-35

Kisha, zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati ya Musa, walikwenda na Yesu hata Yerusalemu, wamweke kwa Bwana, Kila mtoto mwanamume aliye kifungua mimba ya mamaye na aitwe mtakatifu kwa Bwana, wakatoe na sadaka, kama ilivyonenwa katika sheria ya Bwana, Hua wawili au makinda ya njiwa wawili.

Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, yeye mwenyewe alimpokea mkononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, Sasa Bwana, wamruhusu mtumishi wako, kwa Amani kama ulivyosema kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako, uliouweka tayari machoni pa watu wote; nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

Nababye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake. Simeoni akawabariki akawaambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. Naye mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment