Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UVUMILIVU UTAOKOA MAISHA YENU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Novemba 23, 2022
Juma la 34 la Mwaka wa Kanisa

Ufu 15:1-4;
Zab 97:1-3, 7-9;
Lk 21:12-19


UVUMILIVU UTAOKOA MAISHA YENU!


Tofauti na viongozi wengine ambao ni wabinafsi ambao wanapenda kujitafutia watu wengi na wafuasi wengi, Yesu mchungaji mwema na mkweli anasema wazi kabisa kuhusu dhoruba na adha zitakazo lipata Kanisa na mengi yatakayo wapata wafuasi wake. Kitabu cha ufunuo kiliandikwa ili kuwatia moyo wakristo walioteseka. Leo somo la kwanza, linapiga tarumbeta la wimbo wa ushindi wa waadilifu, waliojitoa na kuwa wafuasi waaminifu wa Mwana-kondoo. Katika familia zetu, katika sehemu zetu za kazi, katika parokia yetu, na sehemu nyingine nyingi tuna muda mzuri wa kushuhudia thamani ya Injili ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Pengine mke msumbufu nyumbani, mume asiyejali, watoto wasumbufu na wasio tii, upweke katika maisha, maisha ya kukatisha tamaa, majirani tegemezi, kutokuelewana, uhusiano uliovunjika, magonjwa, ugumu wakupata fedha, ufisadi ulio kithiri, mumonyoko wa maadili,…hali zote hizi si mateso katika ufuasi wetu? “Huu ndio wakati wakutoa ushuhuda; kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu” asema Bwana. Lakini ni nani kati yetu anayekubali kusimama pembeni na kuamua kuchagua njia wasio isafiri wengi, anayo isafiri Seremala wa nazareti? 

Sala: Bwana, tupe nguvu na roho yakuchagua njia yako na kukufuata wewe kwa uvumilivu. Amina.


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment