“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Novemba 23, 2022
Juma la 34 la Mwaka wa Kanisa
Ufu 15:1-4;
Zab 97:1-3, 7-9;
Lk 21:12-19
UVUMILIVU UTAOKOA MAISHA YENU!
Tofauti na viongozi wengine ambao ni wabinafsi
ambao wanapenda kujitafutia watu wengi na wafuasi wengi, Yesu mchungaji mwema
na mkweli anasema wazi kabisa kuhusu dhoruba na adha zitakazo lipata Kanisa na
mengi yatakayo wapata wafuasi wake. Kitabu cha ufunuo kiliandikwa ili kuwatia
moyo wakristo walioteseka. Leo somo la kwanza, linapiga tarumbeta la wimbo wa
ushindi wa waadilifu, waliojitoa na kuwa wafuasi waaminifu wa Mwana-kondoo.
Katika familia zetu, katika sehemu zetu za kazi, katika parokia yetu, na sehemu
nyingine nyingi tuna muda mzuri wa kushuhudia thamani ya Injili ya Bwana wetu
Yesu Kristo.
Pengine mke msumbufu nyumbani, mume asiyejali,
watoto wasumbufu na wasio tii, upweke katika maisha, maisha ya kukatisha tamaa,
majirani tegemezi, kutokuelewana, uhusiano uliovunjika, magonjwa, ugumu
wakupata fedha, ufisadi ulio kithiri, mumonyoko wa maadili,…hali zote hizi si
mateso katika ufuasi wetu? “Huu ndio wakati wakutoa ushuhuda; kwa uvumilivu
wenu, mtayaokoa maisha yenu” asema Bwana. Lakini ni nani kati yetu anayekubali
kusimama pembeni na kuamua kuchagua njia wasio isafiri wengi, anayo isafiri
Seremala wa nazareti?
Sala: Bwana, tupe nguvu na
roho yakuchagua njia yako na kukufuata wewe kwa uvumilivu. Amina.
Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment