Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UPENDO WA KWELI UNAONDOA HOFU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Novemba 25, 2022
Juma la 34 la Mwaka wa Kanisa

Ufu 20:1-4, 11 - 21:2;
Zab 83:3-6, 8;
Lk 21:29-33


UPENDO WA KWELI UNAONDOA HOFU!


Katika Injili ya leo, Yesu anatuambia sisi kwamba kama tunamjua Mungu, tutatambua lengo lake, na tamaa yake juu yetu. Matokeo yake, kama tunavyo elewa kipindi cha mavuno kimekaribia, tutakuwa tayari kusoma alama za nyakati, na wakati wa mwisho utakapo karibia, tutakuwa tayari, kwasababu tutakuwa tumeshalindwa na mawazo kwamba hakuna kiwezacho kututenga na upendo wa Mungu, si wala mwisho wa nyakati/dunia. Yesu alisema “mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayata pita kamwe”, Na maneno ya Mungu ni “nawapenda” hivyo hakuna cha kuogopa tukibaki katika pendo la Mungu daima.
               
Sala: Naomba nijengwa katika mizizi ya Upendo wako Ee Bwana.


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment