Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

UPENDO UNAKAMILISHWA MBINGUNI!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Novemba 19, 2022
Juma la 33 la Mwaka wa Kanisa


Ufu 11:4-12;
Zab 143:1-2, 9-10;
Lk 20:27-40


UPENDO UNAKAMILISHWA MBINGUNI!


Licha ya mtego uliowekwa na Masadukayo kwa swali lao la kinafiki, Yesu anakuwa na jibu kamili, Mungu sio Mungu wa wafu bali ni Mungu wa walio hai, kwani kwake wote wanaishi. Yeye ni chanzo cha maisha, yeye ni maisha ya milele. Ujumbe wa injili ni kuhusu maisha mapya, ulimwengu mpya, kitu kingine tofauti kabisa. Yesu anampa kila mmoja wetu maisha haya huko mbinguni na mbinguni ni ahadi ya maisha mazuri zaidi. Kwa maneno mengine katika maisha ya mbinguni anayowapa Mungu waaminifu wake, kutakuwa hamna tena kifo,hakutakuwa tena na uchungu, wala mateso, wala majaribu ya ulimwengu. Masadukayo walidhani kwamba kwa kifo, uhusiano wa Mungu na watu wake unakuwa umeisha. Ni sawa na sisi pia katika maisha yetu tunapokumbana na hali kama, kukosa msaada, kukataliwa na kuanguka, na tunadhani kwamba Mungu ametukataa kabisa. Yesu anatukumbusha kwamba ukarimu wa Mungu na kujali watu wake haizuiliwi na ulimwengu huu. Sisi sio watoto wa ulimwengu huu, bali watoto wa Mungu katika hali ya upendo wa ajabu ambao tutaupata katika utimilifu wake katika maisha ya mbinguni kwa njia ya ufufuko.

Sala: Bwana, imarisha Imani yetu kwamba tutafufuka nawe katika upendo wa Baba. Amina


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment