“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Novemba 19, 2022
Juma la 33 la Mwaka wa Kanisa
Ufu 11:4-12;
Zab 143:1-2, 9-10;
Lk 20:27-40
UPENDO UNAKAMILISHWA MBINGUNI!
Licha ya mtego uliowekwa na Masadukayo kwa swali
lao la kinafiki, Yesu anakuwa na jibu kamili, Mungu sio Mungu wa wafu bali ni
Mungu wa walio hai, kwani kwake wote wanaishi. Yeye ni chanzo cha maisha, yeye
ni maisha ya milele. Ujumbe wa injili ni kuhusu maisha mapya, ulimwengu mpya,
kitu kingine tofauti kabisa. Yesu anampa kila mmoja wetu maisha haya huko
mbinguni na mbinguni ni ahadi ya maisha mazuri zaidi. Kwa maneno mengine katika
maisha ya mbinguni anayowapa Mungu waaminifu wake, kutakuwa hamna tena kifo,hakutakuwa
tena na uchungu, wala mateso, wala majaribu ya ulimwengu. Masadukayo walidhani
kwamba kwa kifo, uhusiano wa Mungu na watu wake unakuwa umeisha. Ni sawa na
sisi pia katika maisha yetu tunapokumbana na hali kama, kukosa msaada,
kukataliwa na kuanguka, na tunadhani kwamba Mungu ametukataa kabisa. Yesu
anatukumbusha kwamba ukarimu wa Mungu na kujali watu wake haizuiliwi na
ulimwengu huu. Sisi sio watoto wa ulimwengu huu, bali watoto wa Mungu katika
hali ya upendo wa ajabu ambao tutaupata katika utimilifu wake katika maisha ya
mbinguni kwa njia ya ufufuko.
Sala: Bwana, imarisha Imani
yetu kwamba tutafufuka nawe katika upendo wa Baba. Amina
No comments:
Post a Comment