“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu, Novemba 7, 2022
Juma la 32 la Mwaka wa Kanisa
Tit 1:1-9
Zab 23:1-6
Lk 17:1-6
SOMO LA MAISHA YA UFUASI
Kuna sheria tatu katika sehemu ya Injili leo.
Zinaweza kuleta mabadiliko katika maisha ya muumini. Atakayefuata sheria hizi
kikamilifu atafanya mabadiliko katika maisha yake.
Sheria hizi ni:
1.Dhambi haitabiriki kama Yesu alivyosema
‘makwazo hayana budi kuja’ kwa namna nyingine nisawa nakusema, vitu vinavyo
sababisha dhambi havina budi kuja. Lakini kuwaongoza wengine kwenye dhambi ni
kitu kibaya kabisa.
2. Yesu alisema kwamba, kama mtu akikukosea
umuonye, lakini akiomba msamaha, umsamehe, haijalishi ni dhambi kubwa kiasi
ghani, haijalishi ni jiwe kubwa kiasi ghani aliloweka katika njia zetu
.
3. Imani ni ufunguo wa nguvu zote ulimwenguni.
Mfuasi anapaswa kuwa na Imani sahihi. Msisitizo si juu ya Imani kiasi ghani
alionayo mtu, ni kitendo tu cha kuwa na Imani na kuishi nayo.
Yesu katika hali ya mfano anaongelea kuhusu
kungoa mti nakuutupa baharini. Wakati tunapo patwa na mambo ambayo hayawezekani
katika maisha yetu, tunapaswa kutumaini nguvu ya Mungu ili tuweze kufanya
yasiowezekana.
Sala: Bwana, ongeza Imani
yetu ili tuweze kujenga ufalme wako. Amina
No comments:
Post a Comment