“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu, Novemba 21, 2022
Juma la 34 la Mwaka
Kumbukumbu ya kutolewa Bikira Maria Hekaluni
Zek 2:14-17;
Lk 1:46-55;
Mt 12:46-50
SADAKA ILIYO KAMILI!
Leo Kanisa linakumbuka siku ya kutolewa Bikira
Maria Hekaluni katika Hekalu la Yerusalemu. Inawezekana huenda manabii hawa
watakatifu simeoni na Anna. Walioshuhudia kutolewa kwa Yesu hekaluni, kama
inavyo oneshwa katika sura ya pili ya Injili ya Luka, huenda walimfahamu mama
wa Yesu akiwa msichana mdogo hekaluni na kutambua ukweli wa utakatifu wake wa
pekee. Kujiweka Bikira Maria wakfu kwa Mungu kunaeleza sifa zote za sadaka ilio
kamili: alikuwa tayari, mkarimu, mwenye furaha, hakujuta, na hakujibakiza. Ni kwa
jinsi ghani ilimpendeza Mungu! Tunamuomba Mungu kujiweka kwetu wakfu kwake,
kuweze kuwa chini ya ulinzi wa Mama Maria tukisaidiwa na maombi yake yenye
nguvu, na nafasi yake ya pekee alio nayo kwa Mungu.
Katika somo la kwanza Mungu anatuambia tufurahi
kwasababu anakuja kukaa kati yetu. Katika Agano la Kale “binti Sayuni”, ilikuwa
ni kati ya majina mengi ya watu wa Mungu. Tunapo litumia leo katika Liturjia
zetu tuna maanisha Kanisa, lakini pia tuna maanisha Mama wa Mungu aliyekuwa
karibu na Yesu na yeye ni mfano kamili wa kutekeleza mapenzi ya Mungu. Katika
Injili ya leo, tunasikia Mama mmoja akimwambia Yesu “Heri tumbo lililokuzaa,”
na Yesu anatumia muda huo kuelezea thamani ya kuyafanya mapenzi ya Mungu. Nini
maana ya “kufanya” mapenzi ya yake? Kufanya mapenzi mapenzi nikufanya kile
unacho kifahamu kinaendana na mapenzi yake. Neno lake linapaswa kuongoza katika
mioyo yetu. La pili, yeye familia yake ipo ulimwenguni mwote (familia ya Utatu
katika Umoja). Wakristo wanapata kuwa watoto katika familia hii, sio kwa
kuzaliwa, bali kwakufanya mapenzi ya Mungu. La tatu, kufanya mapenzi ya Mungu
inatupasa kuwa na uhusiano mzuri naye. Kitu kinacho haribu uhusiano wetu na
Mungu ni dhambi. Ili kufufua uhusiano wetu na Mungu lazima kukubali makosa yetu
na kuachana nayo. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuungama dhambi zetu na kutubu.
Mungu yupo tayari daima kutupokea ili tufanye mapenzi yake, lakini tupo tayari
kufanya mapenzi yake na kurudi katika kundi lake?
Sala: Ee Maria, tufundishe
jinsi ya kujitoa kama sadaka ilio hai kwa Mungu. Amina.
Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment