MASOMO YA MISA NOVEMBA 29, 2022
JUMANNE , JUMA LA 1 LA MAJILIO
SOMO 1
Isa. 11:1-10
Siku ile litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi
litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda. Na roho ya Bwana atakaa juu
yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa nay a
kumcha Bwana; na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa
kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa
masikio yake; bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawanya wanyenyekevu wa
dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya
midomo yake atawaua wabaya. Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu
mshipi wa kujifungia.
Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala
pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kimono watakuwa pamoja, na mtoto
mdogo atawaongoza. Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala
pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe. Na mtoto anyonayaye atacheza
penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la
fira. Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana
dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yanavyoifunika bahari.
Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo
kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na
mahali pake pa kupumzika patakuwa na utukufu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 72:1-2,7-8,12-13,17 (K) 7
(K) Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi na wingi wa
Amani kwa milele.
Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,
Na mwana wa mfalme haki yako
Atawaamua watu wako kwa haki,
Na watu wako walioonewa kwa hukumu. (K)
Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi,
Na wingi wa Amani hata mwezi utakapokoma.
Na awe na enzi toka bahari hata bahari,
Toka Mto hata miisho ya dunia. (K)
Kwa maana atamwokoa mhitaji aliapo,
Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi,
Atamhurumia aliye dhaifu na maskini,
Na nafsi za wahitaji ataziokoa. (K)
Jina lake na lidumu milele,
Pindi ling’aapo jua jina lake liwe na wazao;
Mataifa yote na wajibariki katika yeye,
Na kumwita heri. (K)
SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Tazama Bwana wetu atakuja na nguvu, na atayaangaza macho
ya watumishi wake.
Aleluya.
INJILI
Lk. 10:21-24
Siku ile, Yesu alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu nan chi, kwa kuwa mambo haya umewaficha
wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa
ndivyo ilivyokupendeza. Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna
amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote ambaye
Mwana apenda kumfunulia.
Akawageukia wanafunzi wake, akasema nao kwa faragha, Heri
macho yaonayo mnayoyaona ninyi. Kwa kuwa nawaambia ya kwamba manabii wengi na
wafalme walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi wasiyaone; na kuyasikia
mnayoyasikia ninyi wasiyasikie.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of
Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha
ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment