MASOMO YA MISA NOVEMBA 20, 2022
JUMAPILI YA MWISHO WA MWAKA C
SHEREHE YA BWANA WETU YESU KRISTU MFALME
WIMBO WA MWANZO: Ufu. 5:12;1-6
Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa kuupokea uweza na
utajiri na hekima na nguvu na heshima.
Utukufu na ukuu una yeye hata milele na milele.
SOMO 1
2Sam. 5:1 -3
Ndipo kabila zote za Israeli wakamwendea Daudi huko
Hebroni, wakasema naye, wakinena, Tazama, sisi tu mfupa wako na nyama yako.
Zamani za kale, hapo Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyewaongoza
Israeli watoke nje, na kuingia ndani. Naye Bwana akakuambia, Wewe utawalisha
watu wangu Israeli, nawe utakuwa mkuu juu ya Israeli. Basi, wazee wote wa
Israeli wakamwendea mfalme huko Hebroni; naye mfalme Daudi akapatana nao huko
Hebraoni mbele za Bwana; wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya Israeli.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 122:1 – 5 (K) 1
(K) Nalifurahi waliponiambia, na twende nyumbani kwa
Bwana.
Nalifurahi waliponiambia,
Na twende nyumbani kwa Bwana.
Miguu yetu imesimama,
Ndani ya malango yako Ee Yerusalemu. (K)
Ee Yerusalemu uliyejengwa,
Kama mji ulioshikamana;
Huko ndiko walikopanda kabila,
Kabila za Bwana. (K)
Ushuhuda kwa Israeli,
Walishukuru jina la Bwana.
Maana huko huko viliwekwa viti vya hukumu,
Viti vya enzi vya nyumba ya Daudi. (K)
SOMO 2
Kol. 1:11 – 20
Mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya
utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha;
mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu
katika nuru. Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza
katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani,
msamaha wa dhambi.
Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa
viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na
vilivyo katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya
nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au
enzi, au mamlaka; vitu vyote viliubwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye
amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hukshikana katika yeye. Naye ndiye
kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza
katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. Kwa kuwa katika yeye
ilipendeza utimilifu wote ukae; na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi
yake, akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu
vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
INJILI
Lk. 23:35 – 43
Watu walisimama wakitazama Yesu. Wale wakuu nao walikuwa
wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye
Kristo wa Mungu, mteule wake. Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea
na kumletea siki, huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe
mwenyewe. Na juu yake palikuwa na anwani: HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.
Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana,
akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili
akamjibu, akamkemea akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu
iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tulivyostahili kwa
matendo yetu; bali huyu hakutenda lolote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu,
nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia,
leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of
Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha
ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment