MASOMO YA MISA, NOVEMBA 14, 2022
JUMATATU, JUMA LA 33 LA MWAKA WA KANISA
SOMO 1
Ufu. 1:1 – 4; 2:1 – 5
Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe
watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa
mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohane: aliyelishuhudia Neno la
Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona. Heri asomaye
na wao wayasikiao yoe aliyoyaona. Heri asomaye na wao wayasikiao maneno ya
unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu.
Yohane, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na
iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na laiyekuwako na atakayekuja;
na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi.
Nilisikia Bwana ananiambia: Kwa malaika wa kanisa
lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba
katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya
dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi
kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio,
ukawaona kuwa waongo; tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina
langu, wala hukuchoka. Lakin nina neno juu yako, nay a kwamba umeuach aupendo
wako wa kwanza. Basi, kumbuka ni wapi ulioanguka; ukatubu, ukayafanye matendo
ya kwanza.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 1:1 – 4, 6 (K) Ufu. 2:7
(K) Yeye ashindaye, nitampa matunda ya mti wa uzima.
Heri mtu yule asiyekwenda,
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. (K)
Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa. (K)
Sivyo walivyo wasio haki;
Nao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,
Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. (K)
SHANGILIO
Mt. 4:4
Aleluya, aleluya,
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo
katika kinywa cha Mungu.
Aleluya.
INJILI
Lk. 18:35-43
Yesu alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa
ameketi kando ya njia, akiomba sadaka; na alipowasikia makutano wakipita,
aliuliza, Kuna nini? Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita. Akapiga kelele,
akisema, Yesu Mwana wa Daudi, unirehemu. Basi wale waliotangulia wakamkemea ili
anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia,
alimwuliza, Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona. Yesu
akamwambia, Upewe kuona; Imani yako imekuponya. Mara hiyo akapata kuona,
akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya,
© Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya
Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment