Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA DESEMBA 1, 2022

MASOMO YA MISA DESEMBA 1, 2022
ALHAMISI, JUMA LA 1 LA MAJILIO


SOMO 1
Isa. 26:1-6

Siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda; Sisi tunao mji ulio na nguvu; ataamuru wokovu kuwa kuta na mamboma. Wekeni wazi malango yake, taifa lenye haki, lishikalo kweli, uingie. Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea katika Amani kamilifu, kwa kuwa tunakutumaini.

Mtumainini Bwana sikuzote, maana Bwana Yehova ni mwamba wa milele. Kwa kuwa amewashusha wakaao juu, mji ule ulioinuka, aushusha, aushusha hata nchi, auleta hata mavumbini. Mungu utaukanyaga chini, naam, miguu yao walio maskini, na hatua zao walio wahitaji.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 118:1,8-9,19-21,25-27a (K) 26

(K) Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana.

Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema
Kwa maana fadhili zak eni za milele,
Ni heri kumkimbilia Bwana,
Kuliko kuwatumainia wanadamu,
Ni heri kumkimbilia Bwana
Kuliko kuwatumainia wakuu. (K)

Nifungulieni malango ya haki,
Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Lango hili ni la Bwana,
Wenye haki ndio watakaoliingia.
Nitakushukuru kwa maana umenijibu,
Nawe umekuwa wokovu wangu. (K)

Ee Bwana, utuokoe, twakusihi,
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana,
Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Bwana ndiye aliye Mungu,
Naye ndiye aliyetupa nuru. (K)



SHANGILIO
Isa. 55:6

Aleluya, aleluya,
Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni maadamu yu karibu.
Aleluya.



INJILI
Mt. 7:21,24-27

Siku ili, Yesu akawaambia wafuasi wake: Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba, mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.



No comments:

Post a Comment